Sidanganyiki - Leo ndio mnajua Tanzania inahitaji katiba mpya?

Sidanganyiki - Leo ndio mnajua Tanzania inahitaji katiba mpya?

katiba mpya Tanzania haikuanza kuzungumzwa leo. Mkapa hajalikalia kimya enzi zake kama mwanakijiji anavyotaka ieleweke.

Katiba mpya imezungumzwa sana na karibu vyama vyote, kwa miaka kadhaa.

Msilete uzishi.
 
MMM

Madai yalikuwapo tokea enzi, ila binafsi nadhani kwa sasa wale hypocrites wamepewa go ahead na kiongo wao na chama chao kudai hivyo ili kudivert attention ya watanzania kama ilivyo ada... sie ni wadanganyika, tumeshasau wizi wa kura, hali ngumu ya maisha, ufisadi, bajeti shenzi kwenda kwa GBS supporters na unafiki wao walioita wapinzani kokoto

TO ME HII VIGOR YA KATIBA MPYA INAPEWA PROMO ZAIDI NA WADANDIA HOJA WA KILA SIKU (CCM)

sababu kubwa ya pili ni kwamba the wind of change has blown and any resistance will just lead to ones peril (including hao wenye vyao kwa sasa)

Salamu wakuu,
Mimi nadhani hii mada ni muafaka sana kwa wakati huu kwa vile kuna hatari kubwa ya hii hoja kuwa "hijacked" na "Wadandia hoja" i.e CCM. Sababu ni kuwa hivi sasa baada ya CDM kujinadi kwa ahadi ya kuanzisha mchakato wa kuandika katiba mpya na wananchi kuwaunga mkono kwa kiasi kikubwa kuliko watawala walivyotarajia wameona kuwa public opinion iko in favour of these changes.So kinachotokea ni kujaribu kuiba hoja hii ya CDM ili kuwa preempt,Lakini pia tofauti na CDM ambayo ilitaka kuoverhaul the Constitution,hawa wasanii wanataka kumanage hii process ili kufanya patch up job kwenye katiba ambayo itaendelea kulinda na kustawisha maslahi na uimla wa kiutawala kwa CCM and cronies wake.Na hapa ndipo ninapoona hatari kubwa sana.Kwamba hawa watu watajipa jukumu la kusimamia huu mchakato kiusanii kama walivyofanya kwa masuala mengine makubwa na nyeti kwa taifa.Matokeo yake ni kutulazimisha kukubali a watered down version ya katiba mpya isiyo na mabadiliko ya msingi na hivyo kutokuwa na tija.
Na hapa ndipo CDM na wapenda mabadiliko wote,ndani na nje,tunapotakiwa kuwa vigilant na kushinikiza meaningful involment and participation ya broader section ya public ili kuzuia hii charade ya CCM na cronies wake.


"True freedom must be expressed through the human ability to think critically, to analyze and to make informed decisions about oneself, his society and the world "- Sidanganyiki2010
 
Mwanakijiji nimekupata..

nami hii kasi ya kudai katiba MPYA, has kutoka kwa viongozi wa zamani waandamizi wa CCM na serikali yao ndo inanishangazaa zaidii. leo balozi mstaafu, brigedia Hashim Mbita kupitia gazeti la mwananchi (10/12/2010) anadai katiba MPYA!!!. Kanishangaza kwamba msukumo wake ni kwamba katiba ya sasa inawapa wahisani NGUVU ya kutupangia nn cha kufanya na kutokufanya..shame on him! huu ni unafiki kwani hii sababu aliyoitoa sio chanzo cha kudai katiba MPYA...Ila ndo hivyo naye ameingia kwenye kundi la walilia KATIBA MPYA 2010..

Kinachowasukuma wengi kutoka ndani ya CCM viongozi wa waastafu ni majerahaa ya uchaguzi 2005-2010,2010 -2015. makundi yamewafikisha hapo na sasa kunyoosheana kidolee kwa masilahi binafsi zaidi kupitia hoja za umma.
 
Acheni wenye sauti waongee. Sote tunaona KATIBA ya sasa inavyotutenda. Na Mwalimu au mtu wa hadhi na heshima yake hatuna. Mzee Mbita na Prof Mpangala jana pale TBC1 walijitahidi kueleza kwa nini tunahitaji KATIBA MPYA. Tena tusipoteze muda kuunda Bunge au Mahakama ya KATIBA. Kenya wameandika vizuri sana KATIBA yao kwa sehemu kubwa. Sio vibaya tukiitumia ile kwa kuondoa yale ambayo yamekaa KiKenya na kuingiza ya KiTanzania
 
Kwenye msafara wa mamba na kenge wapo,hatutegemei kila Kiongozi anayeongelea sasa hivi katiba mpya anamaanisha ile wanayotaka wananchi kama mchakato wa kupata maoni utaanza ndio hapo tutakapojionea nani ni kweli alimaanisha Katiba ya maslahi ya Taifa na nani alitaka Katiba ya kulijali kundi fulani.Hizi tunazozisikia sasa ndo wale 70% aliyosema Kikwete...fuata upepo.
 
Swala la katiba limeonekana kitambo sana. Sababu za wana ccM kudai katiba ni kuchafua akili za watu wahame kwenye msitari. Tusipokua macho ajenda itavutwa hadi uchaguzi 2015. Wanafuata upepo na najua wanatafuta trick ya kutokea ili warudi kwenye chart
 
kwanini sasa hivi tunahitaji sana "katiba Mpya"? nini kimetokea ambacho hao wanaodai Katiba Mpya hawataki kukisema. Kwa sababu as a matter of fact yote wanayoyasema yalikuwa kweli kwa miaka mitano iliyopita; why now?

NAFIKIRI THE PUSH COMES FROM CHADEMA MP'S WALK OUT AMONG OTHER THINGS:angry::angry:
 
Mambo mengine yanashangaza sana; leo kila mmoja wa watu mashuhuri anatafuta gia ya "kutokea"; mwisho Rais na wajumbe wa Kamati Kuu nao watakuja na kusema "wanataka Katiba Mpya". Nimekaa naangalia wanaojitokeza kudai katiba mpya na wanaripotiwa huku wakibeba ujiko wa ofisi na vyeo vyao; ati kuanzia Mkapa na sasa Jaji Mkuu na wote wengine katikati yao ati wote sasa "wanataka Katiba Mpya"! Really? Why?

Ati leo viongozi wa dini nao wanajitokeza na kudai Katiba Mpya! Mwisho wataanza kuja na wabunge wa CCM wakidai Katiba Mpya! Utani mwingine jamani!

Katiba Mpya? Kwani hii iliyopo imegunduliwa ina matatizo gani ambayo hawakuyaona miaka 20 iliyopita? Kwamba mwaka 2010 ndio wamegundua kuwa Katiba ina matatizo? Naam, watasema imejulikana kuanzia 1992. Watasema kuwa miaka yote hii kumekuwa na "kilio" cha Katiba Mpya na wengine watatuambia jinsi walivyojaribu kuzungumzia hili miaka yote hii wakituambia juu ya Ripoti ya Nyalali n.k

Lakini miaka yote hiyo hawakujitokeza hawa kwa nguvu hivi kudai "katiba mpya". Lakini cha kuudhi na ambacho naamini ni cha uzugaji uliokubuhu ni kuwa wote hawa hawakuwa na ujasiri wa kudai Katiba Mpya kabla ya uchaguzi. Tangu 2005 hadi ulipofika uchaguzi huu wengi tumeandika na wengine wamelalamikia matatizo mbalimbali. Suala la ubovu wa tume ya uchaguzi halikuibuliwa kwenye uchaguzi wa 2010; wengine tulishabeza wapinzani kwenda kwenye uchaguzi huu uliopita wakiwa na tume ile ile na mfumo ule ule na tukasema mapema wasije kulalamika "tume ya uchaguzi, tume ya uchaguzi". Tulisema wamekubali kucheza kwa kanuni za mchezo na refa ambaye tayari alishajionesha kuwa ana upendeleo akiwavuruga wasilalamike. Sijui walisahau wapi yaliyotokea Kiteto? Walisahau vipi yaliyotokea Tunduru?

