Kwamba chale ndio zinakutisha mkuu? Mbona vitu vidogo hivyo, wapo waliopitia zaidi ya hayo@analyse , uko serious ulipitia haya au unatupiga kamba?
mpaka chale, hirizi, kuoga sehemu ya wazi....[emoji44][emoji44][emoji44][emoji44][emoji44],
kumbe akina UMUGHAKA mko wengi aiseee...... yeye alipiga miti jini
Theluthi ni moja ya tatu, yaani kitu kimoja ukigawanye sawa sawa katika sehemu tatu. Robo ni moja ya nne, yaani kitu kimoja ukigawanye sawa sawa katika sehemu nne. Mzimu wa KoleloUpo tayari kujuzwa au tukuache ukiendelea kujua vivyo hivyo?
Hapo sasa ndio unaanza kuifaham dunia, kuwa kuna kitu kinaitwa ulimwengu, na huko kuna ulimwengu wa roho, wenye falme mbili, ufalme wa Mungu na ufalme wa Ibilisi.Aisee Hii Dunia ni zaidi ya tuijuavyo. Kuna vitu vingi sana vipo beyond our explanations.......
chai14th Portion
... Nilivyofika kwake, nilipokelewa vizuri kama vile hatukuwa na ugomvi. Nikala, Kisha nikala tena. Zikafatiwa story za hapa na pale. Kutokana na mishe niliyotakiwa kuifanya kesho yake, sikuweza kulala pale. Muda ulivyosogea, nikamwambia inabidi niondoke. Hakunizuia, maana alijua muda wowote anaweza kunipata. Kabla sijaondoka, nikaomba ile PS niondoke nayo.
Hapo ndio kama nilimtibua nyongo, maana sio kwa maneno aliyonitolea. Kana kwamba dakika chache zilizopita, sio sisi tuliokuwa tunafurahi. "Yani wewe unapenda kupokea, kutoa hutaki, haya nenda kaiombe ruhusa familia yako kuwa nataka kukupa zawadi, wakikubali, njoo uchukue, maana maamuzi yako wanafanya wao". Kiufupi alisema kama sipo tayari kukubali takwa lake, basi nisahau kuhusu ile PS. Nikakubaliana na hali. Nikaondoka.
Wakati nipo gheto nawaza dili la kesho tu. Mfano tukipata million 60, pale mgao wangu sio chini ya 10m. Nikaanza kuipangia matumizi kabisa, hapo ndio nikaona Mzee Dingi alikuwa sahihi, dili likifanikiwa naweza survive mwaka mzima bila stress. Baada ya mawazo ya hapa na pale, nikaamua kulala nitulize kichwa.
***** ***** ******* ** ** ****
Niliamka mapema sana, asubuhi ya siku iliyofuata. Ili niwahi pale maeneo ya kisutu, ile njia inapandisha kuelekea mtaa wa Lumumba. Lengo la kwenda pale ilikuwa ni kununua begi lenye muundo wa briefcase. Wakati nipo njiani naelekea pale, Mzee Dingi akanipigia, na kunitaarifu yule mstaafu amepata dharura, hivyo zoezi halitoweza fanyika siku hiyo, tutaenda kesho yake.
Baada ya kuongea nae, niliendelea na safari yangu, maana kivyovyote vile. Lile begi lazima niwe nalo. Baada ya kulininunua, nikaendelea na mishe zangu kama kawaida, kisha nikarudi ghetto. Kesho yake pia dili likabuma. Safari hii likasogezwa mbele wiki nzima.
Ikabidi tukutane wote kujadili nini kifanyike katika iki kipindi tunasubiria yule mstaafu mambo yake yakae sawa. Katika yale maongezi wakawa wanasema kuna kitu hakipo sawa ndio maana dili linakuwa gumu. Mzee Dingi akashauri kama timu, inabidi twende tena kwa mtaalam wao tukaangalie tatizo liko wapi (wao walishaendaga na huwa wanaenda sana). Kwavile Mimi nilikuwa ndio mgeni, wakashauri niwepo siku ya kwenda. Ila Mzee Kesho Yetu akakataa lile swala, akawaambia kwa mganga sio sehemu unayoenda enda tu kila ukitaka. Na kwavile wao walishaenda wiki chache zilizopita, basi ni apostle (Mimi) ndio natakiwa niende.
