Si tatizo kwa Makonda kumwita Mbowe mwanasiasa uchwara na Zitto mshirikina ikiwa Chadema na Act wanaweza pia kumwita Magufuli hivyohivyo, ndio siasa

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Inaonekana wengi wamekasirishwa au kufedheheshwa sana na kitendo cha Makonda kuwaita Mbowe mwanasiasa uchwara na Zitto mshirikina. Sioni kama hili ni tatizo.

Alichofanya Makonda ni kuweka utangulizi au precedent ya aina ya mipasho ya kisiasa unayoweza kufanya kwa kiongozi wa chama cha siasa. Kwa kuwa sio tatizo kwa Makonda kufanya hivyo, sio tatizo kwa viongozi wa vyama vya upinzani kufanya hivyo hivyo kwa Magufuli kama kiongozi wa chama cha siasa.

Ila jambo moja la kukumbuka ni kwamba, Makonda amewaita Mbowe na Zitto mwanasiasa uchwara na mshirikina katika wadhifa wao wa kuwa viongozi wa vyama, jambo ambalo Magufuli pia ana wadhifa huo.

Hivyo basi vyama vya upinzani visitumie mpasho huo katika background ya Magufuli kama raisi wa nchi; yaani huwezi kusema raisi Magufuli ni mwanasiasa uchwara au mshirikina, lakini haitakuwa tatizo ukisema mwenyekiti wa CCM Magufuli ni mwanasiasa uchwara au mshirikina.

Na kama hii ni precedent isiyokubalika, basi na tuone Magufuli au Polisi au msajiri wa vyama vya siasa wakichukua hatua dhidi ya Makonda au hata kumkemea hadharani.

La sivyo ni mpasho unaokubalika kwa viongozi wa vyama vya siasa, awe Mbowe, Zitto au Magufuli. Ni mipasho ya kisiasa tunaishuhudia hata Marekani au Afrika Kusini.
 
Baba,kesi zitakazofunguliwa hapo mashitaka hayatapungua 29, siku hizi biswalo ni mbunifu wa mashitaka hujawahi ona.
 
Baba,kesi zitakazofunguliwa hapo mashitaka hayatapungua 29, siku hizi biswalo ni mbunifu wa mashitaka hujawahi ona.
Hapana. Polisi wetu hawana akili kiasi hicho. Angalau wanazo za kuambiwa na wakasikiliza maagizo.
 
Makonda sio kiongozi wa kisiasa bali ni mtendaji wa serikali hapaswi kujiingiza katika mipasho ya kisiasa labda hilo hulifahamu.
Hata maneno anayotoa Magufuli ya kejeli au anayopewa huwa sio kama Rais bali hayo ni kama mwenyekiti wa Chama.
Rais hakejeli wala hakejeliwi.
 
Umenena vema sana. Tutegemee basi, CCM kuja na kanusho au kemeo dhidi ya huyu kiongozi Makonda katika serikali ya CCM
 
Chadema wana Act hawawezi kutamka kauli hizo kwani action speaks louder than words.
 
Alisikika jamaa mmoja wa upinzani akitamka maneno kama hayo...

Kilichomkuta ni huruma sana...



Cc: mahondaw
 
Mkuu Pascal umeliona hilo eeh? Labda tulipoingia mfumo wa vyama vingi hilo hatukulisisitiza ipasavyo. Tuliona sehemu kubwa ya kuondoa siasa katika utendaji wa kiserikali ilikuwa ni jeshini tu, na kwingine, kutia ndani na Polisi, hatukukumbuka. Lakini tunatakiwa kwenda mbali zaidi ya kufundisha watu - bado hata katika ngazi ya raisi tunatoa majukumu ya kisiasa kwa watu ambao ni watendaji wa serikali. Sasa sijui kama ni kutojua au kiburi tu na kufanya makusudi - impunity by design kwa kuwa hakuna atakaetuuliza. Kuna vitu hatuhitaji kubadili katiba kuvibadilisha au kuvitekeleza, ni common sense tu - ambayo unfortunately, is not common to everyone.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…