DOKEZO Shule ya Msingi Kitonga (Dar) ina Wanafunzi 4,000, Walimu 14, Madarasa 13

DOKEZO Shule ya Msingi Kitonga (Dar) ina Wanafunzi 4,000, Walimu 14, Madarasa 13

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Kitonga1.jpg
Shule ya Msingi Kitonga iliyopo kwenye Halmashauri ya Jiji Dar es Salaam (Ilala) iliyopo Kata ya Msongola, Kitonga ina Wanafunzi zaidi ya 4000 ambao wanatumia madarasa 13 huku wakitegemea Walimu 15.

Utaratibu wa shule hiyo Wanafunzi wote uripoti asubuhi ambapo baadhi ya Wazazi wenye Watoto wanaosoma shuleni hapo wanadai Watoto wao ulazimika kwenda na mifuko au viroba kwa ajili ya kukalia chini ili wasichafuke kwa vumbi au matope.

Nimezungumza na mmoja wa wazazi shuleni hapo anasema "Shule ina Watoto wengi sana, Mwanangu yupo darasa la sita, huwa anaenda na mfuko autumie kukaa kwa kuwa wengi wao wanakaa chini, mfano darasa la sita nasikia wapo zaidi ya 400.

Pia mzazi mwingine ambaye ana Mtoto wa darasa la pili kwenye shule hiyo anadai mtoto wake wa darasa la pili kuna wakati alikuwa akimchapa kutokana na kuja nyumbani akiwa amechafuka, lakini baadae alikuja kugundua anamuonea baada ya kufika shuleni muda vipindi kujionea hali ilivyo.

"Nilichogundua Darasa la pili Watoto karibia wote wamekaa chini na wapo zaidi ya 600 nilipoingia darasani kwao madawati hayafiki hata 10.”
Kitongaa.jpg
Baadhi ya Wazazi wanadai kuna muda baadhi ya watoto kwenye shule hiyo ulazimika kwenda shuleni alfajiri licha ya mazingira yanayouzunguka shule hiyo kutokuwa rafiki hususani Miundombinu ya barabara ili kuwai madawati ya kukalia.

Uchunguzi unaonesha katika vipindi vya mvua zaidi ya nusu ya Wanafunzi huwa awaendi shuleni kutokana na maeneo ya wazi ya chini ambayo uyatumia kama darasa uwa yamejaa maji jambo ambalo linaongeza ugumu.

Vyanzo mbalimbali vinadai katika kipindi ambacho mvua zilikuwa zinanyesha hususani Aprili 2024 wazazi walikuwa hawawaruhusu watoto kwenda shuleni jambo ambalo wanadai linawaumiza lakini hakuna mbadala kwao.

Mwalimu ya shule hiyo anasemaje?
Mwalimu mmoja wa Shuleni hapo anasema "Kuna Watoto kama elfu nne au zaidi kidogo, tunawafundishia wakiwa chini ya miti mara kwa mara."

Pia kila mtoto kwenye shule hiyo anatozwa Tsh. 300 kwa ajili ya mitihani ya kila siku utamaduni ambao ni sehemu ya upigaji kwa kuwa asilimia kubwa madaftari ya Wanafunzi yamejaa mitihani ambayo uifanya kila siku bila kufundishwa kama ratiba zinavyoonesha.

Utamaduni huo umekuwa kama Sheria tangu Mwaka 2023, ambapo hata kipindi cha mitihani Watoto wanatozwa kiasi hicho ambacho udaiwa ni cha mitihani ya kila siku.

Kingine ni kuwa mitihani hiyo usahihishwa na baadhi ya Wanafunzi, ambapo chanzo rasmi kutoka kwenye shule hiyo kinadai kwamba hilo linatokea kutokana na uhaba wa Walimu ambao unaenda sambamba na idadi ya Wanafunzi wengi.

Ambapo baadhi ya wanafunzi wa darasa la saba na la sita upewa jukumu la kusahisha mitihani ya Wanafunzi wa madarasa ya chini, ambapo mmoja kati ya walimu kwenye shule hiyo anakili uwepo wa suala hilo na kudai kuwa linachangiwa na uwaba wa walimu.

Baadhi ya wazazi wamewahi kuwadokeza baadhi ya viongozi ngazi ya Wilaya na Mkoa lakini limefumbiwa macho mpaka sasa hakuna jitihada za haraka zilizooneshwa wazi kuleta ufumbuzi wa changamoto hizo.

