Silaha za Masafa Marefu Zinazomilikiwa na JWTZ

Silaha za Masafa Marefu Zinazomilikiwa na JWTZ

Acha uongo T-4 haijawahi kutumika kwenye vita yeyote.
😅😅😅 Bora ume sema wewe, nimeshangaaa kishenzi na kuona hapa kuna upenzi flani wa ki magharibi na marekani hiyo kifaru nimeshtuka kusikia imetia team hadi ukraine nikapuuza na mada husika
 
Wewe unawaza kitu kimoja tu? Dunia hii ni multidimensional; jifunze kuwaza mambo mengi kwa pamoja. Thread hii ni ya kuhusu silaha za masafa marefu za kutoka Urusi zinazoweza kuwa ziko Tanzania (hatujui kama jeshi letu linazo kweli). Ukitaka mambo ya Kilimo, tukutane kwenye thread nyingine.

Ukraine wanalima sana, in fact ni kati ya nchi zinazozalisha ngano kwa wingi sana duniani lakini leo wamevamiwa. Unadhani wasingekuwa na silaha za kujihami wangekuwa wapi sasa.

Kama hutaki silaha basi futa jeshi.
Usichukie,nukuu point yangu,Tanzania haina uwezekano wa kuvamiwa kama Ukraine,ukiangalia historia ya Ukraine na Tanzania tuko tofauti sana,Tanzania inafanana na nchi kama Uswisi,tukitumia fedha nyingi kwenye zana za kivita ni upotezaji wa fedha,zana zilizopo zinatosha kwa ajili ya maonyesho ya tarehe 9 December na siku ya uhuru.
 
Umeandika mada inayofikirisha Sana. Naamini wahusija JW wanaelewa hasa nini cha kufanya. Pia naamini kama kweli Russia hatengenezi tena mizinga hiyo kutakuwa na another alternative. Kwa kuwa ingawa hatupigani vita lakini huwa wanafanya manunuzi ya vifaa vita.
Mkuu hatuna silaha mkuu ingia online uone.

Active presonnel wenyewe ni 27,000 tu
 
Kiduku aweze Marekani ashindwe? Haya ni maajabu ya dunia. Hata kama hatuwapendi Wamarekani tuwe wakweli yeye ndio mbabe wa dunia.
Kuna watu wanaleta maneno ya vijiwe vya kahawa.
Lini amewapi kusikia majaribio ya silaha Us?

Anatishwa na hivi vimasikini kama Korea kaskazini?
Huyo akiamuliwa ni siku moja tu anapotezwa.
Kwenye sila Us hajapata mshindani.
Ana silaha ambazo hakuna taifa linazo
 
Urusi hajatumia silaha mpya kwa sababu hana.
T14 Armata Elungata dudus
Wanataka atumie silaha gani mpya? T-15 Armata iko kwenye development, Bumerang APC iko kwenye development, Su-57 hazifiki hata 10. Watumie nini kipya sasa, watoe wapi.

Kwani hizi silaha ambazo Ukrainians wanapewa ni mpya? Mbona Marekani inawapa silaha za zamani vilevile, Ujerumani inachukua zilizo outdated ndio inawapa na bado wanazitumia vizuri. Australia, UK na wengineo wanatoa silaha ambazo walitakiwa watupe hawana kazi nazo. Poland mpaka ikataka iwagawie bure Mig-29, jirani yao mwingine sikumbuki ni Estonia kawapa T-72 za zamani.

Silaha mpya za maana walizonazo Ukraine ni NLAW, Bayraktar TB2, Switchblade na Caesar chache sana.
 
Mkuu, Marekani hadi sasa hawana hayo makombora, kama hujui. Wanajaribu kutengeneza, lakini bado hawajafanikiwa.

Ironically. yule kiduku wa Korea Kaskazini tayari anayo!
Kwenye masuala ya ulinzi una safari ndefu sana kama unakaa hapo unaamini North Korea wana hypersonic missiles. Na umekosea mengi hata kwenye uzi huu, kuna sekta zako unafanya vizuri ila hii unaamini mambo yasiyokuwepo
 
Jamani huyu ameuliza kuhusu kijeshi chetu na siyo US wala Russia....
Tumwambie ukweli ni hivi...
Yale magari makubwa ya kizamani unayaonaga siku ya mashujaa, hayo chini ni ya kichina yanajulikana kama A 100, na masfa yake ni kati 40km mpaka 100km, hata Morogoro hayafikishi...
View attachment 2219729



Vile viroket unavinaga uwanja wa taifa ni vya kutungulia ndege za bangaboi sio za kisasa kama Sukhoi za jeshi la Uganda au Northrop 5E za jeshi la kenya,hutu tuanitwa SA-6 (2K12 Kub) kutoka Russia, tulitengenezwa 1958, na tuna masafa ya mpaka 24km
1652222708652-png.2219730



Na hii ndio Uganda Sukhoi, tukizitaka hizi inabidi serkali ianze kugawa basikeli kwa wabunge na mawaziri ili kwenda sambaba na bei ya mafuta na uendeshaji, Uganda wana Mafuta yao.....
View attachment 2219714


Halafu hawa jamaa hapa chini, wanachekesha sana....[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
View attachment 2219732

View attachment 2219731

View attachment 2219733


Na hii ni Kenya Northrop 5E
View attachment 2219718

View attachment 2219730
Hayo magari makubwa ya A100 wenyewe People's Liberation Army waliyakataa hayakukidhi vigezo, sijui ni vigezo gani hivyo.
Sikumbuki yalitengenezwa na kampuni ya NORINCO au nani. Kwahiyo duniani sidhani kama tulionayo ni zaidi ya nchi tatu.

