Shule zenye ubora ni gharama lakini muhimu sana

Shule zenye ubora ni gharama lakini muhimu sana

Sio kila mtanzania ana uwezo wa kumpeleka mwanae shule za gharama ila kwa wale wenye uwezo huo wafanye hivyo. Shule za kata zina msaada mkubwa sana kwa wazazi walio na kipato kidogo na ndio zilizobeba idadi kubwa ya wanafunzi.
Jambo la msingi ni sisi wazazi tushirikiane na walimu kuwasimamia watoto wetu wasome kwa bidii. Jitihada zikifanyika kwa pamoja vijana watafanya vizuri katika mitihani yao.
Kuna ndugu yangu ni afisa wa halmashauri moja ya vijijini alienda kwenye kikao cha wazazi shuleni. Ugomvi ulikuwa ni wazazi kugoma kutoa mchango wa mahindi na maharage ili watoto wao wale shuleni. Wananchi walipangana na kupeana hoja, na kuwapanga wale wazee wanaojua kuongea sana. Walipinga kuchangia chakula eti hawana uwezo na walimu watauza mahindi.

Mwalimu mkuu haamini wananchi wanakosaje vibaba vya mahindi. Wananchi wakamwambia mbona walimu wake wana madeni kwenye maduka ya mangi, kama wana uwezo mbona wanakopa. Mjadala ukaisha wanafunzi watashinda njaa sababu elimu ni bure. Hiyo shule ilikuwa inafelisha, umbali wa kwenda shule wengine ni mkubwa, kijiji hakina umeme. Mipango ikaja ni walimu kufundisha bure muda wa ziada ila wanafunzi watakuwa na njaa hivyo wale shuleni. Wazazi wakagoma kuchanga mahindi elimu ni bure (hapo waliishagoma kuchangia hela ya masomo ya ziada jioni).
Sasa unategemea kufaulu hapo?

Ukiwa mzazi unaishi sehemu ina ugumu usifanye mambo mengi, wewe pambana wanao wasome sehemu zina unafuu. Unategemea miujiza shule kama Mburahati au Mbagala?
Hiyo Mbagala kwanza pembeni kuna danguro, wanafunzi zaidi ya 200 wanagonga sifuri kwenye NECTA, walimu hawatoshi watoto kibao.

Nazungumzia kwa anayeweza. Ambaye hawezi sawa ila akae akijua.
 
Lengo la uzi liko kwenye uzi wenyewe. Unaweza iona imekaa kikuda huo ni mtazamo wako, ila huyo binti kafeli shule kidato cha pili kutokana na shule aliyosoma na maisha ya nyumbani kwao. Mwishowe ameingia kwenye cycle ileile ya umaskini uleule.
Angesoma shule nzuri kidogo tu asingefeli, angekaa shule muda mrefu zaidi akakomaa akili, asingetoroka kwao kuishi kwa mwanaume kisa maisha yamemshinda. Hata angeweza pata marafiki wa maana shule nzuri na hata angeelimika zaidi akaajiriwa au kujiajiri au kuwa jobless ila sio desperate hivi, na angezaa watoto wake anavyojisikia yeye. Sasa yuko kwa mwanaume anateswa kisa hana shule, kazi wala yeyote wa kumsaidia.
Okee okee
 
Shule Namba Moja NI familia Bora,
1. Baba na Mama weñye Elimu Dunia na Elimu akhera,

Shuleni Naona kitu kikubwa wanachopata wanafunzi NI;

1. Exposure
2. Lugha
3. Interpersonal and interpersonal Skills
 
Shule Namba Moja NI familia Bora,
1. Baba na Mama weñye Elimu Dunia na Elimu akhera,

Shuleni Naona kitu kikubwa wanachopata wanafunzi NI;

1. Exposure
2. Lugha
3. Interpersonal and interpersonal Skills
Na familia bora inachunga sana mazoea ya mtoto na wapi anakulia. Hairuhusu mtoto aishi mazingira magumu yasiyowezesha kipaji chake au kufungua akili yake kwa visingizio vya "azoee shida, hata sisi tulitoka uko, mbona hata hizi shule kuna wanaofaulu, kwanza siku hizi hamna ajira hata akienda shule yeyote tu elimu iko mtaani".

Familia bora haikubali mtoto asome shule kuna vibaka, walevi wa gongo, darasa moja wanafunzi 300, shule wanafunzi 2000 walimu wa hesabu wawili.

Kama uwezo upo na mzazi anajifanya bahili kugharamikia elimu huyo ni mzembe na hafai kuigwa.
 
