Sijaamini hadi nilivyoona vijana wamejiajiri kubet. Anashinda kibandani na mikeka hadi jioni

Kiuhalisia mtu aliyeserious na Betting humkuti ktk vibanda. Wengi wapo magetoni.. wanasuka mikeka mirefu (TRENI) then anatafuta hela za kunywea Bia ktk AVIATOR na games zingine za kubashiri.

Na wanapata hela nzuri tu... mtu anaweka laki5 anapata mil 7 ndani ya sikunde 20 tu.
Wewe upo ofisin mpk ufikishe hiyo mil 7 lini?..

Watu wanalipa hela za kodi, umeme, mafuta ya gari na hata kununua gari na viwanja, kusomesha etc kwa hela ya Betting...

Mbaya sana WANAWAKE ndio wataalam sahiv wakubeti.. jana nilikuwa na Pisi moja hivi ikatumiwa code na mwenzake kaweka leo asubuhi kala 50k ktk basket 😂 nimechoka.
 
Kila mtu na ajira yake
unafikiri akipata mishe zingine za kufanya atashinda betting
 
Kila mtu na ajira yake
unafikiri akipata mishe zingine za kufanya atashinda betting
Tatizo ameshaathirika..yaani mlevi kama mlevi wa betting au niiite gambling 🎰 kabisa. Yaani unakuwa umekufa umeoza kwenye kamari.

Kama hujawahi kuona mtu mtu amefall in love hutaelewa.

Kaka mmoja alinipenda sana. Alitongoza kwa kujiamini sana..akanikosa...akanihonga sana..yaani nikikohoa tu atafanya...amenitafutia kila alichoona nakitamani...hana hata ist ananiahidi Range..wanaume! Amekufa ameoza....ananioesha hata akaunti yake salio.....si akahamisha penzi kwenye betting...akawa ana weka mkeka million kwenye kubet.

Hata kazini amefukuzwa. Na anashinda vibandani.
 
Aisee, sa kwanini ulikula vya watu huku ukijua wewe huwezi kuja kumpenda
Onaa sasa amepoteza dira...
 
Umeharibu future yake badae utakuja kusema wanaume mbwa mwanaume akikupenda yuko radhi kufanya lolote akupe furaha, Dah so sad to him wewe ni shetani 😈.
 
Hali imekuwa mbaya, hakuna control orr regulation, lakin pia ni direct impact na result ya ufinyu wa ajira nchini
 
Sijaona mada yako inayobagaza wadangaji na udangaji...

Kwa mtazamo wako, unaamini udangaji ni mzuri kuliko betting?

Au hujui kama udangaji nao upo?

Au kwako ni bora udangaji kuliko ubetiji?

Lengo lako ni kubagaza wabetiji au kukemea maovu, kuwa wazi!
 
Ajira zinazotolewa na serikali ya ccm ni kiduchu sana kulinganisha na vijana walioko kwenye soko la ajira viwanda vya kuzalisha ajira za kutosha hakuna mtu hataki kuiba chaguo pekee linalobaki inakua ni kutandika mikeka tuu, waache maofisa ubashiri waendeshe maisha yao
 
Mnahukumu pasipo Akili ni yupi kituko kati ya wanasiasa wasiotosheka na ufisadi au hao wanaobet...kati ya anaye gawa bandari bure tena milele kwa kupewa phd za kuchambia na anaye cheza michezo ya kubeti nani ni mpumbavu hapo....kwa tanzania wapumbavu wakuu kabisa wanapatikana kwenye
1)SIASA NA MAMBO YA SIASA
2)DINI NA MAMBO YA DINI
3)SERIKALINI NA MAMBO YA SERIKALI.

💥💥💥hakuna wapumbavu zaidi ya hao kwenye hayo makundi matatu💥💥💥

Jiulize mtu anayetoa laki 5 kwa muhuni mwamposa na kiboko ya wachawi koko na anaye tumia laki 5 kubetia yupi ni mpumbavu haswa hapo ...tumieni akili ...je wewe ukitumia sh 50000 kwenda kutazama mpira wa simba na yanga na mimi nikitumia sh 50000 kubetia nani ni mwenye akili zaidi hapo..?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…