Hatuna air defence system ya kueleweka, hizo SAM ni very outdated na bahati mbaya Tanzania najua hatufanyi sana modifications za silaha. Hizo MANPADS sijui ni version ya mwaka gani yani zinakatisha tamaa ukiziona.

Uganda wana ndege za kisasa ila operation cost inawatoa jasho. Hawana training nzuri na ndege zao chache hawana hata zaidi ya squadron moja. Kama South Africa wanazo JAS-39 Gripen sometines wanasuasua training sembuse Uganda uchumi wa kujikongoja. Wenye airforce imara Afrika ni Egypt, Morocco na Algeria.

Afrika hii hakuna nchi inajua kutengeneza silaha kama South Africa. Wana anti aircraft missiles zinaitwa Mokopa niliona Finland walizinunua wakazitumia kwenye corvette zao. Wana helicopter launched anti tank missiles za 10km range. Waliwahi tengeneza attack helicopter Marekani wakaweka sanctions isiuzwe ilikuwa nzuri kabisa. Wana attack boats na MRAP vehicles. Sisi hata shells za vifaru sijui kama tunajua.

Kati ya majirani wote, nikilinganisha jeshi la Kenya na Tanzania kuna kitu nashawishika kuamini
 
Nin wasiwasi sana na silaha za masafa marefu tulizo nazo ndani ya majeshi yetu ya ulinzi. Miaka ya 2000 kuna zile zilizokuwa zinalipuka zenyewe kule Mbagala. Na ninavyokumbuka Tanzania tuliwahi kununua vifaru vingi na Gun Howitzers nyingi sana wakati wa utawala wa Nyerere kutokea Urusi. Silaha zile ndizo kwa kiasi kikubwa sana zinazotumika sasa hivi vitani huko Ukraine.

Urusi inazitumia na Ukraine pia inazitumia. Jambo linalojitokeza ni kuwa mizinga inayotumika katika Howitzers na vifaru hivyo haipatikani tena. Urusi haizitengenezi tena, na Ukraine imekusanya mizinga karibu yote iliyokuwa kwenye nchi za Warsaw pact na haitoshi kwani mizinga mingine imekuwa hailipuki; hiyo imetokea kwenye pande zote mbili za magogoro huo.

Sijaona Tanzania ikitupa vifaru vya zamani na kuleta vipya, na sijui kama Tanzania itapata tena mzinga ya kutumia kwenye vifaru hivyo kama siyo vya shoo tu. Vifaru kama hivyo leo hii vimekuwa scrap zilizosambaa kwenye ardhi ya ukraine.

Ninajua kuwa zamani shirika la Mzinga liliundwa ili kuwa linatengeza mizinga hiyo, ila sasa baada ya kutokuwa na matumizi ya mizinga hiyo kwa muda mrefu sijui tuko wapi. Ila vita hii ya Ukraine tuichukulie kama funzo kuwa utegemezi wa silaha za urusi siyo jawabu la usalama na ulinzi wetu tena. Urusi imeshapitwa na wakati sana kwenye teknolojia ya vita.

View attachment 2219644View attachment 2219645View attachment 2219646

Tim nato mnaangaika sanaa
 
Kwenye modern wafare ni mwehu tu anayetegemea vifaru vitani ... Vifaru vimebak kama magar ya msafara w kijeshi kipind cha Amani , kiufupi vita ya kutegemea vifaru ishapitwa na wakati, Ila ukijidai utegemee vifaru kwenye active battle zone ujue unawatoa kafara askari ....!! Vita ya sa hv ni propaganda , technology na Airforce , kama huna uwezo kwenye maeneo hayo omba maridhiano mapema.... Askari wenu wanaopasua tofali uwanja wa mkapa wanawadanganya

Na Cyber Warfare
 
Kwenye masuala ya ulinzi una safari ndefu sana kama unakaa hapo unaamini North Korea wana hypersonic missiles. Na umekosea mengi hata kwenye uzi huu, kuna sekta zako unafanya vizuri ila hii unaamini mambo yasiyokuwepo
Mkuu, hujui kitu.
Nyamaza na tafuta muda ujiridhishe mwenyewe kwa kutafuta habari.
Weka unazi wa unaowapenda pembeni. Sifaidiki na chochote kwa kukupa wewe taarifa hizo ambazo ni dhahiri huna, halafu unajifanya wewe ni mjuwaji katika maswala hayo.

Hii ndiyo tabia ya kiTanzania isiyofaa kabisa. Kajiridhishe mwenyewe. Katafute taarifa hiyo, imejaa tele kama unajua jinsi ya kutafuta habari.
 
Ninavyoelewa Mimi ni sawa na kichuguu alivyoandika hapo, lakini hata refference uliyoweka hapo inasupport statement ya kichuguu, huwezi kutuma Hyper Missile kutoka chini, lazima ipigwe juu kwa juu.
Kwani hakuna rocket zinazofikia mach 5?
Je, rocket haziwezi kuwa launched toka kwenye fixed station (launchpad) ambayo ipo kwenye earth surface?

Kitu cha msingi ni namna hiyo rocket ikirushwa ikiwa hewani unafanyeje manouvability ya kuifanya iwe Hypersonic glide missile (HGV) kama hiyo Vangad ya Russia au ile version ya mchina.

Soma vizuri hiyo article kuna kitu hujakitilia mkazo au maanani ungeona hii point nimekufafanulia. Soma na zingine zinazoelezea kuhusu hizo silaha utaelewa.
 
Usa ilidanganya tu ili adui aingie Chaka

Kama kuna kitu usa yupo much concerned ni suala la ulinzi wa Taifa lake

So ukijichanganya unapotea
Tatizo lenu kuamini USA hawezi kutanguliwa kwenye kitu chochote cha teknolojia!
Kwa mawazo yenu mngekuwa enzi zile Yuri Gagarin anaenda outer space orbit kabla wamarekani hawajaweza kutengeneza chombo cha kuweza kufika huko msingeamini kama sasa msivyo amini Russia na China Walitangulia kwenye teknolojia ya HGV.

Marekani astronauts walikuwa wanakesha kupiga hesabu za kuvusha chombo chao kwenye point of 'go-no go' wakati huo Yuri ashavuka zamani na chombo chake huku cosmonauts wenzie wanajipongeza na Vodka.
 
Usichukie,nukuu point yangu,Tanzania haina uwezekano wa kuvamiwa kama Ukraine,ukiangalia historia ya Ukraine na Tanzania tuko tofauti sana,Tanzania inafanana na nchi kama Uswisi,tukitumia fedha nyingi kwenye zana za kivita ni upotezaji wa fedha,zana zilizopo zinatosha kwa ajili ya maonyesho ya tarehe 9 December na siku ya uhuru.
Hujui kuwa tuliwahi kuvamiwa na Amin?
 
Tatizo lenu kuamini USA hawezi kutanguliwa kwenye kitu chochote cha teknolojia!
Kwa mawazo yenu mngekuwa enzi zile Yuri Gagarin anaenda outer space orbit kabla wamarekani hawajaweza kutengeneza chombo cha kuweza kufika huko msingeamini kama sasa msivyo amini Russia na China Walitangulia kwenye teknolojia ya HGV.

Marekani astronauts walikuwa wanakesha kupiga hesabu za kuvusha chombo chao kwenye point of 'go-no go' wakati huo Yuri ashavuka zamani na chombo chake huku cosmonauts wenzie wanajipongeza na Vodka.
Historia ya mashindano ya kwenda anga za juu unaikosea. Mpaka mwaka 1957 marekani ilikuwa haifikirri kwenda anga za juu wakati Urusi ilianza mwaka 1951; kwa hiyo urusi ilianza mapema shughuli hiyo. Mwaka 1957 waliporusha satellite ile ya Sputnik, ndipo Marekani nao wakaona kuna haja ya kuingia kwenye anga za juu kwani hiyo spunik inaweza kuangusha Bomu la atomik ndani ya nchi kwa kutokea angani. Ndipo NASA ilipoanzishwa mwaka 1958; kwa hiyo Wakati Gagarin anaingia angani mwaka 1960, ilikuwa ni baada ya warusi kufanya utafiti wa takriban miaka kumi wakati NASA ndipo wanaaza tu. Rais Kennedy alipofungua ile Appolo program mwaka 1961, ndipo NASA nao wakaanza maswala ya safari za anga za juu, juhudi zilioiwezesha marekani ni kuwa ya kwanza kupeleka watu kwenye mwezi; zilipigia safari nyingi sana kwenda mwezini na kurudi; sita zilitua na watu, na nyingine zilikuwa zinazunguka mwezi na kurudi na nyingi sana zililuwa zinakwenda bila watu.

Kwa hiyo ingawa ni kweli kuwa Urusi ilitangulia kujishughulisha kwenye mambo ya anga za juu, siyo kuwa ilishinda mashindano hayo, kwani baadaye NASA ndiyo mshindi. Iwapo wangeanza pamoja mashindano hayo, ni wazi NASA angewaacha Urusi mbali sana. Safari za NASA zimetusaidia vitu vingi sana ikiwemo aina za magodoro ya zero g, viatu vya laba, Inertial navigation Systems zinazotumika kwenye usafiri wa ndege za abiria, na mengine mengi sana ambapo juhudi za urusi zilizokuwa ni za kutaka ufahari tu. Hakuna product kwenye maisha ya kila siku unayoweza kuihusisha moja kwa moja na space program ya Urusi labda satellite tu.
 
Back
Top Bottom