Pre GE2025 Siasa za kuchafuana zashika kasi CCM Moshi mjini

Pre GE2025 Siasa za kuchafuana zashika kasi CCM Moshi mjini

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Ndagullachrles

Senior Member
Joined
Jun 20, 2023
Posts
153
Reaction score
161
Sasa ni dhahiri kwamba kasi ya kuchafuana kwa makada wa chama cha mapinduzi Katika Jimbo la moshi mjini inazidi kushika kasi kadri siku zinavyozidi kuyoyoma kuelekea uchaguzi mkuu hapo mwakani.

Wapo vijana wanaoendesha harakati hizo kupitia magroup ya WhatsApp wakiwalenga makada wa CCM wanaodaiwa kuwa kwenye mpango wa kuomba kuteuliwa kuwania ubunge kwa tiketi ya ccm hapo mwakani kupitia kura za maoni .

Awali vijana hao wanadaiwa kuwa upande wa mfanyabiashara na mkurugenzi wa kampuni ya Ibraline Fllling station ambako inadaiwa walikuwa walichafua viongozi akiwamo mbunge wa Sasa Jimbo la Moshi mjini(ccm),Priscus Tarimo,meya wa Manispaa ya Moshi,Zuberi Kidumo na aliyekuwa meya wa Manispaa hiyo ,Juma Raibu Juma.

Hali hiyo ilipekea baadhi ya makada waanodiwa kuwa katika mpango huo kuitwa kwenye kamati ya maadili ya Chama hicho na kupewa onyo .

Hata hivyo haijawahi kudhibitika kama matendo ya kuwachafua viongozi hao nilikuwa na baraka zozote kutoka kwa mfanyabiashara huyo kwani mara zote alikuwa akikana kufanya hivyo.

Lakini katika hali isiyokuwa ya kawaida vijana hao wanadiwa kumgeuka mfanyabiashara huyo na kuanza kumshambulia kwa maneno makali hatua ambayo imewaibua watu wengi na kudai vijana hao wanasunmbuliwa na njaa ya tumbo .

"Kaka nikuambie tu kwa ufupi hawa vijana wanasumbuliwa na njaa ya tumbo hakuna kitu kingine "
'Lakini hebu tujiulize hawa hawa walikuwa wanamchafua sana mheshimiwa mbunge Priscus Tarimo na mstahiki Meya Kidumo , leo wamegeuka na kuanza kumsifia,unadhani mheshimiwa Mbunge na mstahiki Meya watawaamini tena?,acha tuone lakini wanajidhalilisha sana kwa kweli".

Wengi wanahoji kulikoni vijana hawa Leo wamegeukia upande wa Priscus Tarimo na Kwa Mstahiki Meya,kuna nini,?,ni kuelekea uchaguzi mkuu hapo mwakani ama ni kwa ajili ya tumbo?.

Baada ya vijana hao kuanza kurushq mashambulizi kwa kada huyo na mfanyabiashara ,baadhi ya watu waliokaribu nao wameanza kurusha picha za mnato zikiwaonye wakipata msosi pamoja na mfanyabiashara huyo .

Mpaka Sasa kunatajwa kuwepo makundi hasimu matatu yanayodaiwa kuwa katika harakati za kuwapigania watia nia ya ubunge .

Yetu macho ,kazi kwenu wanasiasa na siasa zenu za majitaka
 
Vijqna wa hiko chama hapo moshi wanaangalia mwenye pesa, ndie watae mpigia campaign
 
Kwa Maafisa Elimu Kata zote, Wakuu wa Shule za Serikali za Msingi na Sekondari, Moshi Manispaa, Kilimanjaro

Mkurugenzi wa Manispaa, Mwajuma Nasombe, kwa mamlaka aliyonayo, anawataka watumishi wote kuchangia fedha kwa ajili ya "Get Together" ya Watumishi Wote wa Moshi Manispaa, ikiwa ni sherehe ya kuukaribisha Mwaka 2025. Sherehe hii itafanyika tarehe 01.02.2025.

Kiwango cha Kuchangia

Wakuu wa Idara na Vitengo, Waratibu Elimu Kata, Wakuu wa Shule za Sekondari, na Walimu Wakuu wa Shule za Msingi: Tsh 50,000/-
Walimu Wote: Tsh 30,000/-
watumishi wengine: Tsh 20,000/-

Mwisho wa kuchangia ni siku ya 26.01.2025 bila kukosa.

Angalizo

Hata hivyo, ni muhimu kuwajulisha watumishi kuhusu baadhi ya masuala yanayohusiana na zoezi hili la kuchangia fedha:

1. Ushirikishwaji: Watumishi wengi hawajashirikishwa kabla ya tangazo hili. Ushirikishwaji wa awali ni muhimu ili kuhakikisha kuwa kila mmoja anafahamu lengo la michango hii.

2. Kamati ya Kuratibu: Hakuna kamati iliyoundwa kwa ajili ya kuratibu zoezi hili. Kukosekana kwa kamati kunaleta hofu miongoni mwa watumishi kuhusu matumizi ya fedha zao.

3. Muda wa Tangazo: Tangazo hili limetolewa muda mfupi sana, kuanzia tarehe 23.01.2025 na mwisho wa kuchangia ni tarehe 25.01.2025. Hii inapunguza nafasi ya watumishi kupanga na kujiandaa kwa michango yao.

4. Mshahara na Madeni: Watumishi wengi wamepokea mshahara wao na tayari wameshatumia kwa kulipa madeni wanayodaiwa. Hali hii inawafanya wengi kuwa na wasiwasi kuhusu kutoa michango zaidi.

5. Kujulishwa kwa Mkuu wa Wilaya: Mkuu wa Wilaya hajajulishwa kuhusu ukusanyaji huu wa fedha za michango, jambo ambalo ni muhimu ili kuweza kufuatilia matumizi ya fedha hizo.

6. *Kuchoshwa na Mkurugenzi:*Watumishi wengi wanasema wanachoshwa na mkurugenzi huyu, kwani mara kwa mara anaitisha michango. Wengi wanahisi kuwa huenda hii ni sehemu ya fedha za kampeni yake kuelekea kwenye uchaguzi wa ubunge.

Ombi

Kwa kuzingatia masuala haya, tunaomba zoezi hili lisitishwe hadi pale ambapo itakapofanyika mabadiliko yanayohitajika ili kuhakikisha kuwa watumishi wanashirikishwa ipasavyo na michango inakusanywa kwa njia ya uwazi na uaminifu.
Hii itasaidia kujenga uhusiano mzuri kati ya watumishi na uongozi wa manispaa.

Tunatumai kuwa maelezo haya yatasaidia katika kueleweka kwa sababu za kutokubali michango hii na kutafutwa kwa suluhisho la kudumu litakalowafaidi watumishi wote wa Moshi Manispaa.

Ahsanteni.
 
Back
Top Bottom