Mzee KY: "Huyu bwana mdogo ndio inabidi kwenda nae kuangalia shida nini, maana kila kitu kilikuwa sawa kabla hajahusishwa"
Mzee Dingi: "Ni wazo zuri pia, kwahiyo anaendaje?"
Mzee KY: "Nitaenda nae Mimi"
Mzee Dingi: "Ungepumzika tu mkuu, acha niende nae"
Mzee KY: "Hapana hakuna haja, nitaenda nae. Maana nataka nimpeleke sehemu tofauti na ile niliyowapeleka last time"
Mzee Dingi: "Sawa hakuna kama ni hvyo"
Nia yao ilikuwa zoezi la kwenda kwa mtaalam lifanyike wik end, ila nikawaomba wik end hiyo waniache nifanye mambo yangu, alafu jumatatu ndio twende huko kwa mtaalam. Baada ya kuelewana, tukasambalatika, kila mtu na uelekeo wake.
Jumapili asubuhi nikawasiliana na yule Mzee wa Kongowe, akaniambia nimsubirie pale pale aliponichukua mtoto wake mara ya mwisho. Mida ya saa nne, tayari nilikuwa pale, alivyofika tukaondoka wote.
Tulivyofika pale shambani, tulizunguka zunguka kwenye mifugo yake huku tunapiga Story. Dhumuni la kwenda kuonana nae safari hii ilikuwa ni kutaka kumuomba kama anaweza kunisaidia kuniunganisha sehemu yoyote ya ajira, maana maisha ya kuunga unga hayanaga dhamana.
Mzee: "Hicho ndicho najaribu kufanya mwanangu, ila sio rahisi kama unavyodhani"
Analyse: "Ila ulikuwa kwenye mfumo wao Mzee, japo ni ngumu, ila huwezi kosa namna"
Mzee: "Mambo hayapo hivyo kijana. Mimi pia nilifanya kuchomekwa tu, kama unavyojua sitokei kwenye familia zenye mashina na mizizi ya kisiasa. Watu wa kupenyezwa wanapigwa vita sana na inner circle. Na kibaya zaidi utawala ni mpya, kila mtu anajaribu kujitengenezea yeye njia, nani atanikumbuka?
Analyse: "Kwahiyo unanisaidiaje kijana wako"
Mzee: "Nitaendelea kuangalia angalia, ukipatikana upenyo, nitakwambia. Ila Sasa hivi wamebana sana mianya yote. Na walengwa tunaobanwa ni sisi, sio wao"
Analyse: "Sawa Mzee"
Mzee: "Mlango mmoja ukifungwa, kuna mwingine mahali fulani utafunguliwa kwa ajili yako, unachotakiwa ni kuwa tayari muda wote maana hujui ni lini, wapi au kutoka Kwa nani mlango wako utafungukia. Kwa umri wako hutakiwi kukata tamaa kabisa, siku zote tumaini ni sauti ya Mungu ndani yetu, bila hiyo huna cha maana utakachofanya".
Analyse: " Nimekuelewa Mzee"
Mzee: "Sawa, nitaendelea kuangalizia upenyo sehemu, ukipatikana nitakwambia, ila am not promising you anything"
Analyse: "Sawa, nashkuru sana"
Tukaendelea na shughuli zingine za hapa na pale, mpaka muda wake wa kuondoka ulivyofika, tukaondoka wote.
Niliendelea kujilaumu mpaka basi, kwa nafasi niliyopoteza. Niliipiga teke njia rahisi, nikachagua kuhangaika kusikokuwa na faida. Kesho jumatatu ilibidi asubuhi ninyonge tai, moka nzuri, unyunyu kisha nielekee ofisini, ila sababu ya uzembe, ntaenda kukutana na wazee wasio na hekima, ili twende kwa mganga. Maisha haya 😅😅😅
Kesho yake mapema nikakutana na Mzee KY maeneo ya mbezi stand ya gari ndogo, safari ya kuelekea Moro ikaanza. Baada ya kufika Moro, tulitembea kwa dakika kama 30 kisha tukaachana na mji, na kuchukua njia kuingia ndani ndani huko. Safari nzima, mawazo yangu yapo kwenye mazungumzo yangu na yule Mzee kule Kongowe.
