aliyetegwa
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 313
- 486
Habari wakuu,
Iko hivi alikuwa ni kijana nadhifu, mchangamfu na kikubwa mwenye uwezo mkubwa darasani. Baada ya harakati za masomo alimaliza shahada yake ya kwanza 2014. Kwa kipindi cha karibia miaka nane hakupata kazi ila alichakarika haswa kwa kufungua genge na kuhudumia familia kwa kazi hiyo.
Mungu si Athumani mwaka huu mwezi wa saba alipata ajira serikalini, hajapokea hata mishahara mitatu shetani ashamvaa, sijui alipatwa na nini. Alianza kama matani siku kama nne kabla siku yake ya mwisho akaanza kusema akilewa kuwa atajiua, ila walio karibu yake wakachukulia poa wakihisi ni ulevi.
Siku ya tukio ndiyo inanifikirisha sana, aliamka vizuri mida ya mchana akawa amelewa chakari. Akaanza tabia yake ya kusema anataka kujiua, ila hii siku hii kauli ilionekana kuwa na nguvu zaidi, watu wakamkamata na kampeleka kituo cha polisi. Polisi walikaa naye kama masaa matatu mpaka walipomuona yuko sawa na pombe zimepungua, wakamwachilia, kumbe hawakujua masikini.
Alipotoka hapo alikwenda kumeza sumu ya panya ila akaona haoni matokea hivyo akaanza kupiga kelele kulalamika kwanini hafi na amekunywa sumu, akaamua kumeza coin mbili za shilingi mia mbili.
Baada ya muda mfupi hali yake ilikua mbaya akakimbizwa hospitali, Mungu saidia akapata huduma na kupata nafuu kubwa. Daktari wake akasema angeshughulika na sarafu alizomeza kesho yake, aliyekuwa akimuhudumia akaagizwa kwenda kumtafutia walau uji maana alikuwa amechoka mno, angejua asingekwenda.
Baada ya kuachwa hospitali alitoroka na kwenda kujizamisha ziwani, kitu kilichopelekea kifo chake. Ameacha mke, ambaye ni mama wa nyumbani na watoto wawili wadogo, mdogo akiwa hajafikisha hata mwaka.
Najiuliza kwanini alifanya jaribio la kujiua kwa nguvu namna hiyo kwa zaidi ya mara mbili kwa ndani siku moja? Ameumiza sana moyo wangu nikiangalia watoto wake wadogo.
Wakuu hii kwenu imekaaje, mnafikiri mwana alipatwa na nini?
Iko hivi alikuwa ni kijana nadhifu, mchangamfu na kikubwa mwenye uwezo mkubwa darasani. Baada ya harakati za masomo alimaliza shahada yake ya kwanza 2014. Kwa kipindi cha karibia miaka nane hakupata kazi ila alichakarika haswa kwa kufungua genge na kuhudumia familia kwa kazi hiyo.
Mungu si Athumani mwaka huu mwezi wa saba alipata ajira serikalini, hajapokea hata mishahara mitatu shetani ashamvaa, sijui alipatwa na nini. Alianza kama matani siku kama nne kabla siku yake ya mwisho akaanza kusema akilewa kuwa atajiua, ila walio karibu yake wakachukulia poa wakihisi ni ulevi.
Siku ya tukio ndiyo inanifikirisha sana, aliamka vizuri mida ya mchana akawa amelewa chakari. Akaanza tabia yake ya kusema anataka kujiua, ila hii siku hii kauli ilionekana kuwa na nguvu zaidi, watu wakamkamata na kampeleka kituo cha polisi. Polisi walikaa naye kama masaa matatu mpaka walipomuona yuko sawa na pombe zimepungua, wakamwachilia, kumbe hawakujua masikini.
Alipotoka hapo alikwenda kumeza sumu ya panya ila akaona haoni matokea hivyo akaanza kupiga kelele kulalamika kwanini hafi na amekunywa sumu, akaamua kumeza coin mbili za shilingi mia mbili.
Baada ya muda mfupi hali yake ilikua mbaya akakimbizwa hospitali, Mungu saidia akapata huduma na kupata nafuu kubwa. Daktari wake akasema angeshughulika na sarafu alizomeza kesho yake, aliyekuwa akimuhudumia akaagizwa kwenda kumtafutia walau uji maana alikuwa amechoka mno, angejua asingekwenda.
Baada ya kuachwa hospitali alitoroka na kwenda kujizamisha ziwani, kitu kilichopelekea kifo chake. Ameacha mke, ambaye ni mama wa nyumbani na watoto wawili wadogo, mdogo akiwa hajafikisha hata mwaka.
Najiuliza kwanini alifanya jaribio la kujiua kwa nguvu namna hiyo kwa zaidi ya mara mbili kwa ndani siku moja? Ameumiza sana moyo wangu nikiangalia watoto wake wadogo.
Wakuu hii kwenu imekaaje, mnafikiri mwana alipatwa na nini?