Siku binti yako akisoma nyuzi na maoni yako atafurahi au atasikitika?

Siku binti yako akisoma nyuzi na maoni yako atafurahi au atasikitika?

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Habari Waheshimiwa!

Najua kuna watu hamjawahi kuitwa Waheshimiwa, ngoja niwatoe lock na ninyi muonjeonje kidogo majina ya heshima. Mimi mara ya kwanza kuitwa Mheshimiwa ni siku nimeenda kutoa posa huko madongo kuinama, niliazima VX ya kijivu, nikaiweka bendera ya Tanzania upande wa mbele, kisha nikatimba Ukweni. Kila mara nilikuwa nikiwakatisha na kuwakataza wasiniite Mheshimiwa, halafu walikuwa wakikosea, walikuwa wakiniita "Mesimiwa", hatari sana. Tuachane na hayo, ilikuwa nje ya mada. Sisi wengine tunapenda stori.

Hivi uliwahi kujiuliza siku mtoto wako akikua, akaingia mitandaoni halafu akasoma posts na comments zako atajisikiaje? Je, atafurahi au atahuzunika? Je, atajivunia baba au mama bora au atajiona ana bahati mbaya kuwa na baba au mama mjinga kama wewe?

Je, utamkatisha tamaa na kumkwaza au utampa moyo?

Mfano, akute ukiwaponda wanawake wasio na shape halafu yeye muda huo mwili wake haueleweki kiuno kiwapi, tumbo li wapi, yaani ni amorphous fulani hivi. Au ulikuwa unaponda wanawake au wanaume wafupi kama mtungi wa gesi, halafu mtoto wako ndio yuko hivyo. Je, atafarijika au atakata tamaa?

Ndugu Mesimiwa, kwa ridhaa yako naomba nihitimishe kwa kusema, ujumbe wowote utakaoutoa basi angalia na kizazi chako ili usijekuwa baba au mama jinga.

Achana na kauli ya kujifariji kuwa hakuna baba au mama jinga. Hizo ni lugha za kujifariji tu, lakini watoto wanajua hapa wana mzazi au hawana.

Acha nipumzike sasa.

Robert Heriel,
Taikon wa Fasihi,
Kwa sasa Dar es Salaam.
 
Swala la kufurahi ama kusikitika ni juu yake mi sijui. Siwezi muongelea kuhusu hisia zake. Maana si kila mtu ataendana kihisia na mimi. Inawezakuwa ninachokifurahia na yeye akakifurahia ama kinyume chake
 
Daaah Mambo ya Mtungi wa gesi hahaaa hatari.

Mimi watafurahi wamepata "MSHUA" konki.
 
Wahuni wanasema kila mtu ashinde mechi zake .
 
Anakuta mzee alikuwa anashinda kwenye uzi wa tunda kimashara
 
Ndio maana hatutumii majina halisi, nyie ndo wa kujiuliza hayo mimi Vishu Mtata wala sijiulizi, hakuna mtandao najulikana kwa jina halisi halafu nikapost ujinga.

Kuna kipindi nilikua napost vipichapicha fesibuku nilipojitambua nikafuta vyote sasa sina post mahali popote kwa jina langu halisi.

Fake id's zinafariji sana.
 
Habari Waheshimiwa!

Najua kuna watu hamjawahi kuitwa Waheshimiwa, ngoja niwatoe lock na ninyi muonjeonje kidogo majina ya heshima. Mimi mara ya kwanza kuitwa Mheshimiwa ni siku nimeenda kutoa posa huko madongo kuinama, niliazima VX ya kijivu, nikaiweka bendera ya Tanzania upande wa mbele, kisha nikatimba Ukweni. Kila mara nilikuwa nikiwakatisha na kuwakataza wasiniite Mheshimiwa, halafu walikuwa wakikosea, walikuwa wakiniita "Mesimiwa", hatari sana. Tuachane na hayo, ilikuwa nje ya mada. Sisi wengine tunapenda stori.

Hivi uliwahi kujiuliza siku mtoto wako akikua, akaingia mitandaoni halafu akasoma posts na comments zako atajisikiaje? Je, atafurahi au atahuzunika? Je, atajivunia baba au mama bora au atajiona ana bahati mbaya kuwa na baba au mama mjinga kama wewe?

Je, utamkatisha tamaa na kumkwaza au utampa moyo?

Mfano, akute ukiwaponda wanawake wasio na shape halafu yeye muda huo mwili wake haueleweki kiuno kiwapi, tumbo li wapi, yaani ni amorphous fulani hivi. Au ulikuwa unaponda wanawake au wanaume wafupi kama mtungi wa gesi, halafu mtoto wako ndio yuko hivyo. Je, atafarijika au atakata tamaa?

Ndugu Mesimiwa, kwa ridhaa yako naomba nihitimishe kwa kusema, ujumbe wowote utakaoutoa basi angalia na kizazi chako ili usijekuwa baba au mama jinga.

Achana na kauli ya kujifariji kuwa hakuna baba au mama jinga. Hizo ni lugha za kujifariji tu, lakini watoto wanajua hapa wana mzazi au hawana.

Acha nipumzike sasa.

Robert Heriel,
Taikon wa Fasihi,
Kwa sasa Dar es Salaam.
Natumaini nimekuwa mtetezi wa wanawake vya kutosha, kwa kiasi ambacho atafurahia.

Hata sasa kuna wanawake wengi hapa JF wanafurahia michango yangu.
 
Back
Top Bottom