Siamini naanza kuacha uhuni, umalaya, ubazazi na ubaradhuli. Huyu mtoto nimemuibua humu humu JamiiForums

asikwambie mtu ukisikia "kupatwa kwa gudume ndo huku" hii huwa inatoka mara moja kila baada ya miaka 1,000. waswahili wanasema "aisifuye mvua imemnyeshea" moyo wangu umepapatika kwa miaka mingi sana na hatimaye umefika kwenye kilindi cha bahari na kutulia tuli kama maji ya mtungini.

Duuh! Hatimaye kaka GuDume umepatwa lol. Sababu sio kwa sifa hizi ulizozimwaga.

Kila la kheri kaka! Ila sio kwa misemo hiyo leo sababu usingeitumia , nadhani uzi wako ungekuwa mrefu hatari.
 
shukrani ndugu yangu... ni upenzi tu wa lugha hii adhimu ambayo haishi hamu na utamu.
Mkuu Leo umetumia vitendawili nahau misemo mithali na tanakali sauti nyingi mno
Hongera ndugu yangu.


Nami naingia chimbo niibuke na mke
 
mkimuibukia ana screen shoot ananitumia... na tayari ameshanitumia wote waliomtaka humu nawafaham ntakuja tu kuwapa onyo muda si mrefu.

Kwa kuwa na sisi tunatafuta humu humu, ni vizuri ungemtaja kama alivyofanya Mshana Jr ili tusije tukajikuta tunamuibukia shemeji yetu pm kwa kutojua[emoji41] [emoji41] [emoji41]
 
hizo ni zako mimi yangu "jasiri haachi asili" yako wewe iandike utakavyo ... hiyo ya ukambaa ni typing error tu.

Umejitahidi na methali, ila umekosea tu kdg. "Jahili aachi asili" na sio"jasiri"...... Ukuukuu wa pamba, si upya ukambaa. Not mkambaa..!
 
Huyo sasa itabidi tumuite Gujike...haha
 
ha ha ha.. mwenye moyo mgumu lakini laini, mwenye macho makali ya kuona ndani lakini mapole kwa kuona nje... mwenye uzuri wa waridi. aliyeogea maji ya majani ya mkaratusi.. mwenye uzuri wa tausi..... sauti ya chiriku.... mwendo wa maringo kama twiga atembeapo kati kati ya msitu... amejawa maneno matamu ya kumtoa nyoka pangoni. hana makuu mwenye moyo wa huruma na upendo wa asili....
Ni mwanamke gan anaweza kumteka gudume
 
SAFI SANA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…