Mimi na Mzee KY hatukupiga story nyingi njiani, ni Mzee ambae sio muongeaji, muda mwingi anasikiliza tu. Na hizo story chache tulizopiga, ni kwamba alikuwa ananiuliza kitu, then ananiacha nibwabwaje.
Baada ya mwendo wa kama lisaa na nusu au mawili, tukafika mwisho wa safari yetu, then tukaelekea kwa huyo mtaalam wake.
Inaonekana alishawasiliana na yule mtaalam, kumjulisha ujio wetu. Maana tulivyofika, baada ya salamu hapakuwa tena na mazungumzo mengi, nikaambiwa niingie kwenye chumba kilichokuwa vyumba vya nyuma. Mzee KY akamwambia mtaalam bwana mdogo atoke kaiva, mganga akacheka tu. Nikaingia kupikwa kwa mara ya kwanza.
Niliambiwa vitu vinavyotakiwa kununuliwa mfano nazi, karatasi nyeupe, wembe, unga nk. Hela ilitolewa, vikafatwa. Palifanyika mambo mengi sana na mazito, tena kwa muda mrefu. Nilianza kwa kusuguliwa na mchanganyiko wa unga wa sembe na tui la nazi mwili mzima. Vikafatia visomo, chale kuanzia unyayoni mpaka utosini. Kiufupi zoezi lilikuwa zito. Kimoyo moyo najiuliza "Huyu ni Mimi ndio nafanyiwa hivi au?''. Baada ya hapo nikatakiwa kutoka nje vile vile na boksa yangu, mpaka katikati ya kiwanja alafu nirudi ndani. Nikamuuliza yule mganga, "Natoka hivi, na wale watu waliopo nje je?". Mganga akanikata jicho, kiasi kwamba nikajikuta nanyanyuka.
Aisee ukiona mtu anahela, wewe muheshimu tu, haijalishi kazipata vipi. Watu wanasuffer mazee, kila njia ni tough.
Mida ya jioni ndio tulimaliza. Nikapewa dawa ambazo nilitakiwa kujifukiza kwa siku kadhaa, na zingine ambazo nilitakiwa kuoga, lakini hizi za kuoga, sikutakiwa kuziogea bafuni au chooni. Kuna dawa ilikuwa mchanganyiko wa unga mweusi, na mafuta mafuta, hiyo nilitakiwa kuichanganya kwenye mafuta ya nazi, kisha niwe napaka viganjani na usoni kabla ya kutoka nyumbani na kwenda kwenye mishe mishe zangu. Lakini pia nilipewa kitu mfano wa hirizi, ambayo upana wake unakaribia kucha ya kidole cha shahada. Hiyo niliambiwa niwe nayo muda wote. Hizi dawa mbili (ya kupaka na hirizi) zilifanya mpaka kesho nina bifu na Mzee Dingi.
Kila kitu kilivyokuwa kimekamilika, tukaaga na kuondoka. Njiani Mzee KY ananiambia, "Bwana mdogo ukiwa serious kwenye maisha utafika mbali sana, ila kwa muda mchache ambao nimespend na wewe, tatizo lako kubwa ni moja tu"
Nikamuuliza tatizo gani??. Akanijibu, "You don't smile easily". Nikatatizika kidogo, "Kuto tabasamu nalo ni tatizo?". Akanijibu "Bado una mengi ya kujifunza". Nikabaki namwangalia tu. Katikati ya story zilizoendelea, nikajikuta namwambia "Sikuwahi fikiria kama siku moja ningeangukia huku". Akacheka.
Mzee KY: "Tukiwa wadogo, ni ndoto ya kila mtoto kuwa rubani. Hii Dunia jinsi ilivyo, ukiteleza kidogo tu inakuchagulia njia"
Hapo ndio akaniambia machache kuhusu yeye. Katika hayo maongezi yetu ndio niligundua kuwa ana masters ya uhandisi wa umeme, lakini pia ana CPA, ana uwezo wa kuzungumza lugha 3 za kimataifa kwa ufasaha kabisa. Chuo alisomeaga Uganda. Na ana ofisi mbili town, lakini just for backup, japo zinafanya vizuri.
Nilimshangaa sana kwanini ameamua kuendelea na njia ile wakati ana uwezo wa kutengeneza decent money?
