Tuishi kwa umakini sana mkuu.Sure mkuu, mikoani wapo serious sana na hizi vita π π
Post namba ngapi mkuu sijapata notificationNdio mkuu. Mbona nimekutag?
Ahahaaaaa...![emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]....! Nimecheka sana anatukana kichini chini. Na tabasamu la mamba3rd Portion:
... Maelezo ambayo nilikuja kupewa baadae na head prefect, ni kuwa inaonekana mshua alinitafuta sana kwenye simu kabla hajaenda pale shule, ila hakufanikiwa kunipata. Kwavile hatujawasiliana muda mrefu, na akisema arudi kijijini, maana yake utapita muda mrefu mwingine bila kuonana, ndio akaona afunge safari mpaka shule. Kufika pale akajitambulisha kama mzazi wangu, na akaomba kuonana na mimi. Walim wakashangaa, mzazi wake Analyse?, Wewe ni baba yake mkubwa au mlezi? Dingi akawa hajaelewa. Akawaambia yeye ni Mzee wangu kabisa, Mwalim wa nidham akaona mshua anamletea masihara, ili swala la wanafunzi kuleta wazazi feki inabidi likomeshwe, akamwambia Mzee akae kwenye benchi. Baada ya kushauriana na mkuu wa shule, wakataka kumpeleka Mzee Polisi. Mshua akawakazia, walivyoona yupo serious sana, wakamuomba ID yoyote.
Akawapa voters ID, walivyoona mfanano wa majina, walim wakachoka. Ikabidi waanze kuulizana, kama wewe ndio baba yake, yule aliyekuja nae ni nani? Hapo ndio wakampa picha nzima. Mzee akacheka (Mzee wangu akiwa na hasira sana, kuna kicheko fulani kinakujaga automatically). Mwisho wa siku wakaazimia head prefect awe ananipigia simu mara kwa mara, akinipata, anipe zile taarifa za kuhitajika shule kwa ajili ya usajili. Na ahakikishe ananishawishi niende na mzazi niliyempeleka last time.
Walimu walikuwa na shauku ya kuniona Mimi maana nimecheza na akili zao, ila Mshua target zake ilikuwa ni kumuona yule mzazi niliyempeleka badala yake. Mwamba Sina ili wala lile, kesho yake nikapanda Simba Mtoto, safari ya shule ikaanza. Nilivyofika, nikaunga moja kwa moja mpaka nguvu mali, nikapoa kwa mshikaji wangu pale Galanosi, kesho yake asubuhi, tukabebana Mimi na yule Mchaga hao mpaka shule.
Ile shule ilivyo, ukishaingia kupitia main entrance, unakata upande wa kulia, ndio kuna ofisi za walim pamoja na head master. Upande wa kushoto, kulikuwa na korido inayoelekea madarasani, lakini pia mwanzoni kuna njia ya kwenda vyooni, na ngazi za kuelekea madarasa ya juu. Sasa kwenye hizi ngazi ndio alikuwa kakaa Mshua ananisubiria Mimi na baba yangu tufike. Na sisi tulivyofika, direct tukakata kona kulia, hatukuangalia nyuma. Mzee akatuungia tela mdogo mdogo. Machale ni kama yalinicheza hivi, nikapata hisia zinaniambia geuka nyuma, kugeuka nakutana na Mshua kakaza sura kimtindo, mikono yote miwili kaikutanisha nyuma ya makalio, kama wanavyopendaga kutembea wazee. Alipoona nimegeuka, akasimama kwa muda Nikapatwa na mshtuko, maana sikutarajia kumuona pale, nikajikuta nimeita "Baba?". Yule Mchaga alikuwa bado hajausoma mchezo, akaitikia "Naam jembe langu". Ila alivyogeuka, na kukuta nimeelekeza attention kwa mtu mwingine, akili yake ikaload faster, akajikuta anatukana kichini chini "Ku***na walai".