Hii ni aibu kubwa kwa shule iliyopo chini ya Halmashauri ya Jiji kuwa na changamoto kubwa ya aina hiyo, ambapo wametoa wito zaidi kwa mamlaka kuchukua hatua za haraka sana kuepusha changamoto hizo kwa maslahi mapana ya jamii.

Bila jitihada za haraka kufanyika kuna wanafunzi wengi wataacha shule au wengine kukosa kabisa kupelekwa shule kutokana na Mazingira duni yanayoikabili shule hiyo iliyopo jijini.
 
Miundo mbinu katika elimu yetu. Inamapungufu mengi. Ila siasa imeikuwa kikwazo, Kila kitu Tanganyika tumeingiza siasa.
Mfano. Akisimama waziri akizungumzia Elimu utahisi shule zote zinavitabu, Nyumbani za walimu, madarasa na madawati/meza za kutosha. Kwa kifupu utahisi shule zote ni sawa na Private school.
Mungu ibariki Tanzania
 
Shule ya Msingi Kitonga iliyopo kwenye Halmashauri ya Jiji Dar es Salaam (Ilala) iliyopo Kata ya Msongola, Kitonga ina Wanafunzi zaidi ya 4000 ambao wanatumia madarasa 13 huku wakitegemea Walimu 15.

Utaratibu wa shule hiyo Wanafunzi wote uripoti asubuhi ambapo baadhi ya Wazazi wenye Watoto wanaosoma shuleni hapo wanadai Watoto wao ulazimika kwenda na mifuko au viroba kwa ajili ya kukalia chini ili wasichafuke kwa vumbi au matope.

Nimezungumza na mmoja wa wazazi shuleni hapo anasema "Shule ina Watoto wengi sana, Mwanangu yupo darasa la sita, huwa anaenda na mfuko autumie kukaa kwa kuwa wengi wao wanakaa chini, mfano darasa la sita nasikia wapo zaidi ya 400.

Pia mzazi mwingine ambaye ana Mtoto wa darasa la pili kwenye shule hiyo anadai mtoto wake wa darasa la pili kuna wakati alikuwa akimchapa kutokana na kuja nyumbani akiwa amechafuka, lakini baadae alikuja kugundua anamuonea baada ya kufika shuleni muda vipindi kujionea hali ilivyo.

"Nilichogundua Darasa la pili Watoto karibia wote wamekaa chini na wapo zaidi ya 600 nilipoingia darasani kwao madawati hayafiki hata 10.”
Baadhi ya Wazazi wanadai kuna muda baadhi ya watoto kwenye shule hiyo ulazimika kwenda shuleni alfajiri licha ya mazingira yanayouzunguka shule hiyo kutokuwa rafiki hususani Miundombinu ya barabara ili kuwai madawati ya kukalia.

Uchunguzi unaonesha katika vipindi vya mvua zaidi ya nusu ya Wanafunzi huwa awaendi shuleni kutokana na maeneo ya wazi ya chini ambayo uyatumia kama darasa uwa yamejaa maji jambo ambalo linaongeza ugumu.

Vyanzo mbalimbali vinadai katika kipindi ambacho mvua zilikuwa zinanyesha hususani Aprili 2024 wazazi walikuwa hawawaruhusu watoto kwenda shuleni jambo ambalo wanadai linawaumiza lakini hakuna mbadala kwao.

Mwalimu ya shule hiyo anasemaje?
Mwalimu mmoja wa Shuleni hapo anasema "Kuna Watoto kama elfu nne au zaidi kidogo, tunawafundishia wakiwa chini ya miti mara kwa mara."

Pia kila mtoto kwenye shule hiyo anatozwa Tsh. 300 kwa ajili ya mitihani ya kila siku utamaduni ambao ni sehemu ya upigaji kwa kuwa asilimia kubwa madaftari ya Wanafunzi yamejaa mitihani ambayo uifanya kila siku bila kufundishwa kama ratiba zinavyoonesha.

Utamaduni huo umekuwa kama Sheria tangu Mwaka 2023, ambapo hata kipindi cha mitihani Watoto wanatozwa kiasi hicho ambacho udaiwa ni cha mitihani ya kila siku.

