Simba na Taifa Stars: Changamoto na Nini Kifanyike Kuleta Mabadiliko ya kweli

Simba na Taifa Stars: Changamoto na Nini Kifanyike Kuleta Mabadiliko ya kweli

covid 19

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2014
Posts
6,967
Reaction score
17,452
Kama wewe ni shabiki wa mpira wa ndani na nje, ni rahisi kugundua tatizo kubwa linaloikabili timu ya Simba, ambalo pia linaathiri timu yetu ya taifa, Taifa Stars. Shida kuu iko kwenye safu ya ushambuliaji—kimsingi, Simba haina makali mbele. Kazi kubwa inafanywa vizuri sana kutoka nyuma hadi katikati, lakini mipira inapofika mbele, inakufa. Hakuna washambuliaji hatari wenye uwezo wa kumaliza mashambulizi. Hii ni hali ile ile inayojitokeza kwenye Taifa Stars. Timu iko imara nyuma, lakini tatizo ni kutoka kwa viungo kuelekea safu ya ushambuliaji.

Nini kifanyike?
Simba haina budi kumwaga pesa ili kupata wachezaji wenye viwango vya juu. Sasa hivi wanapaswa kuachana na tabia ya kuchukua wachezaji wa kawaida au wale waliopigiwa debe kama MVP kwenye mashindano ya kawaida. Badala yake, wanahitaji wachezaji wenye uwezo wa kimataifa, kama walivyokuwa Pacome na Aucho. Kuwekeza kwenye wachezaji hawa, angalau wawili wenye uwezo kama wa Pacome na wawili kama Aucho, kutaleta matokeo ya haraka.

Simba inahitaji wachezaji ambao, ukiwapanga leo, matokeo yanaanza kuonekana mara moja. Katika bara hili la Afrika, vipaji vipo tele—Simba wanapaswa kuwatafuta wachezaji wenye uwezo mkubwa ili kuleta mabadiliko ya haraka. Mo Dewji, ni wakati wa kuacha ubahiri. Unapunguza furaha ya mashabiki, na soka linahitaji uwekezaji wa kweli ili mashabiki wapate furaha na matokeo bora.
 
Kama wewe ni shabiki wa mpira wa ndani na nje, ni rahisi kugundua tatizo kubwa linaloikabili timu ya Simba, ambalo pia linaathiri timu yetu ya taifa, Taifa Stars. Shida kuu iko kwenye safu ya ushambuliaji—kimsingi, Simba haina makali mbele. Kazi kubwa inafanywa vizuri sana kutoka nyuma hadi katikati, lakini mipira inapofika mbele, inakufa. Hakuna washambuliaji hatari wenye uwezo wa kumaliza mashambulizi. Hii ni hali ile ile inayojitokeza kwenye Taifa Stars. Timu iko imara nyuma, lakini tatizo ni kutoka kwa viungo kuelekea safu ya ushambuliaji.

Nini kifanyike?
Simba haina budi kumwaga pesa ili kupata wachezaji wenye viwango vya juu. Sasa hivi wanapaswa kuachana na tabia ya kuchukua wachezaji wa kawaida au wale waliopigiwa debe kama MVP kwenye mashindano ya kawaida. Badala yake, wanahitaji wachezaji wenye uwezo wa kimataifa, kama walivyokuwa Pacome na Aucho. Kuwekeza kwenye wachezaji hawa, angalau wawili wenye uwezo kama wa Pacome na wawili kama Aucho, kutaleta matokeo ya haraka.

Simba inahitaji wachezaji ambao, ukiwapanga leo, matokeo yanaanza kuonekana mara moja. Katika bara hili la Afrika, vipaji vipo tele—Simba wanapaswa kuwatafuta wachezaji wenye uwezo mkubwa ili kuleta mabadiliko ya haraka. Mo Dewji, ni wakati wa kuacha ubahiri. Unapunguza furaha ya mashabiki, na soka linahitaji uwekezaji wa kweli ili mashabiki wapate furaha na matokeo bora.
simba nguvu moja
 
Utanisamehe kama nitakuwa nje ya mada, sijasoma maelezo.

Vilabu vikubwa vimejikita kwenye soka la kibiashara zaidi ambapo sio kosa, ingawa gharama yake ni kubwa kuliko uwezo wa vilabu na nchi kiujumla.
  • Ligi inabebwa wa wachezaji wa nje
  • Hakuna succession plan, tunategemea ready made waliopo sokoni.

Spain iliyotikisa Euro na World cup, 1st eleven ilikuwa na wachezaji 8 toka Barcelona, na waliobaki ni Real Madrid, ligi yao.

Brazil, utamaduni ni kuwa na wachezaji angalau 300 wa ndani wanaoweza kuunda squad ya Taifa;
- Kaka, Gaucho, Neymar, n.k waliwika kupitia National team.

Akina, Diouf, Diop, Essien, n.k wamewika kutokea utaifani

Tuwekeze kwenye academy.
 
Kama wewe ni shabiki wa mpira wa ndani na nje, ni rahisi kugundua tatizo kubwa linaloikabili timu ya Simba, ambalo pia linaathiri timu yetu ya taifa, Taifa Stars. Shida kuu iko kwenye safu ya ushambuliaji—kimsingi, Simba haina makali mbele. Kazi kubwa inafanywa vizuri sana kutoka nyuma hadi katikati, lakini mipira inapofika mbele, inakufa. Hakuna washambuliaji hatari wenye uwezo wa kumaliza mashambulizi. Hii ni hali ile ile inayojitokeza kwenye Taifa Stars. Timu iko imara nyuma, lakini tatizo ni kutoka kwa viungo kuelekea safu ya ushambuliaji.

Nini kifanyike?
Simba haina budi kumwaga pesa ili kupata wachezaji wenye viwango vya juu. Sasa hivi wanapaswa kuachana na tabia ya kuchukua wachezaji wa kawaida au wale waliopigiwa debe kama MVP kwenye mashindano ya kawaida. Badala yake, wanahitaji wachezaji wenye uwezo wa kimataifa, kama walivyokuwa Pacome na Aucho. Kuwekeza kwenye wachezaji hawa, angalau wawili wenye uwezo kama wa Pacome na wawili kama Aucho, kutaleta matokeo ya haraka.

Simba inahitaji wachezaji ambao, ukiwapanga leo, matokeo yanaanza kuonekana mara moja. Katika bara hili la Afrika, vipaji vipo tele—Simba wanapaswa kuwatafuta wachezaji wenye uwezo mkubwa ili kuleta mabadiliko ya haraka. Mo Dewji, ni wakati wa kuacha ubahiri. Unapunguza furaha ya mashabiki, na soka linahitaji uwekezaji wa kweli ili mashabiki wapate furaha na matokeo bora.
Simba ipo vizuri. Ni dhaifu kwa sababu umeilinganisha na Yanga. Simba ni zaidi ya Taifa Stars kimashindano. Yanga wapo juu sana; hivyo Simba kushindwa mbele ya Yanga maana yake Yanga wapo juu sana.
 
Back
Top Bottom