SHIVJI: Serikali tatu ni kuvunja muungano

SHIVJI: Serikali tatu ni kuvunja muungano

Naomba Kama yupo mwenye nakala ya presentation ya Profesa atuwekee humu tafadhali. Ni vigumu kujadili hoja zake on the basis of newspaper reports.
 
Kukaa chini na kuanza kuelezea aina ya muungano ni kutaka kutouchimba mzizi wa tatizo halisia.

Kama anavyobainisha Prof. Shivji na kusema kuwa na serikali tatu ni chanzo cha kuvunjika kwa muungano. Kama matokeo yake ndiyo hayo, kuna kuwa na umuhimu gani wa kuingia gharama ya kuwa na serikali tatu wakati tunafahamu matokeo yake ni kaput.

Mzizi wa tatizo ni sauti ya wananchi kupitia kura ya MAONI (referendum) kujua kwanza kama watataka waendelee na muungano au waachane nao.

Kama wengi wataafiki kuwepo na muungano basi waseme wao wenyewe ni muungano gani wanataka uwepo ili kupata political Legitimacy and political justification kwa wanasiasa wetu kwa kile watakachokifanya baada ya kura ya maoni.

Ninachokiona hapa ni kuchelewesha muda wakati kinachokuja baadaye kinafahamika siyo kwa magwiji wa political science tu bali hata kwa watu wa kwenye vijiwe vya kahawa.

We just need REFERENDUM. Finito.

Hii ishu ya muungano ndiyo imebeba katiba nzima. Mengine yote yanaitegemea. Ni sawa na watu mnataka kununua usafiri, sasa mnajadili rangi, vioo viwe tinted au la, tairi ziwe sport au la, nk... lakini kubwa zaidi kabla ya hayo yote ni kukubaliana mnataka usafiri gari, au pikipiki au kingine?... Maana kuanza kusema aina ya gari wakati pengeine washirika hawataki gari, wanataka bajaji, ni makosa..

Na hapa kama kuna watu wanadhani wanaweza kuwakilisha mawazo ya watanzania wamechemsha. Watanzania waulizwe, wanataka muungano au la... Then baada ya hapo maswali ya aina na rangi ya muungano yatafuata..
 
huyu jamaa ni walewale wa UDSM "matarumbeta ya kukodi"...watakuja kwa fujo na maelezo mengi yakipigiwa upatu ili waje iokoa CCM, na maslahi ya wazenj.


na wewe maslahi ya zenji yanakunyima usingizi si ndio? nyie wakurya mbona husda sana ,,.mumejua kula chapati na maandazi munaleta zarau sasa!!mumshukuru sana yule baba wenu kambare kuliona hlo , mungekula dona hadi mukafanana na furahasi barazul waheed. and dnt ever open your hole talk about my amizing island .MOFO
 
huyu jamaa ni walewale wa UDSM "matarumbeta ya kukodi"...watakuja kwa fujo na maelezo mengi yakipigiwa upatu ili waje iokoa CCM, na maslahi ya wazenj.


na wewe maslahi ya zenji yanakunyima usingizi si ndio? nyie wakurya mbona husda sana ,,.mumejua kula chapati na maandazi munaleta zarau sasa!!mumshukuru sana yule baba wenu kambare kuliona hlo , mungekula dona hadi mukafanana na furahasi barazul waheed. and dnt ever open your hole talk about my amizing island .MOFO
 
Watanganyika hamna pa kutokea na dubwana lenu muungano,lazima tutalizika kama alivyozikwa muasisi wake.
 
Huyu Nae ni mnafiki na hajulikani msimamo wake Yupo kupotosha watu mara hivi mara vile Yuko kutumikia Mabwana wawili

Japo huwa sikubaliani nae katika hili...lakini nachelea kukuambia humjui Shivji....huu ni msimamo wake na maoni yake tangu awali akihimiza uundwaji wa katiba mpya.
 
