TUHUMA ZA UGAIDI ZA MBOWE ZINAWEZA KUWA NA UKWELI WOWOTE?
Mwenyekiti wa CHADEMA Ndugu yangu Freeman Mbowe ametiwa hatiani na polisi kwa tuhuma za ugaidi na kupanga njama za kutaka kuua na kudhuru viongozi wa Serikali. Mbowe alitiwa mbaroni akiwa Jijini Mwanza.
Toka namfahamu Mbowe amekuwa na siasa za aina hiyo, siasa za zilizojaa ukakasi mkubwa, siasa za kuwajaza upepo wanachama wake huku akiwadhuru wote wanaoenda kinyume na matakwa yake na wale wanaohatarisha uenyekiti wake ndani ya CHADEMA.
Tunakumbuka jinsi Chacha Wangwe, mwanasiasa kijana aliyechipukia miaka ya 2005 alivyofariki kwenye kifo chenye utata mzito baada tu ya mwanasiasa huyo kuonyesha nia ya kutaka kugombea Uenyekiti wa CHADEMA ili kumuondoa Mbowe. Alipitia nyakati nzito mpaka kufikia kifo chake cha ajari ya gari ambacho kilihusishwa moja kwa moja na nia yake ya kutaka kumng'oa madarakani Bwana Mbowe.
Baada ya Chacha Wangwe, ikafuata zamu ya Zitto Kabwe ambaye nae pia licha ya kuwa mwanasiasa kijana machachari ndani ya nchi na CHADEMA na ushawishi wake wa kutaka kumng'oa Mbowe, pia akakutana na masaibu ya kutosha ndani ya Chama hicho huku akizushiwa kashfa nzito na viongozi ndani ya CHADEMA mpaka kufika hatua ya kufukuzwa ndani ya CHADEMA na kutishiwa mara kadhaa kuuawa kwasababu tu ya nia yake ya kutaka kugombea kwenye nafasi ya Uenyekiti. Naye Zitto Kabwe akapata matatizo mazito kwa dhamira yake hiyo ya kutaka kugombea na mwisho akafukuzwa CHADEMA.
Mwisho ikawa kwa Mbunge wa Ndanda Mhe Cecil Mwambe ambaye naye baada ya kuonyesha nia ya kutaka kugombea Uenyekiti wa CHADEMA akaanza kutukanwa na kutishiwa maisha yake na viongozi na wanachama wa CHADEMA kwa sababu tu ya kufuata utaratibu wa kidemokrasia ndani ya Chama hicho kutaka kumng'oa Mbowe. Akabananishwa mpaka akaamua kukikimbia Chama hicho kwenda CCM. Alipitia masaibu yote hayo kisa tu kutaka kugombea Uenyekiti wa CCM.
Huyo ndiyo Mbowe ninayemfahamu Mimi na siasa zake.
Zaidi sikushangaa tuhuma za Mbowe kuhusika na ugaidi na njama za kutaka kuua na kudhuru viongozi kwa kuangalia mfululizo wa kauli zake zilizojaa uchochezi, uvunjifu wa amani, uhaini na uchonganishi mzito zilizowahi kutoka kwenye kinywa chake.
Mwaka 2016, Mbowe na wenzake wakaja na operesheni waliyoiita UKUTA ambayo Mbowe alitoa kauli nzito na chonganishi za kutaka kuchochea vurugu ambapo Mbowe mwenyewe alikubali kuitwa mchochezi huku akiwa na mfululizo wa kauli zilizojaa siasa za chuki, kichochezi na zinazohamasisha vurugu ndani ya nchi.
Unakumbuka jinsi Mbowe alivyosimama kule Mbeya na kuwaambia wanachama wake kwamba kwasasa ni lazima waunganishe nguvu ya umma kwa staili ya Libya na Misri? Na kudai wakubali kubeba majeneza kwa kusema "mapambano nchi hii hata kama Watanzania 100 watakufa lakini lazima tukubali kubeba majeneza." Hiyo ilikuwa Januari mwaka 2018.
Na mfululizo wa kauli zake za vitisho kwa vyombo vya ulinzi na usalama?
Kwahiyo kwa haya tu machache ninayomfahamu Bwana Mbowe, basi nakiri sijashangaa wala kushtuka Mbowe kutiwa hatiana na tuhuma za ugaidi na njama za kuua au kudhuru viongozi kwa sababu hizo ndizo aina za siasa za Bwana Mbowe. Anyway, tusubili mahakama itoe maamuzi yake.
