Simba hakuna sababu ya kung'ang'ania wachezaji waliosaliti timu

Simba hakuna sababu ya kung'ang'ania wachezaji waliosaliti timu

Yani mleta uzi unaaminisha watu eti wachezaji walihongwa na yanga ili timu iishie nafasi ya 3? Pia kunampango wakutaka timu apewe mdogo wa gsm? Unaushahidi gani wa kuthibitisha shutuma zako?

Yaani tunashindwa tu kukubali kwamba wenzetu uto wamepata viongozi wa boli hasa?

Yaani wachezaji kama pacome, aziz, ibra bacca pamoja na diara wanaweza cheza timu yoyo hapa afrika ila ukitafta huku kwetu hakuna quality player yeyote ambae anaweza kutakiwa hata na petro atletico tu.

Ifike tu muda tukubali hawa uto wametuzidi na wamepata viongozi ambao ni wa mpira hasahasa.

Tunaona kila mechi ya uto lazima rais wao atakuwepo.
Simba tujenge timu tuache shutuma za kijinga, ukimsusia mchezaji anakwenda upande wa pili na anakiwasha mpaka unajuta.
Kuna mtu kakataa kuwa uto wametuzidi uongozi ndio maana wana timu thabiti?
Pamoja na hayo yote unadhani wanaingiza timu mbele ya Simba kizembe kizembe kama akili za wajinga zinavyodhani?
Unadhani kwa nini wanamtaka Chama na walimwita mzee akicheza chini ya kiwango?Unahisi wao ni wapumbavu ama nani kati yenu?
 
Kwahiyo wewe nawe ukakaa ukaamini huu uongo mnaodanganywa? Nikuulize tu swali dogo, baada ya mechi ya Simba vs Yanga kuisha kwa Simba kufungwa goli tano kuna wachezaji kadhaa viongozi wa Simba walisema wanasimamishwa akiwemo Chama na Inonga. Lakini cha ajabu wote waliokuwa wanasemekana kusimamishwa walikuwa wanaendelea na mazoezi Bunju kama kawaida je kwanini? Kwenye mechi zilizofuata hao wachezaji walicheza je kwanini? Je kwanini hawakupeleka kesi TAKUKURU ili hatua zichukuliwe? Hapo ni kwamba mnachezewa akili tu timu ilikuwa imezidiwa ubora na Yanga ila mnawekewa upofu kwa kuenezwa propaganda. Na uzuri haya yanayofanywa ni faida kwa Yanga kwasababu mtaendelea kulala usingizi hivyo hivyo mkiamini Yanga inahonga na kuroga ila mpo imara kumbe mnazidi kupotea tu.
Hizo habari sikuzitilia maanani kwa sababu najua siasa za Simba na yanga pia hata waandishi wetu wengi hawana uweledi huwa wanatengeneza matukio.
Jiulize Kama hao wachezaji wasimamishwe ilikuwaje wawepo mazoezini.
 
Simba walitakiwa washugulike na huyo anayehonga wachezaji badala ya kushugulika na wachezaji , Kama tuhuma hizo ni za kweli.
Kama utashugulika na wachezaji badala ya mhusika Basi wachezaji wenu wataendelea kuhongwa.
Hilo liko wazi kwani hatuna hao viongozi wa kushughulikia kiini cha tatizo kwani wao ndio tatizo.
Mangungu yupo kuisaidia yanga iweke historia na kuumaliza umaarufu wa Simba kimataifa.Yupo anatumika kimkakati na hivyo tutaendelea kuiona Simba ikipigwa 5,3,2 na hata goli 7 msimu huu.
Bado kuna shida kubwa kwenye uongozi,uwekezaji na kwa mashabiki wengi tumegawanyika wengine wanamwamini mangungu wengine wana mwamini mwekezaji
 
Timu ilikuwa inahitaji maboresho, acheni fikra za rushwa, angalia mechi na power dynamo, tulivyoshikwa Dar, bila juhudi binafs za CHAMA, tusingeingia makundi, ushindi wetu umekuwa wa bahatbahat tu, hao vijana mnaowataka Bado UWEZO ni mdogo, uzoefu hawana, kiundwe kikosi mseto, na ufanyike usajiri Bora.
 
Ukweli lazima usemwe. Wachezaji wengi walilipwa kucheza chini ya kiwango na ndio sababu,hao waliowalipa, wanawataka kwa udi na uvumba.

Ni wakati wa kufanya maamuzi magumu tu na kuachana na wachezaji wote waliokosa kuipigania club.