Zanzibar walipoweka mipaka na kujiomgezea mamaka kupitia katiba yao mpya hakulalamika zaidi kuwatetea kuwa wana haki kama taifa. Sasa hv anaposikia ujio wa serikali ya tatu anaanza kupatwa na hofu ya serikali hizo kuwekeana mipaka, kuna hatarisha muungano.
Wengi hawauhitaji huo muungano, na serikali tatu ni mbinu tu ya kuuvunja huo muungano na hapo ndipo ilipo hofu ya shivji....hana hoja hoja tena bali ni mapenzi yake kwa muungano, asije kushangaa suala hili kumpunguzia credibilities zake.
 
wazanzibar sisi hatutatki 1,2,3 4,5,6,7,8,wala tisa ni zanzibar yeny mamlaka kamili sasa nyinyi mutazunguk mbuyu lakini dubwana muungno lazima life
 
Kwa nilivyomuelewa Shivji, ni kuwa hakubaliani na compromise kama njia ya kuujadili muungano kwa sababu it's a loose-loose situation.
Anashauri kuwe na consesus, yaani ujadiliwe kwa kutumia faida zake versus hasara zake na wananchi wapige kura kidemokrasia.
Serikali tatu sikubaliani nalo, afadhali uvunjwe. Ila serikali moja ndiyo inayomake sense. Watanganyika obviously tumechoka na serikali mbili.
 
Mkuu, ninaona hoja yako unatengeneza kwa fikra tu ambazo hazibebwi na ukweli halisia.

Hii research ya Watanzania kuwa chini ya 30% wanaofahamu kusoma na kuandika sijui umeitoa wapi wakati research za kimataifa kama UNICEF na UNESCO zinagonga kwenye 70% na huwezi kuniambia kuwa nusu ya hawa hawajui kama kuna muungano wa nchi za Tanganyika na Zanzibar.

Mimi nafikiri watanzania tumefikia katika level ya kujiamulia mambo yetu na mstakabali wa taifa kisiasa kama wananchi wote na ndiyo maana hata CCM wameliona hili na wakaamua kutoa maoni katika tume ya katiba kama wanaona ni lazima kuwepo na mgombea binafsi.

Achana na mambo ya takwimu sijui za UN..... nenda kijiji chochote TZ, ongea na watu halafu waulize kuhusu TZ, kuna waTZ tena wengi tu hawajui Tanzania inatokana na nini, kuna watu hata hawajui kama wanaishi ya Tanzania ingawaje wapo TZ, nenda Umasaini huko kamuulize Mmasai kuhusu Tanzania, au Kondoa Irangi huko au Shinyanga vijijini, Karatu, Dodoma huko, n.k!
Haya ni mambo ambayo nimejionea mwenyewe baada ya kusafiri sana ndani ya TZ (vijijini) kutoḱana na kazi yangu na kuongea na watu wengi, sehemu ambayo watu wana uelewa ni Mkoa wa KLM hapo sawa kuna watu wengi hata vijijini wanaelewa kidogo kuhusu TZ kwa sababu ya Elimu na Dar, sehemu zilizobaki huko vijijini wanajua kuhusu Mwenyekiti wao wao wa kijiji, CCM na Nyerere basi, kuna watu wengi tu wanaishi kijijini na hajawahi kufika Wilayani kwake, Sengerema huko, leo ukamwambie sijui kuhusu kura ya maoni kuhusu Muungano wa Bara na Visiwani, hawezi kukuelewa!

Usinielewe vibaya sisemi kwamba haliwezekani lkn inabidi ufanye kazi sana kuwaelimisha watu kabla ya hiyo kura ya maoni, maana hasa ya Tanzania na Muungano, baada ya hapo labda ndio wapige hiyo kura, lkn sasa hiyo gharama, si no bora uwajengee Shule wajifunze kusoma kuandika na kuhesabu au uwapelekee huduma ya Afya?
Tusiige kila kitu bila kuangalia mazingira yetu, jaribu tu kutoka na kwenda vijijini TZ ongea na watu waulize maswali wadadisi ndio utaelewa ninachokiongelea!

 
Japo huwa sikubaliani nae katika hili...lakini nachelea kukuambia humjui Shivji....huu ni msimamo wake na maoni yake tangu awali akihimiza uundwaji wa katiba mpya.

Umenena Shivji si mtu wa kukurupuka ni mtu thabiti na mwenye msimamo imara wa kile akiaminicho. Tatizo la watu humu ndani wanataka wamejue km anashabikia chama gani ndio msimamo wa watu wenye akili finyu. Wengine wana comment tu bila hata kusoma kazi zake na kumfahamu vyema huyu mpenda maendeleo na haki.
 
