Sidanganyiki - Leo ndio mnajua Tanzania inahitaji katiba mpya?

Sidanganyiki - Leo ndio mnajua Tanzania inahitaji katiba mpya?

Mawazo finyu! Nyerere aliacha uongozi wa taifa enzi zile za chama kimoja katika nchi nyingi za africa, na 1992, tayari upepo ulielekea vyama vingi, it was logical kufanya alichokifanya, sidhani kama alikuwa na maslahi binafsi kama huyu mtu wako

Walimu wako walipata shida sana kukuelewesha, ebu rudia tena.....

Ni sawasawa tu Nyerere alivyodai kuwepo kwa mfumo wa vyama vingi mara baada ya kutoka madarakani, nyakati zinabadilika na fikra zinabadilika hasa unapokuwa nje ya uwanja!!
 
Mambo mengine yanashangaza sana; leo kila mmoja wa watu mashuhuri anatafuta gia ya "kutokea"; mwisho Rais na wajumbe wa Kamati Kuu nao watakuja na kusema "wanataka Katiba Mpya". Nimekaa naangalia wanaojitokeza kudai katiba mpya na wanaripotiwa huku wakibeba ujiko wa ofisi na vyeo vyao; ati kuanzia Mkapa na sasa Jaji Mkuu na wote wengine katikati yao ati wote sasa "wanataka Katiba Mpya"! Really? Why?
Mzee Mwanakijiji, Mkapa na Jaji Mkuu will continue to be just fine whether katiba ya zamani inaendelea kutumika au katiba mpya itapatikana. Tutakaoendelea kuumia endapo kama katiba ya zamani itaendelea kutumika ni sisi hapa, wananchi wa kawaida. So swali kwamba, "kwanini wanataka katiba mpya," kwa mtizamo wangu, is very irrelevant question right now. What we need is a new constitution. Period. So hizi hoja zako zaa Mkapa/Jaji Mkuu amesema nini, hazina mpango na wala hazisaidii kabisa katika mchakato huu wa kudai katiba mpya.


Lakini wote hawa wanaojitokeza kudai Katiba Mpya hawataki kusema kitu kilichowazi; Hawataki kusema hasa kwanini sasa baada ya uchaguzi wamepata ujasiri wa kudai Katiba Mpya. Walijua sheria ya uchaguzi, walijua mfumo wa tume ya uchaguzi; walijua malalamiko ya Katiba mpya lakini kwa miaka karibu ishirini walikaa kimya. Lakini sasa kuna kitu kimetokea; kitu ambacho hawana ujasiri wa kukisema au kukiita kwa jina lake... Hoja ya kuandika upya katiba haiwezi kunogeshwa kwa kutokuwa tayari kuita ukweli kwa jina lake. Ni nini kilitokea baada ya uchaguzi; au swali sahihi zaidi ni nini kilitokea wakati wa uchaguzi ambacho kimewafanya watu waamke na kudai Katiba Mpya. Wakiseme kwanza na waseme wasimung'unye maneno; vinginevyo wapo ambao watawasaidia kukisema hicho kinachofanya hoja ya Katiba Mpya iwe na nguvu sasa kuliko 1992.
Lazima utambue kuwa binadamu sio machine. Binadamu wanauwezo wa kubadili mawazo yao muda wowote bila kupata approval yako (na sijui kwanini wewe unadhani hilo ni jambo baya?). Nyerere alikuwa hapendi mfumo wa vyama vingi. Lakini baada ya kuwekewa mbinyo/pressure na mashirika ya fedha ya nchi za magharibi, plus na sababu yingine nyingi ambazo hakuwahi kuzieleza waziwazi, alibadili mawazo yake na kuama ku-embrace ujio wa vyama vingi mwaka 1992. I believe ni Ralph Waldo Emerson aliyewahi kuonywa kuwa, "A foolish consistency is the hobgoblin of little minds." Kwamba, sitegemei kabisa for a smart guy like Mkapa aendelee leo hii (2010) kuamini kile alichokiamini mwaka 1992 bila kutilia manani matukio mbalimbali yaliyotokea mwaka 1992 hadi leo hii. I think umefika wakati sasa kwa Watanzania tuachane na mtizamo kwamba 'wapinzani peke yao ndo' wana haki ya kudai katiba mpya'. Na badala yake tuige utamaduni wa kutoa credit where credit is due. I mean, kama imefika wakati kwa Mkapa kuona kuwa tunahitaji katiba mpya, then let's give him some credit for taking such a courageous step. Kwasababu ni ngumu sana kwa tamaduni zetu kwa mtu kama Mkapa (ambaye bado ni mwanachama wa CCM), kuwa na ujasiri wa kuongelea juu ya suala la katiba (mpya) kama alivyoonyesha hivi karibuni.

