Siku ya Mwanamke: Bi. Mwamtoro bint Chuma wa Mtaa wa Kariakoo

Siku ya Mwanamke: Bi. Mwamtoro bint Chuma wa Mtaa wa Kariakoo

Mzee.
Naona ajabu tena kubwa kila kukicha wataja tu wanaharakati wa Kiislamu kwenye kupigania Uhuru wetu. Yaani ni kama vile Uhuru uliokuwa unatafutwa ulikuwa wa kusimamisha Dola ya Kiislamu
 
Mzee.
Naona ajabu tena kubwa kila kukicha wataja tu wanaharakati wa Kiislamu kwenye kupigania Uhuru wetu. Yaani ni kama vile Uhuru uliokuwa unatafutwa ulikuwa wa kusimamisha Dola ya Kiislamu
Uzalendo...
Hivi ndivyo historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika ilivyokuwa.

Inakushangaza?

Wala haikuwa kusimamisha Dola ya Kiislam.

Waasisi hawa wengi wao wakiwa ni Waislam wangekuwa na fikra hiyo wangeivuruga nchi.

Hili walilitambua na ndiyo kisa cha Nyerere kupewa uongozi wa TAA 1953 na 1954 ikaundwa TANU Mwalimu akaongoza harakati za kudai uhuru.

Tafuta hapa JF historia ya Uchaguzi wa TAA Arnautoglo Hall baina ya Abdul Sykes na Nyerere.

Kisa cha kusisimua.
Angalia hii video utaelewa:

View: https://youtu.be/YnlrD3dVZpo
 
Angalia hapo juu picha ya Bi. Mwamtoro bint Chuma mama yake Sheikh Haidar Mwinyimvua.

Picha hii inamwonyesha Bi. Mwamtoro bint Chuma akipiga kura Uchaguzi Mkuu wa 1970.

Bila ya shaka yoyote kura yake ilikwenda kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Haiwezi kuwa vinginevyo.

Bi. Mwamtoro alikuwa mmoja wa akina mama waliokuwa mstari wa mbele katika TANU.

Bibi huyu aliishi zaidi ya miaka 100 na alifariki tarehe 11 May 1981.

Nyumba yake ilikuwa Mtaa wa Kariakoo na New Street No. 69 nyuma ya ofisi ya TAA miaka ya 1930 na nyuma ya TANU katika miaka ya 1950.

Hii nyumba hivi sasa iko nyuma ya ofisi ndogo ya CCM, Lumumba Avenue.

Nyumba hii yenye historia kubwa katika kupigania uhuru wa Tanganyika bado ipo katika mikono ya familia ya Mzee Haidar Mwinyimvua.

Nyumba mbili hizi, Ofisi ya TANU na nyumba ya Bi. Mwamtoro ilikuwa zilikuwa katika miaka ile zkitenganishwa na ua wa makuti.

Siku ya mkutano wa ndani wa TANU Nyerere akija kuzungumza na wanachama wa TANU haya makuti yalikuwa yanaondolewa hivyo kuunganisha nyua hizi mbili kuwa ua mmoja.

Wanawake wakikaa nyuma na wanaume wakiwa mbele.

Huu ndiyo ulikuwa uwanja wao akina Bi. Titi Mohamed, Bi. Hawa bint Maftah, Bi. Tatu bint Mzee, Bi. Chiku bint Said Kisusa kwa kuwataja wachache.

Wakimaliza mkutano wanawake walikuwa wanaingia kwenye nyumba ya mtoto wa Bi.
Mwamtoro, Haidar Mwinyimvua.

Nyumba hii mlango wake ulikuwa Mtaa wa Udoe ukitumiwa makhsusi na wanawake kwa kuingia na kutoka kuepuka kupishana na wanaume.

Wakati wa uhai wake marehemu Rashid Mfaume Kawawa aliwaambia ndugu zake Sheikh Haidar Mwinyimvua kuwa nyumba yao hii imebeba kumbukumbu nyingi za harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika na endapo watataka kuiuza basi wakifikirie chama kwanza kabla ya mnunuzi mwingine.
Hahahahahaha..kwa jinsi ulivyoandika na vile napajua hapo basi nimevuta taswira ya eneo lote hilo ..je hii nyumba ndio ile inatazama geti la Jengo la ccm mkoa ? Iliko hotel ya wasomali ..baada ya wasomali ofc za gazeti sikumbuki jina
 
Ukisikia msemo "kujitolea hali na mali" basi hawa ndio mfano mkubwa kwa jitihada zao katika kudai uhuru.
Ingefaa hizi sehemu muhimu katika historia zinge bandiikiwa vibao vidogo (plaque) kueleza kwa muhtasari tukio la kihistoria lililo tokea kwenye nyumba hiyo.

Hivi vibao vinatumika sana nchi nyingi kuelezea matukio ya kihistoria katoka jengo hata kama kwa sasa linamilikiwa na mtu mwingine.
Wazo zuri sana
 
Hahahahahaha..kwa jinsi ulivyoandika na vile napajua hapo basi nimevuta taswira ya eneo lote hilo ..je hii nyumba ndio ile inatazama geti la Jengo la ccm mkoa ? Iliko hotel ya wasomali ..baada ya wasomali ofc za gazeti sikumbuki jina
Tre...
Ndiyo hiyo.
 
Back
Top Bottom