Siku 40 bila mwamba: Ulituheshimisha sisi wanyonge na masikini, pumzika kwa amani Hayati Dkt. Magufuli

Siku 40 bila mwamba: Ulituheshimisha sisi wanyonge na masikini, pumzika kwa amani Hayati Dkt. Magufuli

UPUUZI MTUPU!!!
SIKU 40 BILA MWAMBA: ULITUHESHIMISHA SISI WANYONGE NA MASIKINI,PUMZIKA KWA AMANI JPM.

Katika awamu ya nne ya Rais Mstaafu Kikwete kurudi nyuma hadi Azimio la Zanzibar, Matajiri na Wafanyabiashara walikuwa na Jeuri za kila aina,kwa maana walianza kufanikiwa kuifanya CCM kuwa ya Wafanyabiashara, Wakulima na Wafanyakazi kitu ambacho kilikiuka miiko ya CCM iliyokuwa ya Chama Cha Wakulima na Wafanyakazi,na CCM ambayo inaongozwa na itikadi ya Kijamaa,sio ya Kibepari.

Dhana ya Wafanyabiashara kuhodhi mali za CCM na kuitawala CCM iliwapa jeuri Matajiri ambao wengi wao ni Wafanyabiashara waliokuwa wafadhiri lakini pia Mafisadi,jeuri ya Matajiri ilikuwa kubwa hasa awamu ya nne,matajiri walifikia mpaka kuamua uhai wa watu masikini waishi vipi wakae wapi wale nini kwa maana gap la tajiri na masikini lilikuwa kubwa na baadhi ya matajiri walikuwa na utajiri kiasi cha kuweza kuikopesha Serikali.

Alipoingia Hayati Rais Daktari John Pombe Magufuli alituheshimisha wanyonge ambao tulikuwa tukionewa na matajiri hata sauti zetu zisisikike popote, Wanyonge ambao hatukuwa na mtu wa kutupa kimemo ili twende kwa Mkurugenzi fulani atuajiri,Rais wa Awamu ya tano, Daktari John Pombe Magufuli alituheshimisha sisi Masikini (Mimi nikiwemo) kuwa hata sisi pia ndani ya hii Ardhi ya Mama Tanzania tuna thamani yetu,tuliokuwa matombo Morogoro tuliweza kupata ajira tukiwa kijijini matombo na wasiopata walikuwa na matumaini ya kupata, Hayati Rais Magufuli alitupa ujasiri (akatujaza) jeuri sisi masikini mpaka Matajiri nao wakaanza kutunyari (kutuogopa) Wanyonge na masikini nasi tukaanza kuona kuwa Tanzania ni nyumbani kwetu sio nyumbani kwa matajiri peke yao.

Watu wanauliza mnyonge ni nani? wengine wakianzisha kampeni wasiitwe wanyonge,lakini niwaambie mnyonge ni mtu yule anaepata mlo mmoja au miwili kwa siku, akipata milo mitatu kwa shida,inabidi achakarike na asisumbuliwe, mfano Mmachinga anafukuzwa na askari sehemu yake anayofanya biashara. JPM aliwapa kibali cha unafuu, wataacha kumpenda?kwa mnyonge, akipata kile anachotafuta bila kusumbuliwa, ni Raha yake na anamuamini aliyemuwezesha,Hayati Rais John Pombe Magufuli aliweza hilo.

#Ahsante Rais Magufuli
#Pumzika kwa Amani Mwamba.
 
Kama upepo kama movie fulani hivi maisha ya mwanadamu ni upepo.
Amekwenda alipo ben, Azory,lwajaba,na wengine.
 
We kenge kafanye kazi acha kulalamika, unaitwa maskini na mnyonge unakubali?

Acheni tabia za kujilaani kwa kupenda kuitwa maskini na wanyonge, fanyeni kazi kwa bidii! Hukuumbwa kuwa maskini we boya amka!
Usingeweka matusi ungeeleweka zaidi
 
Aliwaheshimu wanyonge kwa kuwatoza 20,000 bila kutungiwa kanuni yyt ile ya kuwalinda?
Rais wa wanyonge anaye tapanya pesa za nchi kama mali yake binafsi?
 
Tafadhali usitute wanyonge kama unyonge ni huko kwenu, tuondolee mikosi hapa ya mataga
 
Back
Top Bottom