Simba wa Teranga: Kikosi cha dhahabu kilichotikisa Dunia

Simba wa Teranga: Kikosi cha dhahabu kilichotikisa Dunia

mechi ile ilichezwa siku ya ijumaa mchana ,ikiwa ni mechi ya ufunguzi wa kombe la dunia, ikihusisha bingwa mtetezi France na timu toka africa,
Mashabiki takribani elfu 60 hawakuamini bingwa mtetezi akidhalilishwa na timu changa toka africa.

watu kama kina Zidane, david trezegut, bathez, viel, thiery henry, Christian kalembeu.

daaah Miaka imekimbia.
Ilikuwa ni mechi ya aibu ya karne kwa ufaransa kufungwa na mtumwa wake.
Kumbuka ufaransa aliwahi mtawala senegal.

Ilikuwa ni fedheha kama sio fadhaha iliyotapakaa kuanzia jiji la paris,marseille,lyon hadi bordeux.
Ilikuwa ni ushindi wa senegal dhidi ya mtawala wake(mkoloni) aliyemtawala kwa karne na dahari.

Ilikuwa ni kama kisasi toka kwa senegali dhidi ya mtawala wake wa zamani.
Naamini furaha,shangwe na nderemo ile toka viwanja vya world cup kule korea/japan viliweza kusambaa kutoka mashariki ya mbali,afrika magharibi dakar na hadi katika malalo(kaburini) kwa baba wa taifa la senegali hayati LEOPARD SEDAR SENGHOR ni kama vijana na vijukuu wa senghor(simba wa teranga) walilipa kisasi kwa niaba yake dhidi ya utawala wa kidhalimu wa ufaransa.

Na kwa francophone wote ilikuwa ni ushindi dhidi ya mtawala wao wa zamani.

Hata sisi inshaaalah siku moja twaweza wafunga watawala wetu wa zamani ujerumani na uingereza kwenye world cup tujisikie furaha kama senegal siku ile walivojisikia furaha.
 
Kumbe huyu dogo musonda wa Chelsea ana asili ya Zambia?
Yaah baba na mama yake wote wazambia mzee wake nae pia alikuwa kiungo akiitwa Charles musonda hata hawa nduguze lamisha na tika wamezaliwa Belgium sababu baba yao alikuwa akikipiga club ya inderlecht ya huko nae musonda jr alizaliwa miaka mitatu baada ya ajali ya wachezaji wa zambia kisa cha kupona baba yake ni kwamba hakuanzia safari zambia yeye ilikuwa wakutane huko huko yeye pamoja na kalusha bwalya. Pia kingine kuna waqt huyu landamila kocha wa Yanga alimualika dogo timu ya Taifa akachomoa pana figisu figisu nyingi kuwa musonda na kalusha hawaelewani sasa inasemekana wazazi wa musonda wanamshinikiza dogo badala ya kuchezea chipolopolo bora achague kati ya England ambapo anaweza kupata haki ya kucheza the three lions kutokana na muda aliokaa wingereza au nchi yake ya kuzaliwa yaani ubeligiji.
 
Kilikuwa kikosi kizuri sana, diouf alikuwa hatari sana, nyuma kiungo pape bouba diop aka kabati. Game ya pili makundi na denmark 1-1 salif diao anamchambua schmeichel game ya tatu na uruguay 1st half wanaongoza 3 bila, 2nd half wakina forlan wanarudisha dakika za majeruhi beki ndiaye anaokoa shuti la forlan kwa kichwa kwani wangefungwa uruguay angeenda na denmark. 2nd round wanampiga sweden golden goal.......... Kikosi kilikuwa kizuri nidhamu ni changamoto kwa timu za kiafrika. Cameroun/masr za sasa zina nidhamu lakini hazifikii kipaji cha akina diouf.
Ahsante mwanamichezo kwa kumbukumbu sahihi.
 
Yaah baba na mama yake wote wazambia mzee wake nae pia alikuwa kiungo akiitwa Charles musonda hata hawa nduguze lamisha na tika wamezaliwa Belgium sababu baba yao alikuwa akikipiga club ya inderlecht ya huko nae musonda jr alizaliwa miaka mitatu baada ya ajali ya wachezaji wa zambia kisa cha kupona baba yake ni kwamba hakuanzia safari zambia yeye ilikuwa wakutane huko huko yeye pamoja na kalusha bwalya. Pia kingine kuna waqt huyu landamila kocha wa Yanga alimualika dogo timu ya Taifa akachomoa pana figisu figisu nyingi kuwa musonda na kalusha hawaelewani sasa inasemekana wazazi wa musonda wanamshinikiza dogo badala ya kuchezea chipolopolo bora achague kati ya England ambapo anaweza kupata haki ya kucheza the three lions kutokana na muda aliokaa wingereza au nchi yake ya kuzaliwa yaani ubeligiji.
Shukran sana mkuu kwa maelezo mazuri. Inaonekana ww ni mfuatiliaji na mdau mzuri wa soka
 
Ilikuwa ni mechi ya aibu ya karne kwa ufaransa kufungwa na mtumwa wake.
Kumbuka ufaransa aliwahi mtawala senegal.