Lakini sasa siyo wapinzani tu hata viongozi wengine wa serikali na hata wa CCM wanaanza kudai Katiba Mpya. Kilichonishangaza ni kuwa Rais Mkapa anadai naye Katiba Mpya! Really? I mean Really? Alikuwa Rais kwa miaka 10; alisimamia mabadiliko ya Katiba ya 2005 - lakini hakutaka Katiba mpya then?

Lakini wote hawa wanaojitokeza kudai Katiba Mpya hawataki kusema kitu kilichowazi; Hawataki kusema hasa kwanini sasa baada ya uchaguzi wamepata ujasiri wa kudai Katiba Mpya. Walijua sheria ya uchaguzi, walijua mfumo wa tume ya uchaguzi; walijua malalamiko ya Katiba mpya lakini kwa miaka karibu ishirini walikaa kimya. Lakini sasa kuna kitu kimetokea; kitu ambacho hawana ujasiri wa kukisema au kukiita kwa jina lake.

Hoja ya kuandika upya katiba haiwezi kunogeshwa kwa kutokuwa tayari kuita ukweli kwa jina lake. Ni nini kilitokea baada ya uchaguzi; au swali sahihi zaidi ni nini kilitokea wakati wa uchaguzi ambacho kimewafanya watu waamke na kudai Katiba Mpya. Wakiseme kwanza na waseme wasimung'unye maneno; vinginevyo wapo ambao watawasaidia kukisema hicho kinachofanya hoja ya Katiba Mpya iwe na nguvu sasa kuliko 1992.

Dare to say it otherwise.. naomba tuachane na hoja ya Katiba Mpya hadi tutakapokuwa tayari kusema hasa ni kwanini tunataka Katiba Mpya hasa baada ya uchaguzi wa 2010.

Hiyo ndiyo tofauti iliyopo kati ya Mzee Mwanakijiji na Malaria Sugu.
 
Hiyo ndiyo tofauti iliyopo kati ya Mzee Mwanakijiji na Malaria Sugu.

Upupu mtupu, anataka kujifanya kana wazo la katiba mpya ni lake! Hakumbuki kuwa miaka michache ya nyuma lilishaundiwa tume chini ya uongozi wa ccm? Nawe pia hukumbuki?

Msitake kujidai ni wazo lenu. Na muelewe, hiyo katiba iliyopo imesharekebishwa mara ngapi? Chini ya uongozi wa ccm. Katiba si msahafu itakwenda ikibadilika, kuundwa mpya, kurekebishwa, kuongezwa, kupunguzwa maisha yote.

Mimi nawashangaa mnaojifanya kuwa mnashinikiza wakati mnajuwa wazi kuwa katiba mpya ni kwa maslahi ya Tanzania, no matter ni wa chama kipi! CCM chini ya Kikwete itahakikisha inafanya mabadiliko ya Katiba ua japo kuanzisha tu mabadiliko ya Katiba. Hicho ni kitu ambacho si siri wala hakina ubishi. Naona ni wabunge wenu tu ndio wazembe kwa kutopeleka mswada siku zote walizokuwa bungeni.

Haya fanyeni hima, pelekeni mswada bungeni, tupate katiba mpya. Sio kupayuka tu hapa JF.
 
kibaya zaidi wote hawa wanamtwisha zigo JK, ilhali walipokuwa wanafyonza kama yeye anavyofyonza leo walikuwa hawasikii kilio cha katiba mpya. Shame on them.