Mzee KY: "Sikia bwana mdogo, hii Dunia inaweza kukuchapa alafu haikupi kabisa muda wa kujutia. Na hata ukiwa kwenye kujutia, inaweza ikakuchapa tena, kiasi kwamba ukiwa kwenye kujutia kwako, ndani yake ukapata majuto mengine".
Wakati najaribu kujiuliza amemaanisha Nini, akaendelea, "Unatakiwa kujutia huku unaenda nayo, maana muda haukusubiri".
"Sema sijui kwanini wewe umeingia huku, ila binafsi kisasi na kinyongo nilichokuwa nacho juu ya mtu fulani ndio kimeniingiza huku. Nilipima kina Cha maji kwa mguu, sasa nimeshazama tayari".
Hakuongea tena mpaka alivyonishusha mbezi mwisho.
. ****** ******** ********** ** ***
Baada ya pale, nikanyoosha mpaka gheto kwangu. Kwavile sikuwa nimejiandaa sehemu ya kuogea, ikabidi nibebe ndoo yangu hadi kwenye kiwanja cha shule ya msingi (nilikuwa jirani na shule), nikaenda kuogea pale chap, then nikarudi ghetto kujifukiza ile dawa nyingine. Baada ya hapo nikalala.
Kabla ya kwenda kwa mganga, kuna vitu vingi sana nilikuwa sivielewagi, na sivipatii majibu. Nilikuwa nikipishana na vijana (wakike kwa wakiume), unakuta mtu smart, lakini macho mekunduu kuliko kawaida, japo sio mlevi wala mvutaji sigara. Au mkipishana unahisi harufu ya moshi tu. Nilikuwa najiuliza, hivi hapa mjini kuna watu wanapikia majiko ya kuni au?. Kumbe hakuna bhana, vijana wanajifukiza sana. Tena wameanza kuoga moshi kabla hata ya Corona.
Hizo siku tatu za kujifukiza, nilikuwa nanuka moshi muda wote. Kibaya zaidi, zile dawa za kuoga hutakiwi kutumia sabuni.
Kipindi naendelea na ile dozi. Mzee Dingi akawa ametupa taarifa kuwa alipigiwa simu na yule mlengwa wetu, wamekubaliana zoezi litafanyika siku 6 tokea hiyo siku. Maana alikuwa anajipanga, akishanunua lile eneo basi mipango yake mingine iende haraka pia.
Nikamaliza masharti, tukabaki tunamsikilizia yule mstaafu, japo tulipiga dili kama mbili, na zote zilitiki vizuri tu.
Kile kihirizi alichonipaga yule mtaalam, aliniambia kwavile natakiwa niwe nacho muda wote mwilini, basi naweza kukihifadhi kwa namna tatu. Mosi, nikifunge kwenye kamba, alaf nikibane mkononi kama wanavyofanya makepteni wa mpira, Pili, nikizungushie big g, alaf nikienda eneo la tukio, nikibane mdomoni, tatu, nikitengenezee bangili, au pete ya kukibana then niivae.
Mimi nilitengeneza pete za kacha zile, alafu nikakishonea pale. Nikaivaa kwenye kidole cha pete, mkono wa kulia.
Zikiwa zimebaki siku tatu twende kwenye lile dili kubwa. Nilikuwa zangu gheto tu nimekaa, wazo likanijia nikajaribishe zile dawa sehemu. Akili ikanituma niende kwa Shani.
Mida ya jioni, nikaoga, nikapaka mafuta yangu ya nazi yenye dawa, mikononi na usoni. Kisha nikatoka.
Aisee Hii Dunia ni zaidi ya tuijuavyo. Kuna vitu vingi sana vipo beyond our explanations.......
Wewe Lete kahawachai
Nani kakuitachai
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]ofisini hatuji na bahasha, jamaa wahuni sana6th Portion:
.... I was a bit disappointed. Tukaongea story zingine mbili tatu, alafu tukaagana. Niliendelea kulifikiria lile swala, mwisho wa siku nikadhamiria nijipange Kisha niende mpaka kijijini, walau nipate kuongea nao ana kwa ana, maana dhamira yangu ilikuwa thabiti. Tofauti na wao walivyohisi, Mimi sikuwa napanga kuoa shangazi, kuna binti nilikuwa nae kwenye mahusiano ambayo kwa kiasi fulani yalikuwa serious.
