Uchaguzi 2020 Siku hazigandi, mwaka 2020 aliotangaza Rais Magufuli kuwa ndiyo mwaka wa kufanya mikutano ya kisiasa, kwa vyama vya upinzani, ndio huo ushafika

Uchaguzi 2020 Siku hazigandi, mwaka 2020 aliotangaza Rais Magufuli kuwa ndiyo mwaka wa kufanya mikutano ya kisiasa, kwa vyama vya upinzani, ndio huo ushafika

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Mara tu baada ya kuapishwa kuwa Rais wa nchi hii, Rais Magufuli alivipiga marufuku vyama vya upinzani nchini kutofanya mikutano ya kisiasa hadi mwaka 2020, kwa madai kuwa uchaguzi umekwisha, kwa hiyo huo ni wakati wa kufanya kazi na siyo wakati wa kampeni.

Wakati akitangaza hivyo Rais Magufuli, alijua wazi kuwa anaisigina Katiba ya Jamhuri wa Muungano ya mwaka 1977, ibara ya 3(1) ambayo inatamka wazi kuwa "Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, itakuwa nchi ya kidemokrasia na yenye kufuata mfumo wa vyama vingi" mwisho wa kunukuu.

Jambo la ajabu ni kuwa Jeshi la Polisi nchini liliichukulia tamko hilo kuwa ni sheria na kuanza kuwakamata viongozi wote waliokuwa wameamua kukiuka kauli hiyo ya Rais, na kuwafungulia mashitaka ya kuleta uchochezi, ambayo ilikuwa ni uvunjaji wa dhahiri wa Katiba yetu ya nchi, kwani Jeshi hilo linajua wazi kuwa vyama hivyo vipo kwa mujibu wa Katiba ya nchi na kufanya mikutano ya kisiasa ni moja ya wajibu wao mkuu.

Wakati hayo yakifanyika kwa vyama vya upinzani wenyewe CCM, akiwemo yeye mwenyewe Rais, Katibu Mkuu wa Chama hicho. Dkt Bashiru Ally na Katibu Mwenezi wa Chama hicho, Humphrey Polepole, walizunguka nchi nzima wakifanya mikutano ya hadhara na ya ndani, wakifanya kampeni, bila kubughuziwa na Jeshi la Polisi.

Hata hivyo kama nilivyoeleza kwenye kichwa changu cha habari, kuwa mwaka 2020 ndiyo ushafika, kwa hiyo ni wito wangu kwa vyama vya upinzani kutumia fursa hii adimu, kwa kufanya mikutano ya kisiasa, ambayo itaratibiwa kisayansi zaidi, ili hatimaye ifikapo mwezi wa Oktoba mwaka huu wa 2020, wananchi tukafanye maamuzi kwenye sanduku la kura kwa kuking'oa chama hiki cha CCM ambacho kimedumu kukaa madarakani tokea tupate Uhuru wetu, kwa "mbeleko" ya vyombo vya dola vya Jeshi la Polisi na TISS, badala ya vyombo hivyo vya dola kuwa "neutral" kama vinavyotakiwa kuwa kwa mujibu wa Katiba, badala yake vimekuwa mstari wa mbele kuwalinda watawala wetu na kujigeuza kuwa vitengo vya CCM ili watawala hao wasing'olewe madarakani.
 
Nakubaliana nawe Mkuu shungurui kuwa Rais alidhani kuwa mwaka 2020 hautafika!

Ndiyo maana nikasema kuwa siku hazigandi na mwaka 2020 ndiyo huo ushawadia, kwa hiyo hao Polisi watafute sababu nyingine za kuzuia mikutano ya kisiasa kwa kuwa mwaka aliosema Rais Magufuli wa kufanya mikutano ya kisiasa na kwa kuwa wanachukulia matamko yake kwenye majukwaa ya kisiasa kuwa sheria, sasa mwaka huo wa 2020 ndiyo huo ushafika
 
Najua kuwa viongozi wa upinzani nchini wamepitia katika kipindi kigumu sana, chini ya utawala huu wa awamu ya tano, kwani kwa kufanya shughuli zao za halali kabisa za siasa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ibara ya 3(1) wamegeuziwa kibao na Jeshi letu la Polisi kwa kuwakamata na kuwafungulia mashitaka ya uchochezi viongozi hao wa upinzani nchini
 
Kuomba vibali pako pale pale. Msifikiri sasa ndio mikutano yenu hovyo hovyo ya hadhara kila siku imeruhusiwa.
Kwa hiyo Mkuu Magonjwa Mtambuka kwa Katibu Mkuu wa CCM, Dkt Bashiru Ally na Katibu mwenezi Humphrey Polepole kufanya mikutano holela ruksa!

Nyiye CCM mmeligeuza Jeshi la Polisi kama kitengo chenu.........

Kumbukeni wosia aliowapa Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete, katika mkutano mkuu wa CCM mwaka 2012 alipowaasa kuwa ni makosa makubwa kulitumia Jeshi la Polisi kama "mbeleko" ya kuendelea kubaki madarakani

cc: Erythrocyte
 
..mbona Katibu Mkuu wa CCM Dr. AL Bashir amekuwa akifanya mikutano ya hadhara nchi nzima? Kwanini iwe dhambi kwa makatibu wakuu wa vyama vingine kufanya mikutano?
Acha kupiga porojo nimeshakuambia anzeni hata kesho.
 
Acha kupiga porojo nimeshakuambia anzeni hata kesho.
Mkuu Magonjwa Mtambuka mbona mnaiogopa mno mikutano ya vyama vya siasa vya upinzani?

Hivi nyinyi si ndiyo mnajiita kuwa chama dume kisichokuwa na upinzani hapa nchini?

Unataka kujifanya huujui ule msemo unaosema kizuri chajiuza na kibaya chajitembeza?

Hivi kwa kuzoa ushindi wa asilimia 99.9 kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa uliopita, hivi si mngeacha tu hivyo vyama mnavyoviita "vinapumulia mashine" vifanye mikutano yao na vikose wasikilizaji?
 
Unaongea kwa authority utadhani ni IGP Sirro kumbe ni vuvuzela wa ccm tuu! Inawezekana hapo kwenu mumeshijipa hata vyeo vya kipolisi kabisa, sajenti Magonjwa, Koplo Jinga lao, Inspector Barbarossa nk kwa jinsi mnavyosikia utamu unyanyasaji
Mnangoja nini sasa?
 
Nakubaliana nawe Mkuu shungurui kuwa Rais alidhani kuwa mwaka 2020 hautafika!

Ndiyo maana nikasema kuwa siku hazigandi na mwaka 2020 ndiyo huo ushawadia, kwa hiyo hao Polisi watafute sababu nyingine za kuzuia mikutano ya kisiasa kwa kuwa mwaka aliosema Rais Magufuli wa kufanya mikutano ya kisiasa kwa vyama vya upinzani ndiyo huo ushafika
Inaonesha una ID mbili
 
Pamoja na tafakuri yako, jaribu kuhangaikia mkate. Siasa za JF hazitakufikisha popote maana
 
Pamoja na tafakuri yako, jaribu kuhangaikia mkate. Siasa za JF hazitakufikisha popote maana
Wewe unafahamu kuwa siasa ndiyo kila kitu?

Hivi wewe kada wa Lumumba njinjo unasema niachane na siasa, wakati kodi nalipa?

Ni muhimu kwa mwananchi yeyote ndani ya nchi hii ai-discuss siasa, kwa kuwa ndiyo itakayoweza,kumuhakikishia maisha ya kila siku
 
Back
Top Bottom