Simba SC yamtambulisha rasmi Afisa Mtendaji Mkuu (CEO) mpya, Senzo Mazingiza kutoka Afrika Kusini

Simba SC yamtambulisha rasmi Afisa Mtendaji Mkuu (CEO) mpya, Senzo Mazingiza kutoka Afrika Kusini

Hivi hivi viongozi wa club nao wanatoka nje.

Watawapoteza washabiki bure na haji manara aanze kulia mbona uwanja haujai.
 
Hivi hivi viongozi wa club nao wanatoka nje.

Watawapoteza washabiki bure na haji manara aanze kulia mbona uwanja haujai.
Hakuna shabiki wa mpira anayeipenda timu ka haifanyi vizuri.
Hapa hakuna hata mmoja mtanzania ambaye ni kiongozi wa timu za liver, Chelsea, man u, man city, Arsenal lakini mashabiki wa kibongo wanazidi kuongezeka.
Labda point yako ni ipi kusema watapoteza mashabiki?
 
 
Ina maana hakuna Mtanzania mwenye sifa za kuwa CEO wa klabu kama Simba? Au ni ugonjwa mpya wa kuamini wageni zaidi. Tumeanza wachezaji, makocha, leo ma CEO, kesho?
Ikiwa ni kweli hakuna, nina watakia SSC kila la kheri.
Hujui kuwa hiyo ni new discipline kwetu?
 
Wrong timing.

Kwao wanauwa Waafrika nyie mnawaajiri.

Simba mngesubiri yanayojiri sasa yapoe. Hapo mnatutukana wote.
 
Ina maana hakuna Mtanzania mwenye sifa za kuwa CEO wa klabu kama Simba? Au ni ugonjwa mpya wa kuamini wageni zaidi. Tumeanza wachezaji, makocha, leo ma CEO, kesho?
Ikiwa ni kweli hakuna, nina watakia SSC kila la kheri.
Labda awe mwana Yanga. Mikia hamna kitu.
 
Tatizo lililopo SA haliwezi kuzuia mambo mengine kuendelea.
Kama hakuna zuio lolote wao kuja huku tatizo liko wapi?
Kila Mwaafrika sasa hivi anatakiwa awagomee Afrika Kusini mpaka wajirekebishe. Hii siyo mara ya kwanza wao kuuwaa na kupora wageni.

Simba wangeonesha mshikamano na Waafrika wengine kipindi hiki.

Si kila jambo lazima litolewe tamko au zuio.

Kuna Watanzania wameuliwa kule.
 
Kila Mwaafrika sasa hivi anatakiwa awagomee Afrika Kusini mpaka wajirekebishe. Hii siyo mara ya kwanza wao kuuwaa na kupora wageni.

Simba wangeonesha mshikamano na Waafrika wengine kipindi hiki.

Si kila jambo lazima litolewe tamko au zuio.

Kuna Watanzania wameuliwa kule.
Amen!
 
Wrong timing.

Kwao wanauwa Waafrika nyie mnawaajiri.

Simba mngesubiri yanayojiri sasa yapoe. Hapo mnatutukana wote.
Mchakato wa CEO ulianza kitambo na makubaliano yalifikiwa kwa huyu Msouth kabla ya hizi vurugu za hivi karibuni..!
 
Aisee why not Saad Kawemba or Patrick Kahemele?

Kwanini wasingetafuta mzungu from UK ambao football culture yetu ni kama copy and paste ya UK ?
Klabu ya Simba leo Septemba 7, 2019, imemtambulisha rasmi Senzo Mazingiza kutoka Afrika Kusini kuwa Afisa Mtendaji Mkuu (CEO), wa klabu hiyo, akichukua nafasi ya Crescentius Magori ambaye amemaliza muda wake.

Akizungumza wakati wa utambulisho huo uliofanyika leo kwenye Hoteli ya Serena Jijini Dar es salaam, Senzo ambaye amewahi kufanya kazi katika Klabu ya Orlando Pirates, Platinum Stars FC pamoja na Chama cha Soka cha Afrika Kusini, ameahidi kuifanya klabu ya Simba kuwa klabu kubwa zaidi barani Afrika.

"Simba ni timu kubwa sana, nimekuwa nikiifuatilia kwa muda sasa. Nimejifunza kuwa ni timu kubwa, na tunaweza kuifanya kubwa zaidi, sio tu ukanda wa Afrika Mashariki bali kuwa klabu kubwa zaidi Afrika" amesema Senzo

Kwa upande wake CEO ambaye amemaliza muda wake Crescentius Magori, amewashukuru Wanasimba kwa ushirikiano waliompa muda wote kwa kipindi chake hadi kumalizika.

"Kuanzia wiki ijayo nitakuwa CEO mstaafu, nawashukuru sana kwa ushirikiano mlionipa. Nawashukuru sana Wanasimba. Kwa wale ambao tumekwazana niombe radhi ilikuwa sababu ya kazi yangu" alisema Magori.

SimbaSCNguvuMoja

View attachment 1200719View attachment 1200720
 
Back
Top Bottom