Mshua akawa anamuangalia tu, huku kaweka tabasam la mamba. Mchaga akapiga hesabu za haraka, akaona hapa akiingia ofisini, basi hatoweza kutoka, anaweza akaishia polisi. Akapitisha wazo la kutoweka eneo lile, ila njia peke rahisi ni kupitia upande aliosimama Mshua, pia japo shule haikuwa na fensi, ila kukimbilia upande waliopo wanafunzi inaweza ikawa msala zaidi, maana wanafunzi hawana dogo. Akaamua kurudi na njia tuliyojia, upande aliosimama Mshua. Kosa alilofanya Mchaga, alim-underestimate Mshua, labda alijiona yeye kijana zaidi akijilinganisha nae, so angemzidi nguvu. Mchaga alitoka speed ghafla, mshua akawahi kumrukia, wakavaana mpaka chini. Kitendo cha kuanguka chini tu, Mshua kama kawaida yake, akamuwahi Mchaga na kabali moja matata. Mchaga kila akirusha ngumi, Mshua hana habari, ndio kwanza anazidi kukaza mikono. Wanafunzi wakajaa madirishani, kelele zikazagaa eneo lile, wengine wakaanza kutoka madarasani kuja kushuhudia kwa ukaribu.
Walim ikabidi waanze zoezi la kuwaachanisha, walipofanikiwa, Mchaga macho yalikuwa mekunduu kama katoka kulala au kulia. Walim wakawa wanafukuza wanafunzi warudi madarasani, Kisha wakawaomba Baba na yule Mchaga waende ofisini kwa mazungumzo, maana kwa umri wao haifai kushikana mashati namna ile. Wakiwa wanakaribia mlango wa ofisi ya walim, yule Mchaga aligeuka, akatoka speed, akaelekea upande zilipo hostels za wanafunzi wa advance, akapita kwenye senyenge, alivyotokea upande wa pili, akaongeza speed, akapotelea kwenye makazi ya watu. Hakuna hata mwalim aliyejisumbua kumkimbiza, wakabaki wanamwangalia tu. Ila wanafunzi ndio wakawa wanamzomea. Jamaa akasepa, msala nikabaki nao peke yangu. Kikao kikafanyikia ofisi ya walimu wote, mwanenu nikapigishwa magoti huku nasemwa..
Ubaya wa ofisi ya walimu, hata yule mwalim ambae hakujui, lazima apate cha kukuongelea. Nilitembezewa fimbo za kufa mtu siku ile, japo mshua hakunipiga, ila alichangia pakubwa sana kuikuza adhabu yangu, maana aliongea mengi sana, kiasi kwamba nikaonekana kituko. Mshua alilipa ile hela ya faini, nikaruhusiwa kwenda darasani. Aliamua kuondoka siku hiyo hiyo, hakujisumbua kuongea na Mimi baada ya kutoka mle ofisini, na hakunipa hata shiling 10 Kwa ajili ya matumizi pale shuleni. Kiufupi aliniacha kikauzu sana. Nimeingia class sina mzuka hata kidogo, mda wote nimelala kwenye dawati. Mida ya mchana baada ya msosi, nikaamsha zangu kuelekea hostel. Nikalala mpaka mida ya jioni.
Wakati natoka kula msosi wa usiku shuleni, yule jamaa yangu wa Galanosi akanipigia simu, anauliza nimemfanya nini Mchaga? Maana kakutana nae ana nundu kwenye kona ya uso, alaf kamuahidi kwamba siku akikutana na Mimi, sitokaa nimsahau maishani mwangu kwa atakachonifanya. Ikabidi nimuelezee kwa ufupi yaliyojili. Jamaa alicheka sana, mwishowe akaniambia nikienda shuleni kwao niende kwa tahadhari, maana Mchaga alimaanisha alichokisema. Tukaishiana hapo, then nikaenda chamber kupiga msuli. Tokea siku ile nikaanza kupiga sana msuli, sikuwa na msala mwingine wowote, japo walimu waliendelea kuwa wananizingua hapa na pale, ila niliamua kuwa mpole.
