Sijaona sababu za TAKUKURU kumshikilia Mkurugenzi TPA

Sijaona sababu za TAKUKURU kumshikilia Mkurugenzi TPA

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2019
Posts
762
Reaction score
6,984
Ipo haja yakubadili mfumo wetu wa utendaji kazi kama nchi ikiwemo vyombo vya dola. Mkurugenzi wa TPA alikuwa na riport au matokeo ya ukaguzi toka ilipofanyika exit meeting. Alielewa Kuna maeneo kuna mianya iliyopelekea mkaguzi kutengeneza hoja zilizokosa ushahidi wakuzifuta nakupelekea hoja hizo kuingia kwenye kitabu Cha taarifa ya CAG ya mwaka 19/20.

Taarifa ile iliposomwa kwa Mhe. Rais haikuelekezwa kamata, ilielekezwa uchunguzi ufanyike na matokeo yapelekee kuchukua hatua.

Kwa suala hili lilivyokaa hakuna namna TAKUKURU wanaweza kusema ndani ya masaa machache waliweza kupata nakala ya riport, wakaangalia hoja, wakupata mapungufu au dosari zakupelekea kuhoji na kisha kumkamata Mkurugenzi kwa mahojiano na kisha kumshikilia.

Uchunguzi wa hoja za CAG nitofauti na uchunguzi wa wizi wa kawaida, CAG kabla ajatoa taarifa tayari wahusika waliokaguliwa wanakuwa wanajua tatizi lililopo na mapungufu yake.

Naamini TAKUKURU walichofanya siyo professional task waliyoelekezwa bali wamekwenda kutisha nakuonyesha makucha. Walipaswa kumpa wito afike baada ya wao kufanya ground work nakuona yeye anahusikaje na wanapohoji Basi wajikite kwenye facts.

Sitaki kuwafundisha ila naamini wanakosea sana na hii ni moja ya sababu zinazopelekea hata wanapofika mahakamani wanakwama kwa technicalities. Unamkamata mtuhuma Leo ukijua ujaandaa hoja za mahojiano, unalazimika kumweka mahabusu nje ya muda wakisheria uliowekwa na mwisho wa siku unajikuja umeandika maelezo mara tano wakati ungetumia taaluma vizuri ungeandika maelezo once na ukafile case panapohusika.

Kwanini nimeweka andiko ili hapa, nataka kuvikumbusha vyombo vya dola visiwekeze kuzuia watu mahabusu bali viwekeze kukusanya ushahidi kabla yakukamata. Kama huyu boss wamekimbilia kumkamata then waanze uchunguzi, vipi kuhusu wanyonge wana Hali gani mahabusu za polisi na Magereza?

Tubadilike, tumewajaza wenzetu wasio na hatia mahabusu kwa sababu yakukimbilia kukamata then ndipo tuanze uchunguzi. Madhara yake tunapeleka holding charges mahakamani tukitapatapa kutafuta makosa nakuwaacha watu wanasota mahabusu bila dhamana na bila tuhuma zinazoeleweka.

Tupige Vita kauli mbiu ya uchunguzi unaendelea huku watuhumiwa wakiwa mahabusu. Fanyeni kwa taaluma siyo kwakutaka mwonekane mnajua kutesa watu.
 
Nakubaliana na wewe.

Huku kwetu badala wachunguze ndio wakamate, wao wanakamata huku hawajaanza uchunguzi, wanakusumbua na mwisho wa siku wanakosa ushahisi wanakuachia.

Tayari walishakupotezea muda, kukudhalilisha na kukutengenezea msongo wa mawazo.

Repoti za kikaguzi mara nyingi sio za kiuchunguzi, hutoa tuhuma general kutokana na ukiukwaji wa taratibu za ndani za taasisi.

Huku kwetu TAKUKURU/Polisi hawana weledi wa uchunguzi, ni kuonea watu, kuwabambikia kesi, vitisho, na sasa wana sheria ya uhujumu uchumi basi kila kitu ni kuhujumu uchumi, mkitongozana mkashindwana ni kuhujumu uchumi.

Dunia nzima ni investigate and then arrest, huku kwetu ni arrest and then investigate.
 
Wewe kakoko aka kamugisha...

Wewe ulivyokuwa unasweka watu Central kimagumash hukujua haya ?
Je, umetesa watu wangapi na dhulumu wangapi na familia zao ?
Vendors wangapi hadi Leo wanateseka na kulia sababu yako...

Malipo hapa hapa duniani payback time ndo hii...

Wewe ndo wa kujiita mnyonge?? Nyambaf
 
Ulishawahi kujiuliza ni team gani huwa inamsaidia CAG kukusanya taarifa?

Are you really familiar with the chain of command of the office of CAG in Tanzania? Bara na Visiwani?

Unafahamu ni “special tasks forces” za aina ngapi zinahusishwa during the investigating and collecting of the report?

In short we have NAOT (The National Audit Office of Tanzania), which is the Supreme Audit Institution of the URT, headed by the CAG!

Anahojiwa, sio mahabusu!
 
Kukamatwa Kakoko siyo kwa sababu yuko guilty, bali amekamatwa kama mshukiwa. Upotevu wa sh billioni tatu siyo mdogo. Haiwezekana kiasi kikubwa kama hicho kikapotea bila mkurugenzi mkuu kujuwa. kama kweli alikuwa hajui basi hiyo kazi imemzidi kimo inabidi aachie ngazi.

Kama alijuwa na kunyamaza basi huenda anakula nao. Ni dhahiri kuwa uchunguzi hauwezi kufanyika na kufanikiwa wakati yeye yuko huru anarandranda mitaani.

Kwa hiyo kukamatwa kwake wakati wa uchunguzi ni muhimu. Kubmbuka hiyo siyo kesi ya wizi wa kawaida. Sijui kama ulimsikia mama Samia! alisema "sijui alyeiba hiyo pesa alikuwa na nia gani".

Read between the lines and try to understand what she meant. Hiyo ni pesa tosha ya kuifanyia uharamia TZ. Je walitaka kuitumia kwa malengo yapi. Ni kweli watu wanaiba, lakini unaiba billioni tatu!
 
Mbona yule aliyekuwa anawakashifu viongozi Wastaafu hawajamkamata?.
 
Unajifanya unaelewa kumbe huna lolote. Takukuru sio wajinga kuchukua hatua Kama hiyo tayari wamefanya investigation. Huwezi kufanya upelelezi wakati mshukiwa Yuko huru anaweza kukwamisha zoezi la kupata data. Na ukumbuke Takukuru wanamshikilia kwa mahojiano na sivinginevyo
 
Tuacheni Unafiki hakuna Mtanzania ambaye akiwekwa katika Nafasi fulani au akipata Wadhifa kwenye Sekta yenye Pesa hatoiba.



Duuh, hao wezi wanapaswa kuuawa wote mpaka waishe.
Na mali zao zitapanywe .
Ni bora nchi ibaki tupu kuliko kuwa nchi ya wezi.
 
Tuacheni Unafiki hakuna Mtanzania ambaye akiwekwa katika Nafasi fulani au akipata Wadhifa kwenye Sekta yenye Pesa hatoiba.
Don't claim ndugu yangu people differ in their personalities. When come the public interest you must surrender your selfish traits for the welfare of your fellow. Note, wapo watu wanaweza kulitumikia bila makashifa makubwa ya rushwa
 
Na hii ndo maana kesi nyingi za TAKUKURU zinafeli mahakamani ikifika pale pa kuleta mashahidi.
 
Back
Top Bottom