Nakushauri rudi tena Mvomero,kaa miezi mitatu kuna kitu muhimu utakigundua!Hii ya sasa ni nadharia,rudi tena ukafanye vitendo halafu uje hapa! Kaulize wazee kwa nini iliitwa Turiani!nilipata nafasi ya kuzungumza na wenyeji walisema ardhi ipo niwewe na Hela Yako.
Swadaktaaaa, Mimi Mara ya kwanza nilishangaa sana, nikasema mbona maeneo mengi, watu wapowapo tu. Nikaambiwa kaa kwa kutulia ndugu. Kuanzia hapa, hadi kuleeeeeee, eneo la mtoto wa mukulu aliyegoma kustaafu, alafu hapa hadi kuleeeeeeeeee la kamanda yule mstaafu, kuanzia hapa hadi unaikuta lami, la wale wenye mabasi ya red red.Kweli wewe unaijua Moro, mimi naifahamu Mvomero ngoja mtoa mada aje kutoa ushuhuda muda siyo mrefu! Eti wenyeji wavivu!Ameendeshwa na mhemko,papara,ushamba,ulimbukeni,kiburi n.k! Rudi tena kwa wenyeji wako wa Mvomero!
Mkuu mimi nalima miwa Vijiji vya Dihinda na Kaole, mbele kidogo ya shamba la mitiki la Mtibwa. Nataka kuja huko Mkulazi/mbigiri aiseee maana Mtibwa Sugar wanasumbua sana kwenye kununua miwa yetu kwa wakati, nitakurafuta.Hingera kwa kuamua kuoambana na kushare na wana JF fursa sio kila saa wawaze ngono tu.
Binafsi nimelima sana na kufanya biashara ya Mahindi Tunguli miaka 2005. Nimefika hadi huko Idibo na askari wake wale sungusungu walikuwa maarufu sana kipindi cha nyuma na tuliwatumia kutishia masai wakati wa mapigano ya wamasai na wakulima miaka hiyo.
Kwa upande wa Mvomero japo we umekosea ukaandika Mvumero nimelima sana huko na hata sasa nalima mpunga kwenye skimu ya umwagiliaji Dakawa chini ya UWAWAKUDA.
Nimefurahi kuona umefika hadi Maskati. Huko nilikuwaga na mchepuko wakati nahangaika kwenye biashara. Hapo Hembeti nikipataga mtoto mmoja mzuri sana miaka hiyo. Sasa ameolewa yule binti Tillya.
Niliishi sana Turiani maeneo ya Kilimanjaro nikichezea Mtibwa Sugar kipindi hiko tukiwa na akina Mkangwa na Zuberi Katwila.
Huko fursa nje nje bro. Njoo tulime mpunga hapa Dakawa au tulime miwa tuuze Mkulazi au tulime nyanya mateteni, Mbigili na Dumila.
Bei ya shamba kwa ekari moja ni kiasi gani huko kwa wastani?Wakati mwingine uje na Kilosa nikutembeze vijijini ujionee fursa za wazi kuanzia:-
Dumila na mateteni-kilimo Cha Nyanya
Kilangali, Tindiga, Kivungu- Kilimo Cha mpunga
Zombo, Ulaya-kilimo Cha mahindi
Lumuma, Pwaga, Mnozi, Ruaha mbuyuni, Kitati, Kidete n.k - kilimo Cha vitunguu na Mahindi
Sehemu zote hizo mazao mchanganyiko kama mbaazi, ufuta, kunde, maharage, alizeti n.k yanalimwa sana pia ufugaji wa kuku, Bata, kanga, mbuzi, nguruwe, Ng'ombe, punda n.k
Karibu Kilosa
Aiseee 😂😂Nina heka 200 handeni ndugu, ardhi safi, maji ya kuchimba, nina tractor na nimesafisha 40 hela 20 sasa, nilichezeshwa mno, nikatafuta wambulu 3 ( nao si haba kishirikina ) nikawanunulia na mifugo, siwalipi, wanajiendesha kwa tractor, mifugo na vibarua, na nimewapa target wasafishe angalau hela 150
Mimi Kule sitarudi mpaka Wageni wewe wengi!
Inategemea unataka kulima niniBei ya shamba kwa ekari moja ni kiasi gani huko kwa wastani?
Sawa mkuu ila kama ni uchawi potelea pote.Nakushauri rudi tena Mvomero,kaa miezi mitatu kuna kitu muhimu utakigundua!Hii ya sasa ni nadharia,rudi tena ukafanye vitendo halafu uje hapa! Kaulize wazee kwa nini iliitwa Turiani!
Acha hizo za negativity. Mwaka 2009 nilitaka kuwekeza kwenye biashara ya mbao maeneo ya Mkolani au Buhongwa hapa Jijini Mwanza. Nikaenda kuomba ushauri kwa ndugu yangu mmoja ambaye alikuwa mwekezaji na mkazi wa maeneo hayo. Alinikatisha tamaa sana, nikaacha kuwekeza kipindi kile.Mkuu nakushauri nmezaliwa morogoro na kukulia morogoro wilaya ambayo sikushauri uwekeze kilimo ni gairo kilimo nenda kilombero mlimba malinyi na mvomero na kilosa baadhi gairo n ufugaji basi
Ni kweli pazuri mnoPazuri kwakweli 🙌🏾
Huyo kama kazaliwa pale ndo wale wale wavivu. Achana nae na asikupunguzie mwendo.Acha hizo za negativity. Mwaka 2009 nilitaka kuwekeza kwenye biashara ya mbao maeneo ya Mkolani au Buhongwa hapa Jijini Mwanza. Nikaenda kuomba ushauri kwa ndugu yangu mmoja ambaye alikuwa mwekezaji na mkazi wa maeneo hayo. Alinikatisha tamaa sana, nikaacha kuwekeza kipindi kile.
Ninachojua, kwenye dunia hii hakuna free milk. Maisha popote pale ni kupambana. Wacha tumpe moyo kijana apambane.
Pamoja sana mkuuMzee tunashukuru sana kwa hilo.
Huko chimbo tutaenda..na kuangalia na kupafanyia kazi.
Mimi nipo Kigoma sasa.
Ngoja tupige mshindo wa betting Mkuu tutanunua na trekta ni ma big big plan tu.Nchi inafulsa hii.. Vijana kazi kwetu kuzichangamkia .
Uoga tu wakati angekuwa verified user pengine angepata wadau wakufanya naye mambo makubwa zaidi, pengine hata angeenda watafutia mashamba hukoNa ni kwanini ufiche sura kijana
Imenipa motisha ya kuja kufanya uwekezaji mkubwa katika ardhi na kilimo hapo mbeleni.Nilivyoona tu hata robo yake Bado hatuja yamaliza mkuu. Na huo uwekezaji wanao fanya ni kupata chakula na Hela ya mboga basi
Panafaa mkuuImenipa motisha ya kuja kufanya uwekezaji mkubwa katika ardhi na kilimo hapo mbeleni.
Hakuna mbadala mkuu wenyeji ni wavivu 90% utajua yote hayo nakwambia na mengine mengi ambayo hujayaandika ukweli ni kwamba ninyi ni wavivu.Kweli wewe unaijua Moro, mimi naifahamu Mvomero ngoja mtoa mada aje kutoa ushuhuda muda siyo mrefu! Eti wenyeji wavivu!Ameendeshwa na mhemko,papara,ushamba,ulimbukeni,kiburi n.k! Rudi tena kwa wenyeji wako wa Mvomero!