Mshua hakuwahi kunitafuta tena, sio kwa simu wala msg. Ni kama alinizila. Kipindi tunakaribia kufanya mtihani wa mwisho, nikaanza kumfukuzia demu mmoja wa O level pale pale shuleni, alikuwa mweupe, sauti nyembamba na kishundu fulani cha kuvunjia shingo, maana akikupita lazima ugeuke. Siku moja nimekaa nae maeneo ya garden mida ya jioni, naendelea kuingizia mistari, maana alikuwa bado hajaeleweka. Katika maongezi akaniambia "Wewe hapa Tanga sio kwenu, unasema unanipenda, wakati siku sio nyingi utamaliza shule, utaacha umenitumia alafu utaondoka".
Nikamjibu kuwa mgeni Tanga hainizuii Mimi kumpenda yeye, umbali sio kikwazo kwangu. Akaniuliza "Unamaanisha unachosema? Kuwa utarudi kwa ajili yangu?, Niambie ukweli, sitaki uongo". Nikasita kidogo kutoa jibu, yeye akaendelea "Mimi ninachohitaji kujua ni Nia yako tu, kama kweli utataka kurudi, mimi nitakurudisha". Ile kauli ikanimakinisha kidogo, nikamuuliza "Utanirudisha kivipi? " Akajibu "Wewe ilo niachie Mimi, je ni kweli unanipenda na ungependa kurudi kwa ajili yangu, nikurudishe??
Nikabaki nimeduwaa kwa muda, najiuliza "Huyu anaongelea nini?".....
Endelea hapa Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu. Mpaka siku niliyokutana na yule Mzee
herio9th Portion:
.....Bi Mkubwa ikabidi aniulize kwa upole tu "Tuambie mwanangu, huyu jamaa unashida nae ipi?". Nikaendelea kuwa kimya tu kwa muda. Fikra ndio zikaanza kunituma, huenda kuumwa kwangu yule Kisauti akawa anahusika. Nilikuwa nishamsahau kabisa. Nilipatwa na hasira kuona nateseka kwa kosa lisilokuwa langu. Mshua alivyoona bado nipo kimya, sijamjibu Mama chochote, akanyanyuka na kuanza kuondoka. Bi mkubwa akamuuliza
Bi Mkubwa: "Baba nanii unaenda wapi sasa?
Mshua: "Sasa mtu haongei, nitakaa hapo siku nzima?"
Bi Mkubwa: "Unajua ili ni tatizo kubwa sana, usilifanyie mzaha"
Mshua: "Mzaha anaufanya huyo hapo, katibua watu mjini huko, karudi kutupa sisi shida"
Bi Mkubwa: "Kwahiyo tumuache afe"
Mshua: "Na akiendelea kukaa kimya, atakufa kweli"
Nilivyoona mzozo utaenda kuwa mkubwa, ikabidi niwafungukie issue nzima ilivyokuwa. Baada ya hapo wakaanza kujadiliana nini kifanyike. Bi Mkubwa akashauri wampigie simu Kisauti ili kumuomba msamaha, Kisha waangalie namna gani wanalimaliza lile jambo. Ila Mshua akagoma.
Bi Mkubwa: "Mwanao hali yake sio nzuri huyu, tuwasiliane na mdeni wake, tumlipe yaishe"
Mshua: "Hatuwezi lipa hela ambayo hatujachukua. Huo ni unyonge, na siwezi kuufanya. Dawa ya moto ni moto, kwavile kaanza yeye, acha tuendeleze, ngoja niwasiliane na Mzee Taba, ili tumpeleke kwa mtaalam"
Bi Mkubwa: "Mwanangu haendi kwa mtaalam wala kilingeni, kesho asubuhi naenda nae kanisani kwenye maombi"
Mshua: "Kwa hali ilivyo, lazima twende tu, na ilo halina mjadala"
Ukatokea mvutano mwingine pale, wapi nipelekwe hiyo kesho. Ila Mshua kutokana na commanding force yake, ikaamriwa nipelekwe kwa mtaalam. Kesho yake asubuhi na mapema tukaenda hadi kilingeni. Bi Mkubwa nae hakutaka kubaki nyumbani, alitaka awe na Mimi muda wote ili kujua hatma yangu.