Kingine ni kuwa mitihani hiyo usahihishwa na baadhi ya Wanafunzi, ambapo chanzo rasmi kutoka kwenye shule hiyo kinadai kwamba hilo linatokea kutokana na uhaba wa Walimu ambao unaenda sambamba na idadi ya Wanafunzi wengi.

Ambapo baadhi ya wanafunzi wa darasa la saba na la sita upewa jukumu la kusahisha mitihani ya Wanafunzi wa madarasa ya chini, ambapo mmoja kati ya walimu kwenye shule hiyo anakili uwepo wa suala hilo na kudai kuwa linachangiwa na uwaba wa walimu.

Baadhi ya wazazi wamewahi kuwadokeza baadhi ya viongozi ngazi ya Wilaya na Mkoa lakini limefumbiwa macho mpaka sasa hakuna jitihada za haraka zilizooneshwa wazi kuleta ufumbuzi wa changamoto hizo.

Hii ni aibu kubwa kwa shule iliyopo chini ya Halmashauri ya Jiji kuwa na changamoto kubwa ya aina hiyo, ambapo wametoa wito zaidi kwa mamlaka kuchukua hatua za haraka sana kuepusha changamoto hizo kwa maslahi mapana ya jamii.

Bila jitihada za haraka kufanyika kuna wanafunzi wengi wataacha shule au wengine kukosa kabisa kupelekwa shule kutokana na Mazingira duni yanayoikabili shule hiyo iliyopo jijini.
Hii shule iko Dar? Du basi hii Safari bado Sana.
 
Tanzania bado sana . Bado tuna uhitaji mkubwa sana wa walimu wa shule za msingi kwa mfano mkoa wa pwani kule wilaya ya mkuranga kuna shule ya msingi ina madarasa hayafiki saba lakin ina wanafunzi kuanzia darasa la kwanza hadi lasaba imagine hao wanasomaje ????
 
Wazazi 4000 wakiungana naamini hao watoto watasoma kwenye madarasa yenye viti vizuri na yaliyopambwa tena ndani ya mda mfupi
Mwenyekiti na diwani wasiishie kusifia TU serikali wajue pia kuwaunganisha watu kuleta maendeleo yao
 
Serikali yetu huwa haina mipango madhubuti hususani kwenye sekta za elimu na afya!
 
Subiri waje.....watakanusha kila kitu...watoto wanateseka....sasa hiyo shule nenda chooni ukajionee...sijui kama wana huduma maji hapo....ni hatari sanaaaa.....
 
Shule ya Msingi Kitonga iliyopo kwenye Halmashauri ya Jiji Dar es Salaam (Ilala) iliyopo Kata ya Msongola, Kitonga ina Wanafunzi zaidi ya 4000 ambao wanatumia madarasa 13 huku wakitegemea Walimu 15.

Utaratibu wa shule hiyo Wanafunzi wote uripoti asubuhi ambapo baadhi ya Wazazi wenye Watoto wanaosoma shuleni hapo wanadai Watoto wao ulazimika kwenda na mifuko au viroba kwa ajili ya kukalia chini ili wasichafuke kwa vumbi au matope.

Nimezungumza na mmoja wa wazazi shuleni hapo anasema "Shule ina Watoto wengi sana, Mwanangu yupo darasa la sita, huwa anaenda na mfuko autumie kukaa kwa kuwa wengi wao wanakaa chini, mfano darasa la sita nasikia wapo zaidi ya 400.

Pia mzazi mwingine ambaye ana Mtoto wa darasa la pili kwenye shule hiyo anadai mtoto wake wa darasa la pili kuna wakati alikuwa akimchapa kutokana na kuja nyumbani akiwa amechafuka, lakini baadae alikuja kugundua anamuonea baada ya kufika shuleni muda vipindi kujionea hali ilivyo.

"Nilichogundua Darasa la pili Watoto karibia wote wamekaa chini na wapo zaidi ya 600 nilipoingia darasani kwao madawati hayafiki hata 10.”
Baadhi ya Wazazi wanadai kuna muda baadhi ya watoto kwenye shule hiyo ulazimika kwenda shuleni alfajiri licha ya mazingira yanayouzunguka shule hiyo kutokuwa rafiki hususani Miundombinu ya barabara ili kuwai madawati ya kukalia.

