Siku ya kwanza kupika ilikuwaje? Ulichopika kiliiva?

Siku ya kwanza kupika ilikuwaje? Ulichopika kiliiva?

Mpaka umri huu sijawahi kumaster jinsi ya kusonga ugali , naweza kuupika ila kipimo huwa kinanipa shida sana ! Naweza kupika mkubwa sana kupitiliza au nikapika ugali mdogo sana hata mtoto hashibi ! Ila ile kukadiria kipimo exactly sijawahi !! Angalau naweza kuuivisha 😂😂😂
Kama mimi tu mkuu. Ila mimi nachojitahidi ni kuchagua sufuria dogo ama kubwa kulingana na ukubwa wa ugali naoutaka.

Kwahiyo hilo nalisolve kiivo ila kama ingekua sufuria size moja apo ningekua nachemka daily.
 
Wakuu,

Mimi nakumbuka nilijaribu kupika wali. Nikaandaa kila kitu freshi, weka mchele wangu safiii 😂😂😂. Wakuu nilitoa bokoboko si la nchi hii, jina likabadilishwa fasta nikaanza kuitwa bokoboko😂😂. Mpaka nilipokuja kuuwezea ubwabwa nilishazoea na jina la bokoboko.

Vipi wewe, siku ya kwanza kupika ilikuaje? Ulichojaribu kupika kilitokea freshi au ulienda kumwaga kimya kimya?
Wali ulikuwa na mawe ya kutosha
 
Nakumbuka nilipewa mchele nianze pishi, nikabandika maji yangu mengii nili nije kupunguza yatanisaidia kuongezea baadaye ikitokea wali bado haujaiva, yalivochemka nikaweka mchele kila nikiangalia maji naona yatatosha bana si mengi sana hivyo haina haja ya kupunguza, Nikatulia zangu nasubiri kila nikifunua maji hayakauki tu, eeh nikaona sasa ngoja nipalie makaa juu na chini uendelee kuchemka, aah maji bado tu, mama akaja kucheki duh boko kama uji kabisa, akaniambia hili boko ntalimaliza mwenyewe na hamna kutupa chakula[emoji3][emoji3]. Akaanza kupika mchele mwingine tu
wee naona tusubiri after 2 -3 yrs, maana uta kuja kupika matapu tapu😃🤣
 
Nilianza kupika nikiwa mdogo, na ndo mtoto pekee pale home aliyejua kupika akiwa mdogo.

Nimeanza kujifunza kupika ugali, nikiwa awali, nlikua kwa shangazi,

Mie ni mtundu na mfukunyuku wa kujua mapishi mbali mbali, hivyo kwenye kuandaa masapta sapta niko [emoji91][emoji91][emoji91]
 
Nakumbuka wife alipojifungua mtoto wa kwanza,kwa siku za mwanzo kazi nyingi ikiwemo ya upishi nilikuwa nafanya mwenyewe,sasa siku hiyo nikasema acha leo nikanunue samaki wale wakubwa nije nipike,nikaenda sokoni nikajipatia kitoweo changu nikarudi nyumbani kupika,nikamwandaa vizuri,nikaandaa na viungo pia vitunguu hoho nyanya limao na tangawizi,nilipomaliza kuweka viungo vyote na samaki jikoni nikasema acha nikaoge maana nilikuwa nahisi joto kutokana na kukaa jikoni muda mrefu,nikasema acha nijaze maji ili asije akaungua,nikaenda kuoga,nilipomaliza nikarudi,nikasema acha nifunue chungu huenda samaki wangu atakuwa ameshaiva Lahaula!!! Kuangalia nakuta samaki alishafufuka na kula vitunguu vyote yupo ananitazama tu,kumbe kile kitendo cha kujaza maji lilikuwa ni kosa kubwa sana.
 
Nakumbuka wife alipojifungua mtoto wa kwanza,kwa siku za mwanzo kazi nyingi ikiwemo ya upishi nilikuwa nafanya mwenyewe,sasa siku hiyo nikasema acha leo nikanunue samaki wale wakubwa nije nipike,nikaenda sokoni nikajipatia kitoweo changu nikarudi nyumbani kupika,nikamwandaa vizuri,nikaandaa na viungo pia vitunguu hoho nyanya limao na tangawizi,nilipomaliza kuweka viungo vyote na samaki jikoni nikasema acha nikaoge maana nilikuwa nahisi joto kutokana na kukaa jikoni muda mrefu,nikasema acha nijaze maji ili asije akaungua,nikaenda kuoga,nilipomaliza nikarudi,nikasema acha nifunue chungu huenda samaki wangu atakuwa ameshaiva Lahaula!!! Kuangalia nakuta samaki alishafufuka na kula vitunguu vyote yupo ananitazama tu,kumbe kile kitendo cha kujaza maji lilikuwa ni kosa kubwa sana.
😂😂😂😂
 
Back
Top Bottom