Kufika kwa mganga tukapokelewa vizuri. Kutokana na hali niliyokuwa nayo, nikapewa kipaumbele kuonana na mtaalam. Tulivyoingia ndani, akaanza kuweka vitu vyake sawa, ongea ongea mambo yake pale.
Kuna muda nadhani alipandisha mashetani, maana lafudhi ilibadilika. Yeye ni mtu wa Kanda ya ziwa, ila ghafla akaanza kuongea lafudhi ya kimasai. Kuna mtu mwingine ambae ni msaidizi wake, ndio akawa anasaidia mwongozo wa yaliyokuwa yanaongelewa. Zoezi lilidumu kama nusu saa, then akarudi normal. Bila hata sisi kuongea sana, akaniambia, "Kijana unabahati sana kuendelea kuliona jua mpaka muda huu. Wapinzani wako, dhamira yao ni ya dhati". Mshua akauliza, kwahiyo nini kifanyike?. Yule mtaalam akasema kwasasa kuna kitu inabidi nimfanyie ili kudhibiti maumivu, alaf usiku ndio tutafanya zoezi kamili la kumtoa kwenye hii hali". Mshua akasema sawa, hakuna shida.
Mtaalam akaanza kufanya kazi yake pale. Mle ndani kulikuwa na kinu kikubwa kama vile wanavyotwangiaga wanawake, ila chenyewe kimechakaa sana, yawezekana ni cha muda mrefu, na rangi yake ilikuwa nyeusi tii, na mistari mistari myeupe. Sasa baada ya mtaalam kufanya mambo yake, akataka kupanda juu ya kile kinu, sikujua dhumuni lake lilikuwa ni lipi, maana wote mle tulibaki kuwa watazamaji tu. Wakati yupo juu ya kile kinu, alianguka yeye na kinu chake na kutanguliza uso chini. Alivyofika chini, kimya kikatawala. Urefu alioanguka ulikuwa mdogo sana, hata mtoto mdogo angeweza kusurvive, ila cha ajabu mganga alizimia. Yule msaidizi wake ndio akamkimbilia ghafla na kumnyanyua. Akachovya ule usinga kwenye kibakuli fulani kilikuwa pembeni, alaf akaanza kumpiga nao, huku anaongea maneno ambayo sikuyaelewa. Baada ya muda, mtaalam akaamka, anaongea ila sauti inatoka kwa mbali sana kama kakabwa au ametoka kukabwa.
Muda huo wote, sisi tupo kimya tu. Fahamu zilipomrudia vizuri na kuwa na utimamu wake. Akatwambia kwa upande wake, ili zoezi lipo nje ya uwezo wake, yani limemshinda. Akatuelekeza kwa mtaalam mwingine, aliyekuwa kijiji cha pili ambaye anaweza kutusaidia. Mshua na Bi Mkubwa wakawa wanajadiliana, Mshua anauliza kama twende siku hiyo hiyo, au kesho yake, ila Mama anataka turudi nyumbani. Yule mtaalam akawaambia, kadiri mnavyochelewa, ndivyo mnavyojisogeza kwenye kilio. Muwahisheni huyu, vinginevyo mtamkosa.
Bila kupoteza muda, tukafunga safari mpaka kwenye hicho kijiji. Tukaulizia hadi tukafanikiwa kumfikia yule mganga. Kutokana na miundombinu ya kijijini ilivyo, tulijikuta tunafika pale jua likiwa limeshaanza kupungua nguvu.
Tulipokelewa vizuri na msaidizi, tukakaa foleni kusubiria zamu yetu ifike.
Mida ya saa kumi na mbili kasoro, ndio tukafanikiwa kuonana nae. Hapo Bi Mkubwa nafsi haijamtulia kabisa. Muda wote kama ana mashaka na mganga. Ile hali ya Bi Mkubwa ikawa inamkera yule mtaalam. Akatwambia "Kuna hii dawa, ili zoezi lifanikiwe, inabidi wote watatu muilambe". Akaanza kutaka kumpa Bi Mkubwa, Mama akasita kidogo. Yule mganga akamkata jicho. Ikabidi Bi Mkubwa akubali kuilamba. Cha ajabu baada ya Bi Mkubwa kuilamba, sisi wengine hatukupewa. Bi Mkubwa akahoji kulikoni? Yule mganga akatoa usinga na kumpiga nao kichwani, Bi Mkubwa akasombwa na usingizi. Mimi na Mshua tukajikuta tunatazamana tu bila kusema chochote.