Wanaong'ang'ania Serikali mbili wana lao Jambo, Watanganyika tumeamua, tunaitaka Nchi yetu Tanganyika na Hakika tutaipata, As for Prof. Shivji HE IS ENTITLED TO HIS OPINION JUST JUST LIKE ANY OTHER CITIZEN, Nimkumbushe tu principle ya democracy kama hatajali, ''Let the majority have their way and the minority(like Shivji and those of his kind) have their say'' Tume ilitaka maoni ya watanzania, watanzania wamenena loud and clear, ''Tupeni Tanganyika yetu, achilia wazanzibari waendelee na mambo yao, na hilo dubwana lenu la Muungano tupa huko.
 
"Jambo la tatu linawagusa wananchi kwa karibu sana. Ib. 107(2)(h) inaeleza kwamba miongoni mwa madaraka ya Bunge ni 'kujadili na kuridhia mikataba yote inayohusisha rasilimali na maliasili zinazosimamiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano.' Jambo hili ni jema kabisa na la kulifurahia, angalau mikataba hii izungumzwe Bungeni kwa uwazi badala ya wananchi kuambiwa kwamba ni siri ya kibiashara. Lakini, rasilimali na maliasili - ardhi, mafuta, madini, gesiasilia, maji, mapori, n.k. - sio jambo la Muungano. Rasilimali na maliasili ni chini ya mamlaka ya Washirika na wao ndio watayasimamia. Katika hali hii, Serikali ya Muungano itaingia kwenye mikataba ipi na kuhusu rasilimali gani? Ni mfano mwingine wa wananchi kulishwa maneno matamu yasiyo na uhalisia. Ni haki hewa" - Issa Shivji (2013), Ukurasa wa 24, Utatanishi na Ukimya Katika Rasimu ya Katiba Mpya: Mhadhara wa Kuaga Kigoda cha [Taaluma cha] Mwalimu [Nyerere Chuo Kikuu cha Dar es Salaam]


"Baada ya kuisoma Rasimu kwa kina, mimi nadhani kwamba masharti mengi ya Rasimu na muundo wake mzima ni matokeo ya mivutano mikali katika Tume. Bahati mbaya hatuna mwenendo wa majadiliano ya Tume wala taarifa yao rasmi, hata taarifa ya awali. Lakini usomaji wangu wa awali unaniambia kwamba Rasimu hii ni maelewano kwa maana ya compromise, na sio mapatano, au mwafaka, kwa maana ya consensus. Nijieleze kidogo. Katika maelewano au compromise, pande zinazokinzana hatimaye zinakubali kwa shingo upande ili kutokwamisha maamuzi. Pande zote zinapata kidogo na kupoteza kidogo, na kila upande huwa na mkakati wake wa kupata zaidi katika duru ya pili. Kwa hivyo, maelewano kamwe hayawezi kuwa kwa moyo safi. Maelewano au compromise, yanazaa uamuzi legelege. Mapatano auconsensus, kwa upande mwingine, ni maafikiano yanayofikiwa baada ya mjadala mrefu, kila mmoja akilenga kuthibitisha hoja yake na kwa njia hii kusadikisha wenzake kwamba hoja yake ni sahihi. Baada ya kufikia uamuzi wa mwafaka, kila mmoja anatoka akiwa ameridhika na amefurahi. Katika compromise, kila mmoja anatoka amenuna. Ni wazi kwamba huwezi ukapata mwafakafastafasta. Lazima utachukua muda" - Issa Shivji (2013), Ukurasa wa 7-8, Utatanishi na Ukimya Katika Rasimu ya Katiba Mpya: Mhadhara wa Kuaga Kigoda cha [Taaluma cha] Mwalimu [Nyerere Chuo Kikuu cha Dar es Salaam]


"Hitimisho langu juu ya muundo wa muungano ni kwamba, mosi, ni tegemezi na, pili, ni dhaifu kwa sababu umejengwa juu ya msingi wa mchanga wa dhamira na nia nzuri badala ya msingi wa mawe ya nguvu za kikatiba zilizowekwa na wananchi wenyewe. Ni kama kwamba suala la Muungano ni ujirani mwema badala ya umoja wa nchi" - Issa Shivji (2013), Ukurasa wa 19, Utatanishi na Ukimya Katika Rasimu ya Katiba Mpya: Mhadhara wa Kuaga Kigoda cha [Taaluma cha] Mwalimu [Nyerere Chuo Kikuu cha Dar es Salaam]


