Sigara "Clipper" aliyokuwa akivuta Mwalimu Nyerere miaka ya 1950's

Sigara "Clipper" aliyokuwa akivuta Mwalimu Nyerere miaka ya 1950's

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
SIGARA "CLIPPER" ALIYOKUWA AKIVUTA MWALIMU NYERERE
Picha hiyo hapo chini imepigwa mwaka wa 1955 Magomeni Mapipa Mtaa wa Jaribu kwenye Tawi la TANU alilofungua Ali Msham nyumbani kwake.

Ali Msham ni huyo upande wa kulia aliyekuwa katika ya vijana wawili wamepiga lubega za kaniki mmoja ana shoka begani.

Hawa walikuwa Bantu Group wahamasishaji umma na walinzi wa viongozi wa TANU.

Waliokaa kulia ni Zuberi Mtemvu, Julius Nyerere na John Rupia.

Ukimwangalia Nyerere utaona ameshika paketi ya sigara na ana sigara mkononi.

Mwalimu katika ujana wake alivuta sigara na sigara yake ilikuwa "Clipper," sigara maarufu enzi hizo. Paketi yake ni hiyo hapo juu.

Mwalimu aliacha kuvuta mwaka wa 1962 baada ya kifo cha rafiki yake kipenzi Hamza Mwapachu kufariki kwa maradhi ya moyo yaliyosababishwa na uvutaji sigara.

Clip 1.jpg


Screenshot_20200503-064033.jpg

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kumbe mwalim nae alikua anatumia mmea
Uvutaji wa sigara na kiko vilikuwa ni fasheni kwa miaka ya hamsini, sitini, na sabini kabla madhara ya tumbaku hayajajulikana. Sehemu kubwa ya vijana wa miaka hiyo walikuwa wanavuta sigara sana tena hadharani tu, hata mbele za watu wengine.

1588521538888.png

John F Kennedy: Rais wa Marekani Enzi hizo
1588521621383.png

Nelson Mandela: Rais wa kwanza Mwafrika wa Afrika ya kusini enzi za ujana wake
1588521713309.png

Winston Churchill: Waziri Mkuu wa Uingereza enzi hizo.

1588521864359.png

Ronald Reagan: Rais wa Marekan enzi za Ujana wake

1588521971124.png

Fidel Castro: Rais wa Cuba enzi za ujana wake

1588522164708.png


Leopold Senghor: Rais wa Senegal enzi za ujana wake


1588522373107.png

Nafikiri unamjua huyo
1588522525577.png

Hakuna mtu wa karne hii asiyemjua mtu huyu
1588522681728.png

Hapo ni General Yitzhak Rabin na General Ariel Shalon wakiwa katika maandaliaiz ya vita ya siku sita iliyofuta majeshi yote ya Misri, Syria na Jordan kwa siku sita tu. Wote Rabin na Sharon baadaye walikuwa mawaziri wakuu wa Israel kwa nyakati tofauti.
 
Uvutaji wa sigara na kiko vilikuwa ni fasheni kwa miaka ya hamsini, sitini, na sabini kabla madhara ya tumbaku hayajajulikana. Sehemu kubwa ya vijana wa miaka hiyo walikuwa wanavuta sigara sana tena hadharani tu, hata mbele za watu wengine.

View attachment 1438923
John F Kennedy: Rais wa Marekani Enzi hizo
View attachment 1438929
Nelson Mandela: Rais wa kwanza Mwafrika wa Afrika ya kusini enzi za ujana wake
View attachment 1438932
Winston Churchill: Waziri Mkuu wa Uingereza enzi hizo.

View attachment 1438934
Ronald Reagan: Rais wa Marekan enzi za Ujana wake

View attachment 1438936
Fidel Castro: Rais wa Cuba enzi za ujana wake

View attachment 1438939

Leopold Senghor: Rais wa Senegal enzi za ujana wake


View attachment 1438942
Nafikiri unamjua huyo
View attachment 1438946
Hakuna mtu wa karne hii asiyemjua mtu huyu
View attachment 1438954
Hapo ni General Yitzhak Rabin na General Ariel Shalon wakiwa katika maandaliaiz ya vita ya siku sita iliyofuta majeshi yote ya Misri, Syria na Jordan kwa siku sita tu. Wote Rabin na Sharon baadaye walikuwa mawaziri wakuu wa Israel kwa nyakati tofauti.
Safi sana 👍
 
Uvutaji wa sigara na kiko vilikuwa ni fasheni kwa miaka ya hamsini, sitini, na sabini kabla madhara ya tumbaku hayajajulikana. Sehemu kubwa ya vijana wa miaka hiyo walikuwa wanavuta sigara sana tena hadharani tu, hata mbele za watu wengine.

View attachment 1438923
John F Kennedy: Rais wa Marekani Enzi hizo
View attachment 1438929
Nelson Mandela: Rais wa kwanza Mwafrika wa Afrika ya kusini enzi za ujana wake
View attachment 1438932
Winston Churchill: Waziri Mkuu wa Uingereza enzi hizo.

