Siku Chief Adam Sapi Mkwawa alipojiunga na TANU mwaka wa 1955

Siku Chief Adam Sapi Mkwawa alipojiunga na TANU mwaka wa 1955

Nafikiri ukitaka kujua historia ya mkwawa nenda karenga kuna sehemu nilisoma kisegere cha mtwa mkwawa akielezea historia ya mkwawa kwamba imetoka kwa mufwimi aliekuwa ametokea ethiopia na muwindaji hodari..mzee mohamed said anasema tena alikuwa mngazija
Our tour of Iringa took us to the museum of the Legendary Chief Mtwa (Abdullah) Mkwawa of the Wahehe tribe. He was a Muslim who fought the Germans in the late 19th century and after his defeat they took his skull to Germany as a trophy.
 
Hakuna udhibitisho wa kujitoshereza kuwa Mkwawa alikuwa Muislam, zinaweza kuwa ni story za kutungwa kama nyingine.

Over.................
Naona akili imekataa kabisa kukubaliana na huu ukweli, kwa faida ya JF tupe wewe basi uthibitisho wa kujitosheleza kuwa Mkwawa alikuwa siyo Muislam.
 
Mkuu! Wamisionari na Wakoloni Ni vitu viwili tofauti?
Powder,
Katika Vita Vya Maji Maji wamishionari na wakoloni walikuwa
wakichukuliwa kama kitu kimoja na wakishambuliwa kama
adui.

Hii ilikuwa mwanzoni mwa miaka ya 1900 wajerumani wakati
wanajaribu kujenga himaya yao Tanganyika.

Katika miaka ya 1930s wakati Waafrika wanaanza kujikusanya
kuleta umoja kupitia African Association wamishionari walikuwa
wakiwakataza waumini wao kujiingiza katika mijumuiko hiyo kwa
kuwa ilikuwa wakiwaeleza watu wao kuwa ilikuwa ikipinga serikali.

Ndiyo maana utaona Wakristo walikuwa wazito sana kujiunga na
harakati za siasa hata TANU ilipoasisiwa 1954.

Taasisi hizi mbili zilikuwa zikisaidiana hili nadhani halina ubishi kwa
ushahidi wa nyaraka za historia.
 
Nimekusoma Sheikh Mohamed Said ingawa andiko lako limejaa ukakasi nianze na hili Uislam ulitangulia kabla ya Ukristo sina ubishi nalo ninapokushangaa ni pale unapoonyesha jaribu kuonyesha Uislam ni dini ya asili ya Afrika (EA) wakati nayo ililetwa na majahari na waarabu.Dini za asili za Afrika zinajulikana wazi Uislam na Ukristo tuliletewa haijalishi ipi ilianza na ipi ilikuja nyuma zote zililetwa.

Umejaribu kuonyesha Ukristo ulifungamana na serekali za kikoloni na Uislam ulipingana na Ukoloni lakini tukichimbua historia ya kudai uhuru wa Tanganyika tunawaona wakristo wa maeneo tofuti tofauti wakipinga ukoloni akiwemo Baba wa Taifa Dr Mwl Julius Kambarage Nyerere.

Sheikh Mohamed Said umeonyesha kupendezwa na ujio wa waarabu/waajemi na Uislam kwa maana hiyo basi kama waaarabu wangebahatika kuitawala Tanganyika wazee wako wa Kiislam wasingekuwa na sababu za kudai uhuru ?????.Dhana hiyo naiona hata leo mnaishabikia huko Zanzibar kwamba Sultan hakuwa na shida utawala wake ulikuwa bora kwakuwa tu ndio walioleta dini ya kiislam na majahazi !.
Mkuu Ngongo kuna kitu hapa kinataka kisiwekwe sawa,Nimemsoma vizuri Mzee wangu Mohamed Said lkn kuna mahali kama anaparuka kupasema:


-Kwanza hapa tujue kuwa Mtwa Mkwawa mwenyewe hakuwa na dini kwa maana ya Muislam au mkristo
Yeye alikuwa mfuasi wa dini ya asili akiamini ktk mizimu na waganga wa kienyeji,baada ya kuwa ameli-
ga jeshi la Mjeruma Mtwa Mkwawa alikimbia na akawa anatafutwa sana na Wajeruma popote alipo.

