Siasa za msikiti Uingereza

Siasa za msikiti Uingereza

Nawewe ni mfia dini kiasi hicho pamoja na kuwa na umri mkubwa?

Ikitokea ukaitwa gaidi, mbaguzi n.k utakataa?
Unafahamu yakwamba taratibu na mafundisho mengi (si yote) ya kiislamu yanabagua na kuwakandamiza wasio waisilamu?


Mfano Mwisilamu nduguye ni mwisilamu hili lilitokea hata Chuo kikuu cha Garisa, pili nimefatilia post zako nyingi zinazohusu dini yako ni dhahiri unahekima ila ni mbaguzi mkubwa kwa wasio waislamu, kuna mtu anaitwa Faizafoxy nimepitia kidogo post zake mama yangu huyu ni Mbaguzi, na nikatili sana dhidi ya dini zingine
Mkuu badilisheni hayo mafundisho image yenu kwa jamii itasafishika
Statarea,
Unaandika ukiwa umeghadhibika.

Ili mjadala uwe na tija na wasomaji pamoja na wachangiaji wanufaike
na mjadal kubwa kwanza ni adabu.

Kuheshimiana.

Ikiwa mchango wako umejaa ''name calling,'' unakuwa tayari ushajitoa
maana.

Utapuuzwa.
Hakuna apendae kusoma kelele na jeuri.

Sasa umechanganya mambo mengi katika post yako.
Kwanza kunishambulia binafsi.

Mjadala hauendeshwi hivyo.
Muhimu ni kutoa hoja.

Umegusa mafunzo ya Uislam ambayo huyajui.
Lakini kubwa hili somo wewe hujapatapo kulisoma na hivyo kulifahamu.

Umeshika kalamu na kuandika huku kichwa kimejaa hasira.

Tuanze na hili la ugaidi na nakuomba usome niliyopata kuandika kwani
kwanza umfahamu huyo unaejadiliananae na pili utalijua somo lenyewe:

Mohamed Said: ISLAM, TERRORISM AND AFRICAN DEVELOPMENT

Ukishasoma hii paper sasa reja hapa barazani na unayotaka kusema na
baada ya hapo tutaendelea na hayo mengine ya ubaguzi ili tupate kumjua
nani mbaguzi katika nchi yetu.
 
Waislamu ni watu wa ajabu sana.

Mbona hamuelezi sababu ya kuvunjwa kwa huo msikiti.Mnajifanya kujua sana haki zenu na mara zote nyie ndiyo huonewa.

Hapo UDOM kuna makanisa yamejengwa??
Sababu wanasema Sie waislamu tumemroga VC aliyefariki hapo majuzi.

Na wale watumishi wote 11 walohamishwa wapo ktk uongozi wa jumuia ya waislam UDOM

Hii ndio sababu zote unazosikia ni kuweka mambo sawa tu.
 
Khan said:
Waislamu mna uwezo finyu sana wa kufikiri, Mnalalama kama mtoto wa kambo, Mnaikumbatia tamaduni ya kigeni (Uislamu) Kuliko utu au ubinadamu, Waislamu hamuaminiki, waislamu ni Magaidi, watu ambao hawana utu, Watu ambao huwezi kuwa na amani kuishi nao, watu wanaoonesha ubaguzi wa kidini wazi wazi! "Waislamu", Achana na tukio tu la Dodoma, Kuna haja ya waislamu kubomolewa Misikiti yao yote..
Khan,
Umeandika kwa hasira nyingi sana.
Ndipo ninapouliza hizi chuki nini sababu na chanzo cheke.

Historia ya udugu iliyowekwa na wazee wetu ni nani kaifuta?

WAISLAM WALIKUWA NA MAPENZI MAKUBWA NA BABA WA TAIFA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE

Hii ndiyo historia yetu ya mapenzi baina yetu. Baba wa Taifa yuko katikati ya Waislam waliomkaribisha Dar es Salaam 1952 wakamchagua kuwa kiongozi wa TAA 1953, 1954 wakaunda TANU Nyerere akiwa rais na 1955 wakamfungia safari ya UNO. Huu uadui na kuwanyanyapaa na kuwabagua Waislam nini chimbuko lake na imesababishwa na nini na nani muhusika? Kuna mtu anaeweza kutoa majibu?