Uchunguzi unaonesha katika vipindi vya mvua zaidi ya nusu ya Wanafunzi huwa awaendi shuleni kutokana na maeneo ya wazi ya chini ambayo uyatumia kama darasa uwa yamejaa maji jambo ambalo linaongeza ugumu.

Vyanzo mbalimbali vinadai katika kipindi ambacho mvua zilikuwa zinanyesha hususani Aprili 2024 wazazi walikuwa hawawaruhusu watoto kwenda shuleni jambo ambalo wanadai linawaumiza lakini hakuna mbadala kwao.

Mwalimu ya shule hiyo anasemaje?
Mwalimu mmoja wa Shuleni hapo anasema "Kuna Watoto kama elfu nne au zaidi kidogo, tunawafundishia wakiwa chini ya miti mara kwa mara."

Pia kila mtoto kwenye shule hiyo anatozwa Tsh. 300 kwa ajili ya mitihani ya kila siku utamaduni ambao ni sehemu ya upigaji kwa kuwa asilimia kubwa madaftari ya Wanafunzi yamejaa mitihani ambayo uifanya kila siku bila kufundishwa kama ratiba zinavyoonesha.

Utamaduni huo umekuwa kama Sheria tangu Mwaka 2023, ambapo hata kipindi cha mitihani Watoto wanatozwa kiasi hicho ambacho udaiwa ni cha mitihani ya kila siku.

Kingine ni kuwa mitihani hiyo usahihishwa na baadhi ya Wanafunzi, ambapo chanzo rasmi kutoka kwenye shule hiyo kinadai kwamba hilo linatokea kutokana na uhaba wa Walimu ambao unaenda sambamba na idadi ya Wanafunzi wengi.

Ambapo baadhi ya wanafunzi wa darasa la saba na la sita upewa jukumu la kusahisha mitihani ya Wanafunzi wa madarasa ya chini, ambapo mmoja kati ya walimu kwenye shule hiyo anakili uwepo wa suala hilo na kudai kuwa linachangiwa na uwaba wa walimu.

Baadhi ya wazazi wamewahi kuwadokeza baadhi ya viongozi ngazi ya Wilaya na Mkoa lakini limefumbiwa macho mpaka sasa hakuna jitihada za haraka zilizooneshwa wazi kuleta ufumbuzi wa changamoto hizo.

Hii ni aibu kubwa kwa shule iliyopo chini ya Halmashauri ya Jiji kuwa na changamoto kubwa ya aina hiyo, ambapo wametoa wito zaidi kwa mamlaka kuchukua hatua za haraka sana kuepusha changamoto hizo kwa maslahi mapana ya jamii.

Bila jitihada za haraka kufanyika kuna wanafunzi wengi wataacha shule au wengine kukosa kabisa kupelekwa shule kutokana na Mazingira duni yanayoikabili shule hiyo iliyopo jijini.
Si mnawasena walimu wana hali ngumu? Napendekeza bei ya mitihani ipande kutika 300 mpaka 500. Hata nauli zimepanda aisee
 
Wazazi 4000 wakiungana naamini hao watoto watasoma kwenye madarasa yenye viti vizuri na yaliyopambwa tena ndani ya mda mfupi
Mwenyekiti na diwani wasiishie kusifia TU serikali wajue pia kuwaunganisha watu kuleta maendeleo yao

Tatizo ni ukosefu wa akili ya kujua namna ya kutatua tatizo

hongera zao hao walimu kwa kujipatia posho ya tsh. 300 kwa kila mtoto
maana 300 * 4000 ni 1.2 m
hata wakigawana elf 50 sio haba wanapunguza stress japo kuwa hy ela inaweza kununua madawati 10
 
CCM unaupiga mwingi.
Mbunge wa Ilala CCM.
Mkuu wa mkoa CCM
Mkuu wa wilaya CCM
Mkurugenzi CCM
Wanànchi CCM.
Nadhani Hilo halituhusu maana waliosababisha na waliosababishiwa wameridhika.
 
Shule ya Msingi Kitonga iliyopo kwenye Halmashauri ya Jiji Dar es Salaam (Ilala) iliyopo Kata ya Msongola, Kitonga ina Wanafunzi zaidi ya 4000 ambao wanatumia madarasa 13 huku wakitegemea Walimu 15.