Baada ya salamu, akatwambia "Poleni sana na safari, maana huku tulipo ni mbali sana na mlipotoka". Baada ya kumuelezea dhumuni letu la kuwa pale, nae akafanya standard procedures zao (naziita standard procedure maana kote nilipoenda naona wanafanya hivyo). Baada ya muda kidogo akaanza kutwambia. Akaendelea "Tatizo lililowaleta hapa nimeliona vizuri sana, ila kwa bahati mbaya lipo nje ya uwezo wangu"
Mshua akamuuliza "Unamaanisha nini?". Yule mganga akasema "Aliyemfanyia hivi kijana wako, ni mtu aliyedhamiria sana, na hata huko alipoenda, ni Kwa mtu mwenye uwezo wa juu kuliko wangu. Hapa ninaweza kuliona tatizo, lakini uwezo wa kulitatua ndio sina"
Mshua akawa kama mtu aliyekata tamaa, akamuuliza yule mtaalam "Sasa unatusaidiaje au unatushauri kitu gani?. Yule mganga akamjibu "Kitu ninachoweza kuwasaidia kwasasa ni kuwapa sehemu ya kupumzika usiku wa leo, na kesho patakapokucha, nawashauri mtafute mganga mwingine".
Kusikia vile, hata Mimi nikajihisi kukata tamaa, Kisauti amedhamiria kunipoteza.
Mshua akamuuliza, dhumuni la yeye kumfanyia vile Bi Mkubwa ni lipi?. Mtaalam akamwambia "Huyu hakuwa na utulivu wa nafsi, kadiri muda unavyoenda angeweza kunikwaza, ila msiwe na wasi, ataamka ndani ya muda mchache ujao.
Mshua akaomba tuondoke siku ile ile. Wakasaidiana kumuweka Bi Mkubwa ndani ya gari, na kumlaza siti za nyuma. Mimi na Mshua tukawa mbele, safari ikaanza.
Tukiwa njiani, Bi Mkubwa ndio fahamu zikamrudia, akajiinua na kukaa. Mshua akageuka na kumuuliza anajiskiaje? Bi Mkubwa hakujibu kitu, ila likamtoka fyonyo moja refu. Kiasi kwamba kule mbele tukapatwa na hali ya kutaka kucheka. Kuzuga ikabidi nigeukie nje, maana ningecheka yangezuka mengine. Mshua sababu ya kuendesha, plus ubovu wa barabara hakuweza kugeukia nje,alaf kicheko kikataka kumponyoka. Akazuga kupiga chafya na kujikoholesha. Picha nzima Bi Mkubwa akawa kaisoma. Bi Mkubwa ni dizaini ya wale wa wamama ambao Ukifanya kosa anaweza akakukata jicho kali hata kwa dakika 5 nzima, sasa ndicho kilichotokea kwenye gari. Alimkata jicho Mshua, kiasi kwamba kule mbele Mshua akawa anahisi ile hali. Ila hapo hapo anajizuia kucheka tena, maana heri ya Mimi, yeye angecheka tena ile safari ingekuwa chungu kwake.
Wote tukawa kimya, unasikika mziki tu kwenye radio. "Zima mamiziki yako inaniumiza kichwa Mimi" Bi Mkubwa akawaka ghafla, Mshua wala hakuongea kitu, akazima, safari ikaendelea.
Njiani nzima akawa anasikika Bi Mkubwa tu, anatusema weee, alaf anakaa kimya. Baada ya muda kidogo anatusema tena, Kisha anakaa kimya.
Mshua yeye yupo kimya tu, macho yako mbele muda wote. Kadiri gari inavyonesa nesa kwenye ile barabara mbovu, na Mimi ndivyo ninavyozidi kugugumia maumivu, Mama nae anakunja sura kwa uchungu, kama vile na yeye anaumia. Mshua yupo kimya, hana story na mtu. Ila kila Bi Mkubwa akimsema, yeye ananikata jicho Mimi, kujaribu kunionesha kuwa Mimi ndio chanzo.....
