Simba SC siku zingine msilirudie tena Kosa hili la Kiufundi na Binafsi mmenikera

Simba SC siku zingine msilirudie tena Kosa hili la Kiufundi na Binafsi mmenikera

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Watu tunaojua kuwa Kesho Kipa Aishi Manula hatocheza tunawashangaa kabisa Kutwa mnavyohangaika kututia Moyo.

Yaani badala ya kutumia muda wenu mwingi kumjenga Kisaikolojia Kipa wangu bora Simba SC Beno David Kakolanya nyie mnahangaika na Aishi Salum Manula wenu kana kwamba ni mzuri kivile wakati ni Ndumba tu za Kwao Kilombero zinambeba, anapendwa na Viongozi wa Juu wa Simba SC na Kucheza Mechi nyingi ndiko Kunambeba pekee.

Hivi mnavyohangaika Kutwa Kulazimisha Kesho Aishi Manula adake wakati tayari hata Daktari wa Timu kawaambia hajapona vyema Jeraha lake mnamjengea Picha gani Kipa mzuri Kumzidi Yeye Beno Kakolanya ambaye Kesho ndiyo ana 95% za Kudaka?

Na mlivyo Wanafiki na Wapuuzi baadhi ya Viongozi wa Simba SC mnaolazimisha Kesho Aishi Manula ikiwezekana apigwe Ganzi ili acheze leo mmeshasahau kuwa sababu Kuu ya Kumleta Simba SC Kipa Beno Kakolanya ni kutokana tu na Kudaka vyema na Kiumahiri kabisa huku akitunyima Ushindi katika Mechi ya Simba na Yanga huku Yeye akidakia Yanga SC.

Sasa kama aliweza Kudaka katika ile 'Derby' na tukavutiwa nae na Kumsajili iweje leo hii tuwe na wasiwasi nae kuelekea 'Derby' yetu nao Kesho? Hivi tunahitaji Elimu Kubwa ya Soka kujua kuwa Kipa Beno Kakolanya ni mzuri kwa kila Kitu kuliko huyu Aishi Manula wenu?

au mnataka sasa tutoboe Siri ya kwanini Aishi Manula wenu aliumia ( Kimaajabu ) na Kioo katika 'Dressing Room' mpaka kila Mchezaji alishangaa? Mwambieni apunguze au aache Kutwa 'Kumroga' Mwenzake Beno Kakolanya kwani Mwenzake ni Mcha Mungu mzuri ile mbaya na ipo Siku yatakuja kumkuta makubwa zaidi ya hilo lililompata.

Hata Kocha wa Makipa ( Mkaburu ) kutoka Bondeni Afrika Kusini tunajua ameshasema kuwa Kipa Beno Kakolanya ni zaidi ya Aishi Manula na kutaka awe anapangwa mno ila baadhi yenu Viongozi na akina Patrick Rweymamu ( Meneja ) na Selemani Matola ( Kocha Msaidizi ) Wana ukaribu nae wa 10% halafu wana Chuki zao Binafsi na Kipa Beno Kakolanya ambaye ni Mtu Mpole, Muungwana ila asiyependa Majungu na Kuonewa hovyo.

Kesho tupangieni Beno Kakolanya tu.
 
Binafsi namkubali Kakolanya kuliko Manula
Ni bahati mbaya tu wana Simba SC hili hatulijui ila hakuna Kipa bora, makini na anayejiamini Golini Simba SC kama Beno David Kakolanya na niliwashangaa Simba SC walivyomsajii 'Kipopoma' na 'Kimhemko' Kipa Jeremia Kisubi kutoka Tanzania Prisons kisha akakosa nafasi na kumtoa kwa Mkopo Mtibwa Sugar FC aliko sasa.
 
😃😃😃 Kukuamini siwezi.
Ila acha tusubiri tu.

Nategemea kukuta uzi ukichanganua muda, kikosi na bahati kulingana na muda 😃😃😃.
Nikifanya yote haya utanilipa Tsh ngapi?
 
Acha chuki binafisi kwa Air manula, manula yupo mazoezi si kwa ajili ya mechi bali kwa support wenzake
 
Watu tunaojua kuwa Kesho Kipa Aishi Manula hatocheza tunawashangaa kabisa Kutwa mnavyohangaika kututia Moyo.

Yaani badala ya kutumia muda wenu mwingi kumjenga Kisaikolojia Kipa wangu bora Simba SC Beno David Kakolanya nyie mnahangaika na Aishi Salum Manula wenu kana kwamba ni mzuri kivile wakati ni Ndumba tu za Kwao Kilombero zinambeba, anapendwa na Viongozi wa Juu wa Simba SC na Kucheza Mechi nyingi ndiko Kunambeba pekee.

Hivi mnavyohangaika Kutwa Kulazimisha Kesho Aishi Manula adake wakati tayari hata Daktari wa Timu kawaambia hajapona vyema Jeraha lake mnamjengea Picha gani Kipa mzuri Kumzidi Yeye Beno Kakolanya ambaye Kesho ndiyo ana 95% za Kudaka?

Na mlivyo Wanafiki na Wapuuzi baadhi ya Viongozi wa Simba SC mnaolazimisha Kesho Aishi Manula ikiwezekana apigwe Ganzi ili acheze leo mmeshasahau kuwa sababu Kuu ya Kumleta Simba SC Kipa Beno Kakolanya ni kutokana tu na Kudaka vyema na Kiumahiri kabisa huku akitunyima Ushindi katika Mechi ya Simba na Yanga huku Yeye akidakia Yanga SC.

Sasa kama aliweza Kudaka katika ile 'Derby' na tukavutiwa nae na Kumsajili iweje leo hii tuwe na wasiwasi nae kuelekea 'Derby' yetu nao Kesho? Hivi tunahitaji Elimu Kubwa ya Soka kujua kuwa Kipa Beno Kakolanya ni mzuri kwa kila Kitu kuliko huyu Aishi Manula wenu?

au mnataka sasa tutoboe Siri ya kwanini Aishi Manula wenu aliumia ( Kimaajabu ) na Kioo katika 'Dressing Room' mpaka kila Mchezaji alishangaa? Mwambieni apunguze au aache Kutwa 'Kumroga' Mwenzake Beno Kakolanya kwani Mwenzake ni Mcha Mungu mzuri ile mbaya na ipo Siku yatakuja kumkuta makubwa zaidi ya hilo lililompata.

Hata Kocha wa Makipa ( Mkaburu ) kutoka Bondeni Afrika Kusini tunajua ameshasema kuwa Kipa Beno Kakolanya ni zaidi ya Aishi Manula na kutaka awe anapangwa mno ila baadhi yenu Viongozi na akina Patrick Rweymamu ( Meneja ) na Selemani Matola ( Kocha Msaidizi ) Wana ukaribu nae wa 10% halafu wana Chuki zao Binafsi na Kipa Beno Kakolanya ambaye ni Mtu Mpole, Muungwana ila asiyependa Majungu na Kuonewa hovyo.

Kesho tupangieni Beno Kakolanya tu.
Watalifanyia kazi wahusika
 
N
Huyu jamaa kweli ni Simba au Popoma?
Naona unataka kuiamsha Mizimu yangu ya Kizanaki na Kimakuwa Mkuu si ndiyo? Wewe endelea tu ila nikikufyatukia usimilaumu wala usikimbilie kwa Mapilato wa Jamvi la Jamiiforums ( Moderators ) sawa?
 
Back
Top Bottom