Sielewi kwanini mtu aliyechakachua msaada wa serikali na kujimilikisha enzi za Kikwete, akaondolewa leo anateuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa

Sielewi kwanini mtu aliyechakachua msaada wa serikali na kujimilikisha enzi za Kikwete, akaondolewa leo anateuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa

Mama yupo katika kona ngumu. JK kwake ni kiongozi aliyemtoa Unguja na kumleta bara, alimlea kisiasa hivyo asemalo hawezi kulipinga.

Hivyo hao wanaorudishwa sasa hivi ambao ni watu wa JK ambao Mama aliwakuta baada ya kuja bara wanatakiwa kuwa ni uzalendo badala ya kuanza kurudisha wizi maofisini na magenge ya kitapeli yanayosubiri pesa za bure bure za udalali.

Wanaorudishwa kwa mgongo wa JK wanayo kazi ya kuitazama Tanzania ya sasa na kuwa na ubunifu wa kuongeza tija badala ya kufikiria kuwa wamepata chaka la kutajirikia.
Nikujibu kwa kifupi mkuu 'Philipo Bukililo'.

Mimi sioni 'strategy' (mkakati) wowote katika teuzi hizi.

Kama ni kumfurahisha Kikwete ndiyo 'strategy', basi hapo nitakuwa nimepoteza dira katika uoni wangu.

Mimi nadhani sasa inaonekana mama anajipigia tu, mradi liende, na siku zisonge.
 
Tatizo kubwa la watanzania ni UBINAFSI, nchi hii ina watu wana hali ngumu sana kiuchumi na wengine ni wazee sana na hawana msaada.

Viongozi wengi kazi yao kubwa in kulipana posho za vikao na marupurupu mengine hivyo wapo tayari kujipendekeza, kuua, kuroga na hata kuhonga ili wapate madaraka au waendelee kuwa kwenye madaraka.

Kuna Watanzania wenzetu ni maskini wa kutupwa.
 
Nadhani hata kazini kwako wanapata tabu sana na wewe. " majungu, majungu, majungu tu na wivu".

Post yako hii imekaa kimajungu
Ufupi wa mawazo yako unajidhihirisha wazi. Kazini kwangu wananijua wakitaka kufanya ujinga wafanye mie sipo. Kuwasema watu waliochakachua mali ya serikali ni majungu, kwamba tuache tu kwa kuwa wao walipata fursa? Kwa hiyo wewe ukiona mtu anahujumu mali za serikali utakaa kimya kwa kuwa kumsema ni kuleta majungu? Hujakaa vizuri kichwani.
 
Team JK imerudi kwa kasi, lakini matumaini ni kwamba hao wanaorudishwa hawatarudi na madudu ya awamu ile.

Matumaini ni Rais Samia kuwa na sauti, maana inakuwa haina faida kwa taifa kama wanarudishwa wanamtandao halafu wakarudi na akili zile zile za wakati ule.
Kurudisha team JK sio tatizo, hata akitaka achanganye na team Mkapa. Suala ni kwamba, kwa nini urudishe watu wenye madoa yasiyofutika? Kwa nini usiibue watu wako wapya na na awamu nyingine zije zichukue team yako?
 
Team JK imerudi kwa kasi, lakini matumaini ni kwamba hao wanaorudishwa hawatarudi na madudu ya awamu ile.

Matumaini ni Rais Samia kuwa na sauti, maana inakuwa haina faida kwa taifa kama wanarudishwa wanamtandao halafu wakarudi na akili zile zile za wakati ule.

..salama yetu inatakiwa iwe kwenye KATIBA.

..vilevile tuwe na bunge lenye utashi wa kuisimamia serikali.
 
Kurudisha team JK sio tatizo, hata akitaka achanganye na team Mkapa. Suala ni kwamba, kwa nini urudishe watu wenye madoa yasiyofutika? Kwa nini usiibue watu wako wapya na na awamu nyingine zije zichukue team yako?
Hakujiandaa na jukumu la urais akitegemea atabakia na umakamu mpaka 2025. Ni mipango ya Mungu kifo, hivyo naamini amefanya kazi ngumu baada ya kifo cha JPM ili apate watu sahihi.