Utaratibu wa shule hiyo Wanafunzi wote uripoti asubuhi ambapo baadhi ya Wazazi wenye Watoto wanaosoma shuleni hapo wanadai Watoto wao ulazimika kwenda na mifuko au viroba kwa ajili ya kukalia chini ili wasichafuke kwa vumbi au matope.

Nimezungumza na mmoja wa wazazi shuleni hapo anasema "Shule ina Watoto wengi sana, Mwanangu yupo darasa la sita, huwa anaenda na mfuko autumie kukaa kwa kuwa wengi wao wanakaa chini, mfano darasa la sita nasikia wapo zaidi ya 400.

Pia mzazi mwingine ambaye ana Mtoto wa darasa la pili kwenye shule hiyo anadai mtoto wake wa darasa la pili kuna wakati alikuwa akimchapa kutokana na kuja nyumbani akiwa amechafuka, lakini baadae alikuja kugundua anamuonea baada ya kufika shuleni muda vipindi kujionea hali ilivyo.

"Nilichogundua Darasa la pili Watoto karibia wote wamekaa chini na wapo zaidi ya 600 nilipoingia darasani kwao madawati hayafiki hata 10.”
Baadhi ya Wazazi wanadai kuna muda baadhi ya watoto kwenye shule hiyo ulazimika kwenda shuleni alfajiri licha ya mazingira yanayouzunguka shule hiyo kutokuwa rafiki hususani Miundombinu ya barabara ili kuwai madawati ya kukalia.

Uchunguzi unaonesha katika vipindi vya mvua zaidi ya nusu ya Wanafunzi huwa awaendi shuleni kutokana na maeneo ya wazi ya chini ambayo uyatumia kama darasa uwa yamejaa maji jambo ambalo linaongeza ugumu.

Vyanzo mbalimbali vinadai katika kipindi ambacho mvua zilikuwa zinanyesha hususani Aprili 2024 wazazi walikuwa hawawaruhusu watoto kwenda shuleni jambo ambalo wanadai linawaumiza lakini hakuna mbadala kwao.

Mwalimu ya shule hiyo anasemaje?
Mwalimu mmoja wa Shuleni hapo anasema "Kuna Watoto kama elfu nne au zaidi kidogo, tunawafundishia wakiwa chini ya miti mara kwa mara."

Pia kila mtoto kwenye shule hiyo anatozwa Tsh. 300 kwa ajili ya mitihani ya kila siku utamaduni ambao ni sehemu ya upigaji kwa kuwa asilimia kubwa madaftari ya Wanafunzi yamejaa mitihani ambayo uifanya kila siku bila kufundishwa kama ratiba zinavyoonesha.

Utamaduni huo umekuwa kama Sheria tangu Mwaka 2023, ambapo hata kipindi cha mitihani Watoto wanatozwa kiasi hicho ambacho udaiwa ni cha mitihani ya kila siku.

Kingine ni kuwa mitihani hiyo usahihishwa na baadhi ya Wanafunzi, ambapo chanzo rasmi kutoka kwenye shule hiyo kinadai kwamba hilo linatokea kutokana na uhaba wa Walimu ambao unaenda sambamba na idadi ya Wanafunzi wengi.

Ambapo baadhi ya wanafunzi wa darasa la saba na la sita upewa jukumu la kusahisha mitihani ya Wanafunzi wa madarasa ya chini, ambapo mmoja kati ya walimu kwenye shule hiyo anakili uwepo wa suala hilo na kudai kuwa linachangiwa na uwaba wa walimu.

Baadhi ya wazazi wamewahi kuwadokeza baadhi ya viongozi ngazi ya Wilaya na Mkoa lakini limefumbiwa macho mpaka sasa hakuna jitihada za haraka zilizooneshwa wazi kuleta ufumbuzi wa changamoto hizo.

Hii ni aibu kubwa kwa shule iliyopo chini ya Halmashauri ya Jiji kuwa na changamoto kubwa ya aina hiyo, ambapo wametoa wito zaidi kwa mamlaka kuchukua hatua za haraka sana kuepusha changamoto hizo kwa maslahi mapana ya jamii.

Bila jitihada za haraka kufanyika kuna wanafunzi wengi wataacha shule au wengine kukosa kabisa kupelekwa shule kutokana na Mazingira duni yanayoikabili shule hiyo iliyopo jijini.
Changeni mtengeneze madawati ya watoto wenu
 
Back
Top Bottom