Simba sc wapoteana Zanzibar ,hali tete imejitokeza kwenye benchi la ufundi ,viongozi watoka jukwaani na kuingilia kati

Mbona Nane naye alikasirikaaa?
 
Daaah inasikitisha sana yaani hawa ndio wachezaji wetu wa bongo,,tambua kwamba timu inaundwa na wachezaji wengi so mwalimu anapokutoa siyo kwamba haujui Ila ni maono yake,, sasa kichuya kamaind kutoka,,afu hata mkude nae katoka kaenda kupiga story na jamaa nje,,,nafikiri leo ndio mmeamini Maneno ya Edo kumwembe,,simba imekosa wanaume bado ina vivulana.Na hivyo vivulana ndio akina kichuya
 
Yamkini kuna mambo hatuyajui kuhusu uhusiano wa Kocha Djuma na wachezaji wake hata hivyo viongozi wamekosea sana kwenda kumbembeleza huyo bwana mdogo kichuya. Hao viongozi wawaombe radhi mashabiki wao kwa kumnyenyekea Kichuya halafu huyo bwana mdogo aonjeshwe kile alichokutana nacho Yahaya Toure pale manchester City wakati wanatunishiashiana misuli na kocha mkuu. Kwa upande mwingine Simba inabidi wafurahi kwa kufungwa huko Zanzibar kwani itakuwa funzo tosha kwa kocha Djuma kwamba huwezi kufundisha timu mfumo mpya wakati wa mashindano, kilichowakumba simba ndicho kilichowakumba Kilimanjaro Star kule katika CECAFA Challenge Cup. Pia hili liwe darasa tosha kwa Ammy Ninje , Masoud Djuma na wengine kwamba mpira hauchezwi mdomoni bali uwanjani.




 
utovu wa nidhamu, yeye nani..mbona hajafunga game za awali....anafanyiwa sub cr7 ije iwe yeye.....akwende zake
 
Kama msemaji wao huyu anachonga sana ana kejeli nyingi sana oh mchezaji wao mmoja tu ni sawa na wachezaji kumi wa timu zingine manara na tambo zake za kitoto
 
Kichuya Karibu Yanga

Yanga ya wapi...akae huko huko aliko...hatutaki mchezaji ambaye anajiona staa wakati hata miaka mitatu hajafikisha kwenye timu...who is kichuya by the way??? Yanga hawataki 'michezaji' ya aina hiyo yenye 'kiburi cha wazi'...hata heshima hamna????
 
Huyu angekutana na Alex ferguson ndo angejua kiburio sio Maungwana.Beckham alileta nyodo akapigwa bei fasta tu.

Jaap stam yeye aliuzwa na ferguson wakiwa kwenye kituo cha mafuta(petrol station) kama mzaha vile hahah
 
Wanawekwa bench akina Sadio Mane seuse wewe Kichuya? Who are you by the way? Jinga kabisa eti limeweka makamba masikioni!
 
Bila nidhamu hakuna mafanikio popote halafu ukimuuliza huyu atakwambia malengo yangu ni kucheza ulaya mweeeh ajabu na kweli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…