Tatizo letu kubwa ni uongozi.Hatujui ni kwa nini wachezaji wetu wanaweza kurubuniwa kirahisi sana na upande wa pili.

Matatizo haya ya viongozi,nina uhakika yataendelea kwani iwapo walirubuniwa wampinge Mo ,ili timu apewe mdogo wake gsm,nani ajuaye jambo hili limekwisha?

Hapo hapo kuna wajinga wenye tamaa zao wanataka Simba ibaki mikononi mwao kwa vile tu ni wanasiasa wakidhani pesa wanazoiba zinaweza kuwafanya waimiliki club.
Matokeo yake sasa yamepafanya Simba pawe uwanja wa vita.Haya yote yamesababishwa na kutoelewana kwa viongozi na tabia ya mwekezaji aliyepo kususa kila anaposakamwa na baadhi ya viongozi.

Matatizo ya Simba sio kusajili pekee,maana unaweza kusajili lakini kwa vile upande wa pili wana mkono Simba, wachezaji wakafanyiwa ya kufanyiwa wakashindwa kucheza kwa kiwango chao.

Kumbukeni yanga ndio waliwapangia mcheze shirikisho na kweli mnacheza huko.Na sasa wanawapangia mtolewe mapema shirikisho na itakuwa hivyo kweli.
Hatuna viongozi kwa sasa tuwe tayari kupitia kila hali ya kunyanyasika.

Kama viongozi wangekuwa na akili,wangesajili vijana chipikizi wasio na majjna wanaojituma na kuachana na majina makubwa.
Msipokubali kuwa mna timu mbovu hamtotoka hapo .....
 
Kwahiyo wewe nawe ukakaa ukaamini huu uongo mnaodanganywa? Nikuulize tu swali dogo, baada ya mechi ya Simba vs Yanga kuisha kwa Simba kufungwa goli tano kuna wachezaji kadhaa viongozi wa Simba walisema wanasimamishwa akiwemo Chama na Inonga. Lakini cha ajabu wote waliokuwa wanasemekana kusimamishwa walikuwa wanaendelea na mazoezi Bunju kama kawaida je kwanini? Kwenye mechi zilizofuata hao wachezaji walicheza je kwanini? Je kwanini hawakupeleka kesi TAKUKURU ili hatua zichukuliwe? Hapo ni kwamba mnachezewa akili tu timu ilikuwa imezidiwa ubora na Yanga ila mnawekewa upofu kwa kuenezwa propaganda. Na uzuri haya yanayofanywa ni faida kwa Yanga kwasababu mtaendelea kulala usingizi hivyo hivyo mkiamini Yanga inahonga na kuroga ila mpo imara kumbe mnazidi kupotea tu.
Kwa hiyo Inonga hana ubora.Chama hana ubora!
Huyo Inonga asiye na ubora Simba anakuwa na ubora timu ya Taifa.Huyo Chama asiye na ubora anasajiliwa na Yanga iliyotuzidi ubora kila idara.
Kuna vitu vinafikirisha lakini hongereni kwa kufanikiwa kuwa na pandikizi pale Simba na mtatumaliza maana sisi mashabiki hatuna akili pia
 
Kama Bado una fikra za namna hii Yanga watatawala mpira daima mbele nyuma mwiko.
 
Kama Bado una fikra za namna hii Yanga watatawala mpira daima mbele nyuma mwiko.
Ata wakati Yanga inatembeza bakuli Bado walifanikiwa kuifunga Simba, Ina maana Yanga alikua ana honga?

Simba ni mbovu na waki endelea na propaganda za ki puuzi wataendelea ku nyooshwa mpaka watakapo jitambua.
 
Hao kina macha ndiyo wasaliti na ndiyo wanagombaniwa na viongozi. Nilikuwa siamini haya mambo ya kuhonga wachezaji mpaka jana nilipoona clip ya Juma Kaseja akikiri kuwa viongozi wa Yanga walikuwa wanamfuata kumhonga acheze afungishe ndipo nimeona hii derby ya Simba na Yanga ya kishenzi sana, takukuru walipaswa wawe washatoa tamko toka hiyo clip itoke maana jinai Haina ukomo wa muda
Hii kitu ipo muda mrefu sana, ni vile tu mamlaka zinqqngalia tu, hii kitu inaharibu mpira
 
Ili simba iwe imara lazima haya yafuatayo yafanyike.

1.Uongozi uliopo hasa upande wa wanachama ukubali kuachia ngazi. Maana sioni kama kitafanyika kitu cha Maana kama viongozi wa pande hizi mbili (mwekezaji na wanachama) hawaelewani.kitakachofuata ni kusalitiana.

Haiingii akilini kocha kumpanga Manula kudaka mechi ya darby huku akitoka majeruhi kama siyo shinikizo la viongozi wasaliti ndani ya klabu.mtokeo 1,5

Darby ya pili Inonga bila hata kuguswa dk ya 15 tu akajivunja na akatolewa nje lakini siku tatu baadae et keshapona na anashinikiza apangwe kwenye mechi zilizofuata(Usaliti wa wazi huo) . Mechi ilishauzwa hiyo.

2.Wachezaji maswahiba wa Hers na Manara ndani ya simba waondolewe mara Moja.(Wanajulikana) Maana ndio wanaotumika kama maduka ya upande wa pili.Wanatumika pia kuwarubuni hata wachezaji wengine kuuza mechi.

3. Udhamini wa GSM kudhamini vilabu zaidi ya kimoja kwenye ligi Moja upigiwe kelele na kila mwanamichezo mpenda michezo. Ligi inaanza tayari Yanga ana uhakika wa pointi karibia 30.(TFF Kazi kwenu)

4.Mwekezaji Mo na wanachama sajilini wachezaji wa ki mkakati .Toa mzigo wa Maana (pesa).Acheni kukimbilia free agent . Vunjeni mikataba ya wachezaji Wanaojulikana toka kwenye vilabu vinavyojulikana na ligi zinazojulikana. Siyo unaenda kuvunja mkataba wa mchezaji toka timu ya ligi ya somalia.
 
Kwa hiyo Inonga hana ubora.Chama hana ubora!
Huyo Inonga asiye na ubora Simba anakuwa na ubora timu ya Taifa.Huyo Chama asiye na ubora anasajiliwa na Yanga iliyotuzidi ubora kila idara.
Kuna vitu vinafikirisha lakini hongereni kwa kufanikiwa kuwa na pandikizi pale Simba na mtatumaliza maana sisi mashabiki hatuna akili pia
Timu bora iliyokamilika ni mkusanyiko wa wachezaji zaidi ya 9 wenye ubora na uwezo. Huwezi kuwa na wachezaji 4 au watano pekee wenye ubora halafu ukasema mna timu bora. Ukitaka kujua Yanga ilikuwa imekamilika kwa ubora ingia kwenye takwimu. Utaona kwenye magoli mengi ya kufunga wapo, kwenye kuruhusu magoli machache wapo. Kwenye wafungaji wenye magoli mengi unakuta wana list ya kutosha kuna Aziz Ki, Max, na Mudathir. Kwenye ulinzi kuna mabeki waliokamilika yaani kuna beki hajawahi pata hata kadi ya njano msimu mzima.
Sasa je timu ya Simba ilikuwa na wachezaji wangapi wenye viwango wangapi kulinganisha na waliopo Yanga?
 
Ukweli lazima usemwe. Wachezaji wengi walilipwa kucheza chini ya kiwango na ndio sababu,hao waliowalipa, wanawataka kwa udi na uvumba.

Ni wakati wa kufanya maamuzi magumu tu na kuachana na wachezaji wote waliokosa kuipigania club.

Tatizo letu kubwa ni uongozi.Hatujui ni kwa nini wachezaji wetu wanaweza kurubuniwa kirahisi sana na upande wa pili.

Matatizo haya ya viongozi,nina uhakika yataendelea kwani iwapo walirubuniwa wampinge Mo ,ili timu apewe mdogo wake gsm,nani ajuaye jambo hili limekwisha?

Hapo hapo kuna wajinga wenye tamaa zao wanataka Simba ibaki mikononi mwao kwa vile tu ni wanasiasa wakidhani pesa wanazoiba zinaweza kuwafanya waimiliki club.
Matokeo yake sasa yamepafanya Simba pawe uwanja wa vita.Haya yote yamesababishwa na kutoelewana kwa viongozi na tabia ya mwekezaji aliyepo kususa kila anaposakamwa na baadhi ya viongozi.

Matatizo ya Simba sio kusajili pekee,maana unaweza kusajili lakini kwa vile upande wa pili wana mkono Simba, wachezaji wakafanyiwa ya kufanyiwa wakashindwa kucheza kwa kiwango chao.

Kumbukeni yanga ndio waliwapangia mcheze shirikisho na kweli mnacheza huko.Na sasa wanawapangia mtolewe mapema shirikisho na itakuwa hivyo kweli.
Hatuna viongozi kwa sasa tuwe tayari kupitia kila hali ya kunyanyasika.

Kama viongozi wangekuwa na akili,wangesajili vijana chipikizi wasio na majjna wanaojituma na kuachana na majina makubwa.
Na tutawapangia mshuke saraja msinu ujao...kila kitu mnasingizia Yanga
 
Ukweli lazima usemwe. Wachezaji wengi walilipwa kucheza chini ya kiwango na ndio sababu,hao waliowalipa, wanawataka kwa udi na uvumba.

Ni wakati wa kufanya maamuzi magumu tu na kuachana na wachezaji wote waliokosa kuipigania club.

Tatizo letu kubwa ni uongozi.Hatujui ni kwa nini wachezaji wetu wanaweza kurubuniwa kirahisi sana na upande wa pili.

Matatizo haya ya viongozi,nina uhakika yataendelea kwani iwapo walirubuniwa wampinge Mo ,ili timu apewe mdogo wake gsm,nani ajuaye jambo hili limekwisha?

Hapo hapo kuna wajinga wenye tamaa zao wanataka Simba ibaki mikononi mwao kwa vile tu ni wanasiasa wakidhani pesa wanazoiba zinaweza kuwafanya waimiliki club.
Matokeo yake sasa yamepafanya Simba pawe uwanja wa vita.Haya yote yamesababishwa na kutoelewana kwa viongozi na tabia ya mwekezaji aliyepo kususa kila anaposakamwa na baadhi ya viongozi.

Matatizo ya Simba sio kusajili pekee,maana unaweza kusajili lakini kwa vile upande wa pili wana mkono Simba, wachezaji wakafanyiwa ya kufanyiwa wakashindwa kucheza kwa kiwango chao.

Kumbukeni yanga ndio waliwapangia mcheze shirikisho na kweli mnacheza huko.Na sasa wanawapangia mtolewe mapema shirikisho na itakuwa hivyo kweli.
Hatuna viongozi kwa sasa tuwe tayari kupitia kila hali ya kunyanyasika.

Kama viongozi wangekuwa na akili,wangesajili vijana chipikizi wasio na majjna wanaojituma na kuachana na majina makubwa.
Kama haya uliyoyaandika ni kweli sasa kwa nini usihamie Yanga ili upate furaha?
 
Mangungu ni wakati uondoke Simba kazi uliyopewa na JK umeikamilisha vizuri sana sasa ni wakati wa JK naye kutimiza sehemu yake ya makubaliano yenu ya kukupatia Ubunge 2025, na ingependeza sana ukasubiria ahadi yako ukiwa nje ya uongozi wa Simba kwani watu wote wameshajua mchezo mzima hivyo kuna siku watakuafanyia kitu mbaya hata wakati wa huo ubunge usiwepo tena duniani au ukawa uko kwenye wheel chair mkononi ukiwa na kikopo cha kukingia mimate inayokutoka bila ya udhibiti wa mdomo kwani nao mdomo utakuwa umemwagika. Huwezi ukawaudhi watu zaidi milioni 20 na ukabaki salama.
 
Mangungu ni wakati uondoke Simba kazi uliyopewa na JK umeikamilisha vizuri sana sasa ni wakati wa JK naye kutimiza sehemu yake ya makubaliano yenu ya kukupatia Ubunge 2025, na ingependeza sana ukasubiria ahadi yako ukiwa nje ya uongozi wa Simba kwani watu wote wameshajua mchezo mzima hivyo kuna siku watakuafanyia kitu mbaya hata wakati wa huo ubunge usiwepo tena duniani au ukawa uko kwenye wheel chair mkononi ukiwa na kikopo cha kukingia mimate inayokutoka bila ya udhibiti wa mdomo kwani nao mdomo utakuwa umemwagika. Huwezi ukawaudhi watu zaidi milioni 20 na ukabaki salama.
Mangungu alishawahi kuwa mbunge Kilwa.
 
Mangungu alishawahi kuwa mbunge Kilwa.
Nafahamu. 2020 alitaka kugombea tena kura za maoni akapita lakini Magu akamkataa. JK alimuahidi kuwa this time atampigania lakini amfanyie kazi yake ndani ya Simba na Mangungu ametimiza sehemu yake ya makubaliano bado JK naye akanilishe agano lao.
 
Nafahamu. 2020 alitaka kugombea tena kura za maoni akapita lakini Magu akamkataa. JK alimuahidi kuwa this time atampigania lakini amfanyie kazi yake ndani ya Simba na Mangungu ametimiza sehemu yake ya makubaliano bado JK naye akanilishe agano lao.
Kwani Mangungu kateuliwa au kachaguliwa na wanachama wa Simba?
 
Back
Top Bottom