NDABO nimepita hapo advance 2009-2011Wale wazee wa Ndanda boy shule safi siku nimeripoti tumelala vizuri saa kumi na moja naskia kiongozi mmoja anapayuka form five amkaaaaaa!!! Huku akiimba wimbo wa blood (the game ft Damian Marley) basi huu wimbo lazima niwe nao kila kwenye music devices zangu!!!
Alirudi kesho yake akafikia ofsini kwa walimu ndio wakamleta mabwenini... Shule za wavulana zina vituko sana..Hahaa daah nimecheka kwa nguvu..na hakuja tena?
Ahaaa sawasawa mtoto wa Lulukila mi 2007-2009NDABO nimepita hapo advance 2009-2011
Mleta mada sijui umewaza nini.
Siku naingia shule kanda ya Pwani nimetoka zangu huko kanda ya ziwa, mambo yote naona hovyo tu, lafudhi yangu haiendani na mtu yeyote mjini, kila ninayezungumza nae ananiuliza umetokea sehem .... eeeh
Wanafunzi wa kidato cha sita walinipokea wakanisaidia kubeba tranka, tukafika ofisini nikakuta jopo kubwa la walimu wanafanya registration, wakaniuliza jina nikataja, wakatafuta fomu zangu wakaziona wakajiridhisha nikatoa barua ya joining instruction.
Nikapangiwa bweni, nikaelekezwa nikazama fresh.
Kimbebe ilikua ni chakula cha jioni ile, ugali una unga unga kibao, maharage machache mchuzi ndio mwingi, unaweza kumwaga mchuzi ukabaki na maharage yako ukayahesabu moja moja. Nikala fresh ila kiungulia kilinisumbua sana.
Maji ya kuoga ni shida, ya kunywa ndio kabisa.
Life likaanza walimu wapo ila hawafundishi kila mtu ana mishe zake tu, kitabu kigumu mimi sikuwahi kusoma tuition ya pre form five kule shule nakuta watu wamekata topics karibu wamemaliza syllabus ya form five, siku ya kwanza tu naona wenzangu wanaenda prepo kujisomea, wanabeba Scientific calculators, mimi hata calculator sina wala sijui kuitumia, sina materials zozote nina madaftari yangu mapya 3 quires mengi tu, hata sijui niandike nini, yaani advertise tu masela wanarudi bwenini saa tano saa sita mi nishalala, mwili wote una nata majasho kwakua maji ya kuoga hakuna.
Suala la msosi ni ishu, chai ya rangi inapikwa nyeusiii majani kibao, maji ya chumvi alafu sukari hawaweki na wakiweka ni kwa mbali sana kitafunwa ujitegemee, ukinywa kama vile unakunywa orals.
Mwalimu wangu wa darasa alikua na roho mbaya kinyama, kosa dogo anaweza kukushupalia ukafukuzwa shule.
Hii shule ndio mtoto wa Rais Magufuli alichemka tumeripoti nae siku moja, asubuhi uzalendo ukamshinda akapiga simu akafatwa na Land Cruiser V8.
Hapana Magu ana mtoto wa kiume nimemsahau jina tu ila tulipangwa nae shule moja na tukaripoti siku mojaMtoto wa Magu Jesca?
Soma title ya uzi mtoa mada amespecify shule za serikaliKila mtu anaongelea form five, wenzenu tumeanza boarding tangu standard 5 enzi hizo za Nyerere tunapiga mchaka mchaka kila asubuhi na kupiga gwaride na ngoma kuingia darasni lakini lazima kwenda kwenye ibada ya asubuhi. Ilikuwa shule ya Fransiscan sisters. Mlo mzuri. Sec. Ilikuwa the best when it comes for food and accademic. Sitasema maana nitajulikana wapi. Ila atakayejua nani waliwaita wenzie Pimbi atajua nilisoma wapi.
Ok hiki ninachoandika ni off topic.
Kuna jamaa aliripoti shule, bishoo si mchezo. Kuna jamaa akawa anamuonea onea tu akimkuta anakula anachukua chakula, anachukua madaftari yake. Halafu anamwambia kama unaweza si upigane? Ishu ilienda kama mwezi.
Maji yakikata kuna kama kijito cha maji ndiyo hua tunayafuata, basi yule bishoo akavaa traki raba na fulana akamkuta mshkaji yupo na sisi akamwambia twende mtoni. Jamaa akajibu kwa dharau "Unataka nikakuf.ire?" mshkaji akajibu hapana nataka tukapigane, Ila tuwe wawili tu atakayerudi shule hapa ndiyo mshindi, jamaa akakubali wakaenda.
Dakika 10 nyingi tunamuona bishoo anarudi. Akatuambia kamchukueni jamaa, tumefika kule yule jamaa kila unapomgusa analia akafuatwa na gari la shule gari lenyewe wipers hazifanyi kazi na ukungu umeshakuja ikabidi mmoja akae kwenye boneti awe anafuta futa na mwendo uwe wa kobe.
Baada ya kupona akatuambia "Yaani sijaambulia hata ngumi moja, huyo jamaa hafai" kumbe yule bishoo ni mshindi wa Judo ngazi ya mkoa huko mkoani kwao. Halafu ikatokea wakawa marafiki vibaya mno.
Kumbe je[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Kwamba bado unakula ujana ee
Ye hauzi sura hataki kuwa mbunge?Hapana Magu ana mtoto wa kiume nimemsahau jina tu ila tulipangwa nae shule moja na tukaripoti siku moja
Hata sijui yuko wapi maana baada ya kuondoka sikuwahi kumsikia tena wala kumuona kwenye tv hata mtandaoni sina uhakika kama anaingia.Ye hauzi sura hataki kuwa mbunge?
Tumesoma wote mbona.Najaribu kusoma comments nione hata mtu nimesoma nae shule moja sioni maana shule yetu ilikuwa mojawapo kati ya shule za ajabu kuwahi kama kutokea
Haha kuwa na baba kama yule ni shida jamani bora awe mlima korosho huko unaweza hata kumpiga chenga ya mwili. Hujawahi kufikiria kuwa huenda ali RIP? (God forbid)Hata sijui yuko wapi maana baada ya kuondoka sikuwahi kumsikia tena wala kumuona kwenye tv hata mtandaoni sina uhakika kama anaingia.
Inaelekea familia ya Magu inaishi kama iko jeshini
Nitakutumia ile sumu ya warusi. Hahaha.[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Ngoja nimfowadie hii sms class mate wako(joking)
Wewe acha mambo yako usome na nani? Enzi hizo mimi niko advance we wanakupangusa kamasiTumesoma wote mbona.
Sijui kwakweliHaha kuwa na baba kama yule ni shida jamani bora awe mlima korosho huko unaweza hata kumpiga chenga ya mwili. Hujawahi kufikiria kuwa huenda ali RIP? (God forbid)
Secondari nilisoma shule ya serikali wakati huo Private zilikuwa kiduchu. Naongelea late sixties and early seventies. Halafu sisi tulikuwa watoto wa wakulima maskini tusingeweza kumudu hizo shule.Soma title ya uzi mtoa mada amespecify shule za serikali