Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hahahahahahhahahaha basi basiKiingereza si masikhara aisee kuna Mzee Mmoja maarufu alishawahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa DSM, kisha Katibu Mkuu wa Chama cha Siasa M... jamaa ngeli ilikuwa haipandi akipata wageni wa kuongea nao kiingereza ama asingizie anaumwa au amsukumie Katibu Tawala ha ha ha... Chezea Lugha wewe
Hii yellow book naijua hii!!Siku moja tupo kwenye seminar ya koz moja inaitwa rural agricultural economy maarufu kama YELLOW BOOK kwa waliosoma SUA wataelewa, basi picha moja ilikua imebandikwa ukutani ikapulizwa upepo ikadondoka chini jamaa kule mbele akiwa na maiki alisema "what is that, ooh the picture drop down without becouse" basi tulicheka sana
Nakumbuka chuo kuna jamaa alikuwa akiulizwa swali, kisha akaambiwa simama kuchangia lazima apumue.... Hadi siku moja Lecture akamuuliza hivi huwa unafanya makusudi au bahati mbaya? Akajibu namimi nashangaa yananikuta nikijibu kwa kingereza.Wandugu kama mjuavyo wengi wetu tumesoma shule za st. Kayumba kwa hiyo Ngeli ni ishu kwetu. Basi kwa kuunga unga hivyo hivyo nikachaguliwa Chuo (UDSM) sasa kufika huko si ndo mambo ya Seminar za DS 101 natakiwa ni-present ilikuwa balaa usiku kabla ya seminar sikulala naogopa.
Kwenye seminar yenyewe sasa jasho lilinitoka mwili mzima balaa yaani naona nyota nyota tu daah! sitaki kukumbuka. Lakini namshukuru Mungu baada ya pale nilifanya bidii y kujifunza kwa kusoma zaidi vitabu vya kiingereza na kuongea na watu wasiojua kiswahili (hasa waganda, Wazambia & Waganda).
Angalau sasa mambo si mabaya Ulimi si mzito tena kiviile!!! English aisee ni hatari jamani. SHIKAMOO KIINGEREZA
Without because hahahaSiku moja tupo kwenye seminar ya koz moja inaitwa rural agricultural economy maarufu kama YELLOW BOOK kwa waliosoma SUA wataelewa, basi picha moja ilikua imebandikwa ukutani ikapulizwa upepo ikadondoka chini jamaa kule mbele akiwa na maiki alisema "what is that, ooh the picture drop down without becouse" basi tulicheka sana
Kumbe jamaa alishiriki na yeye??Hahahaaaa muulize le mutuz alivotoka jasho kwenye upara alipokuwa anaongea kiingereza kuomba kura za ubunge wa EAC
Hahaha kumbe mnakimbiaga wengine.duuh kwa kweli unastahili pongezi mimi mbona ningetoka NDUKI tu kwani Seminar presentation ilikuwa na marks ngapi? sidhani kama zinazidi marks 10
Nakumbuka jamaa kabla ya seminar alikariri sana , sasa wakati wa presentation akasau neno basi akakauka mpaka dakika zake zimekwisha akarudi kukaa, class nzima iliangua kicheko.. seminar leader akampa zero out of ten..... jamaa aliporudi rum akasema ''leo nimeumbuka na kwa mtindo ctapata demu tena hapa chuo.''
mwingine aliwahi sema:
why? then akajibu because kwa sababu.
Yaan mambo ya seminar acha tu.