Siku ya Wanawake Duniani isitumike kutengua maandiko ya vitabu vitakatifu

Siku ya Wanawake Duniani isitumike kutengua maandiko ya vitabu vitakatifu

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2019
Posts
762
Reaction score
6,984
Kuna hii kitu yetu inaitwa siku ya wanawake, kuna hii kitu inaitwa super woman na kuna hii kitu tumeanzisha inasema mwanamke ni kichwa cha familia.

Wanawake kuna sehemu tumetumbukizwa shimoni na wapigania haki za wanawake na bila kujijua tumejaa viburi na sasa tunajitokeza hadharani kudai sisi kwa asilimia kubwa ndio tunalisha familia.

Wanawake wengi wenye mentality kwamba wanalisha familia ndoa zao zimeyumba na watoto wapo taabani kimalezi kwa sababu tu walezi wamepishana.

Dini zipo na zinaeleza vyema lipi jukumu la mwanamke ila kwa kasi tuliyonayo imetufanya twende kinyume kabisa na maandiko, tukipata nguvu kidogo tu ya uteuzi au kupata kamtaji kwetu tayari ni agenda yakuwaumiza wanaume. Wanaume wakituchoka wakaondoka hapo ndipo tunajua sisi kamwe hatuwezi kuwa kichwa cha familia.

Tukubali tukatae tunapaswa kuishi na wanaume kama vichwa vya familia na sisi ni mkia. Tukijitutumua na hadithi za super woman tutaishia kutumiwa na makundi ya wanaume huku tukiwa tunakwama kwenye malezi. Tuwaheshimu waume zetu regardless ya vyeo vyetu na madaraka au fedha zetu.

I'm not thinking of superwoman rather gifted woman.
 
Mama wewe ni moja ya wanawake wenye akili sana.
tutaishia kutumiwa na makundi ya wanaume huku tukiwa tunakwama kwenye malezi
Mwanamke yeyote anaelilia haki sawa hawezi kuishi hata na hawara. Ataishia kutumika tu sababu ya kiburi wanachopewa na Serikali na Wanaharakati haramu wa 50/50.

Ukiwa Mwanaume ukishabukia haki sawa nakuona punguani sana, tena uliebobea.
 
Vitabu vimemfanya mwanamke kuwa chini ya mwanaume, sasa kuna ulazima mwanamke nae apambanie haki yake, kuna wanawake wengi wenye akili na maarifa kuliko wanaume wengi, wanayo haki ya kuwa juu ya wanaume kama wamewazidi akili na maarifa.
 
Wanaanza kutupanda kichwani.. Mmesifiwa mbio mnapitiliza kwenu.
MWANZO 3: 16 Akamwambia mwanamke hakika nitakuzidishia uchungu wako, na kuzaa kwako, kwa utungu utazaa watoto na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, NAYE ATAKUTAWALA.

Wa kulaumiwa siyo wanawake bali viongozi wa dini. Hawa wamekuwa wakifumbia macho maandiko. Wanahubiri kupata watoto, kuwa na maisha mazuri na miujiza mbalimbali, lakini hawataki kuwaambia wanawake maandiko yanataka waishije katika ndoa.

Serikali nayo imekazana kupiga vita mfumo dume wakati mfumo dume ndiyo utawala wa mbinguni. Mbona Yesu hakuchagua mwanamke hata mmoja kuwa mtume katika wale 12, akaona bora Yuda atakayemsaliti. Na ndiyo maana mbinguni HAKUNA MALAIKA MWANAMKE.

Kinachotakiwa kupigwa vita siyo MFUMO DUME bali ni UKATILI WA KIJINSIA.
 
Back
Top Bottom