Barikiwa sana mkuu9th Portion:
.....Bi Mkubwa ikabidi aniulize kwa upole tu "Tuambie mwanangu, huyu jamaa unashida nae ipi?". Nikaendelea kuwa kimya tu kwa muda. Fikra ndio zikaanza kunituma, huenda kuumwa kwangu yule Kisauti akawa anahusika. Nilikuwa nishamsahau kabisa. Nilipatwa na hasira kuona nateseka kwa kosa lisilokuwa langu. Mshua alivyoona bado nipo kimya, sijamjibu Mama chochote, akanyanyuka na kuanza kuondoka. Bi mkubwa akamuuliza
Bi Mkubwa: "Baba nanii unaenda wapi sasa?
Mshua: "Sasa mtu haongei, nitakaa hapo siku nzima?"
Bi Mkubwa: "Unajua ili ni tatizo kubwa sana, usilifanyie mzaha"
Mshua: "Mzaha anaufanya huyo hapo, katibua watu mjini huko, karudi kutupa sisi shida"
Bi Mkubwa: "Kwahiyo tumuache afe"
Mshua: "Na akiendelea kukaa kimya, atakufa kweli"
Nilivyoona mzozo utaenda kuwa mkubwa, ikabidi niwafungukie issue nzima ilivyokuwa. Baada ya hapo wakaanza kujadiliana nini kifanyike. Bi Mkubwa akashauri wampigie simu Kisauti ili kumuomba msamaha, Kisha waangalie namna gani wanalimaliza lile jambo. Ila Mshua akagoma.
Bi Mkubwa: "Mwanao hali yake sio nzuri huyu, tuwasiliane na mdeni wake, tumlipe yaishe"
Mshua: "Hatuwezi lipa hela ambayo hatujachukua. Huo ni unyonge, na siwezi kuufanya. Dawa ya moto ni moto, kwavile kaanza yeye, acha tuendeleze, ngoja niwasiliane na Mzee Taba, ili tumpeleke kwa mtaalam"
Bi Mkubwa: "Mwanangu haendi kwa mtaalam wala kilingeni, kesho asubuhi naenda nae kanisani kwenye maombi"
Mshua: "Kwa hali ilivyo, lazima twende tu, na ilo halina mjadala"
Ukatokea mvutano mwingine pale, wapi nipelekwe hiyo kesho. Ila Mshua kutokana na commanding force yake, ikaamriwa nipelekwe kwa mtaalam. Kesho yake asubuhi na mapema tukaenda hadi kilingeni. Bi Mkubwa nae hakutaka kubaki nyumbani, alitaka awe na Mimi muda wote ili kujua hatma yangu.
Kufika kwa mganga tukapokelewa vizuri. Kutokana na hali niliyokuwa nayo, nikapewa kipaumbele kuonana na mtaalam. Tulivyoingia ndani, akaanza kuweka vitu vyake sawa, ongea ongea mambo yake pale.
Kuna muda nadhani alipandisha mashetani, maana lafudhi ilibadilika. Yeye ni mtu wa Kanda ya ziwa, ila ghafla akaanza kuongea lafudhi ya kimasai. Kuna mtu mwingine ambae ni msaidizi wake, ndio akawa anasaidia mwongozo wa yaliyokuwa yanaongelewa. Zoezi lilidumu kama nusu saa, then akarudi normal. Bila hata sisi kuongea sana, akaniambia, "Kijana unabahati sana kuendelea kuliona jua mpaka muda huu. Wapinzani wako, dhamira yao ni ya dhati". Mshua akauliza, kwahiyo nini kifanyike?. Yule mtaalam akasema kwasasa kuna kitu inabidi nimfanyie ili kudhibiti maumivu, alaf usiku ndio tutafanya zoezi kamili la kumtoa kwenye hii hali". Mshua akasema sawa, hakuna shida.