"Nilisema kwamba ninavyodhani mimi, masharti mengi ya Rasimu yalikuwa maamuzi ya maelewano kwa maana ya compromise na sio mwafaka kwa maana ya consensus. Baada ya uchambuzi wangu, ninadiriki kusema kwamba muundo wenyewe wa serikali tatu uliopendekezwa ni compromise kati ya wale waliosimamia serikali mbili na wale waliopigania muungano wa mkataba, kwa maneno sahihi, kuuvunja muungano. Wanaserikali mbili waliona afadhali kuwa na Muungano, hata kama ni wa serikali tatu, badala ya kuuachia uvunjike; wakajifariji kwa matumaini ya dhamira ya wananchi na nia ya viongozi. Wana-mkataba wakaona kuwa kwa wakati huu wakubali serikali tatu wakijua fika kwamba muundo wa serikali tatu hautadumu na vyovyote vile utavunjika. Nilisema pia kwamba compromise inazaa uamuzi legelege. Compromise juu ya muundo, kwa maoni yangu, imezaa muundo wa muungano legelege. Kuna maeneo mengi nimechambua na kudhihirisha kwamba yatazaa migogoro ambayo hatimaye inaweza kuuvunja Muungano. Kero za Muungano zitaendelea, safari hii kutoka pande zote mbili. Muungano ukivunjika hakuna mwananchi atakayenusurika, awe wa Tanganyika au wa Zanzibar" - Issa Shivji (2013), Ukurasa wa 37-38, Utatanishi na Ukimya Katika Rasimu ya Katiba Mpya: Mhadhara wa Kuaga Kigoda cha [Taaluma cha] Mwalimu [Nyerere Chuo Kikuu cha Dar es Salaam]


"Kwa maoni yangu, kama tungekuwa na mtazamo wa kidemokrasia tungeweza kubuni muundo ambao unakidhi matakwa ya pande zote mbili bila hatari ya kuuvunja Muungano. Mimi binafsi nimewahi kutoa pendekezo la muundo mbadala. Mara ya kwanza niliwasilisha pendekezo langu kwa Baraza la Wawakilishi [...] miezi michache iliyopita. Kwa muhtasari, nilipendekeza dola kamili mbili, la Zanzibar na la Muungano. Bunge la Muungano litakuwa na mabaraza mawili, Baraza la Wananchi na Baraza la Nchi. Wajumbe wa Baraza la Wananchi watachaguliwa moja kwa moja na wananchi wa pande zote mbili kutoka majimboni. Baraza la Nchi litakuwa dogo lenye, tuseme kama wajumbe 30, 15 kutoka Bara na 15 kutoka Zanzibar wakichaguliwa na Bunge la Zanzibar na wabunge kutoka Bara katika Baraza la Wananchi ilimradi wasiwe wajumbe wa bunge lolote lile. Na nilipendekeza orodha tatu - moja ya mambo ya muungano, nyingine ya mambo ya kushirikiana (concurrent matters) na orodha ya tatu ni juu ya mambo ya pamoja (joint interest). Kutokana na muda siwezi kufafanua; nia yangu ni kudhihirisha kwamba muundo mbadala unawezekana" - Issa Shivji (2013), Ukurasa wa 40-41, Utatanishi na Ukimya Katika Rasimu ya Katiba Mpya: Mhadhara wa Kuaga Kigoda cha [Taaluma cha] Mwalimu [Nyerere Chuo Kikuu cha Dar es Salaam]
 
Zanzibar walipoweka mipaka na kujiomgezea mamaka kupitia katiba yao mpya hakulalamika zaidi kuwatetea kuwa wana haki kama taifa. Sasa hv anaposikia ujio wa serikali ya tatu anaanza kupatwa na hofu ya serikali hizo kuwekeana mipaka, kuna hatarisha muungano.
Wengi hawauhitaji huo muungano, na serikali tatu ni mbinu tu ya kuuvunja huo muungano na hapo ndipo ilipo hofu ya shivji....hana hoja hoja tena bali ni mapenzi yake kwa muungano, asije kushangaa suala hili kumpunguzia credibilities zake.
Ahsante mkuu, nakumbuka kabla ya ume ya Wariona Shivji (ambaye namuheshimu sana) alipita sehemu zote za znz katika elimu ya umma. Huko (video zipo) alisema kuwa muungano haukuwa na ridhaa ya wananchi.
Akahoji,kama SMZ ipo wapi mbia mwenza Tanganyika? Alihamasisha sana uundwaji wa serikali 3.