Wiki moja baadae, sister angu akawa ameniita niende kumtembelea Mwanza, lakini pia aweze kuniunganisha na mchongo fulani. Nilivyoenda akafanikisha kuniunganisha na ilo deal, japo halikuwa na muda mrefu, maana nilikaa kule takriban mwezi mmoja.
Kumbe ukiachana na huo mchongo, sister alikuwa na mission nyingine. Nyumbani, wazazi walimpa jukumu la kumfahamu mwanamke wangu, Kisha awape taarifa. Sister nae alichokosea, badala walau aniulize, akawa anapitia simu yangu kimya Kimya. Simu yangu haikuwa na password, fingerprint wala patterns, so ilikuwa rahisi kuaccess information.
Katika mapenzi kuna muda wapenzi huwa wanachatig ujinga ili kusogeza siku. Sasa kuna chatting fulani nilikuwa nachat na shangazi, kiutani utani nilimwambiaga "Yani wewe ningefanikiwa kukuoa, ningekuwa na raha sana", ilikuwa ni chatting za kupoteza muda tu, ila sister akaichukulia serious. Na kwenye gallery alikuta picha zake kadhaa, akajirushia Kisha akakausha, maana hakuwa na namna ya kuniambia, kwasababu info amezipata kwa njia isiyo halali.
Siku zikaenda, na ule mchongo ukafika tamati, nikarudi Dar. Sasa kuna siku yule shangazi alitaka nimpost kwenye status, baada ya kuvutana sana, nikaona isiwe case, nikawahide watu wote muhimu, Kisha nikampost nakuweka caption ya kawaida tu. Sasa kumbe sister alikuwa ameinstall Whatsapp mbili kwenye simu yake, na Mimi sikugundua. Akaiona ile status. Nashangaa kuona amereply "Mdogo wangu ndio maana hata uleje haunenepi, mzigo wote huo kweli?"
Ikabidi nijaribu kumkataa:
Analyse: "Huyo ni Mama wa rafiki yangu"
Sister: "Kwenda huko, niliona picha zenu kwenye simu yako, nikahisi ni yaliyopita, kumbe ndiyo yaliyopo?
Analyse: "Haipo hivyo dad... "
Sister: "Huyo ndio mwanamke unataka kumpeleka nyumbani bila aibu? Hivi akili zako zipoje lakini?"
Ikabidi nikaushie msg zake, akaamua kunipigia simu, alinisema sana siku hiyo, hadi nikahisi kizungu zungu. Nikaanza kujihisi sasa hapa nilipofikia pashakuwa pabaya, wanaonizunguka wote hawana utulivu wala amani, inabidi niachane na haya mambo sasa.
Hata lile wazo la kumpeleka yule binti home, ikabidi nilisimamishe kwa muda. Maana mazingira hayakuwa supportive tena, na Kwa jinsi ninavyomjua Mshua, panaweza pakatokea ngumi nikienda, alaf sikutaka tufikie huko.
Huyu manzi, kipindi namwambia nataka nikamtambulishe nyumbani, alikuwa anasita sita, mara aseme nivute subira kidogo, muda bado. Alivyosikia nimesitisha kumpeleka nyumbani, ukawa ugomvi sasa, maana akawa ana push sana nimpeleke, hadi nikawa najiuliza, hiyo subira aliyokuwa anasema niivute, imekatika au?.
Fast forward kidogo. Niliendelea kufanya mishe zangu za kuunga unga mjini, huku nikipata nafasi, nazungusha bahasha maofisini. Pale gheto nilipokuwa nimepanga, kuna Mzee fulan smart, amechomekea muda wote, ni mtu mzima, ila hana mvi hata moja, panki lake muda mwingi limepakwa super black, nae alikuwa amepanga pale. Sema tofauti yetu, Mimi nilikuwa nimepanga chumba kimoja, yeye alichukuwa vyumba viwili na sebule, maana alikuwa na familia.
