Meneja Wa Makampuni
JF-Expert Member
- Jul 7, 2020
- 7,899
- 10,415
- Thread starter
-
- #81
Wewe ndio umeelewa vibaya..Sasa unajichanganya, shooting yourself in the foot. Umesema mwenyewe Ulaya hutumia PNG (piped natural gas) kutoka Russia, Uzbekistan ndiyo Russia yenyewe? Kwa nini hawakuona umuhimu wa GTL.
Hapa Tanzania (especially Mtwara, Dar na Pwani) tuna nafasi nzuri sana ya kutumia PNG kwa viwanda na households. Tayari tuna PNG mains eneo ka Mikocheni, kijiji cha TPDC. Inaweza kusambazwa kwingine nchi nzima sawa kabisa na mains za TANESCO.
Kwenye nchi zilizo mbali na machimbo, gesi husafirishwa after freezing the natural gas at minus 261 centigrade (hiyo ni LNG, liquified natural gas) na kuipeleka kwa meli au treni hadi Mwanza na Sumbawanga. Ikifika huko inayeyushwa na kusambazwa kama PNG.
I'm not sure about this but I could be wrong. Baada ya USSR kusambaratika zikazaliwa Russia, Ukraine, Belorus, Uzbekistan, Kazakhstan, Georgia, Latvia, Ishengutia, Armenia, nk, utawala bora hakuna, kwa hiyo machimbo hayo ya gesi yamo mikononi mwa sultani, au dictator, au jeshi. Ndiyo maana unakuta SASOL ana ubia na nchi badala ya kuacha funding ifanyike kupitia stock exchange. Wewe unamjua Rais wa Uzbekistan? Au wa Chechnya?
Bado sijakubali: economics za GTL hazilipi Boss wangu.
Lengo la kuwa na GTL sio kwaajili ya kutengeneza gesi. Lengo la GTL ni kwaajili ya kuzalisha Luquid products (jet fuel, diesel na petroli) hizo ndio product zenye soko na uhitaji mkubwa kuliko hiyo gesi. LPG inayopatikana kwenye GTL ni byproduct.