Siku ya Kwanza Kuongea Kiingereza mbele ya Kadamnasi kidogo nizimie

Kwenye mgodi mmoja wa dhahabu jamaa mshahara umechelewa kajikongoja mpaka kwa mzungu akamwaga lugha" I have 3 days without eating"mzungu akamjibu no appetite?jamaa akaona ujinga appetite ya wapi acheni mambo ya kisenge tupeni mishahara yetu kingereza chako huko huko mi nipeni changu
 

Hahahhahaha,,,hatari hii kitu!!
 
English ni janga hasa la kitaifa,nakumbuka mwaka 1995 kuna mbunge (jina kapuni) alihojiwa na waandishi wa habari nje ya ukumbe wa bunge mjini Dodoma baada ya waziri wa fedha kusoma bajeti ya mwaka, aliulizwa anaionaje bajeti yeye akajibu kwa mbwembwe eti "This exellency is very budget"
 

ha ha ha! jomba kwenye ds 101 mm nlikuwa mshka chaki na kufuta ubao chezea ngeli kwa Coet ww
 
Jamani kwa kuwa kiingereza ni cha muhimu kwa kweli ni muhimu kujifunza. Tena kwa vijana wa siku hizi mna fursa tele. Kuna shule wanafundisha kiingereza. Kuna mainternet jamani tutumie fursa mbalimbali ili tuweze kumudu lugha hii ni muhimu. Halafu kuna masomo hayahitaji sana kiingereza hivyo usione aibu polish kiingereza chako kwa kuona wengine watashangaa labda elimu yako ni ya chuo. After all si azima wajue level yako ya education.
Fursazipo nyingi lakini ndio hivyo zinahitaji kiingereza. Juzi tu nimesoma MichuziUN organization zinataka vijana miaka 32 kuteremka chini. Kutakuwa na writtenExam na watakaofaulu watatakiwa kufanya oral Exam. Kwa subject matterwa-Tanzania sisi ni hatari tatizo sasa ni lugha.Tuepushe janga hili kwa watoto wetu jamani. . Hata km hawatasoma English medium schools ( Curriculumyetu bado ni nzuri relatively) tafutanamna yoyote labda masomo ya ziadakwenye kiingereza. Nilifurahia sana nilisoma Historia ya mama yake Obama. Alikuwaanaamka na kumuamsha mtoto wake ( Obama) kila siku saa kumi alfajiri Kumfundishamwanae ku-cover mapungufu ya shule aliyokuwa anasoma Indonesia
 
Kiukweli mazoezi ya kuongea kila mara, kuangalia TV (News, series) za kiingereza, magazeti na Vitabu vya kiingereza vitakuza uwezo wako katika lugha husika
 
mimi marks 10 zisingenifanya nidhalilike mbele ya mademu na ukizngatia chuo nilikuwa tozi balaa si unajua nilikuwa napata hela kila kona Bodi ya mikopo, Home na kwa bro na ndegu wengine, sema sasa maisha yashanichapa sina ujanja.

Hahaaa choka mbayaaa
 
Imenigusa hii mada.mimi nakumbuka ilikuwa form two,nikachukua form ya kugombea uprifekti sasa ishu ikaja kujinadi mbele ya hadhira kwa kiingereza jasho lilinitoka sikujua hata limetoka wapi huku naona kizunguzungu nilichanganya kikwetu na kiingereza sijui kama walinielewa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…