Mwenyekiti wa CHADEMA Ndugu yangu Freeman Mbowe ametiwa hatiani na polisi kwa tuhuma za ugaidi na kupanga njama za kutaka kuua na kudhuru viongozi wa Serikali. Mbowe alitiwa mbaroni akiwa Jijini Mwanza.
Toka namfahamu Mbowe amekuwa na siasa za aina hiyo, siasa za zilizojaa ukakasi mkubwa, siasa za kuwajaza upepo wanachama wake huku akiwadhuru wote wanaoenda kinyume na matakwa yake na wale wanaohatarisha uenyekiti wake ndani ya CHADEMA.
Tunakumbuka jinsi Chacha Wangwe, mwanasiasa kijana aliyechipukia miaka ya 2005 alivyofariki kwenye kifo chenye utata mzito baada tu ya mwanasiasa huyo kuonyesha nia ya kutaka kugombea Uenyekiti wa CHADEMA ili kumuondoa Mbowe. Alipitia nyakati nzito mpaka kufikia kifo chake cha ajari ya gari ambacho kilihusishwa moja kwa moja na nia yake ya kutaka kumng'oa madarakani Bwana Mbowe.
Baada ya Chacha Wangwe, ikafuata zamu ya Zitto Kabwe ambaye nae pia licha ya kuwa mwanasiasa kijana machachari ndani ya nchi na CHADEMA na ushawishi wake wa kutaka kumng'oa Mbowe, pia akakutana na masaibu ya kutosha ndani ya Chama hicho huku akizushiwa kashfa nzito na viongozi ndani ya CHADEMA mpaka kufika hatua ya kufukuzwa ndani ya CHADEMA na kutishiwa mara kadhaa kuuawa kwasababu tu ya nia yake ya kutaka kugombea kwenye nafasi ya Uenyekiti. Naye Zitto Kabwe akapata matatizo mazito kwa dhamira yake hiyo ya kutaka kugombea na mwisho akafukuzwa CHADEMA.
Mwisho ikawa kwa Mbunge wa Ndanda Mhe Cecil Mwambe ambaye naye baada ya kuonyesha nia ya kutaka kugombea Uenyekiti wa CHADEMA akaanza kutukanwa na kutishiwa maisha yake na viongozi na wanachama wa CHADEMA kwa sababu tu ya kufuata utaratibu wa kidemokrasia ndani ya Chama hicho kutaka kumng'oa Mbowe. Akabananishwa mpaka akaamua kukikimbia Chama hicho kwenda CCM. Alipitia masaibu yote hayo kisa tu kutaka kugombea Uenyekiti wa CCM.
Huyo ndiyo Mbowe ninayemfahamu Mimi na siasa zake.
Zaidi sikushangaa tuhuma za Mbowe kuhusika na ugaidi na njama za kutaka kuua na kudhuru viongozi kwa kuangalia mfululizo wa kauli zake zilizojaa uchochezi, uvunjifu wa amani, uhaini na uchonganishi mzito zilizowahi kutoka kwenye kinywa chake.
Mwaka 2016, Mbowe na wenzake wakaja na operesheni waliyoiita UKUTA ambayo Mbowe alitoa kauli nzito na chonganishi za kutaka kuchochea vurugu ambapo Mbowe mwenyewe alikubali kuitwa mchochezi huku akiwa na mfululizo wa kauli zilizojaa siasa za chuki, kichochezi na zinazohamasisha vurugu ndani ya nchi.
Unakumbuka jinsi Mbowe alivyosimama kule Mbeya na kuwaambia wanachama wake kwamba kwasasa ni lazima waunganishe nguvu ya umma kwa staili ya Libya na Misri? Na kudai wakubali kubeba majeneza kwa kusema "mapambano nchi hii hata kama Watanzania 100 watakufa lakini lazima tukubali kubeba majeneza." Hiyo ilikuwa Januari mwaka 2018.
Na mfululizo wa kauli zake za vitisho kwa vyombo vya ulinzi na usalama?
Kwahiyo kwa haya tu machache ninayomfahamu Bwana Mbowe, basi nakiri sijashangaa wala kushtuka Mbowe kutiwa hatiana na tuhuma za ugaidi na njama za kuua au kudhuru viongozi kwa sababu hizo ndizo aina za siasa za Bwana Mbowe. Anyway, tusubili mahakama itoe maamuzi yake.