Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,267
Klabu ya Simba leo Septemba 7, 2019, imemtambulisha rasmi Senzo Mazingiza kutoka Afrika Kusini kuwa Afisa Mtendaji Mkuu (CEO), wa klabu hiyo, akichukua nafasi ya Crescentius Magori ambaye amemaliza muda wake.
Akizungumza wakati wa utambulisho huo uliofanyika leo kwenye Hoteli ya Serena Jijini Dar es salaam, Senzo ambaye amewahi kufanya kazi katika Klabu ya Orlando Pirates, Platinum Stars FC pamoja na Chama cha Soka cha Afrika Kusini, ameahidi kuifanya klabu ya Simba kuwa klabu kubwa zaidi barani Afrika.
"Simba ni timu kubwa sana, nimekuwa nikiifuatilia kwa muda sasa. Nimejifunza kuwa ni timu kubwa, na tunaweza kuifanya kubwa zaidi, sio tu ukanda wa Afrika Mashariki bali kuwa klabu kubwa zaidi Afrika" amesema Senzo
Kwa upande wake CEO ambaye amemaliza muda wake Crescentius Magori, amewashukuru Wanasimba kwa ushirikiano waliompa muda wote kwa kipindi chake hadi kumalizika.
"Kuanzia wiki ijayo nitakuwa CEO mstaafu, nawashukuru sana kwa ushirikiano mlionipa. Nawashukuru sana Wanasimba. Kwa wale ambao tumekwazana niombe radhi ilikuwa sababu ya kazi yangu" alisema Magori.
SimbaSCNguvuMoja
Akizungumza wakati wa utambulisho huo uliofanyika leo kwenye Hoteli ya Serena Jijini Dar es salaam, Senzo ambaye amewahi kufanya kazi katika Klabu ya Orlando Pirates, Platinum Stars FC pamoja na Chama cha Soka cha Afrika Kusini, ameahidi kuifanya klabu ya Simba kuwa klabu kubwa zaidi barani Afrika.
"Simba ni timu kubwa sana, nimekuwa nikiifuatilia kwa muda sasa. Nimejifunza kuwa ni timu kubwa, na tunaweza kuifanya kubwa zaidi, sio tu ukanda wa Afrika Mashariki bali kuwa klabu kubwa zaidi Afrika" amesema Senzo
Kwa upande wake CEO ambaye amemaliza muda wake Crescentius Magori, amewashukuru Wanasimba kwa ushirikiano waliompa muda wote kwa kipindi chake hadi kumalizika.
"Kuanzia wiki ijayo nitakuwa CEO mstaafu, nawashukuru sana kwa ushirikiano mlionipa. Nawashukuru sana Wanasimba. Kwa wale ambao tumekwazana niombe radhi ilikuwa sababu ya kazi yangu" alisema Magori.
SimbaSCNguvuMoja