Dare to say it otherwise.. naomba tuachane na hoja ya Katiba Mpya hadi tutakapokuwa tayari kusema hasa ni kwanini tunataka Katiba Mpya hasa baada ya uchaguzi wa 2010.
Mkuu, naona sasa wewe umeanza kukejeli watanzania. I mean, kampeni hizi ulizoanza za kuwashawishi watanzania wasiendelee kudai Katiba mpya, kwa maoni yangu, ziko misguided na hazisaidii hata kidogo wanaharakati mbalimbali ambao wamekuwa mstari wa mbele kudai katiba mpya. I think kuna watu wengi sana ambao wame-articulate vizuri sababu hasa zinazotulazimu kudai Katiba mpya (sijui wewe unasoma magazeti gani sikuhizi?). Plus, wengi wetu, tuko tayari kuendelea kudai katiba mpya. Tumekuwa tukipiga kelele za kudai katiba mpya kabla hata ya chaguzi za 2000, 2005, na 2010. Na still tutaendelea kupiga kelele na kuishinikiza serikali kuu mpaka hapo itakapotambua kuwa hamna alternative nyingine isipokuwa katiba mpya.

P.S. Endeleeni kusaini petition ya kudai katiba mpya hapa:
TUNAHIHITAJI KATIBA MPYA Petition

Or,

Download PDF/HARD-COPY na kuisambaza kwa wale ambao hawana access na internet
 
Wimbo umekuwa ni Katiba Mpya!

Watu tukiambiwa kuna mpango wa kuandikwa katiba mpya tunafurahiiiiiii wakati wengi hata hatujui katiba ya sasa ina mapungufu gani and whether inahitajika kuandika katiba mpya au kurekebisha tu yale mapungufu ''machache'' yaliyogundulika
 
P.S. Endeleeni kusaini petition ya kudai katiba mpya hapa: [/SIZE]TUNAHIHITAJI KATIBA MPYA Petition

Download PDF/HARD-COPY na kuisambaza kwa wale ambao hawana access na internet


Kwa faida ya akina Karumanzila kama mimi, tungeomba pia utufungue macho kwa kuanisha vipengere vyoooooote ndani ya Katiba ya sasa vinavyohitaji mabadiliko makubwa to necessitate katiba mpya badala ya kurekeisha hivyo vipengere tu ndani ya katiba ya sasa. Nachelea kusaini petition au kuwashawishi wengine wakati sijui ninataka nini na kwa nini
 
NAUNGANA MKONO NA GREAT THINKER MFAMAJI NA MWANAKIJIJI LAKINI PIA YULE ALIYESEMA KISA KIKUBWA UCHAKACHUAJI NA NGUVU YA UMMA KUPITIA KIONGOZI WA UMMA DR SLAA. DAMU INGEMWAGIKA HAPA MANAKE SLAA(PhD) angetamuka tu watu tuingie barabarani basi pangechimbika. Dr Slaa alipata ushindi wa kishindo -masultani wakachakachua na sasa vivuli vyao vinawatoa jasho. Wale usishangae mzee mwanakijiji sababu kubwa ni uchakachuaji wa waziwazi waliofanya mafisadi ccm-sasa nguvu ya umma inataka kuwawakia wanaanza kujiokoa.