Mzee sikuwa na mazoea nae sana, hata jina lake halisi nilikuwa silifahamu, nilizoea kusikia mkewe anamuita baba fulani (jina kapuni), au vijana wengi pale mtaani walipenda kumuita Mzee Dingi (na Mimi humu nitapenda kutumia ilo ilo jina la Mzee Dingi). Huyu Mzee kwa mtazamo wa nje, alikuwa na muonekano fulani wa kimamlaka, yani ukimuona tu kwa mara ya kwanza, unahisi atakuwa mtu mzito au yupo kitengo nyeti somewhere. So, kutokana na mambo yangu kuwa magumu, nikapata wazo la kuongea nae, pengine anaweza akaniunganishia mchongo wowote hapa mjini. Siku ya siku nikamkabili, ilikuwa siku ya jumapili, maana huwa anashindaga home tu.
Nilivyomuelezea shida yangu, kabla ya yote akaniuliza kwanini nimemfata yeye?. Nikamjibu nimejaribu tu, maana siwezi jua nani anaweza nisaidia, maana mjini Sina connection ya maana. Mzee Dingi akaniuliza elimu yangu na taaluma niliyonayo. Nikajielezea vizuri pale. Tukaongea mambo mengi, mwishowe akaniambia, kesho nivae vizuri, Kisha nimpigie simu anielekeze nitakapomkuta. Tukabadilishana namba za simu, nikarudi ghetto kwangu.
Kesho yake nikajiandaa vizuri, Kisha nikampigia simu anipe direction. Akanielekeza niende mpaka city center, maeneo ya Samora, kuna bustan fulani ipo opposite na NBC, nimsubirie pale. Nikabeba copy za vyeti vyangu kwenye bahasha, nikaanza safari ya kuelekea town. Nilivyofika, nikamjulisha, akaniambia nimsubirie atakuja. Nikatulia.
Nilikaa sana pale, karibia masaa mawili, Mzee hajatokea, wala hajanicheki. Sema sifa kubwa ya jobless ni uvumilivu, nikaendelea kuvumilia. Baada ya muda, pembeni yangu alikuja akakaa jamaa, ambae alionekana kama Yuko stressed hivi. Kila muda anapiga simu, na ukimuangalia vizuri kama anataka kulia. Sasa katika kupoteza time maana nilikuwa bored, nikajikuta namuuliza kilichomsibu. Jamaa ndio kunipa story kuwa huwa anafanya biashara ya mkaa, analeta na kuuza kwa jumla, kisha anarudi mkoani. Hii ilikuwa ni trip yake ya kwanza tokea aanze biashara kwa upande wa Dar, mzigo wote umekamatwa na maliasili maana pia alikuwa amebeba vitu ambavyo hakuwa na vibali navyo, So upo kituo cha polisi. Haelewi afanye nini, na wale waliomshika, wanataka mpunga mrefu ili aachiwe. Ndani ya muda ule mfupi, alijikuta tu ananiamini, tukawa tunaongea kama watu ambao tumefahamiana kwa muda mrefu.
Binafsi sikuwa na cha kumsaidia, nikabaki nampa pole na kumtia moyo tu. Ghafla Mzee Dingi akawa amefika, nikanyanyuka kumsalimia, alafu nikawa nasubiria anioneshe direction tunayoenda, ila yeye akawa amemakinika sana na yule jamaa niliyekuwa naongea nae. Akaniuliza "Huyu mwenzako ana Nini?". Nikashangaa kwann amemuita mwenzangu, ila sikujali sana, nikampa briefly tu.
Baada ya kuisikia story ya jamaa, pale pale Mzee Dingi akasema anafahamiana na mwanasheria ambae alishamsaidiaga rafiki yake kwenye mzozo na maliasili. Akamwambia yule jamaa aongozane na sisi wakati yeye anampigia simu mwanasheria. Kilichonishangaza, wakati tunaondoka, ile simu aliyopiga, ikaita kwa Mzee mwingine ambae alikuwa eneo lile lile anakunywa kahawa, sema kakaa benchi jingine. Yule jamaa wa mkaa hakuusoma mchezo, sijui ni stress au vipi.
