Siasa za Kukurupuka: Hatimaye Zimbabwe Yaanza Kuwafidia Mabilioni Wakulima wa Kizungu Walioporwa Mashamba Yao na Mugabe

Siasa za Kukurupuka: Hatimaye Zimbabwe Yaanza Kuwafidia Mabilioni Wakulima wa Kizungu Walioporwa Mashamba Yao na Mugabe

Cha kusikitisha zaidi ni kuwa ule upuuzi alioufanya Mugabe ulishabikiwa na wapuuzi kibao huko Zimbabwe na hata hapa bongo.

Watu weusi kwa kweli wamelaanika
Wanasiasa aina yake ni wale walitaka ku run kila kitu wakati capacity hiyo hawana.
 
Baada ya aliyekuwa Rais wa Zimbabwe Marehemu Mugabe kuwapora Walowezi wa Kizungu na ambao walikuwa raia wa Zimbabwe wenye Asili ya Uingereza,hatimaye Serikali imetangaza kuanza kuwalipa mabilioni ya fidia kutokana na kuporwa Mali Yao.

Uporaji wa mashamba ya Walowezi wa Kizungu ulifanyika kama kete ya Kisiasa ya Mugabe kushinda uchaguzi na ilipelekea Nchi hiyo kuwekewa vikwazo Vikali na kuporomoka Kwa Uchumi na kuigeuza Zimbabwe ambayo ilikuwa na usatwi kuwa Moja ya Mataifa ya kishenzi yaani failed state.


My Take
Hizo ndio hasara za siasa za Kukurupuka na mihemko.Kiko wapi Sasa? Unalipa na fidia Juu.

Kunae yule wa makinikia nae alitaka afanye hayo hayo kabla ya kurudi nyuma japo aliwafanyia wafanyabiashara wa Beureu De Change ambao Samia kawarudishia pesa zao.

View attachment 3152702

Pia soma Zimbabwe: Mamia ya Wakulima wa Kizungu Waliotimuliwa na Hayati Mugabe Warejea kwa wingi kuendeleza kilimo chao

View: https://www.instagram.com/p/DGQIhKPojFv/?igsh=MXF0dTNsNmJzZDAyYQ==


Mugabe alipotoka vibaya sana kunyang'anya Ardhi za Wazungu na kuua uchumi wa nchi hiyo.


Tangu Balozi wa Marekani ate mbelen ofisi za makao makuu ya JF siku chache zilizopita, nahisi kabisa moderators na wamiliki mnashikiwa akili na Mabeberu, na hili jukwaa ni mradi tukufu wa mabeberu against Africanism.

Maana kazi yenu ni kuwaponda viongozi wa kiafrika hasa waliodiriki kuonesha uzalendo wao kwa kutanguliza maslahi ya waafrika kwanza.
Kwangu mimi hii ni aibu hasa kwa mleta maada maana ni wazi uko upande wa hao mabwana zenu.

Mugabe alikosea kutekeleza jambo hili la kutwaa Ardhi ya Wazungu. Aliongozwa na Mihemko, Tamaa na Chuki binafsi dhidi ya Wazungu licha ya kujua kwamba Watu weusi waliopo katika nchi hiyo hawakuwa na uwezo wa kuitumia vizuri Ardhi hiyo.

Mathalani, Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe wakati huo alipokuwa anawapokonya Ardhi raia Wazungu kwenye nchi hiyo alikuja na Sera yake iliyokuwa ikisema kwamba Mtu mmoja anapaswa amiliki shamba moja tu na wala siyo zaidi, yaani: "One Man One Farm." Lakini matokeo yake yeye mwenyewe Mugabe alijitwalia na kujigawia Mashamba mengi yapatayo 28 nchi nzima hali iliyosababisha manung'uniko katika jamii na yeye Rais kuingia kwenye migogoro mikubwa na washirika wake wa karibu Sana kwenye Utawala wake kama vile Mwanasheria Mkuu wa Serikali yake na Mkuu wake wa Majeshi
 
Back
Top Bottom