Ilikuwa ni fedheha kama sio fadhaha iliyotapakaa kuanzia jiji la paris,marseille,lyon hadi bordeux.
Ilikuwa ni ushindi wa senegal dhidi ya mtawala wake(mkoloni) aliyemtawala kwa karne na dahari.

Ilikuwa ni kama kisasi toka kwa senegali dhidi ya mtawala wake wa zamani.
Naamini furaha,shangwe na nderemo ile toka viwanja vya world cup kule korea/japan viliweza kusambaa kutoka mashariki ya mbali,afrika magharibi dakar na hadi katika malalo(kaburini) kwa baba wa taifa la senegali hayati LEOPARD SEDAR SENGHOR ni kama vijana na vijukuu wa senghor(simba wa teranga) walilipa kisasi kwa niaba yake dhidi ya utawala wa kidhalimu wa ufaransa.

Na kwa francophone wote ilikuwa ni ushindi dhidi ya mtawala wao wa zamani.

Hata sisi inshaaalah siku moja twaweza wafunga watawala wetu wa zamani ujerumani na uingereza kwenye world cup tujisikie furaha kama senegal siku ile walivojisikia furaha.
Kwa Tanzania hii ya akina Mshindo Msolla na Wallace Karia ambayo haina hata dira au sera ya maendeleo ya soka letu kwa miaka mitano mbele. Tusitegemee chochote
 
Likiisha hili la simba wa teranga, ina bidi sasa tulichambue kosi la Nigeria eagles . lile la kina amokachi Daniel, tijan Babangida, Emmanuel amunike. Uche .
 
Likiisha hili la simba wa teranga, ina bidi sasa tulichambue kosi la Nigeria eagles . lile la kina amokachi Daniel, tijan Babangida, Emmanuel amunike. Uche .

Kipindi Senegal anampiga France upande mwingine ilikuwepo Nigeria super eagles , pale walikuwepo kina Aghahowa, ife soji , beki mstaarabu Taribo West , kina finidi George , Babayaro n.k ! Hawa jamaa walikuwa wamekamilika kwa bahati mbaya wakaangukia kundi la kifo wakiwa pamoja na England’ ya kina beckam , Owen , Argentina ya kina ortega na batistuta .

Kama kawaida yao walikuwa wagumu sana kufungika, beki yao ilikuwa ngumu sana tatizo likawa kwenye kufunga pia , wao , Argentina na Germany ndo walikuwa my favorite

Mwisho wa siku Ikabidi waage kwenye makundi ila kwa mbinde sana ...

3b1d321d0534388b16445c3c22c658a4.jpg
3240dc5a13114efaa367389c6ab7ab8d.jpg
 
Kipindi Senegal anampiga France upande mwingine ilikuwepo Nigeria super eagles , pale walikuwepo kina Aghahowa, ife soji , beki mstaarabu Taribo West , kina finidi George , Babayaro n.k ! Hawa jamaa walikuwa wamekamilika kwa bahati mbaya wakaangukia kundi la kifo wakiwa pamoja na England’ ya kina beckam , Owen , Argentina ya kina ortega na batistuta .

Kama kawaida yao walikuwa wagumu sana kufungika, beki yao ilikuwa ngumu sana tatizo likawa kwenye kufunga pia , wao , Argentina na Germany ndo walikuwa my favorite

Mwisho wa siku Ikabidi waage kwenye makundi ila kwa mbinde sana ...

3b1d321d0534388b16445c3c22c658a4.jpg
3240dc5a13114efaa367389c6ab7ab8d.jpg

Mwaka 2002 , Kombe la dunia korea kusini na Japan, Mechi kati ya Nigeria na Argentina ilipigwa siku ya jumapili asubuhi mida ya saa tatu asubuhi kwa majira ya africa Mashariki .

Kona ya kumi ilopigwa na Mkongwe Juan Sebastian Veron Ndio iloondoa Matumaini ya waafrica kuendelea hatua ya robo fainali. Katika mechi ili namkumbuka Diego simeon , Huyu Juan sebastian Veron alipotelea manchester.

Katika Kundi hili la kifo Muingeleza alifanikiwa kuvuka pamoja na Mjerumani, Mechi ilofuata muingeleza akalala mbele ya Brazil mida ya mchana. Mjerumani alifanikiwa kufika fainali yeye na Brazil.

Siku ya Jumapili mchana wa saa tisa Ndani uwanja wa Yokohama ,Mjerumani akalala na Vyuma viwili vya mkongwe Ronaldo luis Nazario De Lima.

Wakumbukwe wafuatao:
Oliver Khan,
Gatuso
Idetoshi Nakata,
Suzuki,
Jugen Klinsman Kocha,
Barack namba 6 Ujeruman,
Caf,
Roberto Carlos (alipotelea Real madrid)
Reonaldo,

MIAKA IMEKIMBIA..
 
Back
Top Bottom