Kila mtu analia na katiba mpya, kuanzia mimi wa kalumbalesa mpaka aliye wizarani. kinachochekesha hadi jaji mkuu. Really hata jaji mkuu na majaji?? can't they seek audience na mkuu wa nchi na kumweleza kinagaubaga, badala ya kulia lia na waandishi wa habari?
 
naona watu mnashindwa kupata pointi yenyewe na kama kawaida mnaanza kuuliza kama niko bado na akili zangu timamu. Mnapenda mno mazingaombwe kiasi cha kushangilia mkiona sungura katolewa kwenye kofia na wengine wanaweza kuapa kabisa kuwa ni "muujiza". Sasa leo watu wanaanza kuimba "katiba mpya" basi watu wanatakiwa kushangilia:

Hawawaambii tatizo la Katiba ya sasa ni nini? - of course tunatakiwa tuwe tunajua sote
Hawasemi kwanini sasa hivi na haikuwa kabla- tunaambiwa ni muda tu
Hawasemi wanataka nini hasa - yale yale "katiba mpya" - upya wa nini?
Hawasemi ni vitu gani viboreshwe? Je wakibadilisha tu Tume ya Uchaguzi watu wataridhika? Kwanini isiwe kufanyia mabadiliko vipengele vinavyolalamikiwa halafu tukamaliza kwani hilo halihitaji siku nyingi hata kikao cha bunge kinaweza kufanya hivyo.
Ati Katiba iliyopita haikuandikwa na sisi - well kwani kuandika sisi wenyewe kunatuhakikishia vipi Katiba nzuri? Leo hii miaka 49 ya kujitawala mbona baadhi yetu hatujivunii kuoona tunavyojitawala? kwanini tuamini ati kwa vile tutaandika Katiba sisi wenyewe basi itakuwa nzuri? Jamani, kwani vyama vingine vilirudishwa vipi na leo watu hawafurahii wakati tulishirikishwa kuvirudisha?

Katiba Mpya? kwa manufaa ya nani? Siyo wote wanaosema "nyeupe" wanamaanisha "nyeupe pe" wengine wanamaanisha "rangi ya maziwa!"

Hivi wewe MM hoja zako mbona zinatuchanganya? Wewe unaunga mkono Mkono au unapinga swala la katiba Mpya? Unamtetea nani hapa JK au CCM? Hueleweki, unatumia akili nyingi kuhisi utadhani utafiti wa kisayansi kumbe siasa! Haya mambo ni rahisi, tunataka katiba mpya....upya tunaoutaka utajadiliwa baada ya kukubaliana kwamba tuko tayari kuanza mchakato. Hatutaki Kuongeza vilaka kwenye katiba ya sasa kama unavyotaka wewe pamoja na Waziri wako kombani. Acheni kuchukulia swala hili kwa uzito mdogo tumechokaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa! Hatudanganyikiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii. Peoples pawaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.
 
Mzee M/Kijiji, hongera kwa kuchokoza swali hili hapa JF. Bahati mbaya wachangiaji wengi wameshindwa kulenga shabaha ya swali lako! Upo uwezekano baadhi ya wanaookuunga mkono na wanaotofautiana na wewe hawajaelewa kwa kina swali. Inawezekana, (kama ulivyosema), hata hao viongozi waliotamka uwepo wa haja ya Katiba Mpya (KM), huenda hawana jibu la swali lako, au wana malengo tofauti tofauti.

Kwahiyo ipo haja, kwa wana JF na wa-Tz wote kwa ujumla, kuelewa kwa mapana yake haja hii ya kuwa na KM. Wale wanaodai kwamba ni swala la wakati umefika, sidhani kama ni kweli… kwani hata Mwl. Nyerere alikuwa anafahamu ubovu wa katiba tuliyo nayo, na aliwahi kusema kuwa katiba inampa madaraka makubwa kiasi kwamba kama akiyatumia madaraka hayo atageuka kuwa dictator. Nyerere aliitumia katiba iliyopo kwa kusaidiwa na maadili ya uongozi, sera za Kijamaa, hekima yake na mapenzi yake kwa watu wake. Hivyo watu wengi waliridhika na uongozi wake na haja ya KM haikuwa hitaji la lazima sana wakati wake.

