SEHEMU YA 16
*******************************
Salome alijitahidi kunipa matumaini pale kitanda akaniambia leo nimekuja kukuona nitafanya kila kitu niweze kukuchuku hapa hospitalini nikamwambia sawa,
Salome aliniacha mule chumbani akaenda kuzungumza na madaktari wa pale muhimbili kwamba anataka kunichukua ila madaktari walionekana kukataa salome asinichukue salome alijitahidi sana kuomba na ndipo madaktari walipomwambia aje baada ya siku mbili kwani bado nipo chini ya uangalizi wao ndipo salome alipokubali kishingo upande na kuondoka pale hospitalini akiniacha,
Atimae usiku wa siku hiyo niliweza kurudishwa kwenye wodi ya kawaida na kuchanganyika na wagonjwa wenzangu,
[emoji116]NILIYOYAONA MAMBO YA KUTISHA PALE MUHIMBILI HOSPITALINI USIKU WA SIKU HIYO#
Ndugu msomaji sipo hapa kwa kuisema vibaya hospital ya taifa ya muhimbili naweza kusema hivi kwa kuwa usiku wa siku hiyo niliweza kukutana na mambo ya kutisha sana pale muhimbili,
Ipo hivi usiku wa siku hiyo aisee niliweza kuona mambo ya ajabu sana yanayotendeka muhimbili pale,
1.nilipokuwa nimelala niliweza kuonyeshwa mambo ya ajabu yaliyopo katika vyumba vya mahiti yaani mochwari pale muhimbili nilishuhudia baadhi ya maiti zilizokuwa mule mochwari kumbe usiku uwa zinaamka na kuanza kuzunguka muhimbili nzima,
2.madaktari kuzini na wagonjwa wakati wa usiku,
Ndugu msomaji niliweza kuonyeshwa tabia chafu za baadhi ya madaktari wanaokuwa wakiwabaka wagonjwa wa kike usiku niliweza kuona haya mambo nikiwa pale kitandani najua ni ngumu kueleza mambo yote maana mambo mengine sitapenda kuyaweka adharani lakini jambo moja la mwisho niliweza kuona kuna daktari mmoja pale muhimbili ni wakala wa gamboshi wakala ambae yupo pale kwa kazi moja ya kuaribu mimba na baadhi ya mimba zinazoaribiwa wanazichukua na kuzipeleka gamboshi ambapo wale watoto uchukuliwa na kupikwa kwenye majungu makubwa na wanatengeneza mafuta so yale mafuta wachawi wa gamboshi wanayapaka na yale mafuta yana nguvu sana na kuwapa wachawi uwezo mkubwa wa kutenda mambo yao ya giza,
Ni mengi sana ngoja tuachane na mambo ya muhimbili niendelee na siku ya pili aliyokuja salome kunichukua hii siku salome alikuja pale wakamruhusu salome anichukue pale kweli tulifanikiwa kuondoka muhimbili salome alikuja na gari dogo private nilikuwa sijui naenda kuishi kwa salome na nitaishi vipi nilikuwa nimetulia tu ndani ya gari safari ilianza kuelekea kwa salome ambae alikuwa anakaa mombasa sasa tuliembea mwendo mrefu na atimae kama masaa kadhaa tuliweza kufika kwa salome nilishangaa sana salome alikuwa amepanga katika nyumba nzuri mno alipanganisha nyumba nzima basi tukaingia ndani pale saloome akanikaribisha na kuniambia niwe na amani nitaishi nae hadi nitakapokuwa sawa nikamshukuru kwa wema wake na atimae maisha ya mimi kuishi kwa salome yalianza tulikuwa hatulali chumba kimoja maana nyumba ilikuwa na vyumba vitatu alinipa chumba kingine nilale na yeye alikuwa akilala chumba kingine,
Niliweza kuumaliza mwezi mmoja wa kukaa kwa salome na kila jumapili salome alikuwa akinichukua na kwenda nae kanisani nikajikuta sasa kanisa nishaanza kulizoea niliweza kujiunga na kwaya ya kanisani maana salome nae alikuwa mwanakwaya pia ila pia ni kwamba salome nilimkuta hana mme na alikuwa ameajiliwa ni mwalimu hadi mda huu hadi ninapoandika simulizi hii mimi na salome tunaishi pamoja lakini kwa hivi sasa tupo mkoa wa morogoro tulishahamaga dar na bahati nzuri salome nimefanikiwa kuzaa nae mtoto mmoja juzi kati sasa ni mwezi[emoji39][emoji39] nampenda sana ni mwanamke alienitoa mbali sana.
