Siioni nafasi ya Lukuvi au mwingine aliyeachwa kwenye Baraza la Mawaziri kuwa Spika wa Bunge

Siioni nafasi ya Lukuvi au mwingine aliyeachwa kwenye Baraza la Mawaziri kuwa Spika wa Bunge

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,307
Reaction score
25,932
Ujumbe wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan, kabla ya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri, ulikuwa wazi. Ni kuwa mabadiliko ya Baraza yamefanyika ili 'kubaki' na wa kwenda nao pamoja 2025 na 'kuwapa nafasi' ya maandalizi wenye nia na 2025. Ndiyo kusema, waliotarajiwa kuachwa na Rais Samia ni wale ambao walikuwa wakitingwa na maandalizi yao ya mwaka 2025, mwaka wa uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani. Baada ya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri, kukatokea mjadala mkubwa. Mjadala ni sehemu na ndiyo utamu wa siasa.

Tupo tuliosema kuwa walioachwa ndiyo hasa waliopewa nafasi ya kuendelea na maandalizi yao ya mwaka 2025. Tupo tuliosema kuwa walioachwa ndiyo waliokuwa wakimkwamisha Rais Samia katika utekelezaji wa majukumu yake kiserikali na kusimamia ipasavyo utekelezaji wa Ilani ya CCM. Tupo tuliojaribu kumulika hili na lile lililopelekea huyu au yule kuachwa kwenye Baraza la Mawaziri. Sote tulikuwa sahihi kwakuwa ni maoni yetu.

Nafasi ya Spika ni nafasi kubwa. Spika ni kiongozi wa mhimili wa Bunge. Spika ndiye anayeongoza na kuratibu mijadala Bungeni wakati wa uundwaji wa sheria na hata wakati kujadili na kupitisha bajeti.

Spika hapaswi kuwa na mambo mengi (kama hayo ya kujiandaa na uchaguzi mkuu wa 2025). Spika anapaswa kuwa ni mtu asiyeweza 'kumkwamisha' kwa namna yoyote Rais- sheria zipite na bajeti zipite. Spika anapaswa kuwa pamoja na Rais.

Sisi tulioona kana kwamba walioachwa ndiyo waliosemwa na Mhe. Rais kabla ya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri, hatuoni nafasi yoyote ya Mhe. William Vangimembe Lukuvi au yeyote aliyeachwa akipenya kwenye chujio la kumpata mgombea wa Uspika kupitia CCM. Itakuwa ni kama kuhamisha pesa kutoka mfuko wa shati kuweka wa suruali.

Ikumbukwe kuwa aliyebadili Baraza la Mawaziri kwa sababu alizoueleza umma ndiye pia Mwenyekiti wa CCM Taifa. Ndiye atakayeongoza vikao vya kimaamuzi katika kumpata mgombea wa Uspika.
 
Wala sidhani kama aliliongea ndio alilolifanya, sasa kitila mkumbo, mwambe, na waitala, nao walikuwa wanajiandaa na mbio za urais?mbona Mwigulu na January makamba wamebakia wakati hakuna asiyejua kuwa wao ndio vinara, hasa mwigulu?!!
 
Hapo ndipo jibu la moja kwa moja litapatikana, kama ikitokea Lukuvi na wenzake mmoja wao akawa spika wa bunge basi hakutumbuliwa kwa sababu ya kuutaka urais, lakini wakiukosa uspika itachukuliwa hiyo ndio sababu ya kuukosa uspika.

Kwasababu kwa utaratibu wa huko CCM, spika lazima aendane na msimamo wa mwenyekiti wake ambaye ndie Rais, hawawezi kufanya kazi kama wanatofautiana.
 
Hapo ndipo jibu la moja kwa moja litapatikana, kama ikitokea Lukuvi na wenzake mmoja wao akawa spika wa bunge basi hakutumbuliwa kwa sababu ya kuutaka urais, lakini wakiukosa uspika itachukuliwa hiyo ndio sababu ya kuukosa uspika.

Kwasababu kwa utaratibu wa huko CCM, spika lazima aendane na msimamo wa mwenyekiti wake ambaye ndie Rais, hawawezi kufanya kazi kama wanatofautiana.
Ni kweli Mkuu
 
Lukuvi ile clip ya kuwananga waislamu ndo imeharibiwa asahau kabisa kurudi jikoni.
Akaungane tu na sukuma gang waanzishe chama kipya cha siasa magufuli party
 
Ukiwa mwanasiasa chunga Sana kauli yako ya leo ndio ushindi au anguko lako kesho.Teknologia inatunza kumbukumbu.
Mtaji wa mwanasiasa ni mdomo wake
 

Attachments

  • VID-20220109-WA0001.mp4
    3.1 MB
Ndio maana mimi huwa naandika wazi wazi; Samia ni muongo, mnafiki, mtu wa makundi, na siasa za Mizengwe zilizotawala sana kipindi cha Jakaya Kikwete
 
Ndio maana mimi huwa naandika wazi wazi; Samia ni muongo, mnafiki, mtu wa makundi, na siasa za Mizengwe
Kumbe nilikuwa sahihi!!Lukuvi ana kazi naye nyingine, na prof majalala!!hahaaa kumbe ule ulikuwa ni mkwala tu ina maana alimanisha waitara na mkumbo ndio wanajiandaa kugombea 2025!!??
 
Kumbe nilikuwa sahihi!!Lukuvi ana kazi naye nyingine, na prof majalala!!hahaaa kumbe ule ulikuwa ni mkwala tu ina maana alimanisha waitara na mkumbo ndio wanajiandaa kugombea 2025!!??
Mama kajikosha tu, baada ya kusemwa kachemka ndo anatafuta vikazi visivyo na utaratibu kuwapachika

Ingekuwa lengo lake angetoa taarifa mapema sana
 
Tayari mama ameshamzuia asigombee, anaenda kukalishwa ikulu asome magazeti. Unampaje uspika mtu aliyepanga kuwa Rais? Anaweza kuitisha move akuondoe ili yeye akagombee. Bunge Lina mamlaka ya kumuondoa Rais, hivyo lazima uweke mtu mtiifu kwako
 
Ndio maana mimi huwa naandika wazi wazi; Samia ni muongo, mnafiki, mtu wa makundi, na siasa za Mizengwe zilizotawala sana kipindi cha Jakaya Kikwete
Mnafiq grade A, leo anasema hao wazee Ana Kazi nao baada ya kuambiwa waziwazi kuwa kachemka pumbavu sana siasa za tz
 
Back
Top Bottom