Si kila Mchungaji, Nabii au Mtume anayetumia Biblia kufundisha ni Mkristo, wengine ni matapeli

Si kila Mchungaji, Nabii au Mtume anayetumia Biblia kufundisha ni Mkristo, wengine ni matapeli

Naona andiko lako kama la kuwapiga madongo tu manabii, mitume na wachungaji wa kisasa huku likiwa haliwagusi wale wa zamani, halafu Ukimwi sio matokeo ya dhambi, kuna watu wanazaliwa nao na wengine wanaupata kwa sababu nyingi sana.
Kumekuwa na wimbi kubwa la watu wanaojiita Mitume, Manabii au Wachungaji ambao wamekuwa wakiwakonfyuzi watu hasa wale ambao si waumini wa Dini ya Kikristo.

Kitu kibaya zaidi hao Viongozi wa madhehebu hayo wamekuwa wakitumia Biblia kama njia ya kufanya huo utapeli wao ukaonekana ni ukweli, Watanzania wengi wamejikuta wananaswa kwenye mtego huo kwakuwa kama tujuavyo Watanzania na kusoma vitabu ni kama paka na panya.

Watu wengi kutokusoma Biblia ndiyo imekuwa mtaji mkubwa wa hao matapeli kwasababu wanafahamu hao wanaojiita Wakristo hawaielewi Biblia kwa ufasaha.

Biblia ni kitabu kilicho wazi kabisa kwa wafuasi wa Kristo na hakina mambo mengi kama watu wanavyodhani. Kwakuwa wafuasi wengi wanaojiita "Wakristo" hawapendi kuisoma ndipo hao matapeli wamejipatia huo mwanya wa kuwadanganya.

Neno "Wakristo" lilipatikana kwa mara ya kwanza pale kwenye Mji wa Antiokia, na hii ni baada ya wafuasi wa Yesu kukutana huko kwa muda wa mwaka mmoja na kuungana katika mambo ya kufundishana yale yote ambayo Yesu Kristo aliwafundisha kabla hajapaa.

Hii utaipata katika kitabu cha Matendo ya Mitume 11 : 26

Hivyo neno "Wakristo" kwa kifupi ni watu wanao muamini Yesu Kristo, kuiamini imani yake na yale aliyoyafundisha.

Maswali amabayo Nabii, Mtume au Mchungaji hawezi yajibu;

1. Ni wapi katika Biblia imesema watu wafunge hadi wafe ili waende mbinguni?

2. Ni wapi katika Biblia imesema ukitaka gari uende ukaombewe?

Msingi wa kupata gari ni kufanya kazi, na maandiko yako wazi. "Fanya kazi siku sita na siku ya saba pumzika. Mungu ataibariki kazi ya mikono yako."

3. Ni wapi katika Biblia imesema ukitaka mchumba (mume/mke) upakwe maji au mafuta ya upako?

4. Ni wapi katika Biblia imesema ukiumwa UKIMWI uende kanisani uombewe UKIMWI uondoke?

Kupata UKIMWI ni matokeo ya dhambi, hivyo Mungu kwa uaminifu kabisa anaweza kukusamehe dhambi ila UKIMWI ukaendelea kuishi nao hadi unakuingiza kaburini.

Msipoielewa Biblia hakika mtafia dhambini.

5. Ni wapi katika Biblia imesema biashara yako ikiyumba ukachukue mafuta na maji ya upako uweke kwenye biashara yako?

Fanya biashara kwa uaminifu, fuata taratibu zote za kibiashara, mfanye Mungu awe wa kwanza katika biashara zako hakika utafanikiwa tu. Achaneni na hao matapeli watawaumiza sana tu.

6. Ni wapi katika Biblia imesema ukitaka kumuona Mtume au Nabii ni lazima ulipe fedha?

7. Ni wapi katika Biblia imesema ukitaka kuombewa na mtumishi wa Mungu ulipe fedha?

8. Ni wapi katika Biblia imesema ukitaka mtoto ukapewe mafuta na maji ya upako utumie ili uzae?

Wakristo ni watu wa maandiko (scriptures), ukiona unaingia mkenge kwa hao wapiga ramli wanaojiita Manabii na Mitume tambua wewe si Mkristo bali ni muunga tela la wapagani.

Mtaibiwa na kutapeliwa sana, kibaya zaidi mtakoseshwa na uzima wa milele kwa madanganyo ya matapeli hao.
 
Rudi kajifunze Ubatizo na maana yake
Halafu ujue pia Yesu hakufa, aliyekufa ni Kristo
Ukiuelewa ukristo utaelewa


Yesu ni Mungu

Ma d nawe ubatizo c mnasema ondoleo la dhambi ya asili alofanya Adam na hawa au nini

Tena yesu hakufa? Dah alokufa kristo mhhh tatizo hili.


Yesu ni Mungu dooooh
 
Rc ni matapeli pia
unaweza kutubu kwa binadamu mwenzio
Hakuna Mkatoliki anae Tubú kwa binadamu mwenzie hata mmoja!
Kabla hujaandika ni Heri Umuombe Roho Mtakatifu Akufunulie!
IMEANDIKWA!
[emoji116][emoji116]
John 20:23
[23]Wo wote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa; na wo wote mtakaowafungia dhambi, wamefungiwa.

Matthew 7:1-5
[1]Msihukumu, msije mkahukumiwa ninyi.

[2]Kwa kuwa hukumu ile mhukumuyo, ndiyo mtakayohukumiwa; na kipimo kile mpimiacho, ndicho mtakachopimiwa.

[3]
Basi, mbona wakitazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe huiangalii?

[4]Au utamwambiaje nduguyo, Niache nikitoe kibanzi katika jicho lako; na kumbe! Mna boriti ndani ya jicho lako mwenyewe?

[5]Mnafiki wewe, itoe kwanza ile boriti katika jicho lako mwenyewe; ndipo utakapoona vema kukitoa kile kibanzi katika jicho la ndugu yako. Kutweza Kitakatifu

1 Corinthians 4:5
[5]Basi ninyi msihukumu neno kabla ya wakati wake, hata ajapo Bwana; ambaye atayamulikisha yaliyositirika ya giza, na kuyadhihirisha mashauri ya mioyo; ndipo kila mtu atakapoipata sifa yake kwa Mungu.
 
Back
Top Bottom