1547697413953-png.996785


Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere akiwa kashikwa mkono na Mzee Mshume Kiyate kulia na kushoto kashikwa na Mzee Max Mbwana na Mwinjuma Mwinyikambi. Mwalimu Nyerere kazungukwa na Waislam. Udugu na mshikamano huu umepoteaje? Je, kulikuwa na watu waliokuwa hawafurahishwi na umoja huu? Ni nani hawa? Picha hii ni Uchaguzi Mkuu 1962.

Hawa akina mama wa Kiislam ndiyo walikuwa wanachama wa mwanzo wa TANU 1954. Kulia ni Bi. Tatu bint Mzee akifuatiwa na Bi. Titi Mohamed. Kushoto wa kwanza ni Bi. Chiku bint Said Kisusa (mke wa Shariff Attas) wakimsindikiza Mwalimu Nyerere Uwanja wa ndege safari ya kwanza UNO 1955.
Idd Faiz huyo hapo aliyevaa kanzu, koti na tarbush kulia kwa Nyerere akimsindikiza safari ya UNO 1955.

1547697514425-png.996788


1547697592314-png.996790



1547697743316-png.996791


Kushoto Idd Faiz Mafungo, Sheikh Mohamed Ramiya, Saadan Abdu
Kandoro na Haruna Taratibu, Dodoma 1955. Huyu Idd Faiz ndiye
aliyekuwa mkusanyaji fedha za safari ya Mwalimu Nyerere UNO 1955
ni huyo hapo chini kulia kwa Mwalimu Nyerere aliyevaa kanzu, koti na
tarbush.

1547744875055-png.997514

You always look smart,well educated but your religion and chauvinistic sense has clouded your judgement on many agenda! You were not supposed to issue a one side sad story while leaving the whole facts for the demolition of that Mosque in Dodoma.
Ungeweza kuchambua vema lakini umeacha kwa makusudi ili kuchochea ionekane waislam wanaonewa!
Unafanya dhambi mbaya sana! Ifta berat iyasanuul.
 
Pahamba,
Mimi najiuliza ni kitu gani kimepita kuweza kuwa na nguvu ya kuvunja umoja
uliojengwa na wazee wetu wakati wa kudai uhuru?

View attachment 996606

Hii ndiyo historia yetu ya mapenzi baina yetu. Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere
yuko katikati ya Waislam waliomkaribisha Dar es Salaam 1952 wakamchagua kuwa
kiongozi wa TAA 1953, 1954 wakaunda TANU Nyerere akiwa rais na 1955 wakamfungia
safari ya UNO. Huu uadui na kuwanyanyapaa na kuwabagua Waislam nini chimbuko lake
na imesababishwa na nini na nani muhusika? Kuna mtu anaeweza kutoa majibu?

View attachment 996610

Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere akiwa kashikwa mkono na
Mzee Mshume Kiyate kulia na kushoto kashikwa na Mzee Max
Mbwana na Mwinjuma Mwinyikambi. Mwalimu Nyerere kazungukwa
na Waislam. Udugu na mshikamano huu umepoteaje? Je, kulikuwa
na watu waliokuwa hawafurahishwi na umoja huu? Ni nani hawa?
Picha hii ni Uchaguzi Mkuu 1962.

View attachment 996616

Hawa akina mama wa Kiislam ndiyo walikuwa wanachama wa mwanzo wa TANU
1954. Kulia ni Bi. Tatu bint Mzee akifuatiwa na Bi. Titi Mohamed. Kushoto wa kwanza
ni Bi. Chiku bint Said Kisusa (mke wa Shariff Attas) wakimsindikiza Mwalimu Nyerere
Uwanja wa ndege safari ya kwanza UNO 1955..


View attachment 996618

Kulia Haruna Taratibu, Saadan Abdu Kandoro, Julius Kambarage Nyerere,
Sheikh Mohamed Ramia na Idd Faiz Mafungo Dodoma 1955. Idd Faizi ndiye
aliaminiwa na kukusanya fedha za safari ya Mwalimu Nyerere UNO.