-Baada ya Wajerumani kumkosa wakaamua kumteka mwanae Mtwa Mkwawa aliykuwa anaitwa Sapi Mkwawa
Wakamchukua na kumpeleka Kilwa,kumbuka Kilwa ndio ilikuwa "Escape area" ya Wajeruman wakati wote
Wa utawala wao.Hata Zelewisky anavyokwenda kupigana na Mkwawa alitokea Kilwa kupitia Usagala

Sapi alipelekwa Kilwa ili kumtumia ujumbe Mkwawa kuwa mtoto wake ametekwa hivyo ajitokeze.Baada ya
Kukaa na Sapi Wajeruman wakampenda kwa aina ya uwezo wake wa kuongoza,wakampeleka Ujerumani na
Baadae wakamfanya kuwa Liwali wa Kilwa,na ili awe Liwali ilibidi aendane na utamaduni wa watu wake,hivyo Sapi akaingia kwenye Uislam na akawa Liwali wa Kilwa.

Kuanzia hapo Sapi na kizazi chake cha kuja chini wakawa Waislam,hivyo hata mwanae Adam Sapi Mkwawa alipozaliwa akawa tu "by default" Muislam.Baada ya hapo wale walio ktk ukoo wa Chief kuanzia Sapi na Adam Sapi wakawa Waislam.Hata baada ya Waingereza kurudisha utawala wa machief,Adam na wasaidizi wakke baadhi walioitwa "Wanzagila" walikuwa waislam

Hivyo sehemu ndogo tu ya Wahehe wa kizazi cha Sapi na mwanae Adam ndio walikuwa Waislam,hata wasaidizi wengine na watu wa karibu na Mkwawa kama kina Mwamgongolwa hawakuwa Waislam na Msikiti Kalenga umekuja kujengwa na Chief Adam Sapi miaka ya 1950's

Muingiliano kati ya Wahehe na Waarabu ilikuwa ni sbb ya biashara,Mtwa Mkwawa alikuwa na "shamba lake la pembe za ndovu" ambazo aliwauzia Waarabu,eneo hilo la "shamba" ndio mbuga ya Ruaha National Park ya sasa(Utakumbuka ndio mbuga yenye tembo wengi kuliko zote)

Walichoinga wahehe kwa Waarabu ni vazi,lkn Muhehe hakutaka liwe kama kanzu,yeye aliita "mgolole" na kichwani alijivika kiremba huku chini akivaa "lubega" nyeupa,hili ndio vazi rasmi la Wahehe mpaka leo

Kumbukumbu za Maandishi ya Kiarabu ya Makumbusho ya Mkwawa,ni yale aliokuwa nayo Sapi wakati akiwa Liwali kule Kilwa,akiwasiliana na wafanyabiashara wa kirabu kwa niaba ya Wajerumani,na Adam ndio aliyejengea kaburi la baba yake Sapi kwa mtindo wa kiislam baada ya kurudi toka Makerere na kukabidhiwa Uchief

Wahehe waliupokea Ukristo Ukatoliki toka kwa Wamisionari,na hasa Wamisionari wa Consolata toka Italia mwaka 1896 eneo la Tosamaganga,baadae Wamisionari hao wakasambaa eneo la Madibira bonde la Ihefu,Rujewa eneo la Usangu,Nyabula,Ilole na Pawaga.Toka mwaka 1896 Vatican ilituma Padre Francesco Caligliero(Mwenye jina la shule ya Cagliero iliyopo Ipogoro Iringa) kueneza Ukristo na kuifanya Iringa kama sehemu ya Metroponia ya Nyanda za Juu za Tanganyika,baadae ilipokomaa ndipo Papa akateua Askofu toka Italy kuja kuwa askofu wa Iringa,huyu Mzungu aliitwa Attilio Betlamino na alifia Tosamaganga na kuzikwa ndani ya kanisa hilo.
Cc barafu UncleBen Ngongo Nyani Ngabu Mimi Mwanakijiji Tangawizi Yericko Nyerere naiman64

Mkuu yani Maelezo yako natamani yakae juu hapo, hafu ya Mzee Mohammed Said ndo iwe comments, Maelezo yamenyooka bila ushabiki WA kuvutia upande
 
Kyenju,
Historia ya Mkwawa ni ''documented'' na Wajerumani yaani imehifadhiwa
kwa maandishi na inaeleweka vyema.

Hili la kuwa alikuwa Muislam wala si jambo la kubishania hii leo.
Imekuwa ni bahati mbaya sana kuwa leo wengi wanatishwa na Uislam.