Ninashangaa sana ni Shivji huyo huyo anakataa serikali 3 kuwa zitaua muungano. Sijui alikuwa anahamasisha nini.

Pili, hili suala la serikali 3 linanishangaza sana jinsi ambavyo limegeuka ghafla kuwa shubiri hasa kwa wazanzibar

Jumbe alitolewa kafara kwa serikali 3 kama wanavodai ingawa si hilo bali ukikukaji wa taratibu za kazi za pamoja

CUF ndio walianza na serikali 3 wakati wa vyama vingi. Ipo katika sera zao na wao ni znz 95%

Lipumba kaongea juzi anasema CUF wantaka serikali 3

Tume ya Nyalali, Kisanga na Warioba ziikuja na serikali 3 na wzn wakashupalia sana taarifa zao.

Leo kundi kutoka CUF linalojiita mariidhiano linataka mkataba. Halijawaambia wafuasi wa CUF serikali 3 vipi na kwanini mkataba wakati sera ni serikali 3

Ghafla wazanzibar hawataki serikali 3 walizokuwa wanalilia!!! Hiyo si ajabu kweli.

Nashukuru wapo waliokubali ushauri wetu na sasa wanaibana BLW. Tunawaunga mkono wabaneni sana wawaletee kura ya maoni tupo nyuma yenu na tutawasadia kwa hali na mali.

cc. JokaKuu, Jasusi
 
"Jambo la tatu linawagusa wananchi kwa karibu sana. Ib. 107(2)(h) inaeleza kwamba miongoni mwa madaraka ya Bunge ni 'kujadili na kuridhia mikataba yote inayohusisha rasilimali na maliasili zinazosimamiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano.' Jambo hili ni jema kabisa na la kulifurahia, angalau mikataba hii izungumzwe Bungeni kwa uwazi badala ya wananchi kuambiwa kwamba ni siri ya kibiashara. Lakini, rasilimali na maliasili - ardhi, mafuta, madini, gesiasilia, maji, mapori, n.k. - sio jambo la Muungano. Rasilimali na maliasili ni chini ya mamlaka ya Washirika na wao ndio watayasimamia. Katika hali hii, Serikali ya Muungano itaingia kwenye mikataba ipi na kuhusu rasilimali gani? Ni mfano mwingine wa wananchi kulishwa maneno matamu yasiyo na uhalisia. Ni haki hewa" - Issa Shivji (2013), Ukurasa wa 24, Utatanishi na Ukimya Katika Rasimu ya Katiba Mpya: Mhadhara wa Kuaga Kigoda cha [Taaluma cha] Mwalimu [Nyerere Chuo Kikuu cha Dar es Salaam]


"Baada ya kuisoma Rasimu kwa kina, mimi nadhani kwamba masharti mengi ya Rasimu na muundo wake mzima ni matokeo ya mivutano mikali katika Tume. Bahati mbaya hatuna mwenendo wa majadiliano ya Tume wala taarifa yao rasmi, hata taarifa ya awali. Lakini usomaji wangu wa awali unaniambia kwamba Rasimu hii ni maelewano kwa maana ya compromise, na sio mapatano, au mwafaka, kwa maana ya consensus. Nijieleze kidogo. Katika maelewano au compromise, pande zinazokinzana hatimaye zinakubali kwa shingo upande ili kutokwamisha maamuzi. Pande zote zinapata kidogo na kupoteza kidogo, na kila upande huwa na mkakati wake wa kupata zaidi katika duru ya pili. Kwa hivyo, maelewano kamwe hayawezi kuwa kwa moyo safi. Maelewano au compromise, yanazaa uamuzi legelege. Mapatano auconsensus, kwa upande mwingine, ni maafikiano yanayofikiwa baada ya mjadala mrefu, kila mmoja akilenga kuthibitisha hoja yake na kwa njia hii kusadikisha wenzake kwamba hoja yake ni sahihi. Baada ya kufikia uamuzi wa mwafaka, kila mmoja anatoka akiwa ameridhika na amefurahi. Katika compromise, kila mmoja anatoka amenuna. Ni wazi kwamba huwezi ukapata mwafakafastafasta. Lazima utachukua muda" - Issa Shivji (2013), Ukurasa wa 7-8, Utatanishi na Ukimya Katika Rasimu ya Katiba Mpya: Mhadhara wa Kuaga Kigoda cha [Taaluma cha] Mwalimu [Nyerere Chuo Kikuu cha Dar es Salaam]


