Simba Vs Yanga (1-0) | Shirikisho | Lake Tanganyika. Simba yatwaa ubingwa ASFC

Simba Vs Yanga (1-0) | Shirikisho | Lake Tanganyika. Simba yatwaa ubingwa ASFC

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Ule muda wa lawama umewadia. Akili, macho na masikio yote kwa sasa yameelekezwa Kigoma ambako leo Jumapili, kunapigwa pambano la fainali ya Kombe la Shirikisho (ASFC) baina ya Yanga na Simba itakayochezwa katika Uwanja wa Lake Tanganyika. Shilingi yako iko upande gani?

Kuwa nami kuanzia Saa kumi kamili jioni hii

==========

00' Kipenga kinapulizwa Lake Tanganyika na Yanga inaanza kufika langoni kwa Simba lakini linakuwa shambulizi mfu

01' Yanga inafika tena langoni mwa Simba, Ditram Nchimbi anagongana na Aishi Manula, Refa anaipa faida Simba

07' Ditram Anawekwa chini na Shomari Kapombe nje kidogo ya 18, Free Kick ya Yakuba inapokelewa barabara na Mlinda mlango wa Simba, Aishi Manula

12' Mwamuzi anatoa kadi ya njano kwa Chama baada ya kulalamika Luis Miquissone kufanyiwa madhambi ndani ya Box

22' Almanusura Simba waandike goli la kwanza lakini mpango wao unasimamishwa na Farook Shikalo

25' Tuisila anawekwa chini na Mohammed Hussein na kushindwa mbio, free kicki keelekea lango la Simba

27' Faul ya Adeyum inashindwa kupenya, Yanga wanapata faida ya kona pacha na zote mfu

32' Mugalu na Luis wanacheza vizuri langoni mwa Yanga lakini juhudi zao zinazimwa na beki ya Yanga

37' Luis anafoka baada ya mwamuzi kutoa kona, yeye akiamini ni mkwaju wa penat baada ya mchezaji wa Yanga kumgonga mkononi

45+1' 🟥Mukoko analamba kadi nyekundu baada ya kumpiga kiwiko John Bocco, Yanga sasa itacheza pungufu

45+5' Mpira unaenda mapumziko, Simba 0-0 Yanga

45' Ngwe ya pili na ya mwisho imerejea.

57' Josh Onyango anapewa kadi ya njano kumsukumiza mchezaji wa Yanga

62' Yaqub anashindwa kuitanguliza Yanga baada ya kupiga shuti kali nje ya lango, pasi safi kutoka kwa Ditram

67' Sub: Morrison anaingia upande wa Simba

75' Fisto anaingia kuchukua nafasi ya Abdul kwa upande wa Yanga

78' Nchimba anakwenda bench na nafasi yake kuchukuliwa na Farid Mussa

79' ⚽ Thadeo Lwanga anaiwekea Simba bao la Kwanza baada ya kuunganisha kwa kichwa mpira wa kona

81' Lwanga anapewa kadi ya njano baada ya kuvua jezi wakati anashangalia

83' Chama anakwenda bench

90+6' Mpira umekwisha, Simba mabigwa wa kombe la Shirikisho 2020/21 kwa kushinda goli 1-0

Barbara: Bila muwekezaji tusingefika hapa, tunangoja pre season tutaweka targets

Injinia Hersi: Vijana wetu wamejitahidi sana. Yanga ina kikosi imara mpaka imecheza fainali, kila timu inafanya maboresho, tutafanya next season kwa ushauri wa kocha
 
Kama aligongwa akiwa kamili, haiwezekani asigongwe baada ya Bundi kutua
 
Mapema tu washaanza kutoana kafara

IMG_20210725_142424.jpg
 
Back
Top Bottom