Katika kipindi ambacho misingi ya kijamaa imetupwa, uadilifu umepoteza nafasi na ufisadi kuchukua nafasi yake, watu wamepoteza imani na viongozi. Viongozi wanatumia baadhi ya vifungu dhaifu vya katiba kubaki madarakani, lakini kwa manufaa ya wachache, na walio wengi wakiendelea kubaki masikini.

Watu wameamka na wanaonesha kukataa hiyo hali. Njia ya kukataa hali hiyo ni kura, kwenye uchaguzi, lakini bahati mbaya katiba iliyopo haitoi fursa ya uchaguzi huru! Mwaka huu watu walitaka kufanya mabadiliko ya uongozi na katiba imewanyima fursa hiyo !

Baada ya uchaguzi wa mwaka huu, inaonekana wazi kuwa hamkani si shwari tena, dalili za wazi zinaonesha hitaji la watu. Watu walewale, waliomwamini Nyerere, sasa wanaona kiti cha Nyerere kimekaliwa na Ngedere, na hawako tayari kutoa imani yao kwa Ngedere!

Agenda ya KM ilitumiwa na CDM kwenye election manifesto yao, imeonesha kupokelewa vyema na wananchi wengi. Sera za CDM zilikubalika zaidi kuliko sera za CCM. Kutokana na hali hiyo, yafuatayo ymejitokeza:

(1) CCM haiwezi kuendelea kuizima haja ya KM
(2) CCM imeona dalili za kukataliwa na mwelekeo wa kutoweka kwa utulivu wa zamani
(3) CCM haina uwezo wa kuzalisha sera/agenda mwafaka zaidi ya kudandia sera za upinzani ili kuweza kuwapa imani na kuwatuliza wananchi
(4) CCM ina aibu kubwa na ya kweli kwa matokeo ya sera zake zilizozaa ufisadi,
(5) CCM imefanya vibaya kwenye uchaguzi wa mwaka huu kuliko wakati wowote

Kwahiyo matamko ya viongozi kuhusiana na KM yanatokana na hali hiyo na yataendelea na viongozi wengi zaidi watayasema hata Katibu Mkuu Mzee Makamba atatoa tamko lake very soon.
 
Mwanakiji
Jibu ni rahisi sana.Huko nyuma suala la katiba mpya halikupew uzito sana kama wakati huu kwa sababau haikuwahi kutokea viongozi wa dini kutengeneza ilani za uchaguzi na kuingilia siasa kama ilivyofanyika mara hii.Akina Mkapa na wengine wameona kuna hatari inalinyemelea taifa kwani viongozi wa dini wameanza kuwaadhibu wafuasi wao kwa sababu za kisiasa.Katiba mpya lazima iweke uzio kati ya shughuli za dini na siasa
 
Pia kwa vile sera ya katiba mpya iko kwenye ilani ya cuf ambayo alipew jk
 
Maskini mwanakijij ni kupe pole na wanachama wote wa cdm,sasa mbona mnanyan'anywa mtaji wenu?
Msikubali maana mtaji huu mkiukosa cdm inakufa
Hata hivyo hiyo ndio siasa,na mchezo wa siasa una kanuni zake mnapaswa kuzijua ili muweze kufunga magoli
 
Mzeemwanakijiji, siku zote huwa nasema wewe ni pumba nyingi tu, hamna lolote: hujidai kuwa ni mawazo yako tena mapya! fuata hii link uone ni gazeti lipi na tangu lini lilikuwa linapigia kelele katiba mpya, na mpaka (aina) mapendekezo ya katiba wakawasilisha: An-nuur Na. 168
 
Mzeemwanakijiji, siku zote huwa nasema wewe ni pumba nyingi tu, hamna lolote: hujidai kuwa ni mawazo yako tena mapya! fuata hii link uone ni gazeti lipi na tangu lini lilikuwa linapigia kelele katiba mpya, na mpaka (aina) mapendekezo ya katiba wakawasilisha: An-nuur Na. 168

Answar suna
 
Back
Top Bottom