[emoji116]*************VITA NA JINI FETTY BAADA YA MIMI KUOKOKA
ITAENDELEA BAADAE
[emoji116]BAADA YA SIMULIZI HII KUISHA HAPO KESHO NITAENDELEA NA KISA KINGINE HAPA HAPA NILIVYOWAHI KUPELEKWA GAMBOSHI NA NILIVYOWAHI KUSHIRIKI KUSABABISHA AJALI NA KUUWA WATU HAPA DUNIANI KITUO CHETU KILIKUWA MLIMA SEKENKE
STORI NDIO KWANZA IMEANZA NAOMBENI KWA SASA NIISHIE HAPA USIKU NITAJITAHIDI NIENDELEE VITA NA JINI FETTY BAADA YA MIMI KUOKOKA NA JINSI NILIVYOANZA MAHUSIANO NA SALOME [emoji122]
SEHEMU YA 17
************************
Nikiwa pale naishi kwa salome niliweza kuishi vizuri sana niliweza kuokoka na kuanza kumjua mungu mungu alinibadilisha sana nilifurahia maisha yangu mapya ya kidini siku zilienda zilienda nakumbuka usiku mmoja tupo na salome tumetoka kanisani tulikuwa tunakula chakula salome aliniambia kuwa mungu kanibadilisha nimekuwa kijana mzuri sasa,
Salome alikuwa akiniangalia macho ya kimahaba pale sebureni tukajikuta rasmi tumeanza mahusiano niliweza kulala na salome kwa mara ya kwanza toka niachane nae enzi hizo za shule usiku huo tuliweza kuenjoy sana mahaba yetu salome ni mwanamke mtamu mno na anaejua nn mwanaume anataka aiseee usiku huo ulikuwa usiku mtamu kwangu licha ya kuwa na mahusiano na jini fetty ila hakuwahi kunipa mapenzi kama haya ya salome,
Mahusiano yetu na salome yalipamba moto huku pia nikiendelea kuzidi kumtumikia mungu sasa kanisani nikawa maarufu kutokana na upigaji wangu wa kinanda pale kanisani kwa wakati wote sikuwahi kukutana tena na jini fetty hadi nikahisi huenda atakuwa ameniacha huru,
Ulipita kama miezi sita nipo na salome mke wangu maisha mengine yanaendelea huku mimi pia nikiendelee na shughuli za ufundi wangu kama kawaida maana sasa nilikuwa nishapona nilikuwa naweza fanya kazi,
Nakumbuka siku moja nilikuwa natoka zangu kivule narudi mombasa nilikuwa nipo kwenye piki piki yangu ndugu msomaji mungu alinibariki nikaweza kununua na mimi ka usafiri kangu piki piki,
Tuendelee na stori sasa nipo njiani natoka kivule na rudi kwangu mombasa ghafla nikamuona mdada mmoja ananipungia mkono kuomba lifti na mda huo ulikuwa kama saa moja kasoro ka jiza bado hakajaanza kuingia nilisimama akaniambia kaka samahani naomba lifti nikamuuliza unaelekea wapi ni mdada mzuri mweupe flani hivi akaniambia anaenda mombasa,
Nikajikuta na mwambia woow na mimi naenda mombasa basi wacha twende basi hao safari ikaiva kuelekea mombasa sasa katika kupiga piga stori yule binti alinishangaza sana alikuwa ananijua mimi kuliko mimi ninavyomjua yeye alianza kwa kuniambia naona siku hizi umeokoka? swali ambalo lilinipa shaka nikajiuluza kajuaje nikamjibu umejuaje? Akasema unaonekana tu ni mtu wa mungu nikacheka tu huku nikizuga kwa cheko la kinafiki ila nilishtuka na swali lake,
Sqsa tulipofika mombasa pale akaniambia nimshushe yeye anaelekea mtaa x lakini wakati tunaagana akaniambia kitu kingine kilichonipa mashaka zaidi aliniambia msalimie mkeo salame hii kitu kilinifanya nimuite lakini akaendelea kuondoka nikataka ninfuate nimuulize ww ni nani na unaoekana unanijua mimi vizuri ila nikasita ikabidi na mimi nirudi tu nyumbani usiku wa siku hiyo ulikuwa wa mawazo kwangu ikabidi nimwambie mke wangu salome kile kilichonikuta leo mke wangu akanipa hope akasema usimuwazie sana pengine labda anakufahamu si unajua ww siku hizi unavyofahamika pale kanisani huenda nae ni mshirika mwenzetu pale kanisani nikasema sawa sasa wakati tunapiga stori na mke wangu salome,
Ghafla simu yangu ujumbe wa sms ukaingia ujumbe ambao ulinishtua sana ulikuwa ukisema ongera kwa kunipa lifti leo by mkeo wako wa muda wote fetty sms hii ndio iliyonitoa gizani nikahatamaki sana niliweza kumuelezea mke wangu na kumuonyesha hiyo sms nae akashangaa akasema mume wangu kama jini fetty kaqanza tena kukukufuatilia bqsi hii vita ni kubwa mno inatupaswa tuzidishe maombi kwa mungu wetu suala ambalo nililiona ni la msingi ila asubuhi niliweza kwenda kwa mchungaji wetu pale kanisani sasa nyumbani kwake kumuelezea mambo yamezidi kubwa mabaya mchungaji akanitia hope kuwa leo tutapiga swala nzito na mambo yatakaa sawa kweli usiku wa siku hiyo mchungaji alikuja pale kwetu tukafanya maombi mazito tulifanya maombi kama masaa matano mchungaji akaondoka ila alinishauri kesho tufunge mimi na mke wangu huenda mungu ataepusha ili balaa la jini fetty kunirudia,
Wakuu itaendelea