Siasa za visasi: Rwanda yapandisha ushuru kwa magari ya mizigo yanayotokea Tanzania

Siasa za visasi: Rwanda yapandisha ushuru kwa magari ya mizigo yanayotokea Tanzania

Status
Not open for further replies.
Kwa hili haongezi gharama kwa watu wake ila faida kwa mwenye gari inapungua au inaondoka kabisa. Lengo lake ni kulazimisha waagizaji mizigo watumie bandari ya Mombasa badala ya Dar es Salaam. Watapata msukosuko kwa muda tu then wakianza kupitia Mombasa mambo yatatulia.

Ina maana gani kwetu? Tuboreshe reli ya kati. Hao wenye malori ndio walikuwa wanahujumu reli ya kati isifanye kazi au isiboreshwe. Tena wengi wao ni wakubwa haohao.
Kwani wenye magari watakuwa wapumbavu kiasi hiko na wao ongezeko la gharama si wanawatupia wenye mizigo, hawataki mizigo inadoda bandarini na gharama za kuifadhi juu; mpaka inabaki kuwa mali ya serikali ya Tanzania.

Hapa serikali irudishe compliments tu na magari yatakayo toka Rwanda yapate same treatment for now at least we should gain whilst they are still reinforcing their strategy of diverting their cargo to Mombasa.
 
Rwanda itaumia kwa hilo, chaji hiyo itaingia katika upande wa mtumiaji tu. Pia sisi tujibu kwa kupunguza zaidi kwa magari ya Congo na Burundi, na Bure kabisa kwa magari ya Sudan S.
 
kikwete alivyokua anaongea dharau mlichekelea.
mnazani vita ni kushikiana mtutu pekee???
warwanda wajinga hapa umeongea nini sasa kwani biashara lazima tufanye na rwanda hata sisi tunajua tutakaza wapi.
Kikubwa msije kulia baadaye.
 
warwanda wajinga hapa umeongea nini sasa kwani biashara lazima tufanye na rwanda hata sisi tunajua tutakaza wapi.
Kikubwa msije kulia baadaye.

watz wenye akili timamu wamekiri kuwa kikwete analiponza taifa.
 
Taarifa yako haijakamilika. Haujasema kuwa magari ya rwanda yanayoingia tanzania yamekuwa yakitozwa hiyo dola 500 for many years. Wamejaribu ku plead serikali yenu ipunguze ili hiyo gharama iendane na za nchi nyingine wanachama wa East Africa. Tanzania walikuwa wanajishebedua.
This is "news" to me! Kumbe haya malalamiko yetu hayana msingi wowote kata hali ni hii unayoisema!
 
hilo sio tatizo kwani ni kuongeza gharama za mtumiaji wa mwisho nchini rwanda, unless kama anafanya hivyo kudiscourage matumizi ya transporters wa tanzania which is a wrong tactic and can not give good results to him
 
Siyo lazima kufanya biashara na rwanda.
Wajue hilo ni kaburi ambalo wanajichimbia wenyewe watajizika wenyewe.
 
This is "news" to me! Kumbe haya malalamiko yetu hayana msingi wowote kata hali ni hii unayoisema!

Mkuu, mkiona Kagame anapiga kelele ni amejaribu sana kuwa accomodating ila kuna mahali inafika mtu unashindwa kuvumilia. Tanzania inabidi mjirekebishe katika karne hii ya utandawazi na ushindani.
 
watakaoumia ni wanyarwanda wenyewe,kwani ninachojua hakuna mfanyabiashara anayepata hasara hata siku moja! Hivyo kama bidhaa kama zinapelekwa rwanda bei ya bidhaa zitapanda tu!

umenena vyema! Watakaoumia na wanyarwanda!

Sent from my blackberry 9780 using jamiiforums

wakuu lengo la rwanda hapo ni kuwa lazimisha wafanyabiashara wao wapitie mombasa, na kama hii ikishindwa tutegemee vikwazo zaidi, vita ni vita iwe ya maneno, matendo au uchumi
 
watz wenye akili timamu wamekiri kuwa kikwete analiponza taifa.
tatizo we mwehu kwa tarifa yenu tulishafika mwisho wewe na warwanda wenzako tumewachoka mlizoea kufanya uharifu kagera na kwingineko tumewatimua kwendeni.
 
Wana Jamiii

Nipo hapa Rusumo mpakani mwa Tanzania na Rwanda.....siamini ninachokiona machoni mwangu....kuanzia jana tarehe 1/09/2013 serekali ya Rwanda imeongeza ushuru wa barabara ( ROAD TOLL) kwa magari yote ya Mizigo ( Fuel and Dry Cargo) yenye plate numbers za Tanzania kutoka USD 152 mpaka USD 500 kwa kila gari.