Hongera Dr.Slaa -wewe ni mpiganaji endelea na vita -bhita ni bhita muraaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Mzee Mwanakijiji, Mkapa na Jaji Mkuu will continue to be just fine whether katiba ya zamani inaendelea kutumika au katiba mpya itapatikana. Tutakaoendelea kuumia endapo kama katiba ya zamani itaendelea kutumika ni sisi hapa, wananchi wa kawaida. So swali kwamba, "kwanini wanataka katiba mpya," kwa mtizamo wangu, is very irrelevant question right now. What we need is a new constitution. Period.

Hili ndilo tatizo la kwanza ambalo naliona; haiwezekani tuesema "we need new constitution, perido". Ni wazi huoni hatari ya kusema tupate tu katiba mpya as if katiba mpya just by being "mpya" will become a panacea ya matatizo yetu. This is a gross misconception.




Mkuu, naona sasa wewe umeanza kukejeli watanzania. I mean, kampeni hizi ulizoanza za kuwashawishi watanzania wasiendelee kudai Katiba mpya, kwa maoni yangu, ziko misguided na hazisaidii hata kidogo wanaharakati mbalimbali ambao wamekuwa mstari wa mbele kudai katiba mpya. I think kuna watu wengi sana ambao wame-articulate vizuri sababu hasa zinazotulazimu kudai Katiba mpya (sijui wewe unasoma magazeti gani sikuhizi?). Plus, wengi wetu, tuko tayari kuendelea kudai katiba mpya. Tumekuwa tukipiga kelele za kudai katiba mpya kabla hata ya chaguzi za 2000, 2005, na 2010. Na still tutaendelea kupiga kelele na kuishinikiza serikali kuu mpaka hapo itakapotambua kuwa hamna alternative nyingine isipokuwa katiba mpya.
[/quote]

Matatizo mengine mawili yako wazi; sishawishi watu watu wasidai katiba mpya; ninachotaka ni watu kuwa wa kweli kwanini wanataka Katiba mpya; na hapa sizungumzii watu wengine waliokuwa wanadai katiba mpya toka zamani bali hawa wa sasa ambao wamepata ufunuo wa kutaka kudai katiba mpya bila ya kutuambia ni kipi hicho kinachowafanya sasa waone haja hiyho wakati wengine (kama wewe mwenyewe ulivyosema) wamekuwa wakidai kitu hicho hicho kuanzia 1992. Tatizo la pili ni hilo la kuamini kuwa "Serikali Kuu" ndio inawajibika kukubali haja ya kutengeneza Katiba Mpya na kwa mtindo huo na jinsi ulivyosema mko tayari kuendelea kupiga kelele kuishawishi serikali kukubali maombi "yenu". Kuna tatizo hapo tena kubwa sana ambalo ndilo limetufikisha hapa leo hii.

P.S. Endeleeni kusaini petition ya kudai katiba mpya hapa:

Very good.. mnapetition nani? I hope siyo "serikali kuu"
 
At the end of the day Action will speak louder than words..

Si JK is really mean legacy that is the only one he will live behind nothing else... Si that will not then we will see who mean business.
 
acheni wenye sauti waongee. Sote tunaona katiba ya sasa inavyotutenda. Na mwalimu au mtu wa hadhi na heshima yake hatuna. Mzee mbita na prof mpangala jana pale tbc1 walijitahidi kueleza kwa nini tunahitaji katiba mpya. Tena tusipoteze muda kuunda bunge au mahakama ya katiba. kenya wameandika vizuri sana katiba yao kwa sehemu kubwa. Sio vibaya tukiitumia ile kwa kuondoa yale ambayo yamekaa kikenya na kuingiza ya kitanzania

are you serious??
 
MM Mwanakijiji ana hoja ya msingi sana.

Mtanzania...kula tano kwa mchango wako.

Ni dhahiri Watanzania tumeshindwa kuitetea na kuilinda Katiba ya sasa (Wananchi walio wengi hata hawaielewi)!!

Sasa tutawezaje kuanza mchakato wa Katiba mpya??
 
