Siasa za Tanzania, Shilingi ya Tanzania na Maisha ya Watanzania

Siasa za Tanzania, Shilingi ya Tanzania na Maisha ya Watanzania

Habari wana JF

Nimejaribu kufuatilia kwa undani sana suala la shilingi ya Tanzania ukilinganisha na dollar pendwa ya Kimarekani ,kwanza tumsikilize huyu kiongozi kuhusu shilingi ya Unguja.

View attachment 2210979

Kama umsikia kwa Umakini kipindi hicho Shilingi 1 ilikuwa na thamani sana kulinganisha na Sasa, Lakini pia Ukipitia WORLD DATA ATLAS utagundua kwama miaka ya 1971 utagundua Shilingi zetu 7.1 ilikuwa sawa na dollar 1 ya kimarekani tofauti na sasa ambapo hiyo dollar 1 tunainunua kwa zaidi ya shilingi 2200.

Nimejiuliza sana kwanini imepanda kwa kasi kubwa hivyo Nikagundua Sababu kubwa ni kwamba HATUUZI NJE ,nikajiuliza tena ina maana hatuna vitu tunavyoweza uza Nje? Nikagundua pia tunavyo vingi mno.

Nikawaza pia sababu ni nini? Ni CCM au Watanzania wote nikabaki sina jibu

Hivi Wana JF Tanzania hatuweza jenga viwanda vya kutengeneza Nguo ,watu wakalima Pamba wakainua maisha yao Tukauza Nguo Nje?

Hivi wana JF Tanzania hatuwezi kusomesha watu na kujenga viwanda tukaprocess madini tuliyonayo tukauza vitu vitokanavyo na madini nje?

Hivi wana JF Tanzania hatuwezi imarisha Sekta ya Uvuvi kwa kununua vifaa vya Kisasa na kuwa muuzaji Mkubwa wa Samaki Nje?

Hivi Tanzania Hatuwezi jenga Viwanda vya Sukari ,na wananchi wetu wakalima miwa wakauza wakainua maisha yao na tukauza sukari Nje?

Hivi Tanzania hatuwezi jenga viwanda vya kusindika, watu wakalima mazao tukauza vyakula kwenye makopo

Hivi Tanzania hatuwezi jenga miundombinu mizuri, tukachimba tukauza Gesi Nje?

Hivi Tanzania Hatuwezi kuwa Muuzaji mkubwa wa umeme Africa Mashariki na kati kwa kutumia Gesi Tuliyonayo ,mito na bahari?

Hivi Tanzania hatuwezi jenga Bandari Kubwa sana tukawa wapokeaji mizigo wakubwa kwa Nchi zote zinazo tuzunguka?

Mwisho kabisa hivi hawa viongozi wetu huwa Tunawatoa wapi wanaopiga makofi hata kwenye hamna ,wananchi wanakufa kwa kukosa matibabu kwenye nchi yenye kila kitu? Kwanini Watanzania tuishi maisha magumu kwenye nchi yenye kila kitu?

Mi nadhani kuna haja ya kuwa na katiba ambayo mtu akiteuliwa ana akichaguliwa kuwa kiongozi anawaza mara mbili mara tatu ndio anakubali na hapa sio suala la kulaumu CCM kwa kuwepo kipindi chote hicho ila hao viongozi huwa tuna wachagua wenyewe.
Ndugu ukishaanza kusema hivi Tanzania hatuwezi kujenga sijui kununua tayari umeshafeli na ndio sababu mojawapo iliyotufikisha hapa kwa kukosa watu wenye maarifa..

Serikali haiwezi kufanya biashara ndugu,ukitaka watu waliokariri makaratasi wafanye biashara utaishia kupata hasara , nadhani tuna mifano mingi ila wa hivi karibuni ni korosho zilivyoharibiwa soko kwa serikali kujifanya wananunua na kupeleka malori ya Jeshi..

Jambo la muhimu ni kujenga mazingira wezeshi kama barabara,umeme na maji,taasisi wezeshi za serikali sio udhibiti tuu,kuacha urasimu na mlundikano wa Kodi lukuki na mwisho kuwa na malengo specific na yanayopimika na rasilimali zielekezwe huko sio kufanya mambo kiujumla jumla Bora liende.
 
Kama Nyerere na uzalendo wake wote ule alishindwa! Basi hakuna mwingine atakayeweza!

Labda atokee Nyerere mwingine (Nyerere Junior) mwenye maono na akili mara mbili ya zile za Nyerere Senior, hakika mambo yatakuwa bam bam.
Uzalendo mbuzi na kutumia rasilimali watu na mali eti kukomboa wengine badala ya kuwekeza kwenye elimu ya watu wake..

Huyo uliyemtaja na sera zake za kijamaa ni moja ya waliochangia kukuza ujinga na kuifanya jamii kusubiria serikali Kwa kila kitu na kulalamika.
 
Hivi JPM mtu mwinyi akili timamu narudia tena MWENYE AKILI TIMAMU unaweza kusema alikuwa KIONGOZI BORA labda alikuwa bora kwa UONGO na kuwafanya WATANZANIA walio kuwa na akili ya chini kumuamini hadi na badhi ya wanao jifanya wasomi NJAA kumsupport UONGO wake.

Mtu kaanzisha miradi mikubwa kwa pomoja na kudanya inajengwa kwa fedha za ndani ili hali ni uongo mtupu hadi anakufa hakuna mradi wowote umefika asilimia hata 50%
Kuna msemo unasema sn UONGO UKISEMWA SANA UBADILIKA KUWA UKWELI na hili JPM alifanikiwa sn.
Binafsi nilishasema moja ya Rais wa hovyo tuliowahi kumpata ni huyo mnaemuita JPM..

Sio tuu kwamba hakutekeleza hiyo miradi hata 50% bali mingi ya hiyo miradi ni useless na liability kwa Nchi..
 
Hivi JPM mtu mwinyi akili timamu narudia tena MWENYE AKILI TIMAMU unaweza kusema alikuwa KIONGOZI BORA labda alikuwa bora kwa UONGO na kuwafanya WATANZANIA walio kuwa na akili ya chini kumuamini hadi na badhi ya wanao jifanya wasomi NJAA kumsupport UONGO wake.

Mtu kaanzisha miradi mikubwa kwa pomoja na kudanya inajengwa kwa fedha za ndani ili hali ni uongo mtupu hadi anakufa hakuna mradi wowote umefika asilimia hata 50%
Kuna msemo unasema sn UONGO UKISEMWA SANA UBADILIKA KUWA UKWELI na hili JPM alifanikiwa sn.
Mpe Pongezi Kuna Mazuri Yake Pia Hao Wanaosema JPM muongo hata Wao Ni Waongo .

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Uzalendo mbuzi na kutumia rasilimali watu na mali eti kukomboa wengine badala ya kuwekeza kwenye elimu ya watu wake..

Huyo uliyemtaja na sera zake za kijamaa ni moja ya waliochangia kukuza ujinga na kuifanya jamii kusubiria serikali Kwa kila kitu na kulalamika.
Mwalimu aachwe
 
Tusiogope kukopa panapo hitajika
 
Shillingi 1 ya kenya ni sawa na 20.5tsh mwananchi wa chini akiwa na15ksh ambayo ni sawa na 300tsh anauwezo wa kupata kikombe cha chai na makande maisha yakasogea,kwa upande wa bongo hali ni tofauti...
Kenya wake mbele na serious kuliko kwetu
 
Back
Top Bottom