View attachment 1438934
Ronald Reagan: Rais wa Marekan enzi za Ujana wake

View attachment 1438936
Fidel Castro: Rais wa Cuba enzi za ujana wake

View attachment 1438939

Leopold Senghor: Rais wa Senegal enzi za ujana wake


View attachment 1438942
Nafikiri unamjua huyo
View attachment 1438946
Hakuna mtu wa karne hii asiyemjua mtu huyu
View attachment 1438954
Hapo ni General Yitzhak Rabin na General Ariel Shalon wakiwa katika maandaliaiz ya vita ya siku sita iliyofuta majeshi yote ya Misri, Syria na Jordan kwa siku sita tu. Wote Rabin na Sharon baadaye walikuwa mawaziri wakuu wa Israel kwa nyakati tofauti.
Hili wala halina ubishi mkuu!sijajua lengo la mleta mada lilikuwa ni lipi maana dunia hii mapito katika kila kizazi
 
Kuna baadhi ya maamuzi yanakuaga yanaitaji stimulation ya brain kwaiyo uwa naamini ukiskia tramp anavuta sonyo au kim anakula ugoro usishangae #wanadamshi😅
 
Kuna baadhi ya maamuzi yanakuaga yanaitaji stimulation ya brain kwaiyo uwa naamini ukiskia tramp anavuta sonyo au kim anakula ugoro usishangae #wanadamshi[emoji28]
Kabisa mkuu mi mwenyewe nakuwaga at the best sana Nikitumia walau Alcohol kidogo
 
Hili wala halina ubishi mkuu!sijajua lengo la mleta mada lilikuwa ni lipi maana dunia hii mapito katika kila kizazi
Mtoto...
Nimekutana na picha za vitu vya zamani hapa mtandaoni vitu ambavyo vimenikumbusha historia niijuayo katika vitu hivyo.

Ndipo nikaamua kuwa nitaandika historia hizo kwa nia ya kuweka kumbukumbu na nikaanza na Mwalimu Nyerere na sigara Clipper.

Katika picha hizo kuna picha ya Aspro.

Niliamua baada ya sigara niandike makala kuhusu Aspro ambayo inawahusu watu watatu muhimu sana katika Afrika ya Mashariki na Kati katika miaka ya 1950 hadi 1960 - Peter Colmore, Mwenda Jean Bosco na Eduardo Massengo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtoto...
Nimekutana na picha za vitu vya zamani hapa mtandaoni vitu ambavyo vimenikumbusha historia niijuayo katika vitu hivyo.

Ndipo nikaamua kuwa nitaandika historia hizo kwa nia ya kuweka kumbukumbu na nikaanza na Mwalimu Nyerere na sigara Clipper.

Katika picha hizo kuna picha ya Aspro.

Niliamua baada ya Sigara Clipper niandike makala kuhusu Aspro na historia yake ambayo inawahusu watu watatu muhimu sana katika Afrika ya Mashariki na Kati katika miaka ya 1950 hadi 1960 - Peter Colmore, Mwenda Jean Bosco na Eduardo Massengo.

Katika hawa watu watatu Peter Colmore nikimfahamu vizuri kwanza nikiwa mtoto Dar es Salaam na kisha mtu mzima Nairobi na ndiye aliyenieleza haya ya Aspro.

Hiyo picha ni ya Peter Colmore.

Colmore ndiye aliyemjenga Massengo akawa mwanamuziki mkubwa sana na kupitia kwa Massengo Colmore akamleta Mwenda Jean Bosco Kenya kuja kuitangaza Aspro Afrika ya Mashariki.

"Aspro ni Dawa ya Kweli," lilikuwa tangazo maarufu katika radio zote Afrika ya Mashariki.

Bosco alikuwa pia mwanamuziki mkubwa Congo lakini alikuwa hajafika Afrika ya Mashariki.

Hii ndiyo ilikuwa nia na azma yangu kwa bandiko lile la Baba wa Taifa na Sigara Clipper na nihitimishe na historia ya siku mwaka wa 1961 Ally Sykes alipowachukua Peter Colmore na Eduardo Massengo kuwapeleka nyumbani kwa Nyerere Magomeni kuwatambulisha.

Siku ile ikasadifu kuwa ndiyo siku Patrice Lumumba aliuliwa.

Ziko picha za Mwalimu na Massengo.

Sent using Jamii Forums mobile app

CIMG0449-1.JPG


Sent using Jamii Forums mobile app
 

Attachments

  • ASPRO.jpg
    ASPRO.jpg
    6.8 KB · Views: 61
  • EDUARDO MASSENGO IN STRIPES.jpg
    EDUARDO MASSENGO IN STRIPES.jpg
    12 KB · Views: 52
  • MWENDA JEAN BOSCO.png
    MWENDA JEAN BOSCO.png
    31.7 KB · Views: 59
kuna picha moja inamuonesha mwl. J.K NYERERE akicheza pool table huku pembeni yake akiwepo kamanda mmoja wa polisi. hivi ktk kile kipindi mchezo uo ulikuwepo TZ & MWL amewahi ucheza kweli?
nyerere vs pool table.jpeg
 
Back
Top Bottom