Kwanza, kama baadhi ya wenzangu walivyosema, binadamu kubadili msimamo ni sifa ya all objective people. Siyo kushikilia msimamo hata pale umepata ufahamu mpya tofauti na ulivyofikiri mwanzo.

Pili, mkapa na JMkuu ni objective persons, hivyo wamefanya sawa.

Tatu, huu uchakachuaji wa 2010 haukupa sifa kutoka jamii za kimataifa kama ule wa chaguzi zilizopita. Jamii za kimataifa zilijua mapungufu haya yote lakini zilichagua kusifia chaguzi kwa sababu zao binafsi. Sasa hili lina athari kwa serikali yetu ombaomba. Serkali inayoamini kwamba rasilimali zetu tuwakabidhi wazungu kisha tuwaombe msaada.

Nne, propaganda zilizoenezwa awali kwamba upinzani ni vita, mauaji, uasi, uchu wa madaraka, siyo uzalendo, ni kupinga maendeleo, yote sasa yameonekana ni uongo. Ushahidi umepatikana kwamba kinyume cha hizo propaganda ndiyo uhalisi wa chama tawala. Wanadhulumu wananchi, wanamwaga damu, wanapora wananchi ardhi yao, wanafisadi mali na pesa za umma, na wana uchu wamadaraka. Hivyo, upinzani umekua kwa hoja na idadi ya wanachama wanaothubutu na kwamba katiba ya leo inaweza kupelekea umwagaji wa damu. Mifano ilikuwa Nyamagana, arusha mjini, ubungo, kawe, n.k.

Hii ina maana kwamba viongozi wakuu wa ccm walioanza kudai katiba mpya ni mkakati wa ccm kutidhatiti kwa chaguzi zijazo, lakini wanaamua kupitia kwa mkapa na JMkuu ili mwanzoni mwa 2011 ccm iseme ni mchakato ulioanzia kwao, kama walivyodai kuhusu ufisadi. Ikiwa hivyo upinzani utabweteka na kuona wamefaulu. Lakini Nia ya ccm ni kuandika katiba mpya itakayodhibiti changamoto walizopambana nazo tangu 2006. Tukumbuke kwamba ccm ndiyo yenye wabunge wengi bungeni na katiba hupitishwa kwa kura siyo sauti zilizoafiki.
 
Jamani, tukubaliane ukiwa nje ya uwanja wa mpira au nje ya chumba cha mtihani unayajua mengi kuliko ambavyo uko ndani. Msiwashangae hawa wanaoliongelea wakiwa nje ya madaraka. Suala la akina Mkapa na Warioba and Co. Ltd., tulichukulie ni ushindi kwa walioaisisi madai ya katiba mpya nikiwa na maana wahitaji wanazidi kuongezeka. Hao waliojiunga tuwapokee badala ya kuwabeza kwani watarudi nyuma walikotoka na hatimaye tuchelewe kuipata hiyo katiba mpya.
 
Huku ndiko tulikotoka; kabla hujachangia angalia tarehe ya mada hii kwanza...
 
Mwanakijiji hoja ya Katiba mpya kama unakumbuka ilikuwa ni sera ya CHADEMA kwenye uchaguzi uliopita. CCM wamedaka sera ya wemzao. Wananchi tumeelimishwa umuhimu wa katiba mpya na sababu za kuachana na hiyo ya zamani. Nadhani uombe ilani ya CDM watakuwa wameelezea. Ile ya kwanza ilikuwa kwenye mfumo wa chama kimoja na isitoshe mambo mengi yamebadilika. Kwa mfano azimio la Arusha limekufa na Zanzibar imejitangazia kuwa ni nchi. Kuna umuhimu wa kutengeneza katiba ambayo itatambua kuwa Zanzibar ni nchi na hivyo hiyo nchi ingine iliyoungana na Zanzibar lazima pia ijulikane. Ila Mwanakijij najua unayajua yote haya umechokoza mada tu!
Mambo mengine yanashangaza sana; leo kila mmoja wa watu mashuhuri anatafuta gia ya "kutokea"; mwisho Rais na wajumbe wa Kamati Kuu nao watakuja na kusema "wanataka Katiba Mpya". Nimekaa naangalia wanaojitokeza kudai katiba mpya na wanaripotiwa huku wakibeba ujiko wa ofisi na vyeo vyao; ati kuanzia Mkapa na sasa Jaji Mkuu na wote wengine katikati yao ati wote sasa "wanataka Katiba Mpya"! Really? Why?

Ati leo viongozi wa dini nao wanajitokeza na kudai Katiba Mpya! Mwisho wataanza kuja na wabunge wa CCM wakidai Katiba Mpya! Utani mwingine jamani!

Katiba Mpya? Kwani hii iliyopo imegunduliwa ina matatizo gani ambayo hawakuyaona miaka 20 iliyopita? Kwamba mwaka 2010 ndio wamegundua kuwa Katiba ina matatizo? Naam, watasema imejulikana kuanzia 1992. Watasema kuwa miaka yote hii kumekuwa na "kilio" cha Katiba Mpya na wengine watatuambia jinsi walivyojaribu kuzungumzia hili miaka yote hii wakituambia juu ya Ripoti ya Nyalali n.k

Lakini miaka yote hiyo hawakujitokeza hawa kwa nguvu hivi kudai "katiba mpya". Lakini cha kuudhi na ambacho naamini ni cha uzugaji uliokubuhu ni kuwa wote hawa hawakuwa na ujasiri wa kudai Katiba Mpya kabla ya uchaguzi. Tangu 2005 hadi ulipofika uchaguzi huu wengi tumeandika na wengine wamelalamikia matatizo mbalimbali. Suala la ubovu wa tume ya uchaguzi halikuibuliwa kwenye uchaguzi wa 2010; wengine tulishabeza wapinzani kwenda kwenye uchaguzi huu uliopita wakiwa na tume ile ile na mfumo ule ule na tukasema mapema wasije kulalamika "tume ya uchaguzi, tume ya uchaguzi". Tulisema wamekubali kucheza kwa kanuni za mchezo na refa ambaye tayari alishajionesha kuwa ana upendeleo akiwavuruga wasilalamike. Sijui walisahau wapi yaliyotokea Kiteto? Walisahau vipi yaliyotokea Tunduru?

Lakini sasa siyo wapinzani tu hata viongozi wengine wa serikali na hata wa CCM wanaanza kudai Katiba Mpya. Kilichonishangaza ni kuwa Rais Mkapa anadai naye Katiba Mpya! Really? I mean Really? Alikuwa Rais kwa miaka 10; alisimamia mabadiliko ya Katiba ya 2005 - lakini hakutaka Katiba mpya then?

Lakini wote hawa wanaojitokeza kudai Katiba Mpya hawataki kusema kitu kilichowazi; Hawataki kusema hasa kwanini sasa baada ya uchaguzi wamepata ujasiri wa kudai Katiba Mpya. Walijua sheria ya uchaguzi, walijua mfumo wa tume ya uchaguzi; walijua malalamiko ya Katiba mpya lakini kwa miaka karibu ishirini walikaa kimya. Lakini sasa kuna kitu kimetokea; kitu ambacho hawana ujasiri wa kukisema au kukiita kwa jina lake.

Hoja ya kuandika upya katiba haiwezi kunogeshwa kwa kutokuwa tayari kuita ukweli kwa jina lake. Ni nini kilitokea baada ya uchaguzi; au swali sahihi zaidi ni nini kilitokea wakati wa uchaguzi ambacho kimewafanya watu waamke na kudai Katiba Mpya. Wakiseme kwanza na waseme wasimung'unye maneno; vinginevyo wapo ambao watawasaidia kukisema hicho kinachofanya hoja ya Katiba Mpya iwe na nguvu sasa kuliko 1992.

Dare to say it otherwise.. naomba tuachane na hoja ya Katiba Mpya hadi tutakapokuwa tayari kusema hasa ni kwanini tunataka Katiba Mpya hasa baada ya uchaguzi wa 2010.
 
Back
Top Bottom