View attachment 996620

Idd Faiz huyo hapo aliyevaa kanzu, koti na tarbush kulia kwa Nyerere akinsindikiza
safari ya UNO 1955.

Ndugu zanguni hivi nani katuvurugia historia hii?
Kuna mtu ana majibu ya maswali haya?
Makundi ya kigaidi kama alshabab ndio yamesababisha. Na wanachama wake wengi wanatoka misikitini. Kwahiyo nibora kuivuja wakose pa kukutania kupanga mipango yao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waislamu ni watu wa ajabu sana.

Mbona hamuelezi sababu ya kuvunjwa kwa huo msikiti.Mnajifanya kujua sana haki zenu na mara zote nyie ndiyo huonewa.

Hapo UDOM kuna makanisa yamejengwa??

The Book,
Haya ni mambo ya kuwekwa hadharani yakajadiliwa kuwa tumefikaje
hapa kuwa leo tuna tatizo kama hili?

Haya si mambo ya huyu anaandika hivi mwenzake anajibu vile.
Serikali iache kuogopa tatizo hili kwa kutegemea kuwa litajiondoa lenyewe.

Waulizwe Wakristo ni asilimia ngapi ya Waislam iwepo hapo UDOM na kwengine
ili ionekana hakuna udini?

Tukipata jibu la swali hili hapo ndipo tutaanzia kuondoa huu udini unaolalamikiwa
na Wakristo.

Sasa hivi UDOM Wakristo katika uongozi ni 88.6% na Waislam ni 11.4%.

Swali, hivi ndivyo UDOM inavyoondoa udini?
 
UDOM ni chuo cha serekali mabo ya misikiti au kanisa hayana nafasi.Eka 11 sehemu ya chuo zinatolewa kienyeji kwaajili ya msikiti ???????.Hivi UDOM ni mali ya BAKWATA au Serekali !.

Mimi nisingeshangaa ikiwa msikiti ungepewa kiwanja cha 20 kwa 40 lakini eka 11 duh hivi waTanzania nani kawaloga.KKKT ,Anglican na Catholic wakiomba eka 11kila mmoja Udom itakuwa uwanja wa dini na si chuo kikuu.Uongozi uliopita enzi za Kikwete ulielemea dini sana na haya ndio madhara yake.
 
The Book,
Haya ni mambo ya kuwekwa hadharani yakajadiliwa kuwa tumefikaje
hapa kuwa leo tuna tatizo kama hili?

Haya si mambo ya huyu anaandika hivi mwenzake anajibu vile.
Serikali iache kuogopa tatizo hili kwa kutegemea kuwa litajiondoa lenyewe.

Waulizwe Wakristo ni asilimia ngapi ya Waislam iwepo hapo UDOM na kwengine
ili ionekana hakuna udini?

Tukipata jibu la swali hili hapo ndipo tutaanzia kuondoa huu udini unaolalamikiwa
na Wakristo.

Sasa hivi UDOM Wakristo katika uongozi ni 88.6% na Waislam ni 11.4%.

Swali, hivi ndivyo UDOM inavyoondoa udini?


Kwahiyo wewe kazi yako ni kuanglia asilimia za uongozi kwa kigezo cha dini ?.
 
Mleta mada unawazungumziaje wakristo wanaopata adha, taabu na manyanyaso kutoka upande wenu hasa Zanzibar wakati wa mifungo yenu

Maana bandiko lako linaonyesha ni waislamu wanaonyanyasika kwa kuleta matukio ya 98 nk lkn tumeshuhudia waziwazi padri kapigwa risasi, kamwagiwa tindikali na wakristo wakipigwa hadharani wakipata chakula wakati wa mfungo lkn haya unajitia upofu

Sishabikii ubaguzi Ila jaribu kubalance story yako na siyo kutaka kuonyesha ni waislamu pekee wanaonewa nchi hii.
 