Mzee Dingi aliongea huku simu kaiweka loudspeaker wote watatu tunasikia, mwisho wa siku mwanasheria akasema yupo maaneo ya stesheni,kuna mgahawa anapata chai, so tumfate pale. Tukaongozana Mimi, Mzee Dingi na jamaa wa mkaa. Stesheni kuna mgahawa upo unaface stand direct, ndio tukaingia hapo. Tukamkuta huyo mwanasheria, nilivyoiangalia ile sura, ni Mzee ambae tokea nilivyofika kwenye bustan pale Samora, nilimkuta, muda wote alikuwa anasoma gazeti, story kidogo huku anakunywa kahawa. Yani kiufupi hakuwa na haraka yoyote. Ila tulivyomkuta hapo kwenye mgahawa, akatwambia tuongee tunachotaka kuongea, hana zaidi ya dakika 15, anawahi mahakamani.
Kuna kengele Fulani ikalia kichwani mwangu. Zilipigwa sound za kutosha pale, sound nyingi sana. Mpaka ikafikia hatua, yule jamaa wa mkaa akahitajika kutoa laki 5 ili issue yake iwe solved siku ile ile. Jamaa wa mkaa akawa anajaribu kubargain yule mwanasheria feki akanyanyua briefcase yake akatishia kuondoka, Mzee Dingi akawahi kumtuliza kuwa amsaidie jamaa issue yake, jamaa nae kwa kuhofia kupoteza mtu wa kumsaidia, akakubali kutoa hiyo 500k. Pale pale akili ikaniambia, kuna mtu anatapeliwa muda sio mrefu.
Kati ya wote pale, yule jamaa wa mkaa, alionekana kuniamini Mimi kuliko wengine. Hata ile 500k waliyokubaliana atoe, akanitupia Mimi jicho fulani kama vile kuomba ushauri au kuuliza atoe au asitoe?. Kwa mazingira yalivyokuwa, nikajikuta nampa ishara atoe hela, asiwe na wasi wasi, ila nafsi ilikuwa inanisuta sana.
Wote wanne, tukatoka nje ya ule mgahawa, tukapanda gari ya yule mwanasheria, mpaka ATM, jamaa wa mkaa akatoa hela. Kisha tukarudi mpaka karibu na jengo la mamlaka ya bandari, kufika pale, yule mwanasheria na jamaa wa mkaa wakashuka na kuingia ndani, Nia ni kwenda kuandikishiana hela walizipeana, then ndio waende polisi. Baada ya dakika kama 15, yule mwanasheria akarudi peke yake, akazama kwenye gari haraka, Mzee Dingi akang'oa.
Akili yangu ikawa wazi, kuwa Mzee Dingi ni tapeli tu, yeye na mwenzie. Ikabidi nivunje ukimya ndani ya gari, kwamba kilichafanyika haikuwa haki. Hakuna aliyenijibu, Mzee Dingi akapaki gari kituo cha mnazi mmoja pale, then Mzee Dingi akawa ananiambia "Bahasha wanazunguka nazo vijana wanaotafuta kazi, wewe umeshapata kazi tayari, tafuta briefcase au begi la kubeba mkononi, kesho usije tena kazini na hiyo Bahasha". Nikamwangalia yule Mzee, hana hata chembe ya huruma au kujutia. Yule mwanasheria feki, akaniuliza "Kwani bwana mdogo unachotaka hasa ni nini?". Nikamjibu " Tumrudishie jamaa hela zake". Mzee Dingi akadakia "Sikia apostle, Ungetaka kumsaidia, ungemsaidia kipindi tupo pale mgahawani, acha kutia huruma wakati hela unaitaka"
Nikajikuta hasira zinazidi, hasa alivyoniita apostle, maana ilikuwa ni kama kebehi fulani hivi. Yule mwanasheria feki kwenye ile 500k, yeye akachukua 200k, Mzee Dingi akapewa 200k, alafu akachukua 100k na kunikabidhi Mimi,kisha akanipa na namba ya simu kwenye kikaratasi. Akaniambia "Hiyo ndio namba ya yule jamaa, hiyo 100k ndio mgao wako, mtafute umrudishie walau nusu hasara"
Nikabaki nimetoa macho tu.....
Endelea hapa Sijawahi kujutia kwenye maisha yangu. Mpaka siku niliyokutana na yule Mzee
Umeitwa?chai
Madam[emoji123]Tupo pamoja kipenzi Usijareee!![emoji8]
Thanx kipenzi...leo ndo naperuzi hapaTayukwa Bantu Lady Lovelovie Elissante Kigi Makasi @mmashi Gily Half american mtzmweusi Kalpana sehemu ya 14 tayareeee