"Hitimisho langu juu ya muundo wa muungano ni kwamba, mosi, ni tegemezi na, pili, ni dhaifu kwa sababu umejengwa juu ya msingi wa mchanga wa dhamira na nia nzuri badala ya msingi wa mawe ya nguvu za kikatiba zilizowekwa na wananchi wenyewe. Ni kama kwamba suala la Muungano ni ujirani mwema badala ya umoja wa nchi" - Issa Shivji (2013), Ukurasa wa 19, Utatanishi na Ukimya Katika Rasimu ya Katiba Mpya: Mhadhara wa Kuaga Kigoda cha [Taaluma cha] Mwalimu [Nyerere Chuo Kikuu cha Dar es Salaam]


"Nilisema kwamba ninavyodhani mimi, masharti mengi ya Rasimu yalikuwa maamuzi ya maelewano kwa maana ya compromise na sio mwafaka kwa maana ya consensus. Baada ya uchambuzi wangu, ninadiriki kusema kwamba muundo wenyewe wa serikali tatu uliopendekezwa ni compromise kati ya wale waliosimamia serikali mbili na wale waliopigania muungano wa mkataba, kwa maneno sahihi, kuuvunja muungano. Wanaserikali mbili waliona afadhali kuwa na Muungano, hata kama ni wa serikali tatu, badala ya kuuachia uvunjike; wakajifariji kwa matumaini ya dhamira ya wananchi na nia ya viongozi. Wana-mkataba wakaona kuwa kwa wakati huu wakubali serikali tatu wakijua fika kwamba muundo wa serikali tatu hautadumu na vyovyote vile utavunjika. Nilisema pia kwamba compromise inazaa uamuzi legelege. Compromise juu ya muundo, kwa maoni yangu, imezaa muundo wa muungano legelege. Kuna maeneo mengi nimechambua na kudhihirisha kwamba yatazaa migogoro ambayo hatimaye inaweza kuuvunja Muungano. Kero za Muungano zitaendelea, safari hii kutoka pande zote mbili. Muungano ukivunjika hakuna mwananchi atakayenusurika, awe wa Tanganyika au wa Zanzibar" - Issa Shivji (2013), Ukurasa wa 37-38, Utatanishi na Ukimya Katika Rasimu ya Katiba Mpya: Mhadhara wa Kuaga Kigoda cha [Taaluma cha] Mwalimu [Nyerere Chuo Kikuu cha Dar es Salaam]


"Kwa maoni yangu, kama tungekuwa na mtazamo wa kidemokrasia tungeweza kubuni muundo ambao unakidhi matakwa ya pande zote mbili bila hatari ya kuuvunja Muungano. Mimi binafsi nimewahi kutoa pendekezo la muundo mbadala. Mara ya kwanza niliwasilisha pendekezo langu kwa Baraza la Wawakilishi [...] miezi michache iliyopita. Kwa muhtasari, nilipendekeza dola kamili mbili, la Zanzibar na la Muungano. Bunge la Muungano litakuwa na mabaraza mawili, Baraza la Wananchi na Baraza la Nchi. Wajumbe wa Baraza la Wananchi watachaguliwa moja kwa moja na wananchi wa pande zote mbili kutoka majimboni. Baraza la Nchi litakuwa dogo lenye, tuseme kama wajumbe 30, 15 kutoka Bara na 15 kutoka Zanzibar wakichaguliwa na Bunge la Zanzibar na wabunge kutoka Bara katika Baraza la Wananchi ilimradi wasiwe wajumbe wa bunge lolote lile. Na nilipendekeza orodha tatu - moja ya mambo ya muungano, nyingine ya mambo ya kushirikiana (concurrent matters) na orodha ya tatu ni juu ya mambo ya pamoja (joint interest). Kutokana na muda siwezi kufafanua; nia yangu ni kudhihirisha kwamba muundo mbadala unawezekana" - Issa Shivji (2013), Ukurasa wa 40-41, Utatanishi na Ukimya Katika Rasimu ya Katiba Mpya: Mhadhara wa Kuaga Kigoda cha [Taaluma cha] Mwalimu [Nyerere Chuo Kikuu cha Dar es Salaam]
 