Mtaalam akaanza kufanya kazi yake pale. Mle ndani kulikuwa na kinu kikubwa kama vile wanavyotwangiaga wanawake, ila chenyewe kimechakaa sana, yawezekana ni cha muda mrefu, na rangi yake ilikuwa nyeusi tii, na mistari mistari myeupe. Sasa baada ya mtaalam kufanya mambo yake, akataka kupanda juu ya kile kinu, sikujua dhumuni lake lilikuwa ni lipi, maana wote mle tulibaki kuwa watazamaji tu. Wakati yupo juu ya kile kinu, alianguka yeye na kinu chake na kutanguliza uso chini. Alivyofika chini, kimya kikatawala. Urefu alioanguka ulikuwa mdogo sana, hata mtoto mdogo angeweza kusurvive, ila cha ajabu mganga alizimia. Yule msaidizi wake ndio akamkimbilia ghafla na kumnyanyua. Akachovya ule usinga kwenye kibakuli fulani kilikuwa pembeni, alaf akaanza kumpiga nao, huku anaongea maneno ambayo sikuyaelewa. Baada ya muda, mtaalam akaamka, anaongea ila sauti inatoka kwa mbali sana kama kakabwa au ametoka kukabwa.
Muda huo wote, sisi tupo kimya tu. Fahamu zilipomrudia vizuri na kuwa na utimamu wake. Akatwambia kwa upande wake, ili zoezi lipo nje ya uwezo wake, yani limemshinda. Akatuelekeza kwa mtaalam mwingine, aliyekuwa kijiji cha pili ambaye anaweza kutusaidia. Mshua na Bi Mkubwa wakawa wanajadiliana, Mshua anauliza kama twende siku hiyo hiyo, au kesho yake, ila Mama anataka turudi nyumbani. Yule mtaalam akawaambia, kadiri mnavyochelewa, ndivyo mnavyojisogeza kwenye kilio. Muwahisheni huyu, vinginevyo mtamkosa.
Bila kupoteza muda, tukafunga safari mpaka kwenye hicho kijiji. Tukaulizia hadi tukafanikiwa kumfikia yule mganga. Kutokana na miundombinu ya kijijini ilivyo, tulijikuta tunafika pale jua likiwa limeshaanza kupungua nguvu.
Tulipokelewa vizuri na msaidizi, tukakaa foleni kusubiria zamu yetu ifike.
Mida ya saa kumi na mbili kasoro, ndio tukafanikiwa kuonana nae. Hapo Bi Mkubwa nafsi haijamtulia kabisa. Muda wote kama ana mashaka na mganga. Ile hali ya Bi Mkubwa ikawa inamkera yule mtaalam. Akatwambia "Kuna hii dawa, ili zoezi lifanikiwe, inabidi wote watatu muilambe". Akaanza kutaka kumpa Bi Mkubwa, Mama akasita kidogo. Yule mganga akamkata jicho. Ikabidi Bi Mkubwa akubali kuilamba. Cha ajabu baada ya Bi Mkubwa kuilamba, sisi wengine hatukupewa. Bi Mkubwa akahoji kulikoni? Yule mganga akatoa usinga na kumpiga nao kichwani, Bi Mkubwa akasombwa na usingizi. Mimi na Mshua tukajikuta tunatazamana tu bila kusema chochote.
Baada ya salamu, akatwambia "Poleni sana na safari, maana huku tulipo ni mbali sana na mlipotoka". Baada ya kumuelezea dhumuni letu la kuwa pale, nae akafanya standard procedures zao (naziita standard procedure maana kote nilipoenda naona wanafanya hivyo). Baada ya muda kidogo akaanza kutwambia. Akaendelea "Tatizo lililowaleta hapa nimeliona vizuri sana, ila kwa bahati mbaya lipo nje ya uwezo wangu"
Mshua akamuuliza "Unamaanisha nini?". Yule mganga akasema "Aliyemfanyia hivi kijana wako, ni mtu aliyedhamiria sana, na hata huko alipoenda, ni Kwa mtu mwenye uwezo wa juu kuliko wangu. Hapa ninaweza kuliona tatizo, lakini uwezo wa kulitatua ndio sina"
Mshua akawa kama mtu aliyekata tamaa, akamuuliza yule mtaalam "Sasa unatusaidiaje au unatushauri kitu gani?. Yule mganga akamjibu "Kitu ninachoweza kuwasaidia kwasasa ni kuwapa sehemu ya kupumzika usiku wa leo, na kesho patakapokucha, nawashauri mtafute mganga mwingine".