Kwa taarifa ambazo sio rasmi kwa siku magari ya mizigo takribani 300 yanavuka hapa mpakani, na zaidi ya asilimia 95% ya magari hayo zina plate numbers za Tanzania.

Wanajamii hii ina madhara gani kwa uchumi wa Tanzania kwani akili ya harakaharaka hii ni some sort of Protectionism ila kwa mbali inaweza ikawa ni muendelezo wa chokochoko.

Kwani hiyo inakula kwa msafirishaji au mwenye mzigo....? Hiyo yote inamuongezea gharama mwenye mzigo......anachofanya mwenye gari ni kuongeza gharama ya kukodi gari kwa kiasi tajwa au zaidi...! Wakati huo huo Waziri wa Fedha wa TZ atapata nafasi ya kupitia upya tozo la gari za IT zinazoelekea Rwanda na pia gari za mizigo zenye namba za usajili za Rwanda ili kuongeza tozo
 
wakuu lengo la rwanda hapo ni kuwa lazimisha wafanyabiashara wao wapitie mombasa, na kama hii ikishindwa tutegemee vikwazo zaidi, vita ni vita iwe ya maneno, matendo au uchumi
mkuu liwalo na liwe tujipange kivyetu na sadcc yetu kuwa rafiki na viinchi vya kisilani na ukabila ni poteza mda tu.
 
Mkuu, mkiona Kagame anapiga kelele ni amejaribu sana kuwa accomodating ila kuna mahali inafika mtu unashindwa kuvumilia. Tanzania inabidi mjirekebishe katika karne hii ya utandawazi na ushindani.

Kagame kwenu amekuwa kama ka-mungu kadogo.....! Badala hata kutaja nchi yako unahangaika na jina la Kagame kila kukicha...!
 
Mkuu, nakushukuru sana hapo kwenye RED. Nimepiga sana kelele kuhusu hilo hata kabla ya ugomvi kati ya JK na PK. labda hii itakuwa " a blessing in disguise" Hao wakubwa ndio wenye malori hayo jamani. Kuna wakati bwana mkubwa aliingiza malori 50 na hakulipa ushuru. Mbona yatafumuka mengi.

Sibonike,

Kiongozi ni kweli kabisa.Na ukweli huu Rais Kagame anaujua na anajua ni jinsi gani kuna uozo katika utawala bora hapa kwetu. Yatafumuka mengi sana. Haingii akilini kwa Rais Kagame kukasirishwa na "ushauri" wa Rais Kikwete. Kilichomuudhi kwanza ni ule wepesi ambao mheshimiwa sana Rais Kikwete aliupa ushauri wa kukutana na FDLR ambao wameapa kuiangusha serikali ya Rais Kagame. Vile vile mjiulize hizo silaha wanazotumia makundi yote ya "waasi" mashariki mwa DR Congo zinapitia wapi? Ni nani wafanyabiashara wakubwa wa hizo silaha hapa Afrika Mashariki? Na kwa nini washambuliwe M23 tu na sio makundi mengine 17 huko Eastern DRC? Maswali ni mengi.
 
Watakaoumia ni wanyarwanda wenyewe,kwani ninachojua hakuna mfanyabiashara anayepata hasara hata siku moja! hivyo kama bidhaa kama zinapelekwa Rwanda bei ya bidhaa zitapanda tu!

Hapo umenena
 
Kwa hili haongezi gharama kwa watu wake ila faida kwa mwenye gari inapungua au inaondoka kabisa. Lengo lake ni kulazimisha waagizaji mizigo watumie bandari ya Mombasa badala ya Dar es Salaam. Watapata msukosuko kwa muda tu then wakianza kupitia Mombasa mambo yatatulia.

Ina maana gani kwetu? Tuboreshe reli ya kati. Hao wenye malori ndio walikuwa wanahujumu reli ya kati isifanye kazi au isiboreshwe. Tena wengi wao ni wakubwa haohao.
au ndio keshawajua huku wengi tukiwa tumelala bado?
 
Mbona zipo option nyingi. Malori yanaweza kushushia mzigo hapo mpakani wakachukua kwa lori za Rwanda bila kulipia extra road toll.

All in all gharama za biashara zinaongezeka kwa wanyarwanda zaidi kuliko kwa watanzania.
 
Mbona zipo option nyingi. Malori yanaweza kushushia mzigo hapo mpakani wakachukua kwa lori za Rwanda bila kulipia extra road toll.

All in all gharama za biashara zinaongezeka kwa wanyarwanda zaidi kuliko kwa watanzania.


Tatizo litakuwa ni document utakazokuwa nazo zinaonesha huo mzigo umeshukia Tanzania,hakuna namna ya kukwepa hiyo tozo ya barabara.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom