Utotole
JF-Expert Member
- Oct 28, 2010
- 6,607
- 4,263
Umenikumbusha ID yangu ya kwanza kabisa nahisi ilikuwa 2008 au 2009. Member ambaye ni mfanyakazi mwenzangu alinishauri nijiunge. kwanza nikawa nasoma tu comments za watu ila siwezi kuchangia. Baada ya muda nikajiunga ila ID yangu ilikuwa na jina langu kabisa. Post yangu ya kwanza kwenye mjadala wa kisiasa nikamwaga nyongo ya kutosha dhidi ya serikali. jamaa alipoiona ikabidi anieleze kuwa inatakiwa niweke ID isiyonitambulisha kabisa. Kuanzia hapo nikajizuia kutoa comments zozote, nikawa msomaji tu.Mkuu embui angalia mm na wewe nani wa kwanza kujiunga humuu!!
tena hii ni ID mpyaa, ukitaka nakupa ya 2010
Ila kipindi cha uchaguzi mkuu (mara tu baada) uzalendo ukanishinda, maana nilikuwa na mahasira nisingeweza kusoma tu bila kuwajibu binadamu wa mrengo mwingine. Nikajisajili upyaaaaaaaa, na ile ID nadhani ilishapotelea mbali.