T14 Armata
JF-Expert Member
- Mar 7, 2017
- 12,362
- 41,886
Baada ya kuirudisha kwa Waafrika tija iko wapi? Au waliitumia kuhifadhia waganga wa kienyeji.Anayelipa fidia ni mkurupukaji na mwoga.ardhi walinyang'anywa waafrika na kijimilikisha wazungu pasipo kihalali.Mugabe alichokifanya ni kuirudisha Kwa wenyewe waafrika.
Kiongozi unatakiwa ufanye maamuzi yenye tija kwa nchi na sio maamuzi popular ya maskini. Maskini wa Tanzania ukiwaambia matajiri wote wezi na ndio wanafanya msiwe na hela watafurahia, wataomba kiongozi uwakamate kina Mo Dewji, Bakhresa na wenzao uwapokonye mali. Mwishowe unabaki na uchumi failed.
Iddi Amin alifanya hivyohivyo akafukuza Wahindi na kuwapora mali huku Waganda maskini wakishangilia, wakaenda UK mikono mitupu. Wakaanza uiya kule wakapata hela, wakarudi miaka baadae wakakuta viwanda walivyoporwa na Amin akawagawia maofisa wake vilaza vimekufa. Wakaviendeleza huku Waganda wakicheza kachabari.