Na ni kwa kigezo hicho cha kifo cha rais, mzee Kikwete ndipo anapoingia kazini kumsaidia ili mambo yaende. Miradi imalizike kwa wakati huku nchi ikibakia imara pasipo kutetereka.
 
Hakujiandaa na jukumu la urais akitegemea atabakia na umakamu mpaka 2025. Ni mipango ya Mungu kifo, hivyo naamini amefanya kazi ngumu baada ya kifo cha JPM ili apate watu sahihi.

Na ni kwa kigezo hicho cha kifo cha rais, mzee Kikwete ndipo anapoingia kazini kumsaidia ili mambo yaende. Miradi imalizike kwa wakati huku nchi ikibakia imara pasipo kutetereka.
Mkuu umeongea point sana. Nakumbuka teuzi za JK zilivyokuwa na ukakasi mara nyingine kwa kuwa zilikuwa ni teuzi za Mama na Mwana. Hawa kina Makonda walianzia mgogongozi mwa Ridhiwani - baba mteue huyu Mkuu wa Wilaya, ameniomba sana. Honey huyo mtoto wa ndugu yanug amemaliza Masters degree mpe ukurugenzi pale Wizara ya Elimu!
 
Mkuu umeongea point sana. Nakumbuka teuzi za JK zilivyokuwa na ukakasi mara nyingine kwa kuwa zilikuwa ni teuzi za Mama na Mwana. Hawa kina Makonda walianzia mgogongozi mwa Ridhiwani - baba mteue huyu Mkuu wa Wilaya, ameniomba sana. Honey huyo mtoto wa ndugu yanug amemaliza Masters degree mpe ukurugenzi pale Wizara ya Elimu!
Yupo kiongozi mmoja wa Yanga alibembelezwa cheo lakini akakataa, ni ndugu yake JK ni mwanasheria maarufu.
 
Pamoja na kuhoji kutokutaja jina la mhusika, sehemu pana ya mada iliyowasilishwa ina mantiki sana.

Hawa wateuwaji, hivi wanakosa watu wa kuwateuwa katika nafasi mbalimbali za uongozi, kiasi kwamba watu wale wale, tena walio na rekodi mbaya katika utumishi wao ndio waendelee kuteuliwa?

Tatizo kubwa tulilonalo ni hilo la watu kutuhumiwa, halafu uchunguzi haufanyiki kuhusu wanayotuhumiwa juu yake; wanapumzishwa au wanapangiwa kwingine. Hili ndilo tatizo la msingi. Kwa nini iendelee kuwa hivi?
" jina lake nani, au baba yake nani" kama ni underground, kwa heli!!!
Watu wa vetting ndio chanzo cha haya
 
Ufupi wa mawazo yako unajidhihirisha wazi. Kazini kwangu wananijua wakitaka kufanya ujinga wafanye mie sipo. Kuwasema watu waliochakachua mali ya serikali ni majungu, kwamba tuache tu kwa kuwa wao walipata fursa? Kwa hiyo wewe ukiona mtu anahujumu mali za serikali utakaa kimya kwa kuwa kumsema ni kuleta majungu? Hujakaa vizuri kichwani.
Kama sio majungu kwanini usimtaje sasa
 
Hivi sisi waswahili tuna tatizo gani lakini? kwa nini tunaona kwamba kuna watu fulani wanastahili kupewa fursa za uongozi hata wafanye madhambi ya ajabu kiasi gani? Ina maana hapa nchini suala la uongozi kuna watu wanaostahili na wengine wasiostahili?

Mtu anafanya makosa makubwa katika nafasi fulani, anaondolewa, anapumzishwa na baada ya muda fulani anateuliwa tena katika nafasi nyingine ya uongozi. Au utakuta mtu anaharibu sana katika sehemu moja, badala ya kuwajibishwa anahamishiwa sehemu nyingine.

Imekuwa kawaida sasa kusikia Raisi, au Waziri Mkuu au Waziri wakisema kwamba mtu fulani ameharibu sana hapa. Arudishwe wizarani akapangiwe kazi nyingine. Au Raisi kamtumbua mtu fulani, atapangiwa kazi nyingine. Ina maana apewe nafasi ya kuharibu sehemu nyingine? Hivi ina maana kuna watu ambao wanapewa hati miliki za uongozi? Na wengine hawastahili?