Lakini ili kumjua vyema Mkwawa inakubidi ujue hali ya nchi ilikuwaje katika
miaka ile ya katikati 1800 wakati Wajerumani wanaanza kujipenyeza nchini.

Angalia ni nani alipigana na Wajerumani.

Utamkuta Abushiri bin Salim al Harith, Sultan Songea bin Rauf, Sultan
Mataka bin Hamin Massaninga, Abdallah Mkwawa, Hassan bin Ismail

na wengine wengi.


Massaninga ni watu wa kabila lipi?
hasa huyu Sultan..?
Itakubidi umjue mshirika mkubwa wa Mkwawa, Rumaliza mzaliwa wa Lindi
ambae jina lake halisi ni Muhammad bin Khalfan bin Khamis al Barwani.

Rumaliza ndiye aliyekuwa akimpa silaha Mkwawa apambane na Wajerumani
na silaha hizi alikuwa akizitoa Zanzibar.

Mimi nimebahatika kukutana na kitukuu cha Rumaliza Dubai mwaka wa 1999,
Sheikh Muhammad bin Said na nilipojua kuwa ni kitukuu cha Rumaliza nilitaka
kujua mengi kutoka kwake.

Rumaliza kapigana pamoja na Mkwawa bega kwa bega na mmoja wa majemadari
wa Mkwawa alikuwa ndugu yake akiitwa Yusuf.

Ukitaka kujua zaidi kuhusu historia hii msome Ali Muhsin Barwani: ''Conflict and
Harmony in Zanzibar.''

Nilikuwa Zentrum Moderner Oriente (ZMO) Berlin kama ''Visiting Scholar,'' hii ni taasisi
kubwa sana ya utafiti wa historia na nimeona nyaraka nyingi sana za Tanganyika enzi
za Wajerumani.

Tusitishike na Uislam.
Tufanye utafiti tuijue historia ya kweli ya Tanganyika.
 
Massaninga alikuwa anatoka mkoa upi?
alikuwa kabila gani?
 
Naam, sasa unaanza kuelewa elewa kiduchu.

Sasa muulize anaejiita Yericko Nyerere anaekataa hilo, hajui jina la kwanza la Mkwawa ni Abdallah.
Acha uongo, Ngariba dume kaeleza vizuri kabisa mpaka chanzo cha karatasi za kiarabu, na kuwa mtoto WA Mkwawa Sapi ndo alikua Mwislam ili awe Liwali Kilwa, na Si Mzee Mkwawa! Mzee Mohammed Said akakubari kuwa Kuna vitu hakuvijua, wewe unaendelea kupotosha hapa!!
 
Acha uongo, Ngariba dume kaeleza vizuri kabisa mpaka chanzo cha karatasi za kiarabu, na kuwa mtoto WA Mkwawa Sapi ndo alikua Mwislam ili awe Liwali Kilwa, na Si Mzee Mkwawa! Mzee Mohammed Said akakubari kuwa Kuna vitu hakuvijua, wewe unaendelea kupotosha hapa!!

Abdallah na Kiarabu akiandika. Usisahau hilo.

Eti kawa Muislam ili akawa liwalo Kilwa.

Kilwa hii ambayo wazungu wa krusedi walipokuja walikuta nyumba zina rangi wakati kwao hakuna? Walikuta watu wanatumia hariri za China wakati kwao hakuna?

Kilwa hii iliyofanywa hifadhi ya dunia na Umoja wa Mataifa kwa historia yake ya Uislam?

Hata haya hamuoni?
 
Abdallah na Kiarabu akiandika. Usisahau hilo.

Eti kawa Muislam ili akawa liwalo Kilwa.

Kilwa hii ambayo wazungu wa krusedi walipokuja walikuta nyumba zina rangi wakati kwao hakuna? Walikuta watu wanatumia hariri za China wakati kwao hakuna?

Kilwa hii iliyofanywa hifadhi ya dunia na Umoja wa Mataifa kwa historia yake ya Uislam?

Hata haya hamuoni?
Mbona unazunguka Mbuyu? Na habari zako za kuungaunga? Hunaga point za maana, msome tena Ngariba dume hapo juu! Wewe Bibi Ni Mbishi kama Mshipa WA Mzee Abdallah Nanjenga WA kule Bagamoyo!
 
Back
Top Bottom