Hapa tujadiliane ya April tu mabandiko yanavyosema
Ndiyo maana katika post namba 27 ya uzi huu nikaandika labda nirudi shule ya kushiriki mijadala. Baada ya kupewa sharti la kushiriki mjadala bila kujadili maoni na ushahidi unaoletwa na washiriki kuhusu mada iliyopo mezani.
Leo tumeongezewa sharti lingine la kujadili Mambo ambayo yalisemwa April tu! Sasa ukichunguza yale yaliyosemwa April tu ambayo, nguli wetu wa mijadala ndugu Nguruvi3, ni karibu mengi yanahusiania na mambo yaliyosemwa miezi iliyopita yaani kuanzia March 30, 2022 kurudi nyuma. Yaani mpaka yale ya miaka miwili nyuma. Nimejaribu kuyaanisha mambo yanayoonyesha hayakusemwa ama kutendwa April 2022 bali ni mambo ya nyuma ili niweze kuonyesha tatizo linalonikabili katika kuhusika katika mjadala huu ulio mezani kutokana na "masharti bunifu" anayoyatoa mleta mada kwenye uzi huu kadri anavyojisikia inafaa.
Ni ajabu sana mleta maada ambaye amekuwa mtu muhimu sana katika kuchochea uhuru wa kutoa maoni si katika jukwaa hili nadhani hata kwenye maeneo yake mengine ya kufanyia kazi, naye kuanza kufifisha juhudi za wananchi ama washiriki wa mijadala kutoa maoni yao na hasa mahali pale wanapooneka wanaonyesha udhaifu wa kimtazamo wa mleta mada.
Ni kweli, mleta mada ni Mwalimu wangu muhimu sana hapa JF, lakini kitendo cha kupinga yale aliyonifundisha juu ya uhuru wa kutoa maoni kimenistua sana.
=====
Ni ujumbe ulioashiria nchi haikuwa katika mstakabali mzuri miaka michache iliyopita.
Hapa unazungumizia mika michache iliyopita, hii si April 2022 tena, hivyo lazima turejee miaka michache iliyopita tuone nini kilitokea ili kuimarisha mjadala ulipo mezani.
Washiriki walimweleza Mwalimu Nyerere kadri walivyomfahamu
Lazima turejee matendo ya Mwalimu Nyerere wakati wa uhai wake (siyo April hiyo) ndipo tujikite vyema kwenye mjadala.
Katika kuchangia Bw Lyongo alizungumzia udini, ukabila na ukanda akisema miaka ya karibuni tumerudi nyuma. Hakuna shaka Bw Lyongo alizunguzia utawala wa JPM
Kujadili mazungumzo ya Lyongo lazima tuirejee kwenye hayo matukio ya miaka ya hivi karibu tuone nini hasa kilitokea. Hakuna cha April 2022 hapa!
Ni kwa kuelewa hivyo uchaguzi wa 2020 Mahakama kuu haikupata lalamiko, si kwasababu hayakuwepo bali ilionekana haki ya uchaguzi haitapatikana Mahakamani
Uchaguzi wa 2020 huo. Unaachaje kuyazungumzia matukio ya 2020 katika kujibu ama kutoa maoni kisa lazima tujadili ya April 2022. Kumbukumbu zipo lazima zirejewe kama kweli hatuna ajenda yenye kuficha baadhi ya mambo kisa April 2022 katika mjadala huu!
Ukichukua matukio matatu ya mwezi huu, hadhra na watu walioongelea hakuna shaka miaka awamu ya tano ilipanda mbegu mbaya nchini
Awamu ya tano kwa mujibu ya baadhi ya Watanzania ilikoma mwaka jana baada ya kumpata Mama yetu mpendwa Mama Samia Suluhu Hassan kuwa kiongozi wetu wa nchi yaani Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania. Hawamo ya tano si ya April 2022. Sasa kwa nini unatuzuia tusirejee kile kilichotokea awamu yatano ili kutoa maoni yetu na facts ili kuijenga hoja kwenye mjadala huu, wakati msingi wa mada uliyoleta inajaribu kulinganisha matukio ya wakati uliopita na sasa kwa kisingizio cha yale ya April 2022?
Mwenyekiti aliwahi kuingia matatani kwa kauli ya kutaka ''viongozi wachunguzwe kwani wapo waliokuwa na mafaili Mirembe''
Hii kauli haikutoka April 2022. Sasa tunaachaje kumjadili mtoa kauli hii na mahusiano yake na wale ambao alikuwa najaribu kuwajengea taswira ya udhalilishaji?
======
Kwa kweli, mwalimu wangu
Nguruvi3 umenistaajabisha sana.