Kusikia vile, hata Mimi nikajihisi kukata tamaa, Kisauti amedhamiria kunipoteza.
Mshua akamuuliza, dhumuni la yeye kumfanyia vile Bi Mkubwa ni lipi?. Mtaalam akamwambia "Huyu hakuwa na utulivu wa nafsi, kadiri muda unavyoenda angeweza kunikwaza, ila msiwe na wasi, ataamka ndani ya muda mchache ujao.
Mshua akaomba tuondoke siku ile ile. Wakasaidiana kumuweka Bi Mkubwa ndani ya gari, na kumlaza siti za nyuma. Mimi na Mshua tukawa mbele, safari ikaanza.
Tukiwa njiani, Bi Mkubwa ndio fahamu zikamrudia, akajiinua na kukaa. Mshua akageuka na kumuuliza anajiskiaje? Bi Mkubwa hakujibu kitu, ila likamtoka fyonyo moja refu. Kiasi kwamba kule mbele tukapatwa na hali ya kutaka kucheka. Kuzuga ikabidi nigeukie nje, maana ningecheka yangezuka mengine. Mshua sababu ya kuendesha, plus ubovu wa barabara hakuweza kugeukia nje,alaf kicheko kikataka kumponyoka. Akazuga kupiga chafya na kujikoholesha. Picha nzima Bi Mkubwa akawa kaisoma. Bi Mkubwa ni dizaini ya wale wa wamama ambao Ukifanya kosa anaweza akakukata jicho kali hata kwa dakika 5 nzima, sasa ndicho kilichotokea kwenye gari. Alimkata jicho Mshua, kiasi kwamba kule mbele Mshua akawa anahisi ile hali. Ila hapo hapo anajizuia kucheka tena, maana heri ya Mimi, yeye angecheka tena ile safari ingekuwa chungu kwake.
Wote tukawa kimya, unasikika mziki tu kwenye radio. "Zima mamiziki yako inaniumiza kichwa Mimi" Bi Mkubwa akawaka ghafla, Mshua wala hakuongea kitu, akazima, safari ikaendelea.
Njiani nzima akawa anasikika Bi Mkubwa tu, anatusema weee, alaf anakaa kimya. Baada ya muda kidogo anatusema tena, Kisha anakaa kimya.
Mshua yeye yupo kimya tu, macho yako mbele muda wote. Kadiri gari inavyonesa nesa kwenye ile barabara mbovu, na Mimi ndivyo ninavyozidi kugugumia maumivu, Mama nae anakunja sura kwa uchungu, kama vile na yeye anaumia. Mshua yupo kimya, hana story na mtu. Ila kila Bi Mkubwa akimsema, yeye ananikata jicho Mimi, kujaribu kunionesha kuwa Mimi ndio chanzo.....
Atakusahau vipi, wakati ww ni Unforgettable ? π πmkuu leta mambo hayo usiku mrefu huu Antonnia sugarkidawa ubarikiwe naona hunisahau kwenye maepisode
Mzima mkuu habari yakoShunie mzima?
Eeenh nimefunga huwa siitumiiUmefunga dm
Dooo maliza tu manake ya leo fupi sanaNipo naandika 10th Portion. Nikimaliza in time, nitaiweka hapa
SHETANI BABA YANGU (DEVIL MY FATHER) kuna nyingine huku wametuamuliaAsante dear⦠nitaisoma, saivi wacha iishe tu kwanza maana kipaji cha kusoma nimejaaliwa[emoji28] masaa kadhaa tu imepita shwaaa[emoji23]
Mzichoke nyie tu π π πSHETANI BABA YANGU (DEVIL MY FATHER) kuna nyingine huku wametuamulia