Na familia bora inachunga sana mazoea ya mtoto na wapi anakulia. Hairuhusu mtoto aishi mazingira magumu yasiyowezesha kipaji chake au kufungua akili yake kwa visingizio vya "azoee shida, hata sisi tulitoka uko, mbona hata hizi shule kuna wanaofaulu, kwanza siku hizi hamna ajira hata akienda shule yeyote tu elimu iko mtaani".

Familia bora haikubali mtoto asome shule kuna vibaka, walevi wa gongo, darasa moja wanafunzi 300, shule wanafunzi 2000 walimu wa hesabu wawili.

Kama uwezo upo na mzazi anajifanya bahili kugharamikia elimu huyo ni mzembe na hafai kuigwa.

Yeah ishu kûbwa NI uwezo.

Lakini kingine Kwa Mtu anayeishi kwèñye Miji mikubwa ni Vizuri Afanye juu chini Mtoto asome shule nzuri tofauti na Watu WA vijiini.

Mjini Mtoto kuharibika Kwa hizi Shule zetu za zayumba aka Kayumba ni kugusa
 
Kuna ndugu yangu ni afisa wa halmashauri moja ya vijijini alienda kwenye kikao cha wazazi shuleni. Ugomvi ulikuwa ni wazazi kugoma kutoa mchango wa mahindi na maharage ili watoto wao wale shuleni. Wananchi walipangana na kupeana hoja, na kuwapanga wale wazee wanaojua kuongea sana. Walipinga kuchangia chakula eti hawana uwezo na walimu watauza mahindi.

Mwalimu mkuu haamini wananchi wanakosaje vibaba vya mahindi. Wananchi wakamwambia mbona walimu wake wana madeni kwenye maduka ya mangi, kama wana uwezo mbona wanakopa. Mjadala ukaisha wanafunzi watashinda njaa sababu elimu ni bure. Hiyo shule ilikuwa inafelisha, umbali wa kwenda shule wengine ni mkubwa, kijiji hakina umeme. Mipango ikaja ni walimu kufundisha bure muda wa ziada ila wanafunzi watakuwa na njaa hivyo wale shuleni. Wazazi wakagoma kuchanga mahindi elimu ni bure (hapo waliishagoma kuchangia hela ya masomo ya ziada jioni).
Sasa unategemea kufaulu hapo?

Ukiwa mzazi unaishi sehemu ina ugumu usifanye mambo mengi, wewe pambana wanao wasome sehemu zina unafuu. Unategemea miujiza shule kama Mburahati au Mbagala?
Hiyo Mbagala kwanza pembeni kuna danguro, wanafunzi zaidi ya 200 wanagonga sifuri kwenye NECTA, walimu hawatoshi watoto kibao.

Nazungumzia kwa anayeweza. Ambaye hawezi sawa ila akae akijua.
Hoja nzuri sana mkuu. Natamani sana wazazi tupate mwamko mkubwa tuwajengee watoto wetu mazingira bora ya elimu na maadili.
 
Kwenye mtihani wa kiswahili unagewa bonge la mkeka kisha una-summarize bila kupoteza maana ,inaonekana haijajifunza ku-summarize mambo.
 
Mfumo wetu wa elimu ni mbovu ndiyo maana hizi za binafsi zinaonekana ni nzuri lakini ukweli hizi za English medium Huwa ni kiingereza hakuna kingine.Kama unapesa nyingi peleka international japo kuwa na kwenyewe kunaushoga baadhi ya shule.
 
Kuna baadhi ya nyuzi uwa tunakaza Sana mishipa ya fuvu, kumbe tunabishana na watoto wetu kabisa humu jf. HONGERA mtoa mada, bandiko zuri Sana.😊
 
Sio kila mtanzania ana uwezo wa kumpeleka mwanae shule za gharama ila kwa wale wenye uwezo huo wafanye hivyo. Shule za kata zina msaada mkubwa sana kwa wazazi walio na kipato kidogo na ndio zilizobeba idadi kubwa ya wanafunzi.
Jambo la msingi ni sisi wazazi tushirikiane na walimu kuwasimamia watoto wetu wasome kwa bidii. Jitihada zikifanyika kwa pamoja vijana watafanya vizuri katika mitihani yao.
Duh yani comment yako ilitakiwa ndio iwe Uzi. Comment bora Kuliko uzi
 
Siku ukifa watakao enda kuchimba kaburi ni Hao Hao unao waita WA Kayumba.

Siku nyumba yako ikiungua moto watakao kuja kuokoa ni Hao Hao wa Kayumba rejea Ghorofa la kariakoo.


Usidharau watu . Utu WA mtu haupimwi kwa shule aliyo soma
 
Back
Top Bottom