Achana na mambo ya takwimu sijui za UN..... nenda kijiji chochote TZ, ongea na watu halafu waulize kuhusu TZ, kuna waTZ tena wengi tu hawajui Tanzania inatokana na nini, kuna watu hata hawajui kama wanaishi ya Tanzania ingawaje wapo TZ, nenda Umasaini huko kamuulize Mmasai kuhusu Tanzania, au Kondoa Irangi huko au Shinyanga vijijini, Karatu, Dodoma huko, n.k!
Haya ni mambo ambayo nimejionea mwenyewe baada ya kusafiri sana ndani ya TZ (vijijini) kutoḱana na kazi yangu na kuongea na watu wengi, sehemu ambayo watu wana uelewa ni Mkoa wa KLM hapo sawa kuna watu wengi hata vijijini wanaelewa kidogo kuhusu TZ kwa sababu ya Elimu na Dar, sehemu zilizobaki huko vijijini wanajua kuhusu Mwenyekiti wao wao wa kijiji, CCM na Nyerere basi, kuna watu wengi tu wanaishi kijijini na hajawahi kufika Wilayani kwake, Sengerema huko, leo ukamwambie sijui kuhusu kura ya maoni kuhusu Muungano wa Bara na Visiwani, hawezi kukuelewa!

Usinielewe vibaya sisemi kwamba haliwezekani lkn inabidi ufanye kazi sana kuwaelimisha watu kabla ya hiyo kura ya maoni, maana hasa ya Tanzania na Muungano, baada ya hapo labda ndio wapige hiyo kura, lkn sasa hiyo gharama, si no bora uwajengee Shule wajifunze kusoma kuandika na kuhesabu au uwapelekee huduma ya Afya?
Tusiige kila kitu bila kuangalia mazingira yetu, jaribu tu kutoka na kwenda vijijini TZ ongea na watu waulize maswali wadadisi ndio utaelewa ninachokiongelea!

Mkuu sijakuelewa kabisa unaposema wananchi hawana uelewa kuhusu civics wakati huo huo ni wananchi hao hao wanaopiga kura kuwachagua viongozi kuanzia ngazi ya mtaa mpaka taifa. Sikatai kama kuna baadhi ya wananchi hawafahamu mfumo wa uongozi uliopo Tanzania lakini hiyo haizuii wale waliowengi na wanafahamu mifumo ya uongozi kupewa SAY kuhusu mwelekeo wa nchi yao.

Tume ya Jaji Warioba imepokea maoni ya wananchi chini ya 340,000 na mikutano yao ilihudhuliwa na idadi kama ya watu chini ya 1,370,000 wakati Tanzania ina wananchi zaidi ya 44,900,000. Kwako wewe hii process unaiona ni LEGIT lakini ya kuhusu kura ya maoni kwa idadi hiyo hiyo ya waliotoa maoni unaiona ni ILLEGITIMATE.

Kwa nini idadi ya watu waliotoa maoni wasipewe kura ya maoni kuhusu uwepo au kutokuwepo muungano kwa process kama hiyo iliyotumika kupata maoni haya ambayo yanaelekea kutupatia katiba TATA MPYA yenye nchi TATA.
 
Kukaa chini na kuanza kuelezea aina ya muungano ni kutaka kutouchimba mzizi wa tatizo halisia.

Kama anavyobainisha Prof. Shivji na kusema kuwa na serikali tatu ni chanzo cha kuvunjika kwa muungano. Kama matokeo yake ndiyo hayo, kuna kuwa na umuhimu gani wa kuingia gharama ya kuwa na serikali tatu wakati tunafahamu matokeo yake ni kaput.

Mzizi wa tatizo ni sauti ya wananchi kupitia kura ya MAONI (referendum) kujua kwanza kama watataka waendelee na muungano au waachane nao.

Kama wengi wataafiki kuwepo na muungano basi waseme wao wenyewe ni muungano gani wanataka uwepo ili kupata political Legitimacy and political justification kwa wanasiasa wetu kwa kile watakachokifanya baada ya kura ya maoni.

Ninachokiona hapa ni kuchelewesha muda wakati kinachokuja baadaye kinafahamika siyo kwa magwiji wa political science tu bali hata kwa watu wa kwenye vijiwe vya kahawa.

We just need REFERENDUM. Finito.


Nakubaliana nawe,
Nakubaliana na Prof Shivji...
 
Back
Top Bottom