Simba SC, Mo Dewji na CEO Barbara nawaomba msimjibu lolote (chochote) aliyekuwa Msemaji 'Mnafiki' Haji Manara, ila mtuachie Mashabiki

Simba SC, Mo Dewji na CEO Barbara nawaomba msimjibu lolote (chochote) aliyekuwa Msemaji 'Mnafiki' Haji Manara, ila mtuachie Mashabiki

Hapana tuwe wakweli manara kavumilia mengi sana na hoja zake simba hakuna wakujibu
 
Mi ni Simba ila manara yupo sahihi 100% mo aweke wazi Simba imeingiza kiasi gani kwa hio miaka 4 na manara alichokuwa anakitetea ni image rights zake wengi msiojua soka mtamponda ila mo ni mswahili sana ndo maana walimteka
Unahudhuria mkutano mkuu wa club?
 
kama umenifukuza kwa kashifa mbaya lazima na mimi kama nikipewa nafasi au nina uwezo wa kukuchafua nifanye hivyo lakini kama tumeachana kwa uzuri sawa,hivyo basi manara anashambuliwa kutokana na nguvu ya pesa ya Mo,wala hakuna anaejali.

Haji manara anajua mengi ndani ya simba kuliko nyie mnaomshambulia humu jukwaani,hivyo ni afadhali kujikalia kimya kama huna unalojua kuliko kutetea ujinga.kwa upofu huu ndio maana wakati mwingine serikali ikiwatia jamba jamba hawa matajiri watu wanapiga kelele eti serikali inawaonea wakati wana mambo ya ajabu sana.

Kwani wewe unawajua real Udentity za wanaochangia hapa? Je kama ndiyo hao hao viongozi wa Simba.
 
Kwakukusadia BIl 21 haikuwa ruzuku ni deni na amewasainisha baadhi ya viongozi tunataka hatueleze mkopo kaikopesha simba kwa idhini ya nani?
2. Kumbe huelewi kitu kuhusu hii kitu...sina cha kusema

3. Hata kama ni charity nani kakwambia intangaza bure....unajua hiyo charity inapata wapi pesa? kadanganya nini hao wanaotoa Pesa...unaelewa mambo ya marketing kweli wewe?

haya Mo protector nayo ni charity?
1.Ni deni una uhakika? Au ndio unamchukia, bila ushahidi?
2. Wewe unaelewa afu huna cha kusema?
3. Mkataba wa simba na Metl mbona umesainiwa hadharani, hukuona hili?
 
Nyie ni wajinga sana hiyo miaka sita kwani yote ni ya MO Dewij?

Mbona kuanzia 2015 hamsemi kuwa timu ilikuwa chini ya Evans Aveva na alikuwa hahapewa huo mkataba!

Unajua Mo ameanza kuichukua Simba lini ?


Nyie ni wajinga sana

Sent from my CPH1803 using JamiiForums mobile app
Nimemtaja Dewji kwenye nilichosema hapo?
 
Ila wahindi wanyonyaji sana mil 3 asijisaidie hta chamazi au yanga
 
Totally unprofessional from Manara. Mimi sikuwahi kuwa mfuasi wake tokea akiwa Simba.

Ukiachilia tu sifa yake kubwa ya uhamasishaji Manara hafai kupewa nafasi ya maana sehemu yoyote maana ni mropokaji/msema hovyo.

Hata kama ukiachana na mwajiri wako kwa ubaya kwa mtu anaejitambua huwezi kuenda kumchafua sehemu hasa kwenye media.

Hii itakufanya kutoaminika hata na huyo anaetaka kukuajiri maana atajua tu kuwa siku mkishindwana nae utaenda kumchafua tu. Manara na wanaomtumia wote akili zao finyu sana. Hawana upeo mzuri wa kufikiri.
Kakulia kariakoo ana uswahili mwingi alafu anafaa kuwa makanga stendi.
 
Haji kaongea ukweli mtupu maana tulikuwa tunaongea humu kwamba uyu mo anaifanya simba kuwa ya familia yake mnabisha, wewe utasemaje upati faida kwenye timu miaka yote 4?

Hivi kuna mfanyabiashara anakubali hasara tu kila siku? Ni njia mojawapo ya kuwanyonya watu iyo anaanza kujiwekea ulinzi ili aendelee kufaidika watu wasihoji
Sasa mtu akipata faida kuna shida gani?
 
Manara yuko sahihi, MO sio mara ya kwanza kulalamikiwa na wafanya kazi wake kuwa ana nyanyasa wafanyakazi, team kubwa kama hii itawezaje msemaji wake afanye kazi bila mkataba kwa miaka7? , msemaji wa team asafiri na team kwenda nje kwa gharama zake mwenye hili ni sahihi? huku ni kumnyanyasa , hii tabia sio nzuri nsdhani simba waliangalie vizuri na apewe stahiki sake.
 
Ametumwa kuharibu focus na concentration ya usajili wetu makini. Ignore him completely. Tuko kwenye usajili na maandalizi ya msimu mpya.

Kaongea story za zamaaniiii za nini sasa, awape haohao mabingwa wa kihistoria ndo wanapendaga hizo mambo.
Yani kama unaamini Manara ametumwa basi kazi ipo.Alivyokuwa anaropoka hovyo wakati yupo Simba alikuwa anatumwa na nani?
 
Back
Top Bottom