Neno unyanyasaji,inatakiwa ipewe maana yake halisi
Mfano
Zanzibar,imeweka sheria na kanuni zake kuwa,Haifai mtu kuonekanwa anakula mchana wa Ramadhan au kunywa
Kama kula au kunywa,Basi fanya ukiwa kwako au sehemu usioonekanwa na watu

Iwapo utavunja sheria hii
Ukahukumiwa,Basi hapa hatusemi kuwa umenyanyaswa
Bali tutasema,Sheria imefuata Mkondo wake

Lkn
Kama Sheria hakuna,kisha ukakatazwa au kupigwa au kubezwa na mfano wake,
Hapa maana halisi ya unyanyasaji,itapata hadhi ya kusemwa na kuchukuliwa
Mleta mada unawazungumziaje wakristo wanaopata adha, taabu na manyanyaso kutoka upande wenu hasa Zanzibar wakati wa mifungo yenu

Maana bandiko lako linaonyesha ni waislamu wanaonyanyasika kwa kuleta matukio ya 98 nk lkn tumeshuhudia waziwazi padri kapigwa risasi, kamwagiwa tindikali na wakristo wakipigwa hadharani wakipata chakula wakati wa mfungo lkn haya unajitia upofu

Sishabikii ubaguzi Ila jaribu kubalance story yako na siyo kutaka kuonyesha ni waislamu pekee wanaonewa nchi hii.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ama jambo la kupigwa Risasi kwa Padri
na raia tu,
Hili Uislam unakemea vikali,na hata Sheria zetu za nchi,inakemea vikali

Aliefanya kitendo hicho cha kikatili,lazima atafutwe na Sheria ifuate mkondo wake

Hakuna anaependa Dhulma ikiwa mtu ana akili timamu
Mleta mada unawazungumziaje wakristo wanaopata adha, taabu na manyanyaso kutoka upande wenu hasa Zanzibar wakati wa mifungo yenu

Maana bandiko lako linaonyesha ni waislamu wanaonyanyasika kwa kuleta matukio ya 98 nk lkn tumeshuhudia waziwazi padri kapigwa risasi, kamwagiwa tindikali na wakristo wakipigwa hadharani wakipata chakula wakati wa mfungo lkn haya unajitia upofu

Sishabikii ubaguzi Ila jaribu kubalance story yako na siyo kutaka kuonyesha ni waislamu pekee wanaonewa nchi hii.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kisha
Tuwe waadilifu katika maandishi yetu
Je!Kwa hapo Znz,ni Wakristo tu ndio wanakatazwa kula mchana wa Ramadhaan au hata Waislam wenyewe?!

Na
hao wanaopigwa na kushitakiwa,ni Wakristo tu au hata Waislam?!!

Nitasubiri majibu yako katika Hili Chief

Barikiwa sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Neno unyanyasaji,inatakiwa ipewe maana yake halisi
Mfano
Zanzibar,imeweka sheria na kanuni zake kuwa,Haifai mtu kuonekanwa anakula mchana wa Ramadhan au kunywa
Kama kula au kunywa,Basi fanya ukiwa kwako au sehemu usioonekanwa na watu

Iwapo utavunja sheria hii
Ukahukumiwa,Basi hapa hatusemi kuwa umenyanyaswa
Bali tutasema,Sheria imefuata Mkondo wake

Lkn
Kama Sheria hakuna,kisha ukakatazwa au kupigwa au kubezwa na mfano wake,
Hapa maana halisi ya unyanyasaji,itapata hadhi ya kusemwa na kuchukuliwa

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa hiyo hiyo sheria imetoa uhalali wa mtu yeyote kumuadhibu atendaye hilo kosa acha habari zako wewe Kwa hiyo wewe moyoni mwako huwa unafarijika sana ukiona wenzako wanavyomharass kwa kumpiga in the name of sheria na kanuni mkristo anapopata chakula

Mbona ya padri kapigwa risasi na kamwagiwa tindikali hujajibu au nayo ni kanuni na sheria huko Zanzibar?
 
Soma nilichokiandika vzr

Sheria inahukumu Muislam na asie kuwa Muislam
Ama raia kuchukua Sheria mkononi na kuamua kuadhibu,hili halihalalishi kosa lake!!!

Bali atakuwa mtuhumiwa namba moja kwa kukosea Sheria

Kwa ufupi tu
Usihukumu watu kwa matendo ya baadhi,kwa nia zao chafu
Shukran Chief
Kwa hiyo hiyo sheria imetoa uhalali wa mtu yeyote kumuadhibu atendaye hilo kosa acha habari zako wewe Kwa hiyo wewe moyoni mwako huwa unafarijika sana ukiona wenzako wanavyomharass kwa kumpiga in the name of sheria na kanuni mkristo anapopata chakula

Mbona ya padri kapigwa risasi na kamwagiwa tindikali hujajibu au nayo ni kanuni na sheria huko Zanzibar?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
The Book,
Haya ni mambo ya kuwekwa hadharani yakajadiliwa kuwa tumefikaje
hapa kuwa leo tuna tatizo kama hili?

Haya si mambo ya huyu anaandika hivi mwenzake anajibu vile.
Serikali iache kuogopa tatizo hili kwa kutegemea kuwa litajiondoa lenyewe.

Waulizwe Wakristo ni asilimia ngapi ya Waislam iwepo hapo UDOM na kwengine
ili ionekana hakuna udini?

Tukipata jibu la swali hili hapo ndipo tutaanzia kuondoa huu udini unaolalamikiwa
na Wakristo.

Sasa hivi UDOM Wakristo katika uongozi ni 88.6% na Waislam ni 11.4%.

Swali, hivi ndivyo UDOM inavyoondoa udini?
Kwani wanaajiri kwa vigezo gani?
 
Nimeishi Uingereza kwenye mji mmoja unaitwa Cardiff ambao ni mji mdogo ulioko Wales na kwa kawaida kwa Waingereza watu wa Wales wanadharaulika wanaonekana washamba.

Neil Kinnock alipata kugombea kutaka kuwa Waziri Mkuu wa Uingereza na yeye ni Mwelshi.

Siku moja kaingia mwalimu wetu mmoja yeye ni kutoka England anaitwa Brown Thomas akamsema kwa ubaya sana Kinnock, ‘’Ati na huyu nae anataka kuwa Waziri Mkuu wa Uingereza. Nani atampigia kura Mwelish?’’

Kwa sababu hii na dharau hii mimi nilipokwenda kupiga kura nilimpigia Neil Kinnock wa Labour Party lakini hakushinda aliyeshinda alikuwa John Major wa Conservative.

Najua msomaji wangu unashangaa vipi huyu mtu kutoka Kariakoo apige kura Uingereza?

Naam nimepiga kura. Uingereza sheria yao ni kuwa ukiwa ni mlipaji kodi haijaslishi kama ni mwananchi au mgeni unaweza kupiga kura.

Mbunge wangu mgombea alinifata nyumbani kwangu Column Road kwa adabu zote kuomba kura yangu.

Msikiti wa mtaani kwangu ni jengo ambalo hapo zamani lilikuwa kanisa lakini kwa kuwa watu walikuwa hawaendi kuabudu Wakristo wa sehemu ile wakaamua kuliweka gazetini kutangaza kuuza kanisa lao.

Hapo wakatokea Waislam wakalinunua kanisa lile na kuligeuza kuwa msikiti.

Hivi ndivyo ilivyotokea kwa msikiti huu Darul Isra kuwa katikati ya makazi ambayo wengi wa wakazi ni Wakristo.

Kwa muda wote nilioishi eneo lile sikupata kuhisi uadui wowote kutoka kwa hawa Waingereza kuwa walikuwa na chuki na msikiti ule.

Tatizo lilikuwa moja tu.

Barabara ya kuingia msikitini ilikuwa inakataza kuegesha magari kwa sababu ya ufinyu wa barabara.

Siku ya Ijumaa wanafunzi wengi wanakuja msikitini kwa ajili ya sala ya Ijumaa na baadhi yao ni vijana wanafunzi kutoka ncbi za Kiarabu ni wanafunzi lakini wana magari mazuri tu na lazima waje na magari yao na watayaegesha hapa mtaani na trafiki watakuja na kuweka tiketi.

Hawajali fedha wanazo wanalipa faini.

Ikatokea baada ya kurudi Tanzania nilirudi tena Cardiff nikitokea London na nikaenda Darul Isra msikitini kwangu kwa zaamani.

