Simba SC tusipozicheza 'Kimkakati' na 'Kimafia' hizi Mechi Tatu za Yanga SC tusahau 'Ubingwa' tena na Msimu huu

Simba SC tusipozicheza 'Kimkakati' na 'Kimafia' hizi Mechi Tatu za Yanga SC tusahau 'Ubingwa' tena na Msimu huu

Naomba nipewe hilo jukumu na niwe na watu hawa Idi Kajuna (mtani wangu wa Kihaya), mafia mwenzangu Kassim Dewji (KD), Mandanje mzee wa kujilipua na mvaa mabomu na poti wangu kutoka kwetu mkoani Mara (Musoma), msomi na tajiri Crescentius Magori ili Yanga SC walie katika mechi zao hizi tatu zijazo.

Ya Kagera Sugar FC tunataka watoke sare (waangushe alama mbili), ya Singida Big Stars FC (japo ni ndugu zao kupitia Waziri wa Fedha Nchemba) tunataka nayo watoke sare (waangushe alama mbili tena), na ile ya Namungo FC (ambao ni ndugu zetu kabisa) tunataka Yanga SC wafungwe ili waangushe jumla ya alama (points) saba (7) tu kisha kazi imalizike.

Simba SC nitafuteni haraka GENTAMYCINE na mniwekee kabisa na mzigo (hela) wangu ili nizicheze hizi mechi zao kubwa na muhimu tatu tu sawa?

Nawaonya kama Simba SC tusipozicheza hizi mechi zao tatu na sisi leo dhidi ya Ihefu FC tukatoka sare au hata kufungwa na ile ya Namungo FC wiki ijayo nayo tukafungwa au kutoka sare basi GENTAMYCINE nasema wazi na hapa hapa JamiiForums kuwa Ubingwa wa NBC Premier League kwa msimu huu tena tuusahau na Yanga SC wataubeba (watauchukua) tena.
Yanga sio wenzenu wanacheza mechi zao kimkakati na kwa mahesabu makali sana, Mzunguko huu wa kwanza yanga anacheza mechi nyingi ugenini kwenye viwanja vibovu na anakusanya point, Simba mzunguko huu wa kwanza anacheza mechi nyingi kwa mkapa na kafunga goli 14 kwa mkapa na mechi 2 za mikoani kafunga goli 2 tu nafikiri utaona ugumu atakaokutana nao mzunguko wa pili atakapoanza kucheza mechi nyingi mikoani na wakati huo yanga atakuwa kwa mkapa kwa mechi nyingi, hivyo mtihani mkubwa upo kwa simba ambae tiyali keshadondosha point 2 kwa singida ktk mechi 2 alizocheza mikoani na yanga kaokota alama 9 zote alizocheza mikoani na kesho ataokota alama kwa kagera sugar licha ya uchovu walionao kutokana na ratiba
 
Yanga wakiwa na Utulivu kama ilivyo Sasa ningumu Simba kuchukua kikombe chochote. Yanga Wana network kubwa sana na kwasasa wanakikosi imara na dirisha dogo wataongeza watu.
Na kwa taarifa yao ni kwamba inachukua zaidi ya mechi 45 Yanga kupoteza mechi moja na kwa sasa ili Simba awe bingwa inatakiwa Yanga apoteze mechi mbili kwa hesabu za haraka ni misimu miwili ijayo huu umeisha !
 
Ubingwa wa msimu huu bado sana mkuu narudia bado sanaaaa,hata azam anaweza kuwa kwenye mbio za ubingwa
 
Wachezaji wa Simba wapo kifaza snaa ,nakerekaga Sana wakipata goli moja au mawili wanavyoaanza kucheza na majukwaa au kupiga vi backpasses visivyo na manaa ,yaan hawajui faida ya magoli hapo baadae yanaweza wasaidia.
Ile game na mtibwa ingekuwa ndo yanga kapata ile bahat ya kucheza na timu yenye upungufu wa wachezaj wawil wangejipigia hata kumi ,nawaona watan wangu wapo serious Sana muda wote tofaut na hii Simba yangu ufadha umejaa Sana.

Game ya Leo na ihefu anashinda Simba Tena watajituma Sana kusawazisha draw na singida ,baada ya hapo wachezaj watakimbilia insta na Twitter kujipost na kujinad Sana ,mechi inayofuata watapigwa km sio kudraw .
Kwa Simba hii naziona draw nyingi Sana huko mbelen Sion timu ya kubeba ubingwa huu msimu ,.

Kwani timu gani inaongoza kwa magoli mkuu?
 
Back
Top Bottom