Kwa mfano, watu walilalamika kuhusu tabia za baadhi ya wakuu wa mikoa, kuhusu dharau zao, lugha zao, pamoja na Chalamila, lakini hawakusikilizwa. Kweli ilibidi Raisi Samia asubiri hadi na yeye awe mhanga wa lugha zisizofaa ndio achukue hatua? Kwa nini alipoambiwa hakutaka kusikiliza?

Kuna mkuu wa mkoa mwingine ambae alichakachua msaada wa seikali, JK akakasirika na kumwondoa kwenye nafasi yake. Leo Raisi Samia anaamua kumteua kuwa Mkuu wa Mkoa. Hatuna watu wengine Tanzania wanaoweza kuwa wakuu wa mkoa bali yeye tu?
Taja jina la huyo mtuhumiwa.vingenevyo nyamaza.
 
Kwa hiyo kwa upande wako nyakati zimebaki vilevile, hakuna kilichobadilika toka wakati huo wakati huu, kiasi kwamba yaliyovumiliwa wakati ule ndiyo yavumiliwe wakati huu?
nyakati zimebadilika, ila huyo unknown is known na ni maarufu pande za arusha, sasa watu bado wanalazimisha mtoa mada amtaje...
 
Hivi sisi waswahili tuna tatizo gani lakini? kwa nini tunaona kwamba kuna watu fulani wanastahili kupewa fursa za uongozi hata wafanye madhambi ya ajabu kiasi gani? Ina maana hapa nchini suala la uongozi kuna watu wanaostahili na wengine wasiostahili?

Mtu anafanya makosa makubwa katika nafasi fulani, anaondolewa, anapumzishwa na baada ya muda fulani anateuliwa tena katika nafasi nyingine ya uongozi. Au utakuta mtu anaharibu sana katika sehemu moja, badala ya kuwajibishwa anahamishiwa sehemu nyingine.

Imekuwa kawaida sasa kusikia Raisi, au Waziri Mkuu au Waziri wakisema kwamba mtu fulani ameharibu sana hapa. Arudishwe wizarani akapangiwe kazi nyingine. Au Raisi kamtumbua mtu fulani, atapangiwa kazi nyingine. Ina maana apewe nafasi ya kuharibu sehemu nyingine? Hivi ina maana kuna watu ambao wanapewa hati miliki za uongozi? Na wengine hawastahili?

Kwa mfano, watu walilalamika kuhusu tabia za baadhi ya wakuu wa mikoa, kuhusu dharau zao, lugha zao, pamoja na Chalamila, lakini hawakusikilizwa. Kweli ilibidi Raisi Samia asubiri hadi na yeye awe mhanga wa lugha zisizofaa ndio achukue hatua? Kwa nini alipoambiwa hakutaka kusikiliza?

Kuna mkuu wa mkoa mwingine ambae alichakachua msaada wa seikali, JK akakasirika na kumwondoa kwenye nafasi yake. Leo Raisi Samia anaamua kumteua kuwa Mkuu wa Mkoa. Hatuna watu wengine Tanzania wanaoweza kuwa wakuu wa mkoa bali yeye tu?
JF is the place "WHERE WE DARE TO TALK OPENLY".

Sema ni nani huyo na alichakachua msaada gani na kwa sasa ni RC mkoa upi...?

Don't hide anything because there's no reason to do so....
 
" jina lake nani, au baba yake nani" kama ni underground, kwa heli!!!
Watu wa vetting ndio chanzo cha haya
Hii habari ya "vetting", nadhani tunaaminishwa kitu kisichokuwepo; na kama kipo, basi hicho ni kifaa kisichokuwa na manufaa yoyote, bali kina hasara kubwa kwa taifa.
 
nyakati zimebadilika, ila huyo unknown is known na ni maarufu pande za arusha, sasa watu bado wanalazimisha mtoa mada amtaje...
Maarufu pande za Arusha huku ni Gidbless Lema tu, wengine HAPANA hakuna kitu....SIYO MAARUFU...

Amtaje au mtaje wewe kwa kuwa umeshamjua. Wengine sure kabisa, bado hatumjui...
 
Back
Top Bottom