Safari hii nikapewa habari nyingine ya kufurahisha kuwa msikiti ule umenunua kanisa lingine na kuna mpango wa kulikarabati kuligeuza msikiti lakini kwa wakati ule lile kanisa wakilitumia kama bohari ya kuwekea vitu.

Nimekwenda Tilbury Port huu ni mji nje ya London na ni bandari.

Siku za nyuma bandari hii ilikuwa na biashara kubwa lakini wakati wa Magret Thatcher uchumi ulibadilika na bandari hii ikapoteza umuhimu wake.

Wengi wa wakazi wa mji ule mdogo walikuwa wafanyakazi wa bandari na baada ya bandari kukosa biashara na kazi kuwa haba wafanyakazi wengi walipoteza ajira kwa hiyo wakahama mji.

Niliingia Tilbury mchana kwa treni.

Nilipata mshtuko mkubwa sana.

Mji mzima hakuna mtu anaeonekana barabarani wala gari kupita.

Maduka ya mtaa mzima mkubwa wenyewe wanaita ‘’High Street,’’ yamefungwa lakini matangazo yapo yakitangaza biashara tofauti.

Unatembea barabarani unasikia sauti ya kiatu chako kinapogonga lami ya barabara.
Tilbury ni ‘’ghost town,’’ mji uliohamwa na katika masiaha yangu yote sijapatapo kuona kitu kama hiki.

Inabidi wenyeji waliobakia wakuelekeze mahali ambapo unaweza kwenda kula chakula sehemu inaitwa Stella Maris, hii ni mfano wa huku kwetu wa Mission to Seaman sehemu ambayo zimewekwa maalum kwa kuwahudumia mabaharia kwa malazi na chakula.

Eid Kubwa imenikuta katika mji huu na hakuna msikiti lakini nimefahamishwa kuwa Waislam wapo ingawa hawana msikiti.

Wenyeji wakanieleza kuwa katikati ya mji kuna shule ya msingi ambayo hapo ndiyo Sala ya Eid huswaliwa ndani ya darasa.

Hapo ndipo niliposwali Sala ya Eid na wengi wa Waislam walikuwa Wahindi.

Miaka mingi ikapita siku moja nikajikuta niko Maryland, Washington DC Amerika na Ijumaa imefika.
Mwenyeji wangu Dr. Harith Ghassany akanichukua twende kusali.

Haikunipitikia kuwa sehemu ile hakuna msikiti na hivyo ndivyo ilivyokuwa.
Hapakuwa na msikiti.

Dr. Ghassany alinichukua John Hopkins University na tuliswali ndani ya moja ya madarasa ya chuo hicho.

Tanzania nchi ambayo Waislam ni umma mkubwa kuna chuki dhidi ya Uislam kupelekea kuvunjwa misikiti...

Swali la kujiuliza ni nchi yetu nani kaifikisha hapa?
Nini chanzo cha uadui huu?
kuna kitu cha kujifunza hapo..
 
Na baada ya ulaya yote kuwa Islamic continent nchi zote za huko zitakuwa shithole kama nchi za kiislam za sasa. Sas a sijui baada ya hapo mtakimbilia wapi! China?Japan au Korea? Uzuri waislam wakiwa majority kwenye nchi lazima hiyo nchi iwe na kila aina ya uonevu hadi wenyewe mnakimbia!

Kama ipo nchi duniani ya kiislam yenye kitenda haki sawa kwa watu wake bila ubaguzi wowote nitajie. Na mm nitakutajia mbili za makafir!
Sio kweli mimi hivi sasa naandika message niko Muscat, Oman hamna shida yoyote wakristo wapo na wana makanisa yao wanatekeleza ibada zao bila ya shida yoyote
Huku huwa tunapumzika ijumaa na jumamosi jumapili tunapiga mzigo kama kawa hivyo kama wewe ni mkristo unataka kwenda kanisani jumapili una option aidha unaomba kutokuja kabisa au unachelewa kuja ukipitia kanisani kwanza na kazi zinaenda vzuri
Yaani katika public life hakuna kitu kinaweza kukufanya ujisikie kubaguliwa labda uwe na inferiority complex uwe mtu wa kujishtukia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom