Simba SC haiwezi kuwa kubwa bila kupigana na wakubwa

Simba SC haiwezi kuwa kubwa bila kupigana na wakubwa

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001
9ed5fb82e0344fce9da266a0f291c764_339357160_3343745542607532_3787559884867132776_n.jpg


Lazima tukiri kuwa tumepata mpinzani mgumu kwenye hatua ya Robo Fainali, na pengine ni mpinzani mgumu zaidi tangu tuanze kushiriki hatua hii.

Hapa unamzungumzia bingwa mtetezi, unamzungumzia mshiriki wa Club World Cup, unazungumzia timu yenye wachezaji waliotoka Nusu Fainali ya Kombe la Dunia.

Huu ni mlima mrefu kwetu lakini hatuna budi kuupanda na kufika kileleni. Ili uwe mkubwa Afrika ni lazima uwafunge wakubwa wa bara hili.

Inawezekana sana Simba kupata ushindi dhidi ya Wydad kama tuu kila idara ndani ya taasisi yetu itatimiza wajibu wake kwa asilimia 100

Kama tulivyomvua Ubingwa Zamalek mwaka 2003 ni wakati sasa kumvua Ubingwa Wydad.

Let’s goo wana Lunyasi, Let’s goo wana Simba let’s wana Msimbazi mapambano yanaanza sasa. ☄️☄️

Credit Tajiri Mo Dewji
Credit Semaji la CAF

My Take
Wote tumeshuhudia nguvu ya mashabiki kwa Simba. Majamaa ya Al Ahl yalitisha uwanja ukatanda mpaka Al Hilal wamabaki kutetemeka tu. Ule moto wa derby ya Raja Vs Waydad ilikuwa hatari sana.

Huu ni wakati wa mashabiki kuingia bure, labda ibaki VIP A na B. Maandalizi yabaki namna ya kupiga vibe la kufa mtu pale Lupaso.

Simba Nguvu Moja
 
Iwe mvua iwe jua kutoboa hatua hii ni ngumu hata Kama akishinda home. Hata hivyo naona alichopata Kwa Raja yaani kupigwa in and out kinaenda kujirudia na Sasa Kwa tofauti kubwa ya magoli yaani Ile Ili kua jumla ya 6-1 lakini hii Kuna uwezekano wa jumla ya 10-0 yaani 5-0 kwakila mechi
 
SIMBA KAMTOA ZAMALECK BINGWA MTETEZI NYUMBANI KWAO MISRI 2003.

1. Juma kaseja.
2. Said swedi.
3. Ramadhani waso.
4. Victor Costa.
5. Boniface pawasa.
6. Christofer Alex.
7. Yusuph Macho.
8. Suleiman MATOLA.
9. Emanuel Gabliel.
10. Otman Machupa.
11. Ulmboka mwakingwe.

Atakuwa wydad????
 
Nliona hadi rais anafurahi kupangiwa rivers,yaani wameshangilia sana walikuwa wanahofu kupangiwa wamorocco as far rabart...sasa watapata wapi ukubwa kama kila siku wanacheza na vibonde??timu pekee kubwa ambayo simba haijacheza nayo mpaka sasa ni mamelodi na kina pyramid hao ndo wakubwa wenzetu.
 
Nliona hadi rais anafurahi kupangiwa rivers,yaani wameshangilia sana walikuwa wanahofu kupangiwa wamorocco as far rabart...sasa watapata wapi ukubwa kama kila siku wanacheza na vibonde??timu pekee kubwa ambayo simba haijacheza nayo mpaka sasa ni mamelodi na kina pyramid hao ndo wakubwa wenzetu.
Historia ya marehemu imekuwa fupi sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom